< 2 Mojzes 23 >
1 Ne boš dvignil napačnega poročila. Svoje roke ne podaj z zlobnim, da bi bil nepravična priča.
“Usieneze habari za uongo. Usimsaidie mtu mwovu kwa kuwa shahidi mwenye nia ya kudhuru wengine.
2 Ne boš sledil množici, da počneš zlo. Niti ne boš govoril v zadevi, da se ne nagneš za mnogimi, ki pačijo sodbo.
“Usifuate umati wa watu katika kutenda mabaya. Unapotoa ushahidi kwenye mashtaka, usipotoshe haki ukijumuika na umati wa watu,
3 Niti ne boš podpiral reveža v njegovi zadevi.
nawe usimpendelee mtu maskini katika mashtaka yake.
4 Če srečaš vola svojega sovražnika ali njegovega osla zaiti, mu ga boš zagotovo ponovno privedel nazaj k njemu.
“Kama ukikutana na maksai au punda wa adui yako anapotea, hakikisha umemrudisha kwake.
5 Če vidiš osla tistega, ki te sovraži, ležati pod svojim bremenom in odlašaš, da mu pomagaš, mu boš zagotovo z njim vred pomagal.
Ukiona punda wa mtu anayekuchukia ameanguka na mzigo wake, usimwache hapo alipoangukia; hakikisha kuwa umemsaidia.
6 Ne boš pačil sodbe ubogega v njegovi zadevi.
“Usiwanyime haki watu wako walio maskini katika mashtaka yao.
7 Drži se proč od napačne stvari. Nedolžnega in pravičnega ne ubij, kajti zlobnega ne bom opravičil.
Ujiepushe na mashtaka ya uongo, wala usimuue mtu asiye na hatia au mtu mwaminifu, kwa maana sitamhesabia hana hatia yeye aliye na hatia.
8 In ti ne boš prejel nobenega daru, kajti dar slepi modrega in izkrivlja besede pravičnega.
“Usipokee rushwa, kwa kuwa rushwa hupofusha wale waonao, na kupinda maneno ya wenye haki.
9 Tudi ne boš zatiral tujca, kajti poznate srce tujca, glede na to, da ste bili tujci v egiptovski deželi.
“Usimwonee mgeni; ninyi wenyewe mnajua jinsi mgeni anavyojisikia, kwa sababu mlikuwa wageni Misri.
10 Šest let boš sejal svojo zemljo in zbiral njene sadove,
“Kwa muda wa miaka sita mtapanda mashamba yenu na kuvuna mazao,
11 toda sedmo leto jo boš pustil počivati in mirno ležati, da ubogi izmed tvojega ljudstva lahko jedo. Kar bodo pustili, naj pojedo živali polja. Na podoben način boš postopal s svojim vinogradom in s svojim oljčnim nasadom.
lakini katika mwaka wa saba usiilime ardhi wala kuitumia, ili watu walio maskini miongoni mwenu waweze kupata chakula kutoka kwenye hayo mashamba, nao wanyama pori wapate chakula kwa yale mabaki watakayobakiza. Utafanya hivyo katika shamba lako la mizabibu na la mizeituni.
12 Šest dni boš opravljal svoje delo, na sedmi dan pa boš počival, da bosta tvoj vol in tvoj osel lahko počivala in bosta sin tvoje pomočnice in tujec lahko osvežena.
“Kwa siku sita fanya kazi zako, lakini siku ya saba usifanye kazi, ili maksai wako na punda wako wapate kupumzika, naye mtumwa aliyezaliwa nyumbani mwako, pamoja na mgeni, wapate kustarehe.
13 V vseh stvareh, ki sem ti jih rekel, bodi preudaren. In ne omenjaj imena drugih bogov niti naj tega ne bo slišati iz tvojih ust.
“Uzingatie kutenda kila kitu nilichokuambia. Usiombe kwa majina ya miungu mingine, wala usiyaruhusu kusikika kinywani mwako.
14 Trikrat v letu mi boš ohranjal praznovanje.
“Mara tatu kwa mwaka utanifanyia sikukuu.
15 Ohranjal boš praznik nekvašenega kruha (sedem dni boš jedel nekvašeni kruh, kakor sem ti zapovedal, v določenem času meseca abíba, kajti v njem si prišel iz Egipta in nihče se pred menoj ne bo prikazal prazen)
“Utaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu; kwa siku saba utakula mikate isiyotiwa chachu kama nilivyokuagiza. Fanya jambo hili kwa wakati uliopangwa katika mwezi wa Abibu, ndio mwezi wa nne, kwa sababu katika mwezi huo ulitoka Misri. “Mtu yeyote asije mbele yangu mikono mitupu.
16 in praznik žetve, prve sadove svojih trudov, ki si jih posejal na polju in praznik spravljanja, ki je ob koncu leta, ko si svoje trude pospravil s polja.
“Utaadhimisha Sikukuu ya Mavuno kwa malimbuko ya mazao yako uliyopanda katika shamba lako. “Utaadhimisha Sikukuu ya Kukusanya mavuno mwishoni mwa mwaka, unapokusanya mavuno yako toka shambani.
17 Trikrat na leto naj se vsi tvoji možje prikažejo pred Gospodom Bogom.
“Mara tatu kwa mwaka wanaume wote watakuja mbele za Bwana Mwenyezi.
18 Krvi moje klavne daritve ne boš žrtvoval z vzhajanim kruhom niti naj maščoba mojega darovanja ne ostane do jutra.
“Msitoe damu ya dhabihu kwangu pamoja na kitu chochote kilicho na chachu. “Mafuta ya mnyama wa sadaka ya sikukuu yangu yasibakizwe mpaka asubuhi.
19 Prvine od prvih sadov svoje zemlje boš prinesel v hišo Gospoda, svojega Boga. Kozlička ne boš zavrel v mleku njegove matere.
“Utaleta malimbuko bora ya ardhi yako katika nyumba ya Bwana Mungu wako. “Usimchemshe mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.
20 Glej, pred teboj pošiljam Angela, da te varuje na poti in te privede na kraj, ki sem ga pripravil.
“Tazama, ninamtuma malaika akutangulie mbele yako akulinde njiani na kukuleta mpaka mahali nilipoandaa.
21 Pazi se ga in ubogaj njegov glas, ne izzivaj ga, kajti ne bo oprostil tvojih prestopkov, kajti moje ime je v njem.
Mtamtii na kusikiliza kile anachokisema. Usiasi dhidi yake; hatakusamehe uasi wako, kwa maana Jina langu limo ndani yake.
22 Toda če boš zares ubogal njegov glas in storil vse, kar ti govorim, potem bom sovražnik tvojih sovražnikov in nasprotnik tvojih nasprotnikov.
Kama ukitii kweli kweli kile asemacho na kufanya yote nisemayo, nitakuwa adui wa adui zako, na nitawapinga wale wakupingao.
23 Kajti moj Angel bo šel pred teboj in te privede k Amoréjcem, Hetejcem, Perizéjcem, Kánaancem, Hivéjcem in Jebusejcem, in jaz jih bom odrezal.
Malaika wangu atatangulia mbele yako na kukuleta katika nchi ya Waamori, Wahiti, Waperizi, Wakanaani, Wahivi na Wayebusi, nami nitawafutilia mbali.
24 Ne boš se priklanjal njihovim bogovom niti jim služil niti počel po njihovih delih, temveč jih boš popolnoma premagal in popolnoma zlomil njihove podobe.
Usiisujudie miungu yao, au kuiabudu, wala kufuata desturi yao. Utayabomoa kabisa na kuvunjavunja mawe yao ya ibada vipande vipande.
25 Služili boste Gospodu, svojemu Bogu in on bo blagoslovil tvoj kruh in tvojo vodo, in iz tvoje srede bom odvzel bolezen.
Utamwabudu Bwana Mungu wako, na baraka zake zitakuwa juu ya vyakula vyako na maji yako. Nami nitaondoa maradhi miongoni mwako,
26 V tvoji deželi nič ne bo zavrglo svojih mladih niti ne bo jalovo. Število tvojih dni bom izpolnil.
na hakuna atakayeharibu mimba wala atakayekuwa tasa katika nchi yako. Nami nitakupa maisha makamilifu.
27 Pred teboj bom poslal svoj strah in uničil bom vsa ljudstva, h katerim boš prišel in vsem tvojim sovražnikom bom storil, da svoje hrbte obrnejo k tebi.
“Nitapeleka utisho wangu mbele yako na kufadhaisha kila taifa utakalolifikia. Nitafanya adui zako wote wakupe kisogo na kukimbia.
28 Pred teboj bom poslal sršene, ki bodo izpred tebe napodili Hivéjce, Kánaance in Hetejce.
Nitatanguliza manyigu mbele yako kuwafukuza Wahivi, Wakanaani na Wahiti waondoke njiani mwako.
29 Izpred tebe jih ne bom pognal v enem letu, da ne bi zemlja postala zapuščena in bi se zoper tebe namnožile poljske zveri.
Lakini sitawafukuza kwa mara moja, kwa sababu nchi itabaki ukiwa na wanyama pori watakuwa wengi mno kwako.
30 Po malo in malo jih bom podil izpred tebe, dokler ne boš narasel in podedoval dežele.
Nitawafukuza kidogo kidogo mbele yako, mpaka uwe umeongezeka kiasi cha kutosha kuimiliki nchi.
31 Tvoje meje bom postavil od Rdečega morja, celo do morja Filistejcev in od puščave do reke, kajti jaz bom prebivalce dežele izročil v tvojo roko, ti pa jih boš pognal pred seboj.
“Nitaweka mipaka ya nchi yako kuanzia Bahari ya Shamu hadi Bahari ya Wafilisti, na kuanzia jangwani hadi Mto Frati. Nitawatia watu wanaoishi katika nchi hizo mikononi mwako, nawe utawafukuza watoke mbele yako.
32 Z njimi ne boš sklenil nobene zaveze niti z njihovimi bogovi.
Usifanye agano lolote nao wala na miungu yao.
33 Naj ne prebivajo v tvoji deželi, da te ne bi pripravili grešiti zoper mene, kajti če boš služil njihovim bogovom, ti bodo le-ti zagotovo zanka.«
Usiwaache waishi katika nchi yako, la sivyo watakusababisha utende dhambi dhidi yangu, kwa sababu ibada ya miungu yao hakika itakuwa mtego kwako.”