< Daniel 6 >
1 Dareju je ugajalo, da postavi nad kraljestvo sto dvajset princev, ki naj bi bili nad celotnim kraljestvom,
Ilimpendeza Dario kuchagua juu ya ufalme magavana wa majimbo 120 ambao wangetawala juu ya ufalme wote.
2 in nad temi tri predstojnike, od katerih je bil Daniel prvi, da bi jim princi lahko dajali obračun in kralj ne bi trpel nobene škode.
Juu yao kulikuwa na watawala wakuu watatu, na Daniel alikuwa mmoja wao. Hawa watawala waliwekwa ili waweze kuwasimamia magavana wa majimbo, ili kwamba mfalme asipate hasara.
3 Potem je bil ta Daniel povišan nad predstojnike in prince, ker je bil v njem odličen duh, in kralj ga je mislil postaviti nad celotno območje.
Danieli alipambanuliwa juu ya watawala wakuu na juu ya magavana wa majimbo kwasababu alikuwa na roho isiyo ya kawaida. Mfalme alikuwa akipanga kumweka juu ya ufalme wote.
4 Potem so predstojniki in princi iskali, da najdejo povod zoper Daniela glede kraljestva, toda niso mogli najti nobenega povoda niti krivde, ker je bil zvest niti ni bilo na njem najti nobene napake ali krivde.
Basi watawala wakuu wengine na magavana wa majimbo walitafuta makosa katika kazi ambazo Danieli alizifanya kwa ufalme, lakini hawakuweza kuona ufisadi au kushindwa katika majukumu yake kwasababu alikuwa mwaminifu. Hakuna kosa au uzembe uliopatikana ndani yake.
5 Potem so ti možje rekli: »Nobenega razloga ne bomo našli zoper tega Daniela, razen če zoper njega najdemo to, kar se tiče postave njegovega Boga.«
Kisha watu hawa wakasema, “Hatukuweza kupata sababu yoyote ya kumshitaki huyu Danieli isipokuwa tukitafuta kitu fulani dhidi yake kuhusiana na sheria za Mungu wake.'”
6 Potem so se ti predstojniki in princi zbrali skupaj h kralju in mu rekli takole: »Kralj Darej, živi na veke.
Ndipo watawala hawa na magavana walileta mpango mbele ya mfalme. Walimwambia, “Mfalme Dario, uishi milele!
7 Vsi predstojniki kraljestva, voditelji in princi, svetovalci in poveljniki, smo se skupaj posvetovali, da bi osnovali kraljevo pravilo in da bi naredili trden odlok, da kdorkoli bi prosil prošnjo od kateregakoli Boga ali človeka v tridesetih dneh, razen od tebe, oh kralj, bo vržen v levji brlog.
Watawala wote wakuu wa ufalme, magavana wa mikoa, na magavana wa majimbo, washauri, na magavana wameshauriana kwa pamoja na kuamua kuwa wewe, mfalme, unapaswa kupitisha amri na kuitekeleza, ili kwamba mtu yeyote anayefanya dua kwa mungu yeyote au mtu kwa siku thelathini, isipokuwa wewe mfalme, mtu huyo lazima atupwe katika tundu la simba.
8 Torej, oh kralj, uveljavi odlok in podpiši pisanje, da to ne more biti spremenjeno, glede na postavo Medijcev in Perzijcev, ki se ne predrugači.«
Sasa mfalme, litoe agizo na utie saini nyaraka ili kwamba isije ikabadilika, kama ilivyoelekezwa katika sheria za Wamedi na Waajemi, hivyo haiweze ikabatilishwa.
9 Zatorej je kralj Darej podpisal pisanje in odlok.
Basi, mfalme Dario alitia saini nyaraka kwa kuifanya amri kuwa sheria.
10 Torej ko je Daniel izvedel, da je bilo pisanje podpisano, je odšel v svojo hišo. Pri svojih oknih v svoji sobi, odprtih proti Jeruzalemu, je trikrat na dan pokleknil na svoja kolena in molil ter se zahvaljeval pred svojim Bogom, kot je to delal poprej.
Danieli alipojua kuwa nyaraka imekwisha kusainiwa kuwa sheria, alienda ndani ya nyumba yake (madirisha yake katika chumba cha juu yalikuwa wazi kuelekea Yerusalemu), na alipiga magoti yake, kama alivyokuwa akifanya mara tatu kwa siku, na aliomba na kushukuru mbele ya Mungu wake, kama alivyofanya hapo kabla.
11 Potem so se ti možje zbrali in našli Daniela, kako moli in dela ponižne prošnje pred svojim Bogom.
Kisha watu hawa walikuwa wameunda hila kwa pamoja walimwona Danieli akiomba na kutafuta msaada kutoka kwa Mungu.
12 Potem so prišli blizu in pred kraljem spregovorili glede kraljevega odloka: »Mar nisi podpisal odloka, da katerikoli človek, ki bo prosil prošnjo od kateregakoli Boga ali človeka, znotraj tridesetih dni, razen od tebe, oh kralj, bo vržen v levji brlog?« Kralj je odgovoril in rekel: »Stvar je resnična glede na postavo Medijcev in Perzijcev, ki se ne predrugači.«
Ndipo walipomwendea mfalme na kuongea naye kuhusiana na amri yake: “Je haukuweka amri kwamba mtu yeyote akayefanya maombi kwa mungu mwingine au kwa binadamu ndani ya siku thelathini zijazo, isipokuwa kwako wewe, mfalme, lazima mtu huyo atupwe katika tundu la simba? Mfalme akajibu, “Jambo hili ni la hakika, kama ilivyoelekezwa katika sheria za Wamedi na Waajemi; ambazo haziwezi zikabatilishwa.”
13 Potem so odgovorili in pred kraljem rekli: »Tisti Daniel, ki je od otrok Judovega ujetništva, te ne upošteva, oh kralj niti odloka, ki si ga podpisal, temveč trikrat na dan opravlja svojo prošnjo.«
Kisha wakamjibu mfalme, “Mtu yule Daniel, ambaye ni mmoja wa watu wa mateka kutoka Yuda, hakutii wewe, mfalme wala maagizo yako uliyoyasaini. Yeye humwomba Mungu wake mara tatu kwa siku.”
14 Potem je bil kralj, ko je slišal te besede, sam pri sebi boleče nejevoljen in je svoje srce naravnal na Daniela, da ga osvobodi, in do sončnega zahoda se je trudil, da ga osvobodi.
Mfalme aliposikia haya, alisikitishwa sana, alitumia akili jinsi ya kumwokoa kutoka katika utawala huu. Alisumbuka sana mpaka wakati wa kuzama kwa jua akijaribu kumwokoa Danieli.
15 Potem so se tisti možje zbrali h kralju in kralju rekli: »Vedi, oh kralj, da je postava Medijcev in Perzijcev: ›Da noben odlok niti nobeno pravilo, ki ga je osnoval kralj, ne more biti spremenjeno.‹«
Kisha watu hawa waliokuwa wamepanga njama walikusanyika kwa pamoja na mfalme, na wakamwambia, “Ujue mfalme kwamba ni sheria ya Wamedi na Waajemi kwamba hakuna amri au sanamu ambayo mfalme anaipitisha yaweza kubadilishwa.”
16 Potem je kralj ukazal in privedli so Daniela ter ga vrgli v levji brlog. Kralj je torej spregovoril in Danielu rekel: »Tvoj Bog, ki mu nenehno služiš, on te bo osvobodil.«
Ndipo mfalme alitoa agizo, na walimleta ndani Danieli, na kisha wakamtupa katika tundu la simba. Mfalme akamwambia Danieli, “Mungu wako, ambaye unamtumikia daima, na akuokoe.''
17 Prinesen je bil kamen in položen na odprtino brloga in kralj ga je zapečatil s svojim lastnim pečatom in s pečati svojih gospodov, da se namen glede Daniela ne bi mogel spremeniti.
Jiwe lililetwa katika mlango wa tundu, na mfalme alilitia muhuri wa pete yake mwenyewe na pamoja na muhuri wa wakuu wake ili kwamba chochote kisiweze kubadilishwa kuhusiana na Danieli.
18 Potem je kralj odšel v svojo palačo in noč prebil v postu niti predenj niso bili prineseni glasbeni instrumenti in njegovo spanje je odšlo od njega.
Basi mfalme alienda kwenye ikulu yake na usiku ule alikuwa na mfungo. Hakuna starehe yoyote iliyoletwa mbele yake, nao usingizi ulimkimbia.
19 Potem je kralj zelo zgodaj zjutraj vstal in v naglici odšel k levjemu brlogu.
Kisha katika mapambazuko mfalme aliamka na kwa haraka alienda kwenye tundu la simba.
20 Ko je prišel k brlogu, je z žalostnim glasom zaklical k Danielu, in kralj je spregovoril ter Danielu rekel: »Oh Daniel, služabnik živega Boga, ali te je tvoj Bog, ki mu nenehno služiš, mogel osvoboditi pred levi?«
Na alipokaribia kwenye tundu, alimwita Danieli kwa sauti ya huzuni, akimwambia Danieli, “Danieli, mtumishi wa Mungu aliye hai, je Mungu wako ambaye anamtumkia daima ameweza kukuokoa kutoka katika simba?
21 Potem je Daniel rekel kralju: »Oh kralj, živi na veke.
Ndipo Danieli akamwambia mfalme, “Mfalme, uishi milele!
22 Moj Bog je poslal svojega angela in zaprl levom usta, da me niso poškodovali, ker je bila v meni najdena nedolžnost pred njim in tudi pred teboj, oh kralj, nisem storil nobene škode.«
Mungu wangu amemtuma mjumbe na amevifunga vinywa vya simba, na hazijaweza kunidhuru. Kwa kuwa sikuwa na hatia yoyote mbele yake na pia mbele yako, ewe mfalme, na sijakufanyia jambo lolote la kukudhuru.”
23 Potem je bil kralj zaradi njega silno vesel in zapovedal, da naj Daniela izvlečejo iz brloga. Tako je bil Daniel vzet gor iz brloga in nobena vrsta poškodbe ni bila najdena na njem, ker je veroval v svojega Boga.
Basi mfalme alikuwa na furaha sana. Alitoa agizo kwamba wanatakiwa wamtoe Danieli nje ya tundu. Hivyo Danieli aliondolewa kutoka katika tundu. Hakuna dhara lolote lililoonekana kwake, kwa kuwa alikuwa amemtumainia Mungu wake.
24 In kralj je zapovedal in privedli so tiste može, ki so Daniela obtožili in jih vrgli v levji brlog, njih, njihove otroke in njihove žene. Levi so imeli oblast nad njimi in vse njihove kosti so zlomili na koščke, še preden so prileteli na dno brloga.
Mfalme alitoa agizo, waletwe wale watu waliomshitaki Danieli na kisha akawatupa wao katika tundu la simba - wao, na watoto wao, na wake zao. Kabla hawajafika sakafuni, simba waliwararua na kuvunjavunja mifupa yao vipande vipande.
25 Potem je kralj Darej napisal vsemu ljudstvu, narodom in jezikom, ki prebivajo na vsej zemlji: »Mir naj se vam pomnoži.
Kisha mfalme Dario aliandika ujumbe kwa watu wote, mataifa na lugha ambazo ziliishi katika dunia yote: “Amani na iongezeke kwenu.
26 Naredim odlok: ›Da v vsakem gospostvu mojega kraljestva ljudje trepetajo in se bojijo pred Danielovim Bogom, kajti on je živi Bog in neomajen na veke in njegovo kraljestvo tisto, ki ne bo uničeno in njegovo gospostvo bo celo do konca.
Ninaagiza kwamba katika utawala wote wa ufalme wangu watu watetemeka na kumcha mbele ya Mungu wa Danieli, kwa kuwa ni Mungu aliye hai na huishi milele, na ufalme wake hauwezi kuharibiwa; utawala wake utakuwepo hadi mwisho.
27 On osvobaja in rešuje, dela [preroška] znamenja in čudeže v nebesih in na zemlji, ki je Daniela osvobodil pred oblastjo levov.‹«
Yeye anatuhifadhi salama na kutuokoa, na anafanya ishara na maajabu mbinguni na duniani; amemhifadhi Danieli salama dhidi ya uwezo wa simba.”
28 Tako je ta Daniel uspeval v Darejevem kraljevanju in v kraljevanju Perzijca Kira.
Na hivyo basi, Danieli alifanikiwa katika utawala wa Dario na katika utawala wa Koreshi Mwajemi.