< Kološanom 1 >

1 Pavel, po Božji volji apostol Jezusa Kristusa in naš brat Timótej,
Paulo, mtume wa Kristo Yesu, kwa mapenzi ya Mungu, na Timotheo ndugu yetu:
2 svetim in zvestim bratom v Kristusu, ki ste v Kolósah: ›Milost bodi vam in mir od Boga, našega Očeta in Gospoda Jezusa Kristusa.‹
Kwa ndugu watakatifu na waaminifu katika Kristo, waishio Kolosai: Neema na amani zitokazo kwa Mungu Baba yetu ziwe nanyi.
3 Zahvaljujemo se Bogu in Očetu našega Gospoda Jezusa Kristusa, ko nenehno molimo za vas,
Siku zote tunamshukuru Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, tunapowaombea ninyi,
4 odkar smo slišali o vaši veri v Kristusa Jezusa in o ljubezni, ki jo imate do vseh svetih;
kwa sababu tumesikia kuhusu imani yenu katika Kristo Yesu, na upendo wenu mlio nao kwa watakatifu wote:
5 zaradi upanja, ki je za vas prihranjeno v nebesih, o katerem ste prej slišali v besedi resnice evangelija,
imani na upendo ule utokao katika tumaini mlilowekewa akiba mbinguni, na ambalo mmesikia habari zake katika neno la kweli, yaani, ile Injili
6 ki je prišel k vam tako, kakor je po vsem svetu; in prinaša sad, kakor tudi v vas, od dneva, ko ste slišali o njem in spoznali Božjo milost v resnici;
iliyowafikia ninyi. Duniani kote Injili hii inazaa matunda na kuenea kama ilivyokuwa kwenu tangu siku ile mlipoisikia na kuielewa neema ya Mungu katika kweli yote.
7 kakor ste se tudi naučili od Epafrá, našega dragega soslužabnika, ki je za vas zvest Kristusov služabnik,
Mlijifunza habari zake kutoka kwa Epafra, mtumishi mwenzetu mpendwa, yeye aliye mhudumu mwaminifu wa Kristo kwa ajili yenu,
8 ki nam je tudi pojasnil vašo ljubezen v Duhu.
ambaye pia ametuambia kuhusu upendo wenu katika Roho.
9 Zaradi tega razloga tudi mi od dneva, ko smo to slišali, ne prenehamo moliti za vas in želimo, da bi bili vi lahko izpolnjeni s spoznanjem njegove volje, v vsej modrosti in duhovnem razumevanju,
Kwa sababu hii, tangu siku ile tuliposikia habari zenu, hatujakoma kuomba kwa ajili yenu na kumsihi Mungu awajaze ninyi maarifa ya mapenzi yake katika hekima yote ya kiroho na ufahamu.
10 da bi lahko hodili vredno Gospoda v vsej všečnosti, bili rodovitni v vsakem dobrem delu in rastli v spoznanju Boga;
Nasi tunaomba haya ili mpate kuishi maisha yanayostahili mbele za Bwana, na mpate kumpendeza kwa kila namna: mkizaa matunda kwa kila kazi njema, mkikua katika kumjua Mungu,
11 okrepljeni z vso močjo, glede na njegovo veličastno moč, v vsej vztrajnosti in potrpežljivosti, z veseljem;
mkiwa mmetiwa nguvu kwa uwezo wote kwa kadiri ya nguvu yake yenye utukufu, ili mpate kuwa na wingi wa saburi na uvumilivu. Nanyi kwa furaha
12 in se zahvaljevali Očetu, ki nas je naredil primerne za udeležence dediščine svetih v svetlobi,
mkimshukuru Baba, ambaye amewastahilisha kushiriki katika urithi wa watakatifu katika ufalme wa nuru.
13 ki nas je osvobodil pred oblastjo teme in nas prenesel v kraljestvo svojega ljubljenega Sina;
Kwa maana ametuokoa kutoka ufalme wa giza na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wake mpendwa,
14 v katerem imamo po njegovi krvi odkupitev, torej odpuščanje grehov;
ambaye katika yeye tunao ukombozi, yaani msamaha wa dhambi.
15 ki je podoba nevidnega Boga, prvorojenec vsakega ustvarjenega bitja,
Yeye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.
16 kajti po njem so bile ustvarjene vse stvari, ki so na nebu in ki so na zemlji, vidne in nevidne, bodisi so to prestoli ali gospostva ali kneževine ali oblasti; vse stvari so bile ustvarjene po njem in zanj;
Kwake yeye vitu vyote vilivyoko mbinguni na juu ya nchi viliumbwa: vitu vinavyoonekana na visivyoonekana, viwe ni viti vya enzi au falme, au wenye mamlaka au watawala; vitu vyote viliumbwa na yeye na kwa ajili yake.
17 in on je pred vsemi stvarmi in po njem vse stvari stojijo skupaj.
Yeye alikuwepo kabla ya vitu vyote, na katika yeye vitu vyote vinashikamana pamoja.
18 In on je glava telesa, cerkve; ki ji je začetek, prvorojenec od mrtvih; da bi lahko v vseh stvareh imel prvenstvo.
Yeye ndiye kichwa cha mwili, yaani kanisa, naye ndiye mwanzo na mzaliwa wa kwanza kutoka kwa wafu, ili yeye awe mkuu katika vitu vyote.
19 Kajti Očetu je ugajalo, da bi v njem prebivala vsa polnost;
Kwa kuwa ilimpendeza Mungu kwamba utimilifu wake wote ukae ndani yake,
20 in je sklenil mir po krvi njegovega križa, da po njem pobota k sebi vse stvari; po njem, pravim, bodisi, da so stvari na zemlji ali stvari v nebesih.
na kwa njia yake aweze kuvipatanisha vitu vyote na yeye mwenyewe, viwe ni vitu vilivyo duniani au vilivyo mbinguni, kwa kufanya amani kwa damu yake, iliyomwagika msalabani.
21 In vas, ki ste bili nekoč odtujeni in v svojem mišljenju po zlobnih delih sovražniki, je vendar sedaj pobotal
Hapo kwanza mlikuwa mmetengana na Mungu, na mlikuwa adui zake katika nia zenu kwa sababu ya mienendo yenu mibaya.
22 v telesu njegovega mesa skozi smrt, da vas predstavi svete in neoporečne in brezgrajne v svojem pogledu,
Lakini sasa Mungu amewapatanisha ninyi kwa njia ya mwili wa Kristo kupitia mauti, ili awalete mbele zake mkiwa watakatifu, bila dosari wala lawama,
23 če utemeljeni in ustaljeni nadaljujete v veri in se ne boste oddaljili od upanja evangelija, ki ste ga slišali in ki je bil oznanjen vsakemu ustvarjenemu bitju, ki je pod nebom; katerega sem jaz, Pavel, postal služabnik;
ikiwa mnaendelea katika imani yenu mkiwa imara na thabiti, pasipo kuliacha tumaini lililoahidiwa katika Injili. Hii ndiyo ile Injili mliyoisikia, ambayo imehubiriwa kwa kila kiumbe chini ya mbingu, na ambayo mimi Paulo nimekuwa mtumwa wake.
24 ki se sedaj veselim v svojih trpljenjih za vas in v svojem mesu dopolnjujem to, kar je zaradi njegovega telesa, ki je cerkev, primanjkovalo Kristusovim stiskam;
Sasa nafurahia kule kuteseka kwangu kwa ajili yenu, na katika mwili wangu ninatimiliza yale yaliyopungua katika mateso ya Kristo kwa ajili ya mwili wake, ambao ni kanisa.
25 katerega služabnik sem postal, glede na Božjo razdelitev, ki mi je bila dana za vas, da izpolnim Božjo besedo;
Mimi nimekuwa mtumishi wa kanisa kwa wajibu alionipa Mungu ili kuwaletea ninyi Neno la Mungu kwa ukamilifu:
26 celó skrivnost, ki je bila skrita pred veki in pred rodovi, toda sedaj je razodeta njegovim svetim, (aiōn g165)
Hii ni siri iliyokuwa imefichika tangu zamani na kwa vizazi vingi, lakini sasa imefunuliwa kwa watakatifu. (aiōn g165)
27 katerim je Bog hotel razodeti kakšna so bogastva slave te skrivnosti med pogani; ki je Kristus v vas, upanje slave,
Kwao, Mungu amechagua kujulisha miongoni mwa watu wa Mataifa utukufu wa utajiri wa siri hii, ambayo ni Kristo ndani yenu, tumaini la utukufu.
28 katerega oznanjamo in vsakega človeka svarimo in vsakega človeka učimo v vsej modrosti; da lahko vsakega človeka prikažemo popolnega v Kristusu Jezusu;
Yeye ndiye tunayemtangaza, tukimwonya kila mtu na kumfundisha kila mtu kwa hekima yote ili tuweze kumleta kila mmoja akiwa amekamilika katika Kristo.
29 zato se tudi trudim in se borim, glede na njegovo delovanje, ki v meni mogočno deluje.
Kwa ajili ya jambo hili, ninajitaabisha, nikijitahidi kwa kadiri ya nguvu zake ambazo hutenda kazi ndani yangu kwa uweza mwingi.

< Kološanom 1 >