< Ezekiel 32 >
1 In pripetilo se je v dvanajstem letu, v dvanajstem mesecu, na prvi dan meseca, da je prišla k meni Gospodova beseda, rekoč:
Kisha ikawa katika mwezi wa kumi na mbili wa mwaka wa kumi na mbili, siku ya kwanza ya mwezi, lile neno la Yahwe likanijia, kusema,
2 »Človeški sin, vzdigni žalostinko za faraonom, egiptovskim kraljem in mu reci: ›Podoben si mlademu levu izmed narodov in ti si kakor kit v morjih in prihajaš naprej s svojimi rekami in s svojimi stopali burkaš vode in usmrajuješ njihove reke.‹
“Mwanadamu, inua maombolezo kuhusu Farao mfalme wa Misri; mwambie, 'Wewe ni kama simba mdogo juu ya mataifa, lakini kama jitu la kutisha, unatoka kwenye maji, unayachafua maji kwa miguu yako na kuyachafua maji yao.
3 Tako govori Gospod Bog: ›Zato bom nad teboj razprostrl svojo mrežo s spremstvom mnogih ljudstev; in privedli te bodo gor v mojo mrežo.
Bwana Yahwe asema hivi: Basi nitautandaza wavu wangu juu yako katika kusanyiko la watu wengi, na watawainua juu katika wavu wangu.
4 Potem te bom pustil na deželi, vrgel te bom naprej na odprto polje in vsej perjadi neba bom povzročil, da ostanejo na tebi in s teboj bom nasitil živali celotne zemlje.
Nitakuacha katika nchi. Nitakutupa kwenye shamba na kufanya ndege wote wa angani watue juu yako; njaa ya wanyama wote waishio juu ya nchi watashibishwa na wewe.
5 In tvoje meso bom položil na gore in s tvojo višino napolnil doline.
Kwa kuwa nitaiweka nyama yako juu ya milima, na nitayajaza mabonde kwa funza wako waliokufa.
6 Tudi s tvojo krvjo bom namočil deželo, v kateri plavaš, celó do gora; in reke te bodo polne.
Kisha nitamwaga damu yako juu ya milima, na vitanda vya kijito vitajazwa kwa damu yako.
7 Ko te bom ugasnil, bom pokril nebo in zatemnil zvezde; sonce bom pokril z oblakom in luna ne bo dajala svoje svetlobe.
Kisha wakati nitakapokuzimisha, nitazifunika mbingu na kuzitia giza nyota zake; nitalifunika jua kwa mawingu, na mwezi hautatoa nuru yake usiku.
8 Vse svetle luči neba nad teboj bom otemnil in postavil temo nad tvojo deželo, ‹ govori Gospod Bog.
Mianga ya mbinguni nitaiweka giza juu yako, na nitaweka giza juu ya nchi-hivi ndivyo asemavyo Bwana Yahwe.
9 Prav tako bom dražil srca mnogih ljudi, ko bom med narode privedel tvoje uničenje, v dežele, ki jih nisi poznal.
Hivyo nitaitisha mioyo ya watu wengi katika nchi ambao huwajui, wakati nitakapoleta kuhusu uvunjifu miongoni mwa mataifa, miongoni mwa nchi ambazo hukuzijua.
10 Da, naredil bom, da bodo mnoga ljudstva osupla nad teboj in njihovi kralji bodo strašno prestrašeni zaradi tebe, ko bom pred njimi vihtel svoj meč; in trepetali bodo ob vsakem trenutku, vsak človek za svoje lastno življenje, na dan tvojega padca.‹
Nitawashangaza watu wengi kuhusiana na wewe; wafalme wao watatetemeka kwa hofu kuhusiana na wewe nitakapoutikisa upanga wangu mbele yao. Kila wakati kila mmoja atatetemeka kwa sababu yako, katika siku ya kuanguka kwako.
11 Kajti tako govori Gospod Bog: ›Meč babilonskega kralja bo prišel nadte.
Kwa kuwa Bwana Yahwe asema hivi: Upanga wa mfalme wa Babeli utakuja juu yako.
12 Z meči mogočnega bom tvoji množici povzročil, da pade, strašni izmed narodov, vsi izmed njih, in oplenili bodo pomp Egipta in vsa njegova množica bo uničena.
Nitawafanya watu wako kuanguka kwa panga za mashujaa-kila shujaa ni tishio la mataifa. Hawa mashujaa watateketeza kiburi cha Misri na kuangamiza watu wake wote.
13 Prav tako bom uničil tudi vse njegove živali, ki so poleg velikih vodá. Niti jih ne bo več vznemirjalo človeško stopalo niti jih ne bodo vznemirjala kopita živine.
Kwa kuwa nitaiharibu mifugo yote kutoka karibu na maji mengi; na mguu wa mtu hautayatibua tena, wala kwato za wanyama hazitayatibua.
14 Potem bom njihove vode naredil globoke in njihovim rekam povzročil, da tečejo kakor olje, ‹ govori Gospod Bog.
Kisha nitayafanya maji yao kuwa matulivu na kufanya mito yao kukimbia kama mafuta-hivi ndivyo asemavyo Bwana Yahwe.
15 ›Ko bom egiptovsko deželo naredil zapuščeno in bo dežela oropana tega, česar je bila polna, ko bom udaril vse tiste, ki prebivajo tam, takrat bodo vedeli, da jaz sem Gospod.
Wakati nitakapoifanya nchi ya Misri sehemu iliyojitenga, wakati nchi iliyopungukiwa na vitu viijazavyo, wakati nitakapo washambulia wakaao ndani yake, watajua yakwamba mimi ni Yahwe.
16 To je žalostinka, s katero ga bodo objokovali. Hčere narodov ga bodo objokovale. Žalovali bodo za njim, celó za Egiptom in za vso njegovo množico, ‹ govori Gospod Bog.‹«
Kutakuwa na maombolezo; binti za mataifa wataomboleza juu yake; wataomboleza juu ya Misri, juu ya watu wake wote wataomboleza-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”'
17 In prav tako se je pripetilo v dvanajstem letu, na petnajsti dan meseca, da je k meni prišla Gospodova beseda, rekoč:
Kisha ikawa katika mwaka wa kumi na mbili, siku ya kumi na tano ya mwezi, lile neno la Yahwe likanijia, kusema,
18 »Človeški sin, tarnaj za egiptovsko množico in vrzi jo dol, celó njo in hčere slavnih narodov, v spodnje dele zemlje, s tistimi, ki gredo dol v jamo.
“Mwanadamu, omboleza kwa ajili watu wa misri na walete chini-yeye na binti za mataifa mashuhuri-hata chini ya dunia pamoja na wale walioshuka chini kwenye shimo.
19 Koga prekašaš v lepoti? Pojdi dol in bodi položen z neobrezanimi.
'Je! wewe ni mzuri zaidi kuliko mtu mwingine yeyote? Nenda chini na lala chini pamoja na wasiotahiriwa.'
20 Padli bodo v sredo tistih, ki so umorjeni z mečem. Izročen je meču. Potegni njega in vse njegove množice.
Wataanguka miongoni mwao waliokuwa wameuawa kwa upanga. Upanga ulikuwa umewekwa! Alikuwa amepatiwa upanga; watamkamata na watu wake.
21 Močni izmed mogočnih mu bodo govorili iz srede pekla s tistimi, ki mu pomagajo. Odšli so dol, ležijo neobrezani, umorjeni z mečem. (Sheol )
Hodari wa wapiganaji katika Sheoli atasema kuhusu Misri na rafiki zake, 'Wameshuka chini hapa! Watalala pamoja na wasiotahiriwa, pamoja na wale waliokuwa wameuawa kwa upanga.' (Sheol )
22 Tam je Asúr in vse njegovo spremstvo. Njegovi grobovi so okoli njega, vsi izmed njih umorjeni, padli pod mečem,
Ashuru yupo huko pamoja na kusanyiko lake. Makaburi yake yamemzunguka; wote waliuawa kwa upanga.
23 katerih grobovi so postavljeni ob straneh jame in njegovo spremstvo je naokoli njegovega groba; vsi izmed njih umorjeni, padli pod mečem, ki so povzročili strahoto v deželi živih.
Wale ambao makaburi yao yamewekwa katika maficho ya mashimo yaliyo huko, pamoja na kusanyiko lake. Makaburi yake yakiwazunguka wote waliokuwa wameuawa, walioanguka kwa upanga, wale walioleta hofu juu ya nchi ya walio hai.
24 Tam je Elám in vsa njegova množica naokoli njegovega groba, vsi izmed njih umorjeni, padli pod mečem, ki so neobrezani odšli dol, v spodnje dele zemlje, ki so povzročili njihovo strahoto v deželi živih; vendar so nosili svojo sramoto s tistimi, ki gredo dol v jamo.
Elamu yupo huko pamoja na watu wake wote. Makaburi yake yamemzunguka; wote walikuwa wameuawa. Wale walioawa kwa upanga, walioshuka chini wasiotahiriwa hata sehemu ya chini kabisa ya dunia, waliowatia hofu juu ya nchi ya walio hai na wale waliobeba aibu yao wenyewe, pamoja na wale washukao chini kwenye shimo.
25 Pripravili so mu posteljo v sredi umorjenih, z vso njegovo množico. Njegovi grobovi so okoli njega; vsi izmed njih neobrezani, umorjeni z mečem. Čeprav je bila njihova strahota storjena v deželi živih, so vendar nosili svojo sramoto s tistimi, ki gredo dol v jamo. Položen je v sredo tistih, ki so umorjeni.
Wamemuwekea kitanda kwa ajili ya Elamu na watu wake wote kati ya wachinjaji; kaburi lake limemzunguka. Wote hawajatahiriwa, kukatwa vipande kwa upanga, kwa sababu waliwaleta mashujaa wao juu ya nchi ya walio hai. Hivyo wamechukua aibu yao wenyewe, pamoja na wale washukao kwenye shimo miongoni mwa wote waliouawa, wale washukao kwenda shimoni. Elamu yu miongoni mwa wale waliokuwa wameuawa.
26 Tam je Mešeh, Tubál in vsa njegova množica. Njegovi grobovi so okoli njega; vsi izmed njih neobrezani, umorjeni z mečem, četudi so svojo strahoto povzročali v deželi živih.
Mesheki, Tubali, na watu wake wote wako huko! Makaburi yao yamewazunguka. Wote hawajatahiriwa, wameuawa kwa upanga, kwa sababu walileta utiisho wao juu ya nchi ya walio hai.
27 Ne bodo ležali z mogočnimi, ki so padli od neobrezancev, ki so odšli dol k peklu z njihovimi bojnimi orožji. Njihove meče so položili pod njihove glave, toda njihove krivičnosti bodo na njihovih kosteh, čeprav so bili strahota mogočnih v deželi živih. (Sheol )
Wasilale pamoja mashujaa walioanguka wa wasiotahiriwa walioshuka chini kwa Sheoli pamoja na silaha zao zote za vita, na pamoja na panga zao zote walizoziweka chini ya vichwa vyao na maovu yao juu ya mifupa yao. Kwa kuwa walikuwa tishio kwa mashujaa katika nchi ya walio hai. (Sheol )
28 Da, zlomljen boš v sredi neobrezancev in ležal boš s tistimi, ki so umorjeni z mečem.
Basi wewe, Misri, utavunjika kati yao wasiotahiriwa! Utalala karibu nao waliokuwa wamekatwa vipande vipande kwa upanga.
29 Tam je Edóm, njegovi kralji in vsi njegovi princi, ki so s svojo močjo položeni od tistih, ki so bili umorjeni z mečem. Ležali bodo z neobrezanimi in s tistimi, ki gredo dol v jamo.
Edomu yuko huko na wafalme na viongozi wake wote. Walikuwa wamehifadhiwa katika uwezo wao pamoja na wale walioawa kwa upanga. Pamoja na wasiotahiriwa wamelala, pamoja na wale walioshuka kwenye shimo.
30 Tam bodo princi iz severa, vsi izmed njih in vsi Sidónci, ki so odšli dol z umorjenimi; s svojo strahoto se sramujejo svoje moči; in ležijo neobrezani, s tistimi, ki so umorjeni z mečem in svojo sramoto nosijo s tistimi, ki gredo dol v jamo.
Wakuu wa kaskazini wako huko-wote na Wasidoni wote walioshuka chini pamoja na hao waliokuwa wamekatwa vipande vipande. Walikuwa na nguvu na kuwafanya wengine kuogopa, lakini sasa wako huko kwa aibu, wasiotahiriwa pamoja na wale waliokatwa vipande vipande kwa upanga. Wamebeba aibu yao wenyewe, pamoja nao waendao kwenye shimo.
31 Faraon jih bo videl in potolažen bo nad vso svojo množico, celó faraon in vsa njegova vojska, umorjena z mečem, ‹ govori Gospod Bog.
Farao ataona na kupata faraja kuhusu kundi lake waliokatwa vipande vipande kwa upanga -Farao na jeshi lake lote-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
32 ›Kajti povzročil sem svojo strahoto v deželi živih in položen bo v sredo neobrezancev, s tistimi, ki so umorjeni z mečem, celó faraon in vsa njegova množica, ‹ govori Gospod Bog.‹«
Natamuweka kama utiisho wangu katika nchi ya walio hai, lakini atakuwa amelazwa chini katikati yao wasiotahiriwa, miongoni mwa wale walio katwa vipande kwa upanga, Farao na makundi yake yote-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.