< Izaija 36 >
1 Pripetilo se je torej v štirinajstem letu kralja Ezekíja, da je asirski kralj Senaherib prišel gor zoper vsa obrambna Judova mesta in jih zavzel.
Katika mwaka wa kumi na nne wa utawala wa Mfalme Hezekia, Senakeribu mfalme wa Ashuru akaishambulia miji yote ya Yuda yenye ngome na kuiteka.
2 Asirski kralj je poslal Rabšakéja iz Lahíša v Jeruzalem h kralju Ezekíju z veliko vojsko. In ta se je ustavil pri kanalu gornjega ribnika, na glavni cesti pralčevega polja.
Kisha mfalme wa Ashuru akamtuma jemadari wa jeshi pamoja na jeshi kubwa kutoka Lakishi hadi kwa Mfalme Hezekia huko Yerusalemu. Jemadari wa jeshi akasimama kwenye mfereji wa Bwawa la Juu, lililojengwa katika barabara iendayo kwenye Uwanja wa Dobi.
3 Potem so prišli k njemu Hilkijájev sin Eljakím, ki je bil nad hišo, pisar Šebná in Asáfov sin Joáh, letopisec.
Eliakimu mwana wa Hilkia aliyekuwa msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna aliyekuwa katibu, na Yoa mwana wa Asafu mwandishi wakamwendea.
4 Rabšaké jim je rekel: »Povejte torej Ezekíju: ›Tako govori veliki kralj, kralj Asirije: ›Kakšno zaupanje je to, v katero zaupaš?‹
Jemadari wa jeshi akawaambia, “Mwambieni Hezekia, “‘Hili ndilo asemalo mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru: Ni wapi unapoweka hili tumaini lako?
5 Jaz pravim, ti govoriš (toda to so samo prazne besede) imam nasvet in moč za vojno. Torej komu zaupaš, da si se uprl zoper mene?
Unasema mnayo mikakati na nguvu za kijeshi, lakini unasema maneno matupu tu. Je, wewe unamtegemea nani, hata ukaniasi mimi?
6 Glej, zanašaš se na palico tega zlomljenega trsta, na Egipt, na katerega, če se človek naslanja, se bo zadrl v njegovo roko in jo prebodel. Tako je faraon, egiptovski kralj, vsem, ki zaupajo vanj.
Tazama sasa, unaitegemea Misri, fimbo ile ya mwanzi uliopasuka, ambayo huuchoma na kuujeruhi mkono wa mtu akiiegemea! Hivyo ndivyo alivyo Farao mfalme wa Misri, kwa wote wanaomtegemea.
7 Toda če mi rečeš: ›Mi zaupamo v Gospoda, svojega Boga.‹ Mar ni to tisti, katerega visoke kraje in katerega oltarje je Ezekíja odvzel ter Judu in Jeruzalemu rekel: ›Oboževali boste pred tem oltarjem?‹
Nawe kama ukiniambia, “Tunamtumainia Bwana Mungu wetu”: je, siyo yeye ambaye Hezekia aliondoa mahali pake pa juu pa kuabudia miungu na madhabahu zake, akiwaambia Yuda na Yerusalemu, “Ni lazima mwabudu mbele ya madhabahu haya”?
8 Zdaj torej daj jamstva, prosim te, mojemu gospodarju, asirskemu kralju, jaz pa ti bom dal dva tisoč konjev, če boš na svoji strani nanje zmožen postaviti jezdece.
“‘Njooni sasa, fanyeni mapatano na bwana wangu, mfalme wa Ashuru: Nitakupa farasi elfu mbili, kama unaweza kuwapandisha waendesha farasi juu yao!
9 Kako boš potem odvrnil obličje enega poveljnika, izmed najmanjših služabnikov mojega gospodarja in svoje upanje položil v Egipt zaradi bojnih vozov in konjenikov?
Utawezaje kumzuia hata afisa mmoja aliye mdogo kati ya maafisa wa bwana wangu, ijapo unategemea Misri kwa magari ya vita na wapanda farasi?
10 Sem mar sedaj brez Gospoda prišel gor zoper to deželo, da jo uničim? Gospod mi je rekel: ›Pojdi gor zoper to deželo in jo uniči.‹«
Zaidi ya hayo, je, nimekuja kushambulia na kuangamiza nchi hii bila Bwana? Bwana mwenyewe ndiye aliniambia niishambulie nchi hii na kuiangamiza.’”
11 Nato so Eljakím, Šebná in Joáh rekli Rabšakéju: »Govori, prosimo te, svojim služabnikom v sirskem jeziku, kajti razumemo ga in ne govori nam v judovskem jeziku v ušesa ljudstva, ki je na obzidju.«
Ndipo Eliakimu, Shebna na Yoa wakamwambia yule jemadari wa jeshi, “Tafadhali zungumza na watumishi wako kwa lugha ya Kiaramu, kwa kuwa tunaifahamu. Usiseme nasi kwa Kiebrania watu walioko juu ya ukuta wakiwa wanasikia.”
12 Toda Rabšaké je rekel: »Me je mar moj gospodar poslal k tvojemu gospodarju in k tebi, da ti govorim te besede? Mar me ni poslal k možem, ki sedijo na obzidju, da bodo lahko jedli svoj lastni iztrebek in z vami pili svoj lastni seč?«
Lakini yule jemadari wa jeshi akajibu, “Je, bwana wangu amenituma kutoa ujumbe huu kwa bwana wenu na kwenu tu? Je, hakunituma pia kwa watu walioketi ukutani, ambao, kama ninyi, itawabidi kula mavi yao na kunywa mikojo yao wenyewe?”
13 Potem se je Rabšaké ustopil in z močnim glasom zaklical v judovskem jeziku in rekel: »Poslušajte besede velikega kralja, asirskega kralja.
Kisha yule jemadari wa jeshi akasimama na kuita kwa lugha ya Kiebrania, akasema: “Sikieni maneno ya mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru!
14 Tako govori kralj: ›Ne dopustite, da vas Ezekíja zavede, kajti ne bo vas mogel osvoboditi.
Hili ndilo asemalo mfalme: Msikubali Hezekia awadanganye. Hawezi kuwaokoa!
15 Niti naj vas Ezekíja ne primora zaupati v Gospoda, rekoč: › Gospod nas bo zagotovo osvobodil, to mesto ne bo izročeno v roko asirskega kralja.‹
Msikubali Hezekia awashawishi kumtumaini Bwana kwa kuwaambia, ‘Hakika Bwana atatuokoa. Mji huu hautaangukia mikononi mwa mfalme wa Ashuru.’
16 Ne prisluhnite Ezekíju, kajti tako govori kralj Asirije: › Z darilom sklenite dogovor z menoj in pridite ven k meni in jejte vsak od svoje trte in vsak od svojega figovega drevesa in pijte vode, vsak iz svojega lastnega vodnega zbiralnika,
“Msimsikilize Hezekia. Hili ndilo mfalme wa Ashuru asemalo: Fanyeni amani nami na mje kwangu. Kisha kila mmoja wenu atakula kutoka kwa mzabibu wake na mtini wake mwenyewe, na kunywa maji kutoka kisima chake mwenyewe,
17 dokler ne pridem in vas ne vzamem proč v deželo, podobno vaši lastni deželi, deželo žita in vina, deželo kruha in vinogradov.
mpaka nije nikawapeleke katika nchi iliyo kama nchi yenu wenyewe, nchi ya nafaka na divai mpya, nchi ya mkate na ya mashamba ya mizabibu.
18 Pazite, da vas Ezekíja ne prepriča, rekoč: › Gospod nas bo osvobodil.‹ Mar je katerikoli izmed bogov narodov svojo deželo osvobodil iz roke asirskega kralja?
“Msikubali Hezekia awapotoshe asemapo, ‘Bwana atatuokoa.’ Je, yuko mungu wa taifa lolote aliyewahi kuokoa nchi yake kutoka mkononi mwa mfalme wa Ashuru?
19 Kje so bogovi Hamáta in Arpáda? Kje so bogovi Sefarvájima? Mar so le-ti Samarijo osvobodili iz moje roke?
Iko wapi miungu ya Hamathi na ya Arpadi? Iko wapi miungu ya Sefarvaimu? Je, imeokoa Samaria kutoka mkononi mwangu?
20 Kdo so tisti izmed vseh bogov teh dežel, ki so svojo deželo osvobodili iz moje roke, da bi Gospod Jeruzalem osvobodil iz moje roke?«
Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya nchi hizi ameweza kuokoa nchi yake mkononi mwangu? Inawezekanaje basi Bwana aiokoe Yerusalemu mkononi mwangu?”
21 Toda molčali so in mu niso odgovorili niti besede, kajti kraljeva zapoved je bila, rekoč: »Ne odgovarjajte mu.«
Lakini wale watu wakakaa kimya, wala hawakujibu lolote, kwa kuwa mfalme alikuwa amewaamuru, “Msimjibu lolote.”
22 Potem so prišli Hilkijájev sin Eljakím, ki je bil nad družino, pisar Šebná in Asáfov sin Joáh, letopisec, k Ezekíju s svojimi pretrganimi oblačili in mu povedali Rabšakéjeve besede.
Kisha Eliakimu mwana wa Hilkia msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna katibu, na Yoa mwana wa Asafu, mwandishi wakamwendea Hezekia, nguo zao zikiwa zimeraruliwa, na kumwambia yale jemadari wa jeshi aliyoyasema.