< Jeremija 18 >

1 Beseda, ki je prišla Jeremiju od Gospoda, rekoč:
Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
2 »Vstani in pojdi dol k lončarjevi hiši in tam ti bom povzročil, da boš slišal moje besede.«
“Shuka uende mpaka nyumba ya mfinyanzi, nami huko nitakupa ujumbe wangu.”
3 Potem sem odšel dol k lončarjevi hiši in glej, izdeloval je delo na kolesih.
Kwa hiyo nikashuka mpaka kwenye nyumba ya mfinyanzi, nikamkuta akifinyanga kwa gurudumu lake.
4 Posoda, ki jo je naredil iz ila je bila iznakažena v lončarjevi roki. Tako je še enkrat naredil drugo posodo, kakor se je lončarju zdelo dobro, da jo naredi.
Lakini chombo alichokuwa akikifinyanga kutokana na udongo kilivunjika mikononi mwake, hivyo mfinyanzi akakifanya kuwa chombo kingine, umbo jingine kama vile ilivyoonekana vyema kwake yeye.
5 Potem je k meni prišla Gospodova beseda, rekoč:
Kisha neno la Bwana likanijia kusema:
6 »Oh Izraelova hiša, mar ne morem narediti z vami kakor ta lončar?« govori Gospod. »Glejte, kakor je ilo v lončarjevi roki, tako ste vi v moji roki, oh Izraelova hiša.
“Ee nyumba ya Israeli, je, siwezi kuwafanyia kama huyu mfinyanzi afanyavyo?” asema Bwana. “Kama vile udongo ulivyo katika mikono ya mfinyanzi, ndivyo mlivyo katika mkono wangu, ee nyumba ya Israeli.
7 V kakšnem trenutku bom govoril glede naroda in glede kraljestva, da ga izruvam, poderem in uničim.
Ikiwa wakati wowote nikitangaza kuwa taifa au ufalme utangʼolewa, utaangushwa na kuangamizwa,
8 Če [pa] se ta narod, zoper katerega sem proglasil, obrne od svojega zla, se bom pokesal od zla, ki sem jim ga mislil storiti.
ikiwa lile taifa nililolionya litatubia uovu wake, ndipo nitakapokuwa na huruma, wala sitawapiga kwa maafa niliyokuwa nimewakusudia.
9 V kakšnem trenutku bom govoril glede naroda in glede kraljestva, da ga zgradim in zasadim.
Ikiwa wakati mwingine nitatangaza kuwa taifa ama utawala ujengwe na kuwekwa wakfu,
10 Če [pa] dela zlo v mojem pogledu, da ne uboga mojega glasu, potem se bom pokesal dobrega, s katerim sem rekel, da bi jim koristil.
ikiwa utafanya maovu mbele zangu na hukunitii, ndipo nitakapoghairi makusudio yangu mema niliyokuwa nimeyakusudia.
11 Zdaj torej pojdi, govori Judovim možem in prebivalcem Jeruzalema, rekoč: ›Tako govori Gospod; ›Glejte, zoper vas oblikujem zlo in zoper vas naklepam naklep. Torej se vrnite, vsakdo iz svoje hudobne poti in naredite svoje poti in svoja dejanja dobra.‹«
“Basi kwa hiyo waambie watu wa Yuda na wale waishio Yerusalemu, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Tazama! Ninaandaa maafa kwa ajili yenu, nami ninabuni mabaya dhidi yenu. Kwa hiyo geukeni kutoka njia zenu mbaya, kila mmoja wenu, tengenezeni njia zenu na matendo yenu.’
12 Rekli so: »Tam ni nobenega upanja, temveč bomo hodili po svojih lastnih naklepih in vsakdo izmed nas bo počel zamisel svojega zlega srca.«
Lakini wao watajibu, ‘Hakuna faida. Tutaendelea na mipango yetu wenyewe, kila mmoja wetu atafuata ukaidi wa moyo wake mbaya.’”
13 Zato tako govori Gospod: »Vprašajte torej med pogani, kdo je slišal takšne stvari. Izraelova devica je storila zelo strašno stvar.
Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana: “Ulizia miongoni mwa mataifa: Ni nani alishasikia jambo kama hili? Jambo la kutisha sana limefanywa na Bikira Israeli.
14 Mar bo človek zapustil libanonski sneg, ki prihaja iz poljske skale? Mar bodo hladne tekoče vode, ki prihajajo iz drugega kraja, zapuščene?
Je, barafu ya Lebanoni iliwahi kutoweka kwenye miteremko yake ya mawe wakati wowote? Je, maji yake baridi yatokayo katika vyanzo vilivyo mbali yaliwahi kukoma kutiririka wakati wowote?
15 Ker me je moje ljudstvo pozabilo so zažigali kadilo ničnostim in le-ti so jim storili, da se spotikajo na svojih poteh od starodavnih steza, da hodijo po stezah, na poti, ki ni nasuta,
Lakini watu wangu wamenisahau mimi, wanafukizia uvumba sanamu zisizofaa kitu, zilizowafanya wajikwae katika njia zao na katika mapito ya zamani. Zimewafanya wapite kwenye vichochoro na kwenye barabara ambazo hazikujengwa.
16 da naredijo svojo deželo zapuščeno in neprestan posmeh; vsak, kdor gre tam mimo, bo osupel in bo zmajeval z glavo.
Nchi yao itaharibiwa, itakuwa kitu cha kudharauliwa daima; wote wapitao karibu nayo watashangaa na kutikisa vichwa vyao.
17 Pred sovražnikom jih bom razkropil kakor z vzhodnim vetrom; pokazal jim bom hrbet in ne obraza, na dan njihove katastrofe.«
Kama upepo utokao mashariki, nitawatawanya mbele ya adui zao; nitawapa kisogo wala sio uso, katika siku ya maafa yao.”
18 Potem so rekli: »Pridite in naklepajmo naklepe zoper Jeremija; kajti postava ne bo izginila od duhovnika, niti nasvet od modrega, niti beseda od preroka. Pridite in udarimo ga z jezikom in ne dajmo pozornosti katerikoli izmed njegovih besed.«
Wakasema, “Njooni, tutunge hila dhidi ya Yeremia; kwa kuwa kufundisha sheria kwa kuhani hakutapotea, wala shauri litokalo kwa mwenye hekima, wala neno la manabii. Hivyo njooni, tumshambulie kwa ndimi zetu na tusijali chochote asemacho.”
19 Nakloni mi pozornost, oh Gospod in prisluhni glasu tistih, ki se pričkajo z menoj.
Nisikilize, Ee Bwana, sikia wanayosema washtaki wangu!
20 Mar bo zlo poplačilo za dobro? Kajti izkopali so jamo za mojo dušo. Spomni se, da sem stal pred teboj, da govorim dobro zanje in da odvrnem tvoj bes od njih.
Je, mema yalipwe kwa mabaya? Lakini wao wamenichimbia shimo. Kumbuka kwamba nilisimama mbele yako na kunena mema kwa ajili yao, ili wewe ugeuze hasira yako kali mbali nao.
21 Zato njihove otroke izroči lakoti in njihovo kri izlij s silo meča; in naj bodo njihove žene oropane svojih otrok in bodo vdove; in naj bodo njihovi možje usmrčeni; naj bodo njihovi mladeniči v bitki umorjeni z mečem.
Kwa hiyo uwaache watoto wao waone njaa; uwaache wauawe kwa makali ya upanga. Wake zao wasiwe na watoto, na wawe wajane; waume wao wauawe, nao vijana wao waume wachinjwe kwa upanga vitani.
22 Naj bo krik slišan od njihovih hiš, ko boš nadnje nenadoma privedel krdelo, kajti izkopali so jamo, da bi me ujeli in skrili pasti za moja stopala.
Kilio na kisikike kutoka kwenye nyumba zao ghafula uwaletapo adui dhidi yao, kwa kuwa wamechimba shimo ili kunikamata na wameitegea miguu yangu mitego.
23 Vendar, Gospod, ti poznaš vse njihove namere zoper mene, da me ubijejo. Ne odpusti njihove krivičnosti niti njihovega greha ne izbriši pred svojim pogledom, temveč naj bodo zrušeni pred teboj; tako postopaj z njimi v času svoje jeze.
Lakini unajua, Ee Bwana, hila zao zote za kuniua. Usiyasamehe makosa yao wala usifute dhambi zao mbele za macho yako. Wao na waangamizwe mbele zako; uwashughulikie wakati wa hasira yako.

< Jeremija 18 >