< Job 12 >
1 Job je odgovoril in rekel:
Ndipo Ayubu akajibu:
2 »Brez dvoma ste vi samo ljudje in modrost bo umrla z vami.
“Bila shaka ninyi ndio watu, nayo hekima itakoma mtakapokufa!
3 Toda jaz imam razumevanje prav tako kakor vi. Nisem slabši od vas. Da, kdo ne pozna takšnih stvari, kakor so te?
Lakini mimi ninao ufahamu kama ninyi; mimi si duni kwenu. Ni nani asiyejua mambo haya yote?
4 Jaz sem kakor nekdo, zasmehovan od svojega bližnjega, ki kliče k Bogu in ta mu odgovarja. Pravičen človek je zasmehovan do norčevanja.
“Nimekuwa mtu wa kuchekwa na rafiki zangu, ingawa nilimwita Mungu naye akanijibu: mimi ni mtu wa kuchekwa tu, ingawa ni mwadilifu na nisiye na hatia!
5 Kdor je pripravljen, da zdrsne s svojimi stopali, je kakor svetilka, prezirana v mislih tistega, ki je ohol.
Wanadamu wakiwa katika utulivu huwa na dharau kwa wale wenye msiba kana kwamba ndiyo haki ya wale ambao miguu yao inateleza.
6 Šotori roparjev uspevajo in tisti, ki izzivajo Boga, so varni; v katerih roko Bog obilno prinaša.
Hema za wanyangʼanyi hazisumbuliwi, wale wanaomghadhibisha Mungu wako salama: wale wamchukuao mungu wao mikononi mwao.
7 Toda vprašaj sedaj živali in te bodo poučile in perjad neba in ti bodo povedale.
“Lakini ulizeni wanyama, nao watawafundisha, au ndege wa angani, nao watawaambia;
8 Ali govori zemlji in te bo poučila in morske ribe ti bodo oznanile.
au zungumzeni na dunia, nayo itawafundisha, au acheni samaki wa baharini wawape taarifa.
9 Kdo v vsem tem ne spoznava, da je to naredila Gospodova roka?
Ni nani miongoni mwa hawa wote asiyejua kwamba mkono wa Bwana ndio uliofanya hili?
10 V čigar roki je duša vsake žive stvari in dih vsega človeštva.
Mkononi mwake kuna uhai wa kila kiumbe, na pumzi ya wanadamu wote.
11 Mar uho ne preizkuša besed? In usta ne okusijo njegove hrane?
Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula?
12 S starcem je modrost, in v dolžini dni razumnost.
Je, hekima haipatikani katikati ya wazee? Je, maisha marefu hayaleti ufahamu?
13 Z njim je modrost in moč, on ima nasvet in razumevanje.
“Hekima na nguvu ni vya Mungu; shauri na ufahamu ni vyake yeye.
14 Glej, on poruši in to ne more biti ponovno zgrajeno. On zapre človeka in ne more biti odpiranja.
Kile anachokibomoa hakiwezi kujengeka tena; mtu aliyefungiwa naye hawezi kufunguliwa.
15 Glej, on zadržuje vode in se posušijo. On jih prav tako pošilja ven in razrijejo zemljo.
Akizuia maji, huwa pana ukame; akiyaachia maji, huharibu nchi.
16 Z njim je moč in modrost; prevarani in slepar sta njegova.
Kwake kuna nguvu na ushindi; adanganywaye na adanganyaye, wote wawili ni wake.
17 Svetovalce odvede oplenjene in sodnike dela bedake.
Yeye huwaondoa washauri wakiwa wametekwa nyara, naye huwapumbaza wanaotoa maamuzi.
18 Kraljem razvezuje vez in njihova ledja opasuje s pasom.
Huondoa pingu zilizofungwa na wafalme, na kuwafunga mishipi ya kiunoni.
19 Prince odvede oplenjene in podira močne.
Huwaondoa makuhani wakiwa wametekwa nyara, na kuwaangusha waliojiimarisha muda mrefu.
20 Odstranja govor zanesljivih in odvzema razumnost ostarelih.
Hunyamazisha midomo ya washauri wanaoaminika, na kuondoa busara ya wazee.
21 Na prince izliva zaničevanje in slabi moč močnih.
Huwamwagia dharau wanaoheshimika, na kuwavua silaha wenye nguvu.
22 Odkriva globoke stvari teme in na svetlobo prinaša smrtno senco.
Hufunua mambo ya ndani ya gizani, na kuyaleta nuruni yale yaliyositirika sana.
23 Povečuje narode in jih uničuje. Razširja narode in jih ponovno vodi v suženjstvo.
Huyafanya mataifa yatukuke na kuyaangamiza; hufanya mataifa kuwa makubwa, naye huyatawanya.
24 Odvzema srce vodjem ljudstva zemlje in jim povzroča, da tavajo v divjini, kjer ni poti.
Huwaondolea viongozi wa nchi akili zao; huwapeleka watangetange nyikani pasipo na njia.
25 Tipajo v temi brez svetlobe in on jim povzroča, da se opotekajo kakor pijan človek.
Hupapasa gizani pasipokuwa na mwanga; huwafanya wapepesuke kama walevi.