< Daniel 8 >

1 V tretjem letu kraljevanja kralja Belšacárja se mi je prikazalo videnje, celo meni, Danielu, po tistem, ki se mi je prikazalo najprej.
Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Mfalme Belshaza, mimi Danieli, nilipata maono, baada ya maono ambayo yalikuwa yamenitokea mbeleni.
2 Videl sem v videnju in pripetilo se je, ko sem gledal, da sem bil v [mestu] Suze, v palači, ki je v provinci Elám, in videl sem v videnju in bil sem pri reki Uláj.
Katika maono yangu, nilijiona nikiwa ndani ya ngome ya Shushani katika jimbo la Elamu. Katika maono nilikuwa kando ya Mto Ulai.
3 Potem sem povzdignil svoje oči, videl in glej, tam pred reko je stal oven, ki je imel dva rogova in dva rogova sta bila visoka. Toda eden je bil višji kakor drug in višji je prišel zadnji.
Nikatazama juu, na hapo mbele yangu kulikuwa na kondoo dume mwenye pembe mbili, akiwa amesimama kando ya mto, nazo pembe zake zilikuwa ndefu. Pembe moja ilikuwa ndefu kuliko hiyo nyingine, lakini iliendelea kukua baadaye.
4 Videl sem ovna bosti proti zahodu in proti severu in proti jugu, tako, da noben zvernik ni mogel stati pred njim niti tam ni bilo nikogar, ki bi ga lahko osvobodil iz njegove roke, temveč je počel glede na svojo voljo in postal velik.
Nikamtazama yule kondoo dume alivyokuwa akishambulia kuelekea magharibi, kaskazini na kusini. Hakuna mnyama yeyote aliyeweza kusimama dhidi yake, wala hakuna aliyeweza kuokoa kutoka nguvu zake. Alifanya kama atakavyo, naye akawa mkuu.
5 Ko sem preudarjal, glej, je od zahoda prišel kozel na obličje celotne zemlje, tal pa se ni dotaknil, in kozel je imel med svojimi očmi opazen rog.
Nilipokuwa ninatafakari hili, ghafula beberu mwenye pembe moja kubwa sana katikati ya macho yake alikuja kutoka magharibi, akiruka kasi juu ya dunia yote bila kugusa ardhi.
6 Ta je prišel k ovnu, ki je imel dva rogova, ki sem ga videl stati pred reko in stekel k njemu v razjarjenosti svoje moči.
Alikuja akimwelekea yule kondoo dume mwenye pembe mbili niliyemwona akisimama kando ya mto, akamshambulia kwa hasira nyingi.
7 Videl sem ga približevati se ovnu in prevzet je bil z gnevom zoper njega in udaril ovna ter zlomil dva njegova rogova. V ovnu pa ni bilo moči, da stoji pred njim, temveč ga je vrgel dol k tlom in ga poteptal, in nikogar ni bilo, ki bi mogel ovna osvoboditi iz njegove roke.
Nikamwona akimshambulia yule kondoo dume kwa hasira nyingi, akimpiga yule kondoo dume na kuvunja pembe zake mbili. Yule kondoo dume hakuwa na nguvu za kumzuia yule beberu, hivyo akamwangusha yule kondoo dume chini na kumkanyaga, wala hakuna aliyeweza kumwokoa yule kondoo dume kutoka nguvu za huyo beberu.
8 Zato je kozel postal zelo velik, in ko je bil močan, je bil veliki rog zlomljen in za tem so prišli gor štirje opazni, [razdeljeni] proti štirim vetrovom neba.
Yule beberu akawa mkubwa sana, lakini katika kilele cha nguvu zake ile pembe yake ndefu ilivunjika, na mahali pake pakaota pembe nne kubwa kuelekea pande nne za dunia.
9 Iz enega izmed njih je prišel majhen rog, ki je postal silno velik, proti jugu in proti vzhodu in proti prijetni deželi.
Kutoka mojawapo ya zile pembe nne palitokea pembe ndogo ukaongezeka nguvu kuelekea kusini, na kuelekea mashariki, na kuelekea Nchi ya Kupendeza.
10 Ta je postal velik, celó do nebeške vojske, in ta je vrgel dol nekatere izmed vojske in od zvezd k tlom in poteptal nad njimi.
Pembe hiyo ikaendelea kukua hadi kufikia jeshi la mbinguni, nayo ikalitupa baadhi ya jeshi la vitu vya angani hapa chini duniani, na kulikanyaga.
11 Da, poveličeval je samega sebe, celo do princa vojske in z njim je bilo odvzeto dnevno žrtvovanje in prostor njegovega svetišča je bil vržen dol.
Pembe hiyo ikajikweza ili iwe kama Mkuu wa hilo jeshi; ikamwondolea dhabihu ya kila siku, napo mahali pake patakatifu pakashushwa chini.
12 In dana mu je bila vojska zoper dnevno žrtvovanje zaradi razloga prestopka in ta je vrgel resnico dol k tlom in to izvedel in uspel.
Kwa sababu ya uasi, jeshi la watakatifu na dhabihu za kila siku vikatiwa mikononi mwake. Ikafanikiwa katika kila kitu ilichofanya, nayo kweli ikatupwa chini.
13 Potem sem zaslišal nekega svetega govoriti in drugi sveti je rekel temu nekemu svetemu, ki je govoril: »Doklej bo videnje glede dnevnega žrtvovanja in prestopka zapuščenosti, da bosta tako svetišče kakor vojska pogažena pod stopalom?«
Kisha nikamsikia mtakatifu mmoja akizungumza na mtakatifu mwingine, akamwambia, “Je, itachukua muda gani maono haya yatimie: maono kuhusu dhabihu ya kila siku, uasi unaosababisha ukiwa, kutwaliwa kwa mahali patakatifu, na jeshi litakalokanyagwa chini ya nyayo?”
14 Rekel mi je: »Do dva tisoč tristo dni, potem bo svetišče očiščeno.«
Akaniambia, “Itachukua siku 2,300. Ndipo mahali patakatifu patawekwa wakfu tena.”
15 Pripetilo se je, ko sem jaz, celó jaz, Daniel, videl videnje in si prizadeval najti pomen, potem, glej, je tam pred menoj stal kakor videz moža.
Mimi Danieli nilipokuwa ninaangalia maono na kujaribu kuelewa, mbele yangu alisimama mmoja aliyefanana na mwanadamu.
16 Zaslišal sem človeški glas med bregovoma Ulája, ki je zaklical in rekel: »Gabriel, stôri temu človeku, da razume videnje.«
Kisha nikasikia sauti ya mwanadamu kutoka Mto Ulai ikiita, “Gabrieli, mwambie mtu huyu maana ya maono haya.”
17 Tako se je približal, kjer sem stal. Ko je prišel, sem bil prestrašen in padel na svoj obraz, toda rekel mi je: »Razumi, oh človeški sin, kajti videnje bo ob času konca.«
Alipokuwa akikaribia pale nilipokuwa nimesimama, niliogopa, nikaanguka kifudifudi. Akaniambia, “Mwana wa mwanadamu, fahamu kuwa maono haya yanahusu siku za mwisho.”
18 Torej, ko je govoril z menoj, sem bil v globokem spanju, s svojim obrazom proti tlom, toda dotaknil se me je in me postavil pokonci.
Alipokuwa akinena nami, nilikuwa katika usingizi mzito, huku nimelala kifudifudi. Ndipo aliponigusa na kunisimamisha wima.
19 Rekel je: »Glej, dal ti bom spoznati kaj bo v zadnjem koncu ogorčenja, kajti ob določenem času bo konec.
Akaniambia, “Nitakuambia yale yatakayotokea baadaye wakati wa ghadhabu, kwa sababu maono haya yanahusu wakati wa mwisho ulioamriwa.
20 Oven, ki si ga videl, ki je imel dva rogova, sta kraljestvi Medije in Perzije.
Kondoo dume mwenye pembe mbili ambaye ulimwona anawakilisha wafalme wa Umedi na Uajemi.
21 Razmršen kozel je kralj Grčije, in velik rog, ki je med njegovimi očmi, je prvi kralj.
Yule beberu mwenye nywele nyingi ni mfalme wa Uyunani, nayo ile pembe ndefu katikati ya macho yake ni mfalme wa kwanza.
22 Torej ta je bil zlomljen, medtem ko so štirje vstali namesto tega; štiri kraljestva bodo vstala iz naroda, toda ne v njegovi moči.
Zile pembe nne zilizoota badala ya ile pembe iliyovunjika zinawakilisha falme nne ambazo zitatokea kutoka taifa lake, lakini hakuna hata mmoja utakaokuwa na nguvu kama ule uliovunjika.
23 V zadnjem času njihovega kraljestva, ko pridejo prestopniki v polni meri, bo vstal kralj krutega obličja in razumevanja temnih razsodb.
“Katika sehemu ya mwisho ya utawala wao, wakati waasi watakapokuwa waovu kabisa, atainuka mfalme mwenye uso mkali, aliye stadi wa hila.
24 Njegova moč bo mogočna, toda ne z njegovo lastno močjo. Ta bo izvrstno uničeval in uspeval bo in izvedel in uničil bo mogočnega in sveto ljudstvo.
Atakuwa na nguvu nyingi, lakini si kwa uwezo wake mwenyewe. Atasababisha uharibifu wa kutisha, na atafanikiwa kwa chochote anachofanya. Atawaangamiza watu maarufu na watu watakatifu.
25 Zaradi svoje strategije bo tudi povzročil, da bo prebrisanost uspevala v njegovi roki, in poveličeval se bo v svojem srcu in z mirom bo uničil mnoge. Stal bo tudi zoper Princa princev, toda zlomljen bo brez roke.
Atasababisha udanganyifu ustawi, naye atajihesabu mwenyewe kuwa bora. Wakati wajisikiapo kuwa wako salama, atawaangamiza wengi, na kushindana na Mkuu wa wakuu. Lakini ataangamizwa, isipokuwa si kwa uwezo wa mwanadamu.
26 Videnje večera in jutra, ki je bilo povedano, je resnično. Zato zastri videnje, kajti to bo za mnoge dni.
“Maono kuhusu jioni na asubuhi ambayo umepewa ni kweli, lakini yatie muhuri maono haya, kwa maana yanahusu wakati mrefu ujao.”
27 Jaz, Daniel, sem bil nekaj dni slaboten in bolan. Potem sem se dvignil in opravljal kraljeva opravila, bil pa sem osupel nad videnjem, toda nihče ga ni razumel.
Mimi Danieli nilikuwa nimechoka sana, na nikalala nikiwa mgonjwa kwa siku kadhaa. Ndipo nikaamka, nikaenda kwenye shughuli za mfalme. Nilifadhaishwa na maono hayo, nami sikuweza kuyaelewa.

< Daniel 8 >