< Izaija 34 >

1 Pridite bliže, vi narodi, da slišite in prisluhnite ve ljudstva. Naj zemlja sliši in vsi, ki so na njej, zemeljski [krog] in vse stvari, ki pridejo iz njega.
Njooni karibu, enyi mataifa, nanyi msikilize; sikilizeni kwa makini, enyi kabila za watu! Dunia na isikie, navyo vyote vilivyo ndani yake, ulimwengu na vyote vitokavyo ndani yake!
2 Kajti ogorčenje od Gospoda je nad vsemi narodi in njegova razjarjenost nad vsemi njihovimi vojskami. Popolnoma jih je uničil, izročil jih je v klanje.
Bwana ameyakasirikia mataifa yote; ghadhabu yake ni juu ya majeshi yao yote. Atawaangamiza kabisa, atawatia mikononi mwa wachinjaji.
3 Tudi njihovi umorjeni bodo vrženi ven in njihov smrad bo prišel iz njihovih trupel in gore bodo stopljene z njihovo krvjo.
Waliouawa watatupwa nje, maiti zao zitatoa uvundo, milima itatota kwa damu zao.
4 Vse vojske neba bodo razpadle in nebo bo zvito skupaj kakor zvitek pergamenta. Vse njihove vojske bodo padle, kakor list pade s trte in kakor figa pade iz figovega drevesa.
Nyota zote za mbinguni zitayeyuka na anga litasokotwa kama kitabu, jeshi lote la angani litaanguka kama majani yaliyonyauka kutoka kwenye mzabibu, kama tini iliyonyauka kutoka kwenye mtini.
5 Kajti moj meč bo potešen na nebu. Glejte, ta bo prišel dol nad Edóm in nad ljudstvo mojega prekletstva, k sodbi.
Upanga wangu umekunywa na kushiba huko mbinguni, tazama, unashuka katika hukumu juu ya Edomu, wale watu ambao nimeshawahukumu, kuwaangamiza kabisa.
6 Gospodov meč je poln krvi, zamaščen s tolščo in s krvjo jagnjet in koz, s tolščo ledvic ovnov, kajti Gospod ima klavno daritev v Bocri in velik pokol v edómski deželi.
Upanga wa Bwana umeoga katika damu, umefunikwa na mafuta ya nyama: damu ya kondoo na mbuzi, mafuta kutoka figo za kondoo dume. Kwa maana Bwana ana dhabihu huko Bosra, na machinjo makuu huko Edomu.
7 Samorogi bodo z njimi prišli dol in bikci z biki in njihova dežela bo namočena s krvjo in njihov prah zamaščen z mastnostjo.
Nyati wataanguka pamoja nao, ndama waume na mafahali wakubwa. Nchi yao italowana kwa damu, nayo mavumbi yataloa mafuta ya nyama.
8 Kajti to je dan Gospodovega maščevanja in leto povračil zaradi Sionove pravde.
Kwa sababu Bwana anayo siku ya kulipiza kisasi, mwaka wa malipo, siku ya kushindania shauri la Sayuni.
9 Njegovi vodotoki bodo spremenjeni v smolo, njegov prah v žveplo in njegova dežela bo postala goreča smola.
Vijito vya Edomu vitageuka kuwa lami, mavumbi yake yatakuwa kiberiti kiunguzacho, nchi yake itakuwa lami iwakayo!
10 Ta ne bo pogašena ne ponoči ne podnevi; njen dim se bo dvigoval na veke. Od roda do roda bo ležala opustošena; nihče ne bo šel skoznjo na veke vekov.
Haitazimishwa usiku wala mchana, moshi wake utapaa juu milele. Kutoka kizazi hadi kizazi itakuwa ukiwa, hakuna mtu yeyote atakayepita huko tena.
11 Toda kormoran in bobnarica jo bosta vzela v last; tudi sova in krokar bosta v njej prebivala. Nadnjo bo razširil vrvico zmede in kamne praznine.
Bundi wa jangwani na bundi mwenye sauti nyembamba wataimiliki, bundi wakubwa na kunguru wataweka viota humo. Mungu atanyoosha juu ya Edomu kamba ya kupimia ya machafuko matupu, na timazi ya ukiwa.
12 Njene plemenite bodo poklicali h kraljestvu, toda tam ne bo nikogar in vsi njeni princi bodo nič.
Watu wake wa kuheshimiwa hawatakuwa na chochote kitakachoitwa ufalme huko, nao wakuu wao wote watatoweka.
13 Trnje bo pognalo v njenih palačah, koprive in trnovo grmovje v njenih trdnjavah, in ta bo prebivališče zmajem in dvor za sove.
Miiba itaenea katika ngome za ndani, viwawi na michongoma itaota kwenye ngome zake. Itakuwa maskani ya mbweha, makao ya bundi.
14 Divje živali iz puščave se bodo prav tako srečale z divjimi živalmi z otoka in kozjenog bo klical svojemu tovarišu; tudi skovir bo tam počival in zase našel mesto počitka.
Viumbe vya jangwani vitakutana na fisi, nao mbuzi-mwitu watalia wakiitana; huko viumbe vya usiku vitastarehe pia na kujitafutia mahali pa kupumzika.
15 Tam si bo velika sova naredila svoje gnezdo, polegla, izvalila in [jih] zbrala pod svojo senco. Tam bodo zbrani tudi jastrebi, vsak s svojo družico.
Bundi wataweka viota huko na kutaga mayai, atayaangua na kutunza makinda yake chini ya uvuli wa mabawa yake; pia huko vipanga watakusanyika, kila mmoja na mwenzi wake.
16 Poiščite si iz Gospodove knjige in berite. Nobeden izmed teh ne bo manjkal, nobeden ne bo pogrešal svoje družice, kajti moja usta so to zapovedala in njegov duh jih je zbral.
Angalieni katika gombo la Bwana na msome: Hakuna hata mmoja katika hawa atakayekosekana, hakuna hata mmoja atakayemkosa mwenzi wake. Kwa kuwa ni kinywa chake Mungu kimeagiza, na Roho wake atawakusanya pamoja.
17 Zanje je vrgel žreb in njegova roka jim je to razdelila po vrvici. Vzeli jo bodo v last na veke, od roda do roda bodo prebivali v njej.
Huwagawia sehemu zao, mkono wake huwagawanyia kwa kipimo. Wataimiliki hata milele na kuishi humo kutoka kizazi hadi kizazi.

< Izaija 34 >