< Ezekiel 14 >

1 Potem so prišli k meni nekateri izmed Izraelovih starešin in se usedli pred menoj.
Baadhi ya wazee wa Israeli walinijia na kuketi mbele yangu.
2 In k meni je prišla Gospodova beseda, rekoč:
Ndipo neno la Bwana likanijia kusema:
3 »Človeški sin, ti možje so si v srcih postavljali malike in so si pred svoj obraz postavljali kamen spotike svoje krivičnosti; ali naj bi me oni potem sploh spraševali?«
“Mwanadamu, watu hawa wameweka sanamu katika mioyo yao na kuweka vitu viovu vya kukwaza mbele ya macho yao. Je, kweli niwaruhusu waniulize jambo lolote?
4 Zato jim govori in jim povej: »Tako govori Gospod Bog: ›Vsak mož iz Izraelove hiše, ki si v svojem srcu postavlja malike in pred svoj obraz polaga kamen spotike svoje krivičnosti in prihaja k preroku; jaz, Gospod, bom odgovoril tistemu, ki prihaja, glede na množico njegovih malikov,
Kwa hiyo sema nao uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Wakati Mwisraeli yeyote anapoweka sanamu moyoni mwake na kuweka kitu kiovu cha kukwaza mbele ya macho yake na kisha akaenda kwa nabii, Mimi Bwana nitamjibu peke yangu sawasawa na ukubwa wa ibada yake ya sanamu.
5 da bi Izraelovo hišo lahko ujel v njihovem lastnem srcu, ker so se zaradi svojih malikov vsi odtujili od mene.‹
Nitafanya jambo hili ili kukamata tena mioyo ya watu wa Israeli, ambao wote wameniacha kwa ajili ya sanamu zao.’
6 Zato reci Izraelovi hiši: ›Tako govori Gospod Bog: ›Pokesajte se in odvrnite se od svojih malikov; odvrnite svoje obraze od vseh svojih ogabnosti.‹
“Kwa hiyo iambie nyumba ya Israeli, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Tubuni! Geukeni kutoka kwenye sanamu zenu na mkatae matendo yenu yote ya machukizo!
7 Kajti vsakomur izmed Izraelove hiše, ali izmed tujca, ki začasno biva v Izraelu, ki se ločuje od mene in si v svojem srcu postavlja svoje malike in polaga kamen spotike svoje krivičnosti pred svoj obraz in prihaja k preroku, da bi od njega povprašal glede mene, mu bom jaz, Gospod, sam odgovoril.
“‘Mwisraeli yeyote au mgeni yeyote anayeishi katika Israeli anapojitenga nami na kujiwekea sanamu katika moyo wake na kwa hivyo kuweka kitu kiovu cha kukwaza mbele ya macho yake na kisha akamwendea nabii kuuliza shauri kwangu, mimi Bwana nitamjibu mwenyewe.
8 Svoj obraz bom naravnal zoper tega moža in naredil ga bom za znamenje in pregovor in odrezal ga bom iz srede svojega ljudstva; in spoznali boste, da jaz sem Gospod.
Nitaukaza uso wangu dhidi ya mtu huyo na kumwadhibu na kumfanya ishara kwa watu. Nitamkatilia mbali kutoka watu wangu. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
9 Če pa je prerok zaveden, ko je govoril besedo, sem jaz, Gospod, zavedel tega preroka in jaz bom iztegnil svojo roko nanj in ga uničim iz srede svojega ljudstva Izraela.
“‘Naye nabii kama atakuwa ameshawishika kutoa unabii, Mimi Bwana nitakuwa nimemshawishi nabii huyo, nami nitaunyoosha mkono wangu dhidi yake na kumwangamiza kutoka miongoni mwa watu wangu Israeli.
10 Nosila bosta kazen svoje krivičnosti. Kazen preroka bo celo kakor kazen tistega, ki poizveduje k njemu;
Watachukua hatia yao, nabii atakuwa na hatia sawa na yule mtu aliyekuja kuuliza neno kwake.
11 da Izraelova hiša ne bo več zašla od mene niti ne bo več oskrunjena z vsemi svojimi prestopki; temveč da bodo lahko moje ljudstvo in bom jaz lahko njihov Bog, govori Gospod Bog.‹«
“‘Ndipo watu wa Israeli hawataniacha tena, wala kujitia unajisi tena kwa dhambi zao zote. Ndipo watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao, asema Bwana Mwenyezi.’”
12 Gospodova beseda je prišla ponovno k meni, rekoč:
Neno la Bwana likanijia kusema,
13 »Človeški sin, kadar dežela greši zoper mene z mučnimi prekršitvami, takrat bom nadnjo iztegnil svojo roko in zlomil bom njeno oporo kruha in nadnjo bom poslal lakoto in iz nje bom iztrebil človeka in žival.
“Mwanadamu, kama nchi itanitenda dhambi kwa kutokuwa waaminifu nami nikinyoosha mkono wangu dhidi yake kukatilia mbali upatikanaji wake wa chakula na kuipelekea njaa na kuua watu wake na wanyama wao,
14 Čeprav bi bili v njej ti trije možje: Noe, Daniel in Job, bi s svojo pravičnostjo rešili zgolj svoje lastne duše, ‹ govori Gospod Bog.
hata kama watu hawa watatu: Noa, Danieli na Ayubu wangekuwa ndani ya nchi hiyo, ndio hao tu wangeweza kujiokoa wenyewe kwa uadilifu wao, asema Bwana Mwenyezi.
15 ›Če povzročim ogabnim živalim, da gredo skozi deželo, jo oplenijo tako, da je ta zapuščena, da zaradi živali noben človek ne bo mogel iti skoznjo;
“Au kama nikipeleka wanyama pori katika nchi hiyo yote na kuifanya isiwe na watoto, nayo ikawa ukiwa kwamba hakuna mtu apitaye katika nchi hiyo kwa sababu ya wanyama pori,
16 čeprav bi bili ti trije možje v njej, kakor jaz živim, ‹ govori Gospod Bog, ›ne bodo osvobodili niti sinov niti hčera; samo oni sami bodo osvobojeni, toda dežela bo zapuščena.
hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hata kama watu hawa watatu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kuokoa wana wao wala binti zao. Wao peke yao wangeokolewa, lakini nchi ingekuwa ukiwa.
17 Ali če privedem meč nad to deželo in rečem: ›Meč, pojdi skozi to deželo; ‹ tako, da iz nje iztrebim ljudi in živali;
“Au kama nikileta upanga dhidi ya nchi hiyo na kusema, ‘Upanga na upite katika nchi yote,’ nami nikiua watu wake na wanyama wao,
18 čeprav bi bili ti trije možje v njej, kakor jaz živim, ‹ govori Gospod Bog, ›ne bi osvobodili niti sinov niti hčera; samo oni sami bi bili osvobojeni.
hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hata kama watu hawa watatu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kuokoa wana wao wala binti zao. Wao wenyewe tu wangeokolewa.
19 Ali če pošljem v to deželo kužno bolezen in če nanjo v krvi izlijem svojo razjarjenost, da iztrebim iz nje človeka in žival;
“Au kama nikipeleka tauni katika nchi hiyo na kumwaga ghadhabu yangu juu yake kwa njia ya kumwaga damu, kuua watu wake na wanyama wao,
20 čeprav bi bili v njej Noe, Daniel in Job, kakor jaz živim, ‹ govori Gospod Bog, ›ne bi osvobodili niti sinov niti hčera, temveč bodo po svoji pravičnosti osvobodili zgolj svoje lastne duše.‹
hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hata kama Noa, Danieli na Ayubu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kumwokoa mwana wala binti. Wao wangeweza kujiokoa wenyewe tu kwa uadilifu wao.
21 Kajti tako govori Gospod Bog: ›Koliko bolj, ko pošljem svoje štiri boleče sodbe nad Jeruzalem: meč, lakoto in ogabno zver in kužno bolezen, da iztrebim iz nje ljudi in živali?
“Kwa maana hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Itakuwa vibaya kiasi gani nitakapopeleka dhidi ya Yerusalemu hukumu zangu nne za kutisha, yaani, upanga, njaa, wanyama pori na tauni, ili kuua watu wake na wanyama wao!
22 In vendar, glejte, bo tam ostal ostanek, ki bo izpeljan, tako sinov kakor hčera. Glejte, prišli bodo k vam in videli boste njihovo pot in njihova dejanja in potolaženi boste glede zla, ki sem ga privedel nad Jeruzalem, celó glede vsega, kar sem privedel nadenj.
Lakini watakuwepo wenye kuokoka, wana na binti wataletwa kutoka nje ya nchi hiyo. Watawajia ninyi, nanyi mtakapoona mwenendo wao na matendo yao, mtafarijika kuhusu maafa niliyoleta juu ya Yerusalemu, kwa ajili ya yale yote niliyoleta juu yake.
23 In potolažili vas bodo, ko boste videli njihove poti in njihova dejanja, in spoznali boste, da nisem brez vzroka storil vsega, kar sem storil v njem, ‹ govori Gospod Bog.‹«
Mtafarijika wakati mtakapoona mwenendo wao na matendo yao, kwa kuwa mtajua kwamba sikufanya lolote ndani yake bila sababu, asema Bwana Mwenyezi.”

< Ezekiel 14 >