< Daniel 3 >
1 Kralj Nebukadnezar je naredil podobo iz zlata, katere višina je bila šestdeset komolcev, njena širina pa šest komolcev. Postavil jo je na ravnini Dura v provinci Babilon.
Mfalme Nebukadneza alitengeneza sanamu ya dhahabu, yenye kimo cha dhiraa sitini, na upana wa dhiraa sita, akaisimamisha kwenye tambarare ya Dura katika jimbo la nchi ya Babeli.
2 Potem je kralj Nebukadnezar poslal, da zbere skupaj prince, voditelje in poveljnike, sodnike, zakladnike, svetovalce, šerife in vse vladarje provinc, da pridejo k posvetitvi podobe, ki jo je postavil kralj Nebukadnezar.
Kisha mfalme akaita wakuu, wasimamizi, watawala, washauri, watunza hazina, waamuzi, mahakimu na maafisa wengine wote wa jimbo kuja kuizindua sanamu ambayo Mfalme Nebukadneza alikuwa ameisimamisha.
3 Potem so bili princi, voditelji in poveljniki, sodniki, zakladniki, svetovalci, šerifi in vsi vladarji provinc zbrani skupaj k posvetitvi podobe, ki jo je postavil kralj Nebukadnezar in stali so pred podobo, ki jo je postavil Nebukadnezar.
Basi wakuu, wasimamizi, watawala, washauri, watunza hazina, waamuzi, mahakimu na maafisa wengine wa jimbo walikusanyika ili kuizindua sanamu ile Mfalme Nebukadneza alikuwa ameisimamisha, nao wakasimama mbele ya hiyo sanamu.
4 Potem je glasnik naglas zavpil: »Vam je to zapovedano, oh ljudstvo, narodi in jeziki,
Ndipo mpiga mbiu akatangaza kwa sauti kubwa, “Enyi watu wa kabila zote, mataifa na watu wa kila lugha, hili ndilo mnaloamriwa kulifanya:
5 da kadar zaslišite zvok kornéta, flavte, harfe, pozavne, plunke, citer in vseh vrst glasbe, padite dol in obožujte zlato podobo, ki jo je postavil kralj Nebukadnezar.
Mara mtakaposikia sauti ya baragumu, filimbi, marimba, zeze, kinubi, zumari na aina zote za sauti za ala za uimbaji, lazima mwanguke chini na kuabudu sanamu ya dhahabu ambayo Mfalme Nebukadneza ameisimamisha.
6 Kdorkoli ne pade dol in ne obožuje, bo isto uro vržen v sredo goreče ognjene talilne peči.«
Mtu yeyote ambaye hataanguka chini na kuiabudu sanamu hiyo, atatupwa saa iyo hiyo ndani ya tanuru iwakayo moto.”
7 Zatorej ob tistem času, ko je vse ljudstvo zaslišalo zvok kornéta, flavte, harfe, pozavne, plunke in vseh vrst glasbe, so vsa ljudstva, narodi in jeziki padli dol in oboževali zlato podobo, ki jo je postavil kralj Nebukadnezar.
Kwa hiyo, mara waliposikia sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, kinanda na aina zote za ala za uimbaji, watu wa kabila zote, mataifa na watu wa kila lugha wakaanguka chini na kuiabudu ile sanamu ya dhahabu ambayo Mfalme Nebukadneza alikuwa ameisimamisha.
8 Zaradi česar so se ob tistem času približali neki Kaldejci in obtožili Jude.
Wakati huo baadhi ya Wakaldayo walijitokeza na kuwashtaki Wayahudi.
9 Spregovorili so in rekli kralju Nebukadnezarju: »Oh kralj, živi na veke.
Wakamwambia Mfalme Nebukadneza, “Ee mfalme, uishi milele!
10 Ti, oh kralj, si izdal odlok, da naj vsak človek, ki bo zaslišal glas kornéta, flavte, harfe, pozavne, plunke in citer in vseh vrst glasbe, pade dol in obožuje zlato podobo.
Ee mfalme, umetoa amri kwamba kila mmoja atakayesikia sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, kinanda, zumari na aina zote za ala za uimbaji lazima aanguke chini na kuiabudu ile sanamu ya dhahabu,
11 Kdorkoli pa ne pade dol in je ne obožuje, ta bo vržen v sredo goreče ognjene talilne peči.
na kwamba yeyote ambaye hataanguka chini na kuiabudu atatupwa saa iyo hiyo ndani ya tanuru iwakayo moto.
12 Tam so nekateri Judje, ki si jih postavil nad zadeve babilonske province: Šadráh, Mešáh in Abéd Negó. Ti možje, oh kralj, te niso upoštevali. Ne služijo tvojim bogovom niti ne obožujejo zlate podobe, ki si jo ti postavil.«
Lakini wako baadhi ya Wayahudi ambao umewaweka juu ya mambo ya jimbo la Babeli: yaani, Shadraki, Meshaki na Abednego, ambao hawakujali wewe, ee mfalme. Hawaitumikii miungu yako wala kuiabudu ile sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha.”
13 Potem je Nebukadnezar v svoji besnosti in razjarjenosti zapovedal, da privedejo Šadráha, Mešáha in Abéd Negója. Potem so te može privedli pred kralja.
Mfalme Nebukadneza, akiwa amekasirika na mwenye ghadhabu kali, akawaita Shadraki, Meshaki na Abednego. Hivyo watu hawa wakaletwa mbele ya mfalme,
14 Nebukadnezar je spregovoril in jim rekel: » Je to res, oh Šadráh, Mešáh in Abéd Negój, [da] ne služite mojim bogovom niti ne obožujete zlate podobe, ki sem jo postavil?
naye Nebukadneza akawauliza, “Je, ni kweli kwamba ninyi Shadraki, Meshaki na Abednego hamuitumikii miungu yangu wala kuiabudu sanamu ya dhahabu niliyoisimamisha?
15 Torej če ste pripravljeni, da kadar zaslišite zvok kornéta, flavte, harfe, pozavne, plunke in citer in vse vrste glasbe, padete dol in obožujete podobo, ki sem jo naredil; dobro. Toda če je ne obožujete, boste isto uro vrženi v sredo goreče ognjene talilne peči, in kdo je tisti Bog, ki vas bo osvobodil iz mojih rok?«
Basi wakati mtakaposikia sauti ya baragumu, filimbi, marimba, zeze, kinubi, zumari na aina zote za ala za uimbaji, kama mtakuwa tayari kusujudu na kuiabudu hiyo sanamu niliyoitengeneza, vyema sana. Lakini kama hamtaiabudu, mtatupwa saa iyo hiyo ndani ya tanuru iwakayo moto. Naye ni mungu yupi atakayeweza kuwaokoa ninyi, kutoka mkono wangu?”
16 Šadráh, Mešáh in Abéd Negó so odgovorili in kralju rekli: »Oh Nebukadnezar, mi nismo zaskrbljeni, da ti odgovorimo v tej zadevi.
Shadraki, Meshaki na Abednego wakamjibu mfalme, “Ee Nebukadneza, hatuhitaji kujitetea mbele zako kuhusu jambo hili.
17 Če bo temu tako, naš Bog, ki mu služimo, nas je zmožen osvoboditi pred gorečo ognjeno talilno pečjo in on nas bo osvobodil iz tvoje roke, oh kralj.
Ikiwa tutatupwa ndani ya tanuru iwakayo moto, Mungu tunayemtumikia anaweza kutuokoa na moto, naye atatuokoa kutoka mkononi mwako, ee mfalme.
18 Toda če ne, bodi to znano tebi, oh kralj, da ne bomo služili tvojim bogovom niti oboževali zlate podobe, ki si jo postavil.«
Lakini hata ikiwa hatatuokoa, ee mfalme, tunataka ufahamu kwamba, hatutaitumikia miungu yako wala kuiabudu sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha.”
19 Potem je bil Nebukadnezar poln razjarjenosti in videz njegovega obličja je bil spremenjen napram Šadráhu, Mešáhu in Abéd Negóju. Zatorej je spregovoril in zapovedal, da naj talilno peč sedemkrat bolj segrejejo, kot je bila običajno segreta.
Ndipo Nebukadneza akawa na ghadhabu kali sana kwa Shadraki, Meshaki na Abednego, nayo nia yake ikabadilika kwao. Akaagiza tanuru ichochewe moto mara saba kuliko kawaida yake
20 Zapovedal je najmočnejšim možem, ki so bili v njegovi vojski, da zvežejo Šadráha, Mešáha in Abéd Negója in da jih vržejo v gorečo ognjeno talilno peč.
na kuwaamuru baadhi ya askari wake wenye nguvu zaidi katika jeshi lake kuwafunga Shadraki, Meshaki na Abednego na kuwatupa ndani ya tanuru iwakayo moto.
21 Potem so bili ti možje zvezani v njihovih plaščih, njihovih hlačah in njihovih klobukih in drugih njihovih oblačilih in vrženi so bili v sredo goreče ognjene talilne peči.
Hivyo watu hawa, walifungwa na kutupwa ndani ya tanuru iwakayo moto wakiwa wamevaa majoho yao, suruali, vilemba na nguo zao nyingine.
22 Torej, ker je bila kraljeva zapoved nujna in talilna peč izjemno vroča, je plamen ognja usmrtil tiste može, ki so vzdignili Šadráha, Mešáha in Abéd Negója.
Amri ya mfalme ilikuwa ya haraka sana na tanuru ilikuwa na moto mkali kiasi kwamba miali ya moto iliwaua wale askari waliowapeleka Shadraki, Meshaki na Abednego.
23 Ti trije možje, Šadráh, Mešáh in Abéd Negó so zvezani padli dol v sredo goreče ognjene talilne peči.
Watu hawa watatu walianguka ndani ya tanuru iwakayo moto wakiwa wamefungwa kwa uthabiti sana.
24 Potem je bil kralj Nebukadnezar osupel, v naglici vstal in spregovoril ter svojim svetovalcem rekel: »Mar nismo v sredo ognja vrgli treh zvezanih mož?« Odgovorili so in rekli kralju: »Resnica, oh kralj.«
Ndipo Mfalme Nebukadneza akashangaa, akainuka kwa haraka na kuwauliza washauri wake, “Je, hawakuwa watu watatu ambao tuliwafunga na kuwatupa ndani ya moto?” Washauri wakajibu, “Hakika, ee mfalme.”
25 Ta je odgovoril in rekel: »Glejte, vidim štiri razvezane može, ki hodijo v sredi ognja in nimajo nobene poškodbe, oblika četrtega pa je podobna Božjemu Sinu.«
Mfalme akasema, “Tazama! Naona watu wanne wakitembeatembea ndani ya moto, hawajafungwa wala kudhurika, naye mtu yule wa nne anaonekana kama mwana wa miungu.”
26 Potem se je Nebukadnezar približal odprtini goreče ognjene talilne peči in spregovoril ter rekel: »Šadráh, Mešáh in Abéd Negó, vi služabniki najvišjega Boga, pojdite ven in pridite sem.« Potem so Šadráh, Mešáh in Abéd Negó prišli naprej iz srede ognja.
Ndipo Nebukadneza akaukaribia mdomo wa ile tanuru iwakayo moto na kupaza sauti, “Shadraki, Meshaki na Abednego, watumishi wa Mungu Aliye Juu Sana, tokeni! Njooni hapa!” Ndipo Shadraki, Meshaki na Abednego wakatoka ndani ya moto.
27 Princi, voditelji, poveljniki in kraljevi svetovalci, ki so bili zbrani skupaj, so videli te može, nad čigar telesi ogenj ni imel nobene oblasti, niti las njihove glave ni bil osmojen, niti njihovi plašči niso bili spremenjeni, niti nanje ni prešel vonj ognja.
Nao maliwali, wasimamizi, watawala na washauri wa mfalme wakakusanyika kuwazunguka. Waliona kwamba moto haukudhuru miili yao, wala unywele wa vichwa vyao haukuungua, majoho yao hayakuungua, wala hapakuwepo na harufu ya moto kwenye miili yao.
28 Potem je Nebukadnezar spregovoril in rekel: »Blagoslovljen bodi Bog Šadráha, Mešáha in Abéd Negója, ki je poslal svojega angela in rešil svoje služabnike, ki so zaupali vanj in spremenili kraljevo besedo in predali svoja telesa, da ne bi služili niti oboževali kateregakoli boga, razen svojega lastnega Boga.
Ndipo Nebukadneza akasema, “Ahimidiwe Mungu wa Shadraki, Meshaki na Abednego, ambaye amemtuma malaika wake na kuwaokoa watumishi wake. Walimtumaini na kukaidi amri ya mfalme, nao wakawa tayari kufa kuliko kutumikia au kuabudu mungu mwingine yeyote isipokuwa Mungu wao.
29 Zato izdajam odlok: ›Da bo vsako ljudstvo, narod in jezik, ki spregovori karkoli neprimernega zoper Boga Šadráha, Mešáha in Abéd Negója, razrezano na koščke in njihove hiše bodo narejene za gnojišče, zato ker ni drugega Boga, ki lahko reši na ta način.‹«
Kwa hiyo ninaamuru kwamba watu wa taifa lolote au lugha yoyote watakaosema kitu chochote dhidi ya Mungu wa Shadraki, Meshaki na Abednego wakatwe vipande vipande na nyumba zao zifanywe kuwa malundo ya kokoto, kwa maana hakuna mungu mwingine awezaye kuokoa namna hii.”
30 Potem je kralj povišal Šadráha, Mešáha in Abéd Negója v provinci Babilon.
Kisha mfalme akawapandisha vyeo Shadraki, Meshaki na Abednego katika jimbo la Babeli.