< Job 1 >

1 Bil je mož v deželi Uc, katerega ime je bilo Job, in ta mož je bil popoln in iskren in nekdo, ki se je bal Boga in se ogibal zla.
Katika nchi ya Usi paliishi mtu ambaye aliitwa Ayubu. Mtu huyu alikuwa hana hatia, naye alikuwa mkamilifu; alimcha Mungu na kuepukana na uovu.
2 Tam se mu je rodilo sedem sinov in tri hčere.
Alikuwa na wana saba na binti watatu,
3 Njegovo imetje je bilo tudi sedem tisoč ovc, tri tisoč kamel, petsto jarmov volov, petsto oslic in zelo velika družina, tako da je bil ta človek največji izmed vseh mož vzhoda.
naye alikuwa na kondoo elfu saba, ngamia elfu tatu, jozi mia tano za maksai, na punda mia tano, tena alikuwa na idadi kubwa ya watumishi. Alikuwa mtu mkuu sana miongoni mwa watu wa Mashariki.
4 Njegovi sinovi so šli in praznovali v svojih hišah vsak svoj dan. Poslali so in dali poklicati svoje tri sestre, da jedo in pijejo z njimi.
Wanawe walikuwa na desturi ya kufanya karamu katika nyumba zao kwa zamu, nao wangewaalika umbu zao watatu ili kula na kunywa pamoja nao.
5 Bilo je tako, da ko so se dnevi njihovega praznovanja iztekli, je Job poslal, jih posvečeval in vstajal zgodaj zjutraj ter daroval žgalne daritve glede na število njih vseh, kajti Job je rekel: »Morda so moji sinovi grešili in v svojih srcih prekleli Boga.« Tako je Job nenehno delal.
Wakati kipindi cha karamu kilimalizika, Ayubu angetuma waitwe na kuwafanyia utakaso. Angetoa dhabihu ya sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya kila mmoja wao asubuhi na mapema, akifikiri, “Pengine wanangu wametenda dhambi na kumlaani Mungu mioyoni mwao.” Hii ilikuwa ndiyo desturi ya kawaida ya Ayubu.
6 Bil je torej dan, ko so prišli Božji sinovi, da se pokažejo pred Gospodom in tudi Satan je prišel med njimi.
Siku moja wana wa Mungu walikwenda kujionyesha mbele za Bwana. Shetani naye akaja pamoja nao.
7 Gospod je rekel Satanu: »Od kod prihajaš?« Nató je Satan odgovoril Gospodu in rekel: »Od potikanja sem ter tja po zemlji in od hoje gor in dol po njej.«
Bwana akamwambia Shetani, “Umetoka wapi?” Shetani akamjibu Bwana, “Natoka kuzunguka pote duniani, nikitembea huku na huko humo.”
8 Gospod je rekel Satanu: »Si kaj preudaril [o] mojem služabniku Jobu, ker na zemlji ni nikogar podobnega njemu; popoln in pošten človek je, ki se boji Boga in se ogiblje zla?«
Ndipo Bwana akamwambia Shetani, “Je, umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Hakuna mtu mwingine duniani aliye kama yeye, asiye na hatia, ni mnyofu, mwenye kumcha Mungu, na kuepukana na uovu.”
9 Potem je Satan odgovoril Gospodu in rekel: »Mar se Job zastonj boji Boga?
Shetani akamjibu Bwana, “Je, Ayubu anamcha Mungu bure?
10 Mar nisi ti naredil ograje okoli njega, okoli njegove hiše in okoli vsega, kar ima na vsaki strani? Blagoslovil si delo njegovih rok in njegovo imetje se je povečalo v deželi.
Je, wewe hukumjengea boma pande zote yeye na wa nyumbani mwake pamoja na kila kitu alicho nacho? Kazi za mikono yake umezibariki na hivyo makundi yake ya kondoo na mbuzi pamoja na ya wanyama yameenea katika nchi nzima.
11 Toda iztegni sedaj svojo roko in se dotakni vsega, kar ima in preklinjal te bo v tvoj obraz.«
Lakini nyoosha mkono wako na kupiga kila kitu alicho nacho, naye kwa hakika atakulaani mbele za uso wako.”
12 Gospod je rekel Satanu: »Glej, vse, kar ima, je v tvoji oblasti, samo nanj ne iztegni svoje roke.« Tako je Satan odšel izpred Gospodove prisotnosti.
Bwana akamwambia Shetani, “Vema sana, kwa hiyo, kila kitu alicho nacho kiko mikononi mwako, lakini juu ya huyo mtu mwenyewe usimguse hata kwa kidole.” Ndipo Shetani akatoka mbele za Bwana.
13 Bil je dan, ko so njegovi sinovi in njegove hčere jedli in pili vino v hiši njihovega najstarejšega brata.
Siku moja watoto wa Ayubu walipokuwa wakifanya karamu wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa,
14 K Jobu je prišel poslanec in rekel: »Voli so orali in osli so se pasli poleg njih
akaja mjumbe kwa Ayubu na kusema, “Maksai walikuwa wakilima na punda walikuwa wakilisha karibu nao,
15 in Sabejci so padli nadnje ter jih odvlekli proč. Da, z ostrino meča so umorili služabnike in samo jaz sam sem pobegnil, da ti povem.«
Waseba wakawashambulia na kuchukua mifugo. Kisha wakawaua watumishi kwa upanga, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari!”
16 Medtem ko je še govoril, je prišel še drugi in rekel: »Ogenj od Boga je padel z neba in sežgal ovce in služabnike, jih použil in samo jaz sam sem pobegnil, da ti povem.«
Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Moto wa Mungu ulishuka kutoka mbinguni na kuteketeza kondoo na watumishi, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari!”
17 Medtem ko je še govoril, je prišel še drugi in rekel: »Kaldejci so postavili tri čete in vpadli na kamele in jih odvedli proč. Da, in z ostrino meča umorili služabnike in samo jaz sam sem pobegnil, da ti povem.«
Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Wakaldayo waliunda vikosi vitatu vya uvamizi na kuwaangukia ngamia wako na kuwachukua wakaondoka nao. Wakawaua watumishi kwa upanga, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari.”
18 Medtem ko je še govoril, je prišel še drugi in rekel: »Tvoji sinovi in tvoje hčere so jedli in pili vino v hiši njihovega najstarejšega brata.
Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Wana wako na binti zako walipokuwa wakifanya karamu, wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa,
19 Glej, iz divjine je prihrumel mogočen veter in udaril štiri vogale hiše in ta je padla na mladeniče in ti so mrtvi. Samo jaz sam sem pobegnil, da ti povem.«
ghafula upepo wenye nguvu ukavuma kutoka jangwani, nao ukaipiga nyumba hiyo pembe zake nne. Ikawaangukia hao watoto nao wamekufa, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari!”
20 Potem je Job vstal, raztrgal svoje ogrinjalo, obril svojo glavo, padel dol na tla in oboževal
Ndipo Ayubu akasimama, akararua joho lake na kunyoa nywele zake. Kisha akaanguka chini katika kuabudu
21 ter rekel: »Nag sem prišel iz maternice svoje matere in nag se bom vrnil tja. Gospod je dal in Gospod je vzel. Blagoslovljeno bodi Gospodovo ime.«
na kusema: “Nilitoka tumboni mwa mama yangu uchi, nami nitaondoka uchi, Bwana alinipa, naye Bwana ameviondoa, jina la Bwana litukuzwe.”
22 V vsem tem Job ni grešil niti ni nespametno obdolžil Boga.
Katika mambo haya yote, Ayubu hakutenda dhambi kwa kumlaumu Mungu kwa kufanya ubaya.

< Job 1 >