< Estera 1 >

1 Pripetilo se je torej v dneh kralja Ahasvérja (to je Ahasvérja, ki je kraljeval od Indije celo do Etiopije, nad sto sedemindvajsetimi provincami),
Hili ndilo lililotokea wakati wa utawala wa Mfalme Ahasuero, yule aliyetawala juu ya majimbo mia na ishirini na saba tangu Bara Hindi hadi Kushi.
2 da je v tistih dneh, ko je Kralj Ahasvér sedel na prestolu svojega kraljestva, ki je bilo v palači Suze,
Wakati huo Mfalme Ahasuero alitawala katika kiti chake cha enzi katika ngome ya mji wa Shushani.
3 v tretjem letu njegovega kraljevanja, priredil gostijo vsem svojim princem in svojim služabnikom; moči Perzije in Medije, plemičem in princem provinc, ki so bili pred njim,
Katika mwaka wa tatu wa utawala wake, alifanya karamu kwa ajili ya wakuu wake wote pamoja na maafisa. Akawaalika viongozi wa jeshi wa Uajemi na Umedi, wana wa wafalme na wakuu wa majimbo.
4 ko jim je mnogo dni kazal bogastva svojega veličastnega kraljestva in čast svojega odličnega veličanstva, celó sto osemdeset dni.
Kwa siku zote 180 mfalme alionyesha utajiri mwingi wa ufalme wake, fahari na utukufu wa enzi yake.
5 Ko so ti dnevi minili, je kralj priredil gostijo vsemu ljudstvu, ki je bilo prisotno v palači Suze, tako velikim kakor malim, sedem dni na dvoru vrta kraljeve palače,
Siku hizo zilipopita, mfalme alifanya karamu kwa muda wa siku saba, katika bustani ya ndani katika jumba la kifalme, kwa ajili ya watu wote kuanzia mdogo hadi mkubwa, waliokuwa katika ngome ya mji wa Shushani.
6 kjer so bile bele, zelene in modre tanke preproge, pritrjene z vrvicami iz tankega lanenega platna in vijolične, k srebrnim obročem in stebrom iz marmorja. Postelje so bile iz zlata in srebra, na tlaku iz rdečega, modrega, belega in črnega marmorja.
Bustani ilikuwa na mapazia ya kitani nyeupe na buluu, yaliyofungiwa kamba za kitani nyeupe na kitambaa cha zambarau, kwenye pete za fedha juu ya nguzo za marmar. Kulikuwepo viti vya dhahabu na vya fedha vilivyokuwa vimewekwa kwenye ile sakafu iliyotengenezwa kwa mawe ya rangi, marmar, lulumizi na mawe mengine ya thamani.
7 Dajali so jim piti iz zlatih posod (posode so bile različne ena od druge) in kraljevega vina v obilju, glede na kraljevo razkošje.
Vyombo vya dhahabu vilitumika kwa watu kunywea mvinyo, kila kimoja tofauti na kingine, naye mfalme akatoa mvinyo kwa wingi kwa kadiri ya ukarimu wake.
8 Pitje je bilo glede na postavo. Nihče ni silil, kajti tako je kralj določil vsem častnikom njegove hiše, da naj storijo glede na užitek vsakega človeka.
Kwa amri ya mfalme kila mgeni aliruhusiwa kunywa alichotaka, kwa kuwa mfalme alitoa maagizo kwa watumishi wote wa kuhudumu mvinyo kumhudumia kila mtu kwa jinsi alivyotaka.
9 Prav tako je kraljica Vaští pripravila gostijo za ženske v kraljevi hiši, ki je pripadala Kralju Ahasvérju.
Malkia Vashti pia akawafanyia wanawake karamu katika jumba la kifalme la Mfalme Ahasuero.
10 Na sedmi dan, ko je bilo kraljevo srce veselo od vina, je ukazal Mehumánu, Bizetáju, Harbonáju, Bigtáju, Abagtáju, Zetárju in Karkásu, sedmim glavnim dvornim upraviteljem, ki so služili v prisotnosti Kralja Ahasvérja,
Siku ya saba, wakati Mfalme Ahasuero alikuwa amesisimka roho yake kwa mvinyo, aliamuru matowashi saba waliokuwa wakimhudumia, yaani, Mehumani, Biztha, Harbona, Bigtha, Abagtha, Zethari na Karkasi,
11 da privedejo kraljico Vaští s kraljevo krono pred kralja, da ljudstvu in princem pokaže njeno lepoto, kajti bila je lepa na pogled.
kumleta Malkia Vashti mbele ya mfalme akiwa amevaa taji lake la kifalme, ili aonyeshe uzuri wake kwa watu na wakuu, kwa kuwa alikuwa ni mzuri wa kupendeza.
12 Toda kraljica Vaští je odklonila, da pride na kraljevo zapoved po njegovih glavnih dvornih upraviteljih. Zato je bil kralj zelo ogorčen in njegova jeza je gorela v njem.
Lakini wakati watumishi walipotoa amri ya mfalme, Malkia Vashti alikataa kuja. Ndipo mfalme alighadhibika, na hasira yake ikawaka.
13 Potem je kralj rekel modrim možem, ki so poznali čase (Kajti tak je bil kraljev običaj do vseh teh, ki so poznali postavo in sodbo
Kwa kuwa ilikuwa desturi ya mfalme kupata ushauri kwa wataalamu katika mambo ya sheria na haki, alizungumza na watu wenye busara, ambao walijua nyakati,
14 in takoj poleg njega so bili Karšenáj, Šetár, Admát, Taršíš, Meres, Marsenáj in Memuhán, sedem princev iz Perzije in Medije, ki so videli kraljevo obličje in ki so prvi sedeli v kraljestvu.)
nao waliokuwa karibu na mfalme ni Karshena, Shethari, Admatha, Tarshishi, Meresi, Marsena na Memukani, wakuu saba wa Uajemi na Umedi waliokuwa na nafasi ya pekee kwa mfalme nao walikuwa na vyeo vya juu kabisa katika utawala wake.
15 »Kaj naj storimo kraljici Vaští, glede na postavo, ker po glavnih dvornih upraviteljih ni izpolnila zapovedi Kralja Ahasvérja?«
Mfalme akauliza, “Kulingana na sheria, Malkia Vashti anapaswa kutendewa nini? Malkia hakutii amri ya Mfalme Ahasuero ambayo matowashi walimpelekea.”
16 Memuhán je pred kraljem in princi odgovoril: »Kraljica Vaští ni storila narobe samo kralju, temveč tudi vsem princem in vsemu ljudstvu, ki so po vseh provincah Kralja Ahasvérja.
Kisha Memukani akajibu mbele ya mfalme na wakuu, “Malkia Vashti si kwamba amemkosea mfalme tu bali pia amewakosea wakuu wote na watu wa himaya yote ya Mfalme Ahasuero.
17 Kajti to dejanje kraljice bo prišlo povsod do vseh žensk, tako da bodo v svojih očeh prezirale svoje soproge, ko bo to sporočeno: ›Kralj Ahasvér je zapovedal kraljici Vaští, da bi bila privedena predenj, toda ni prišla.‹
Kwa maana tendo hili la malkia litajulikana kwa wanawake wote, kwa hiyo watawadharau waume zao na kusema, ‘Mfalme Ahasuero aliagiza Malkia Vashti aletwe mbele yake, lakini alikataa.’
18 Podobno bodo gospe iz Perzije in Medije, ki so slišale o kraljičinem dejanju, ta dan rekle vsem kraljevim princem. Tako bo vstalo preveč zaničevanja in besa.
Leo hii wanawake wa wakuu wa Uajemi na Umedi ambao wamesikia juu ya tabia ya malkia watawatendea wakuu wote wa mfalme vivyo hivyo. Hapatakuwepo na mwisho wa dharau na magomvi.
19 Če to ugaja kralju, naj gre od njega kraljeva zapoved in naj bo ta zapisana med postave Perzijcev in Medijcev, da ta ne bo predrugačena: ›Da Vaští ne pride več pred Kralja Ahasvérja. Kralj pa naj njen kraljevi stan izroči drugi, ki je boljša kakor ona.‹
“Kwa hiyo, kama itampendeza mfalme, atoe amri ya kifalme na iandikwe katika sheria ya Uajemi na Umedi, ambayo haitabadilika, kwamba Vashti kamwe asije tena mbele ya Mfalme Ahasuero. Pia mfalme na atoe hiyo nafasi yake ya umalkia kwa mwanamke mwingine aliye bora kumliko yeye.
20 Ko bo kraljevi odlok, ki ga bo izdal, razglašen po vsem njegovem kraljestvu (kajti to je veliko), bodo vse žene dale svojim soprogom spoštovanje, tako malim, kakor velikim.«
Kisha mbiu hii ya mfalme itakapotangazwa katika himaya yake iliyo kubwa sana, wanawake wote watawaheshimu waume zao, kuanzia mdogo hadi mkubwa.”
21 Govor je ugajal kralju in princem in kralj je storil glede na Memuhánovo besedo.
Mfalme na wakuu wake walipendezwa na shauri hili, hivyo basi mfalme akafanya kama Memukani alivyopendekeza.
22 Kajti poslal je pisma v vse kraljeve province, v vsako provinco glede na njeno pisavo in vsakemu ljudstvu glede na njihov jezik, da bi vsak mož vladal v svoji lastni hiši in da bi bilo to razglašeno glede na jezik vsakega ljudstva.
Alipeleka barua katika sehemu zote za ufalme wake, kwa kila jimbo kwa maandishi yake mwenyewe na kwa kila watu katika lugha yao wenyewe, akitangaza kwa msemo wa kila watu kwamba inampasa kila mwanaume kuwa mtawala wa nyumba yake mwenyewe.

< Estera 1 >