< Apostolska dela 13 >

1 Torej v cerkvi, ki je bila v Antiohiji, so bili določeni preroki in učitelji, kot Barnaba in Simeon, ki so ga imenovali Niger in Lukij iz Cirene in Manaén, ki je bil vzgojen s Herodom, vladarjem četrtinskega dela province ter Savel.
Katika kanisa huko Antiokia ya Shamu walikuwako manabii na walimu, yaani: Barnaba, Simeoni aitwaye Nigeri, Lukio Mkirene, Manaeni aliyekuwa amelelewa pamoja na Mfalme Herode Agripa, na Sauli.
2 Medtem ko so služili Gospodu in se postili, je Sveti Duh rekel: »Oddvojite mi Barnaba in Savla za delo, kamor sem ju poklical.«
Walipokuwa wakimwabudu Bwana na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, “Nitengeeni Sauli na Barnaba kwa kazi ile maalum niliyowaitia.”
3 In ko so se postili ter molili in svoje roke položili nanju, so ju odposlali.
Ndipo baada ya kufunga na kuomba, wakawawekea mikono yao na wakawatuma waende zao.
4 Tako sta, odposlana po Svetem Duhu, odšla v Selevkíjo in od tam sta odjadrala na Ciper.
Hivyo, wakiwa wametumwa na Roho Mtakatifu, wakashuka kwenda Seleukia na kutoka huko wakasafiri baharini mpaka kisiwa cha Kipro.
5 In ko sta bila v Salamini, sta v judovskih sinagogah oznanjala Božjo besedo in za svojo službo sta imela tudi Janeza.
Walipowasili katika mji wa Salami, wakahubiri neno la Mungu katika sinagogi la Wayahudi. Pia walikuwa na Yohana Marko kuwa msaidizi wao.
6 In ko sta šla prek otoka do Pafosa, sta našla nekega čarodeja, lažnega preroka, Juda, katerega ime je bilo Barjezus,
Walipokwisha kupita katika nchi zote hizo wakafika Pafo, ambapo walikutana na Myahudi mmoja mchawi aliyekuwa nabii wa uongo, jina lake Bar-Yesu.
7 ki je bil z namestnikom dežele, Sergijem Pavlom, razsodnim človekom, ki je dal poklicati Barnaba in Savla ter želel slišati Božjo besedo.
Mtu huyu alikuwa pamoja na Sergio Paulo, mtu mwenye hekima aliyekuwa msaidizi wa mwakilishi wa mtawala wa kile kisiwa. Sergio Paulo akawaita Sauli na Barnaba akitaka kusikia neno la Mungu.
8 Toda čarodej Elíma (kajti takšno je po razlagi njegovo ime), se jima je zoperstavil ter si prizadeval namestnika odvrniti od vere.
Lakini Elima yule mchawi (hii ndiyo maana ya jina lake), aliwapinga Barnaba na Sauli na kujaribu kumpotosha yule mkuu wa kile kisiwa aiache imani.
9 Potem je Savel (ki se imenuje tudi Pavel), izpolnjen s Svetim Duhom, svoje oči uprl vanj
Ndipo Sauli, ambaye pia aliitwa Paulo, akiwa amejawa na Roho Mtakatifu, akamkazia macho Elima huyo mchawi,
10 in rekel: »Oh poln vseh premetenosti in vseh vragolij, ti hudičev otrok, ti sovražnik vse pravičnosti, ali ne boš prenehal izkrivljati Gospodovih ravnih poti?
akamwambia, “Ewe mwana wa ibilisi, wewe ni adui wa kila kilicho haki! Umejaa kila aina ya udanganyifu na ulaghai. Je, hutaacha kuzipotosha njia za Bwana zilizonyooka?
11 In sedaj glej, Gospodova roka je nad teboj in oslepel boš ter za nekaj časa ne boš videl sonca.« In takoj sta padla nanj zamegljenost in tema in krožil je ter iskal nekoga, da ga vodi za roko.
Nawe sasa sikiliza, mkono wa Bwana u dhidi yako. Utakuwa kipofu, wala hutaona jua kwa muda.” Mara ukungu na giza vikamfunika, naye akaenda huku na huko akitafuta mtu wa kumshika mkono ili amwonyeshe njia.
12 Potem je namestnik, ko je videl, kaj se je zgodilo, veroval in bil osupel nad Gospodovim naukom.
Yule mkuu wa kile kisiwa alipoona yaliyotukia, akaamini kwa sababu alistaajabishwa na mafundisho kuhusu Bwana.
13 Torej ko so Pavel in njegova skupina odpluli iz Pafosa, so prišli v Pergo v Pamfiliji. Janez pa se je ločil od njiju in se vrnil v Jeruzalem.
Kisha Paulo na wenzake wakasafiri toka Pafo wakafika Perga huko Pamfilia. Lakini, Yohana Marko akawaacha huko, akarejea Yerusalemu.
14 Toda ko sta se odpravila iz Perge, sta prišla v Antiohijo v Pizidiji in na šabatni dan odšla v sinagogo ter se usedla.
Kutoka Perga wakaendelea hadi Antiokia ya Pisidia. Siku ya Sabato wakaingia ndani ya sinagogi, wakaketi.
15 Po branju postave in prerokov pa so predstojniki sinagoge poslali ponju, rekoč: » Vidva moža in brata, če imata kako spodbudno besedo za ljudi, povejta.«
Baada ya Sheria ya Mose na Kitabu cha Manabii kusomwa, viongozi wa sinagogi wakawatumia ujumbe wakisema, “Ndugu, kama mna neno la kuwafariji watu hawa, tafadhali lisemeni.”
16 Tedaj je Pavel vstal in s svojo roko dal znamenje ter rekel: »Možje Izraelci in vi, ki se bojite Boga, poslušajte.
Paulo akasimama, akawapungia mkono na kusema: “Enyi wanaume wa Israeli na ninyi nyote mnaomcha Mungu.
17 Bog teh ljudi iz Izraela je izbral naše očete in povišal ljudi, ko so kot tujci prebivali v egiptovski deželi in jih s povzdignjenim laktom privedel ven iz nje.
Mungu wa watu hawa wa Israeli aliwachagua baba zetu, akawafanya kustawi walipokuwa huko Misri, kwa uwezo mwingi akawaongoza na kuwatoa katika nchi ile.
18 In približno okoli štirideset let je prenašal njihovo obnašanje v divjini.
Kwa muda wa miaka arobaini alivumilia matendo yao walipokuwa jangwani.
19 In ko je v kánaanski deželi uničil sedem narodov, jim je njihovo deželo razdelil z žrebom.
Naye baada ya kuyaangamiza mataifa saba waliokuwa wakiishi katika nchi ya Kanaani, akawapa Waisraeli nchi yao iwe urithi wao.
20 Nató pa jim je dajal sodnike za približno štiristo petdeset let, do preroka Samuela.
Haya yote yalichukua kama muda wa miaka 450. “Baada ya haya, Mungu akawapa waamuzi mpaka wakati wa nabii Samweli.
21 In zatem so zahtevali kralja in Bog jim je dal Savla, Kiševega sina, moža iz Benjaminovega rodu, za približno štirideset let.
Ndipo watu wakaomba wapewe mfalme, naye Mungu akawapa Sauli mwana wa Kishi wa kabila la Benyamini, aliyetawala kwa miaka arobaini.
22 In ko ga je odstranil, jim je dvignil Davida, da bi bil njihov kralj, ki mu je dal tudi pričevanje ter rekel: ›Našel sem Davida, Jesejevega sina, moža po svojem lastnem srcu, ki bo izpolnil vso mojo voljo.‹
Baada ya kumwondoa Sauli katika ufalme, akawainulia Daudi kuwa mfalme wao. Mungu pia alimshuhudia, akisema, ‘Nimemwona Daudi mwana wa Yese, mtu anayeupendeza moyo wangu, atakayetimiza mapenzi yangu yote.’
23 Iz semena tega človeka je Bog, glede na svojo obljubo, Izraelu obudil Odrešenika, Jezusa,
“Kutoka uzao wa mtu huyu, Mungu amewaletea Israeli Mwokozi Yesu, kama alivyoahidi.
24 ko je pred njegovim prihodom Janez oznanjal krst kesanja vsem ljudem iz Izraela.
Kabla ya kuja kwa Yesu, Yohana alihubiri toba na ubatizo kwa watu wote wa Israeli.
25 In ko je Janez izpolnil svoj tek, je rekel: ›Kdo mislite, da sem jaz? Jaz nisem on. Toda glejte, za menoj prihaja nekdo, čigar čevljev z njegovih stopal nisem vreden odvezati.‹
Yohana alipokuwa anakamilisha kazi yake, alisema: ‘Ninyi mnadhani mimi ni nani? Mimi si yeye. La hasha, lakini yeye yuaja baada yangu, ambaye mimi sistahili kufungua kamba za viatu vya miguu yake.’
26 Možje in bratje, otroci Abrahamove rase ter kdorkoli se med vami boji Boga, vam je poslana beseda te rešitve duš.
“Ndugu zangu, wana wa Abrahamu, nanyi watu wa Mataifa mnaomcha Mungu, ujumbe huu wa wokovu umeletwa kwetu.
27 Kajti tisti, ki prebivajo v Jeruzalemu in njihovi vladarji, ker niso spoznali njega niti glasov prerokov, ki se berejo vsak šabatni dan, so jih izpolnili z njegovo obsodbo.
Kwa sababu wakaao Yerusalemu na viongozi wao hawakumtambua wala kuelewa maneno ya manabii yasomwayo kila Sabato, bali waliyatimiza maneno hayo kwa kumhukumu yeye.
28 In čeprav na njem niso našli nobenega razloga za smrt, so od Pilata zahtevali, da naj bi bil umorjen.
Ijapokuwa hawakupata sababu yoyote ya kumhukumu kifo, walimwomba Pilato aamuru auawe.
29 In ko so izpolnili vse, kar je bilo pisano o njem, so ga sneli z lesa ter ga položili v mavzolej.
Walipokwisha kufanya yale yote yaliyoandikwa kumhusu, walimshusha kutoka msalabani na kumzika kaburini.
30 Toda Bog ga je obudil od mrtvih,
Lakini Mungu alimfufua kutoka kwa wafu.
31 in mnogo dni so ga videli tisti, ki so prišli z njim iz Galileje v Jeruzalem, ki so njegove priče ljudem.
Naye kwa siku nyingi akawatokea wale waliokuwa pamoja naye kuanzia Galilaya hadi Yerusalemu. Nao sasa wamekuwa mashahidi wake kwa watu wetu.
32 In mi vam razodevamo vesele novice, kako je to obljubo, ki je bila narejena očetom,
“Nasi tunawaletea habari njema, kwamba yale Mungu aliyowaahidi baba zetu
33 Bog izpolnil nam, njihovim otrokom, v tem, da je ponovno dvignil Jezusa, kakor je tudi pisano v drugem psalmu: ›Ti si moj Sin, danes sem te rodil.‹
sasa ameyatimiza kwetu sisi watoto wao, kwa kumfufua Yesu, kama ilivyoandikwa katika Zaburi ya pili: “‘Wewe ni Mwanangu; leo mimi nimekuzaa.’
34 In glede na to, da ga je obudil od mrtvih, sedaj ni več vrnitve k trohnenju, je rekel na ta način: ›Dal vam bom zanesljive Davidove milosti.‹
Kwa kuwa Mungu alimfufua kutoka kwa wafu asioze kamwe, alitamka maneno haya: “‘Nitakupa wewe baraka takatifu zilizo za hakika nilizomwahidi Daudi.’
35 Zato tudi pravi v še enem psalmu: ›Svojemu Svetemu ne boš dal videti trohnenja.‹
Kama ilivyosemwa mahali pengine katika Zaburi, “‘Hutamwacha Aliye Mtakatifu wako kuona uharibifu.’
36 Kajti David je, potem ko je po Božji volji služil svojemu lastnemu rodu, zaspal in bil položen k svojim očetom ter videl trohnenje,
“Kwa maana Daudi akiisha kulitumikia kusudi la Mungu katika kizazi chake, alilala; akazikwa pamoja na baba zake na mwili wake ukaoza.
37 toda ta, ki ga je Bog ponovno obudil, ni videl trohnenja.
Lakini yule ambaye Mungu alimfufua kutoka kwa wafu hakuona uharibifu.
38 Naj bo torej znano vam, možje in bratje, da se vam po tem človeku oznanjuje odpuščanje grehov,
“Kwa hiyo ndugu zangu, nataka ninyi mjue kwamba kwa kupitia huyu Yesu msamaha wa dhambi unatangazwa kwenu.
39 in po njem ste vsi, ki verujete, opravičeni vseh stvari, od katerih niste mogli biti opravičeni po Mojzesovi postavi.
Kwa kupitia yeye, kila mtu amwaminiye anahesabiwa haki kwa kila kitu ambacho asingeweza kuhesabiwa haki kwa sheria ya Mose.
40 Pazite se torej, da ne pride nad vas to, o čemer je govora v prerokih:
Kwa hiyo jihadharini ili yale waliyosema manabii yasiwapate:
41 ›Glejte, vi prezirljivci in čudite se ter izginite, kajti v vaših dneh delam delo, delo katerega nikakor ne boste verovali, četudi vam ga človek razodene.‹«
“‘Angalieni, enyi wenye dhihaka, mkastaajabu, mkaangamie, kwa maana nitatenda jambo wakati wenu ambalo hamtasadiki, hata kama mtu akiwaambia.’”
42 In ko so Judje odšli iz sinagoge, so pogani prosili, da bi jim bile te besede lahko oznanjene naslednjo šabat.
Paulo na Barnaba walipokuwa wakitoka nje ya sinagogi, watu wakawaomba wazungumze tena mambo hayo Sabato iliyofuata.
43 Torej ko je bila skupnost razpuščena, so mnogi izmed Judov in religioznih spreobrnjencev sledili Pavlu in Barnabu, ki sta jim govorila in jih prepričevala naj nadaljujejo v Božji milosti.
Baada ya kusanyiko la Sinagogi kutawanyika, wengi wa Wayahudi na waongofu wa dini ya Kiyahudi wakawafuata Paulo na Barnaba, wakazungumza nao na kuwahimiza wadumu katika neema ya Mungu.
44 Naslednji šabatni dan pa je prišlo skupaj skoraj celotno mesto, da sliši Božjo besedo.
Sabato iliyofuata, karibu watu wote wa mji walikuja kusikiliza neno la Bwana.
45 Toda ko so Judje videli množice, so bili izpolnjeni z zavistjo in ugovarjali ter preklinjali in govorili proti tem stvarem, ki jih je govoril Pavel.
Lakini Wayahudi walipoona ule umati mkubwa wa watu walijawa na wivu, wakayakanusha maneno Paulo aliyokuwa akisema.
46 Tedaj sta Pavel in Barnaba postala pogumna in rekla: »Potrebno je bilo, da bi se Božja beseda najprej spregovorila vam, toda ker ste jo postavili proč od sebe in sebe sodite nevredne večnega življenja, glejte, se obračava k poganom. (aiōnios g166)
Ndipo Paulo na Barnaba wakawajibu kwa ujasiri, wakisema, “Ilitupasa kunena nanyi neno la Mungu kwanza. Lakini kwa kuwa mmelikataa, mkajihukumu wenyewe kuwa hamstahili uzima wa milele, sasa tunawageukia watu wa Mataifa. (aiōnios g166)
47 Kajti tako nam je ukazal Gospod, rekoč: ›Postavil sem te, da bi bil svetloba poganom, da naj bi bil za rešitev duš do koncev zemlje.‹«
Kwa maana hili ndilo Bwana alilotuamuru: “‘Nimewafanya ninyi kuwa nuru kwa watu wa Mataifa, ili mpate kuuleta wokovu hadi miisho ya dunia.’”
48 In ko so pogani to slišali, so bili veseli in slavili Gospodovo besedo; in kolikor jih je bilo odrejenih za večno življenje, je verovalo. (aiōnios g166)
Watu wa Mataifa waliposikia haya wakafurahi na kulitukuza neno la Bwana; nao wote waliokuwa wamekusudiwa uzima wa milele wakaamini. (aiōnios g166)
49 In Gospodova beseda je bila razglašena po vsem celotnem področju.
Neno la Bwana likaenea katika eneo lile lote.
50 Toda Judje so razvneli predane in častitljive ženske ter vodilne može mesta ter dvignili preganjanje zoper Pavla in Barnaba ter ju izgnali iz svojih krajev.
Lakini Wayahudi wakawachochea wanawake wenye kumcha Mungu, wenye vyeo pamoja na watu maarufu katika mji, wakachochea mateso dhidi ya Paulo na Barnaba na kuwafukuza kutoka eneo hilo.
51 Vendar sta proti njim otresla prah s svojih stopal in prišla v Ikónij.
Hivyo Paulo na Barnaba wakakungʼuta mavumbi ya miguu yao ili kuwapinga, nao wakaenda Ikonio.
52 Učenci pa so bili izpolnjeni z radostjo in s Svetim Duhom.
Wanafunzi wakajawa na furaha na Roho Mtakatifu.

< Apostolska dela 13 >