< Job 5 >

1 »Sedaj kliči, če bo tam kdorkoli, ki ti bo odgovoril. H kateremu izmed svetih se boš obrnil?
“Ita kama unataka, lakini ni nani atakayekujibu? Ni yupi kati ya hao watakatifu utakayemgeukia?
2 Kajti bes ubija nespametnega človeka in zavist ubija neumnega.
Kuweka uchungu moyoni humuua mpumbavu, nao wivu humchinja mjinga.
3 Videl sem nespametnega, da se ukoreninja, toda nenadoma sem preklel njegovo prebivališče.
Mimi mwenyewe nimemwona mpumbavu akistawi, lakini ghafula nyumba yake ikawa imelaaniwa.
4 Njegovi otroci so daleč od varnosti in zdrobljeni so pri velikih vratih niti tam ni nikogar, da jih osvobodi.
Watoto wake wako mbali na usalama, hushindwa mahakamani bila mtetezi.
5 Katerega žetev pojedo lačni in jo pobirajo celo iz trnja in ropar požira njihovo imetje.
Wenye njaa huyala mavuno yake, wakiyatoa hata katikati ya miiba, nao wenye kiu huitamani sana mali yake.
6 Čeprav stiska ne prihaja iz prahu niti težava ne poganja iz tal,
Kwa maana taabu haioti kutoka kwenye udongo, wala udhia hauchipui kutoka ardhini.
7 vendar je človek rojen za stisko, kakor iskrice letijo navzgor.
Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zirukavyo kuelekea juu.
8 Iskal bi Boga in Bogu bi izročil svojo zadevo,
“Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.
9 ki dela velike stvari in nedoumljive, čudovite stvari brez števila,
Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
10 ki daje dež na zemljo in vode pošilja na polja,
Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
11 da tiste, ki so nizki, postavi visoko; da bi tisti, ki žalujejo, lahko bili povišani do varnosti.
Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
12 On razočara naklepe prebrisanega, tako da njihove roke ne morejo opravljati svoje podjetnosti.
Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.
13 Modre jemlje v njihovi prebrisanosti in nasvet kljubovalnega je naglo izvršen.
Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
14 Srečajo se s temo podnevi in tipajo opoldan kakor ponoči.
Giza huwapata wakati wa mchana; wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.
15 Toda on rešuje ubogega pred mečem, pred njihovimi usti in pred roko mogočnih.
Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao; huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.
16 Tako ima ubogi upanje in krivičnost ustavlja svoja usta.
Kwa hiyo maskini analo tarajio, nao udhalimu hufumba kinywa chake.
17 Glej, srečen je človek, ki ga Bog graja, zatorej ne preziraj karanja Vsemogočnega.
“Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.
18 Kajti on dela rane in jih povezuje, on ranja in njegove roke ozdravljajo.
Kwa kuwa hutia jeraha, lakini pia huyafunga; huumiza, lakini mikono yake pia huponya.
19 Osvobodil te bo v šestih težavah. Da, v sedmi se te nobeno zlo ne bo dotaknilo.
Kutoka majanga sita atakuokoa; naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.
20 V lakoti te bo odkupil pred smrtjo in v vojni pred močjo meča.
Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.
21 Skrit boš pred bičanjem jezika niti se ne boš bal uničenja, kadar to prihaja.
Utalindwa kutokana na kichapo cha ulimi, wala hutakuwa na sababu ya kuogopa maangamizi yatakapokujia.
22 Ob uničenju in lakoti se boš smejal niti se ne boš bal zemeljskih zveri.
Utayacheka maangamizo na njaa, wala hutakuwa na sababu ya kuwaogopa wanyama wakali wa mwituni.
23 Kajti v zavezi boš s kamni polja in poljske zveri bodo v miru s teboj.
Kwa kuwa utakuwa na agano na mawe ya mashamba, nao wanyama wa mwitu watakuwa na amani nawe.
24 Vedel boš, da bo tvoj šotor v miru in obiskal boš svoje prebivališče in ne boš grešil.
Utajua ya kwamba hema lako li salama; utahesabu mali zako wala hutakuta chochote kilichopungua.
25 Vedel boš tudi, da bo tvojega semena veliko in tvojega potomstva kakor trave zemlje.
Utajua ya kuwa watoto wako watakuwa wengi, nao wazao wako wengi kama majani ya nchi.
26 K svojemu grobu boš prišel v polni starosti, podobno kakor kopica žita prihaja v svojem obdobju.
Utaingia kaburini ukiwa na umri wa uzee mtimilifu, kama masuke ya ngano yakusanywapo kwa wakati wake.
27 Glej to, mi smo to preiskali, tako je to. Poslušaj to in spoznaj to v svoje dobro.«
“Tumelichunguza hili, nalo ni kweli. Hivyo lisikie na ulitendee kazi.”

< Job 5 >