< 1 Mojzes 5 >
1 To je knjiga Adamovih rodov. Na dan, ko je Bog ustvaril človeka, ga je naredil po Božji podobnosti.
Hii ni orodha iliyoandikwa ya vizazi vya Adamu. Wakati Mungu alipomuumba Adamu, alimfanya kwa sura ya Mungu.
2 Moškega in žensko ju je ustvaril in ju blagoslovil in njuno ime imenoval Adam, na dan, ko sta bila ustvarjena.
Aliwaumba mwanaume na mwanamke, akawabariki. Walipokwisha kuumbwa, akawaita “mwanadamu.”
3 Adam je živel sto trideset let in zaplodil sina po svoji lastni podobnosti, po svoji podobi in imenoval ga je Set.
Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, alikuwa na mwana aliyekuwa na sura yake, mwenye kufanana naye. Akamwita Sethi.
4 Adamovih dni, potem ko je zaplodil Seta, je bilo osemsto let, in zaplodil je sinove in hčere.
Baada ya Sethi kuzaliwa, Adamu aliishi miaka 800, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
5 Vseh dni, ko je Adam živel, je bilo devetsto trideset let, in je umrl.
Adamu aliishi jumla ya miaka 930, ndipo akafa.
6 Set je živel sto pet let ter zaplodil Enóša.
Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.
7 Potem ko je Set zaplodil Enóša, je živel osemsto sedem let ter zaplodil sinove in hčere,
Baada ya kumzaa Enoshi, Sethi aliishi miaka 807, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
8 in vseh Setovih dni je bilo devetsto dvanajst let, in je umrl.
Sethi aliishi jumla ya miaka 912, ndipo akafa.
9 Enóš je živel devetdeset let in zaplodil Kenána,
Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
10 in potem, ko je Enóš zaplodil Kenána, je živel osemsto petnajst let ter zaplodil sinove in hčere.
Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815, naye alikuwa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
11 Vseh Enóševih dni je bilo devetsto pet let, in je umrl.
Enoshi aliishi jumla ya miaka 905, ndipo akafa.
12 Kenán je živel sedemdeset let ter zaplodil Mahalaléla.
Kenani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
13 Potem ko je Kenán zaplodil Mahalaléla, je živel osemsto štirideset let ter zaplodil sinove in hčere.
Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
14 Vseh Kenánovih dni je bilo devetsto deset let, in je umrl.
Kenani aliishi jumla ya miaka 910, ndipo akafa.
15 Mahalalél je živel petinšestdeset let ter zaplodil Jereda.
Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Yaredi.
16 Potem ko je Mahalalél zaplodil Jereda, je živel osemsto trideset let ter zaplodil sinove in hčere.
Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
17 Vseh Mahalalélovih dni je bilo osemsto petindevetdeset let, in je umrl.
Mahalaleli aliishi jumla ya miaka 895, ndipo akafa.
18 Jered je živel sto dvainšestdeset let ter zaplodil Henoha.
Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, akamzaa Enoki.
19 Potem ko je Jered zaplodil Henoha, je živel osemsto let ter zaplodil sinove in hčere.
Baada ya kumzaa Enoki, Yaredi aliishi miaka 800, naye akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
20 Vseh Jeredovih dni je bilo devetsto dvainšestdeset let, in je umrl.
Yaredi aliishi jumla ya miaka 962, ndipo akafa.
21 Henoh je živel petinšestdeset let ter zaplodil Matuzalema.
Enoki alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela.
22 Potem ko je Henoh zaplodil Matuzalema, je tristo let hodil z Bogom ter zaplodil sinove in hčere.
Baada ya kumzaa Methusela, Enoki alitembea na Mungu miaka 300, na akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
23 Vseh Henohovih dni je bilo tristo petinšestdeset let.
Enoki aliishi jumla ya miaka 365.
24 Henoh je hodil z Bogom in ni ga bilo, kajti Bog ga je vzel.
Enoki akatembea na Mungu, kisha akatoweka, kwa sababu Mungu alimchukua.
25 Matuzalem je živel sto sedeminosemdeset let in zaplodil Lameha.
Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, akamzaa Lameki.
26 Potem ko je Matuzalem zaplodil Lameha, je živel sedemsto dvainosemdeset let ter zaplodil sinove in hčere.
Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
27 Vseh Matuzalemovih dni je bilo devetsto devetinšestdeset let, in je umrl.
Methusela aliishi jumla ya miaka 969, ndipo akafa.
28 Lameh je živel sto dvainosemdeset let ter zaplodil sina.
Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana.
29 Njegovo ime je imenoval Noe, rekoč: »Ta isti nas bo tolažil, glede našega dela in garanja naših rok, zaradi tal, ki jih je Gospod preklel.«
Akamwita jina lake Noa, akasema, “Yeye ndiye atakayetufariji katika kazi na maumivu makali ya mikono yetu yaliyosababishwa na ardhi iliyolaaniwa na Bwana.”
30 Potem ko je Lameh zaplodil Noeta, je živel petsto petindevetdeset let ter zaplodil sinove in hčere.
Baada ya Noa kuzaliwa, Lameki aliishi miaka 595, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
31 Vseh Lamehovih dni je bilo sedemsto sedeminsedemdeset let, in je umrl.
Lameki aliishi jumla ya miaka 777, ndipo akafa.
32 Noe je bil star petsto let in Noe je zaplodil Sema, Hama ter Jafeta.
Baada ya Noa kuishi miaka 500, aliwazaa Shemu, Hamu na Yafethi.