< 2 Samuel 11 >

1 Pripetilo se je, potem ko je minilo leto, ob času, ko gredo kralji na bitko, da je David poslal Joába in z njim svoje služabnike in ves Izrael in uničili so Amónove otroke in oblegali Rabo. Toda David se je še vedno zadrževal v Jeruzalemu.
Katika mwanzo wa mwaka mpya, wakati wafalme watokapo kwenda vitani, Daudi akamtuma Yoabu pamoja na watu wa mfalme na jeshi lote la Israeli. Wakawaangamiza Waamoni na kuuzunguka kwa jeshi mji wa Raba. Lakini Daudi akabaki Yerusalemu.
2 Ob večernem času se je pripetilo, da se je David dvignil iz svoje postelje in hodil po strehi kraljeve hiše in s strehe je videl žensko, ki se je umivala in ženska je bila na pogled zelo krasna.
Ikawa siku moja wakati wa jioni Daudi aliinuka kitandani mwake na kutembeatembea juu ya paa la jumba lake la kifalme. Kutokea kule kwenye paa, akamwona mwanamke akioga. Mwanamke huyo alikuwa mzuri sana wa sura,
3 David je poslal in poizvedel za žensko. Nekdo je rekel: » Mar ni to Batšéba, Eliámova hči, žena Hetejca Urijája?«
naye Daudi akatuma mtu mmoja kuuliza habari za huyo mwanamke. Huyo mtu akamwambia Daudi, “Je, huyu si Bathsheba binti Eliamu, naye ni mke wa Uria, Mhiti?”
4 David je poslal poslance in jo vzel. Vstopila je k njemu in ležal je z njo, kajti očiščena je bila od svoje nečistosti in vrnila se je v svojo hišo.
Ndipo Daudi akatuma wajumbe kumleta. Huyo mwanamke akaja kwa Daudi, Daudi akakutana naye kimwili. (Huyo mwanamke ndipo tu alikuwa amejitakasa kutoka siku zake za hedhi.) Kisha akarudi nyumbani kwake.
5 Ženska je spočela in poslala in povedala Davidu ter rekla: »Jaz sem z otrokom.«
Huyo mwanamke akapata mimba akampelekea Daudi ujumbe, kusema, “Mimi ni mjamzito.”
6 David je poslal k Joábu, rekoč: »Pošlji mi Hetejca Urijája.« In Joáb je poslal Urijája k Davidu.
Ndipo Daudi akapeleka ujumbe kwa Yoabu, “Unipelekee Uria, Mhiti.” Naye Yoabu akamtuma Uria kwa Daudi.
7 Ko je Urijá prišel k njemu, je David od njega zahteval, kako je šlo Joábu in kako je šlo ljudstvu in kako je uspevala vojna.
Uria alipofika, Daudi akamuuliza habari za Yoabu, hali za askari na vita kwamba inaendeleaje.
8 David je Urijáju rekel: »Pojdi dol k svoji hiši in si umij stopala.« Urijá je odšel iz kraljeve hiše in sledilo mu je darilo kraljeve jedi.
Kisha Daudi akamwambia Uria, “Teremka nyumbani kwako ukanawe miguu yako.” Basi Uria akaondoka kutoka kwenye jumba la kifalme, tena zawadi zikamfuata kutoka kwa mfalme.
9 Toda Urijá je spal pri vratih kraljeve hiše z vsemi služabniki svojega gospoda in ni odšel dol k svoji hiši.
Lakini Uria akalala kwenye ingilio la jumba la kifalme pamoja na watumishi wote wa bwana wake, na hakuteremka kwenda nyumbani kwake.
10 Ko so Davidu povedali, rekoč: »Urijá ni odšel dol k svoji hiši, « je David rekel Urijáju: »Ali ne prihajaš iz svojega potovanja? Zakaj potem nisi šel dol k svoji hiši?«
Daudi alipoambiwa kwamba, “Uria hakwenda nyumbani,” Daudi akamuuliza, “Je, si ndiyo tu umefika kutoka safari ya mbali? Kwa nini hukwenda nyumbani?”
11 Urijá je Davidu rekel: »Skrinja, Izrael in Juda prebivajo v šotorih in moj gospod Joáb in služabniki mojega gospoda so utaborjeni na odprtih poljih; ali bom jaz potem šel v svojo hišo, da jem, da pijem in da ležim s svojo ženo? Kakor ti živiš in kakor živi tvoja duša, ne bom storil te stvari.«
Uria akamwambia Daudi, “Sanduku la Mungu, na Israeli na Yuda wanakaa kwenye mahema, naye bwana wangu Yoabu na watu wa bwana wangu wamepiga kambi mahali pa wazi. Ningewezaje kwenda nyumbani kwangu ili nile, ninywe na kukutana na mke wangu? Hakika kama uishivyo sitafanya jambo la namna hiyo!”
12 In David je rekel Urijáju: »Ostani tukaj tudi danes, jutri pa ti bom pustil oditi.« Tako je Urijá ostal v Jeruzalemu ta dan in naslednji dan.
Ndipo Daudi akamwambia, “Kaa hapa siku moja zaidi, nami kesho nitakutuma urudi.” Kwa hiyo Uria akakaa Yerusalemu siku ile na siku iliyofuata.
13 Ko ga je David poklical, je pred njim jedel in pil in ga je opijanil in zvečer je odšel ven, da bi s služabniki svojega gospoda legel na svojo posteljo, toda ni šel dol k svoji hiši.
Kwa ukaribisho wa Daudi, Uria akala na kunywa pamoja naye, Daudi akamlevya. Lakini jioni Uria alitoka kwenda kulala juu ya mkeka wake miongoni mwa watumishi wa bwana wake, hakwenda nyumbani.
14 Zjutraj pa se je zgodilo, da je David napisal pismo Joábu in to poslal po Urijájevi roki.
Asubuhi yake Daudi akamwandikia Yoabu barua, akamtuma Uria kuipeleka.
15 V pismu je napisal, rekoč: »Postavite Urijája na sprednji del najbolj vroče bitke in se umaknite od njega, da bo lahko udarjen in umre.«
Ndani ya barua aliandika, “Mweke Uria mstari wa mbele mahali ambapo mapigano ni makali sana. Kisha wewe uondoke ili Uria aangushwe chini na kuuawa.”
16 Pripetilo se je, ko je Joáb opazoval mesto, da je Urijája določil na kraj, kjer je vedel, da so bili hrabri možje.
Hivyo Yoabu alipokuwa ameuzingira mji kwa jeshi, akamweka Uria mahali ambapo alijua kuwa ulinzi wa adui ulikuwa imara sana.
17 Možje iz mesta so odšli ven in se borili z Joábom in tam so padli nekateri izmed ljudstva, izmed Davidovih služabnikov in tudi Hetejec Urijá je umrl.
Wakati watu wa mjini walipotoka kwenda kupigana dhidi ya Yoabu, baadhi ya watu katika jeshi la Daudi wakauawa, zaidi ya hayo, Uria, Mhiti, akafa.
18 Potem je Joáb poslal in Davidu povedal vse stvari glede vojne
Yoabu akampelekea Daudi maelezo yote ya vita.
19 in naročil poslancu, rekoč: »Ko boš končal s sporočanjem stvari kralju glede vojne
Akamwagiza mjumbe hivi, “Utakapokuwa umemaliza kumpa mfalme maelezo ya vita,
20 in če bo tako, da se bo vzdignil kraljevi bes in ti reče: ›Zakaj ste se približali tako blizu mesta, ko ste se bojevali? Mar niste vedeli, da bodo streljali iz obzidja?
hasira ya mfalme yaweza kuwaka, naye aweza kukuuliza, ‘Kwa nini mlisogea karibu hivyo na mji kupigana? Hamkujua kuwa wangeweza kuwapiga mishale kutoka ukutani?
21 Kdo je udaril Jerubéšetovega sina Abiméleha? Ali ni ženska iz obzidja vrgla nanj kos mlinskega kamna, da je umrl v Tebécu? Zakaj ste se približali obzidju?‹ Potem reci: ›Tudi tvoj služabnik Hetejec Urijá je mrtev.‹«
Ni nani aliyemuua Abimeleki mwana wa Yerub-Besheth? Je, mwanamke hakutupa juu yake jiwe la juu la kusagia kutoka ukutani, kwa hiyo akafa huko Thebesi? Kwa nini mlisogea hivyo karibu ya ukuta?’ Ikiwa atakuuliza hivi, ndipo umwambie, ‘Pia mtumishi wako Uria, Mhiti, amekufa.’”
22 Tako je poslanec odšel in prišel in pokazal Davidu vse, za kar ga je Joáb poslal.
Mjumbe akaondoka. Alipowasili akamwambia Daudi kila kitu alichokuwa ametumwa na Yoabu kusema.
23 Poslanec je Davidu rekel: »Ljudje so zagotovo prevladali zoper nas in prišli ven, k nam na polje in mi smo bili nad njimi celo do vhoda velikih vrat.
Mjumbe akamwambia Daudi, “Watu walituzidi nguvu wakatoka nje ya mji dhidi yetu kwenye eneo la wazi, lakini tuliwarudisha nyuma mpaka kwenye ingilio la mji.
24 In strelci so streljali iz obzidja na tvoje služabnike; in nekateri izmed kraljevih služabnikov so mrtvi in tudi tvoj služabnik Hetejec Urijá je mrtev.«
Ndipo wapiga upinde walitupa mishale kwa watumishi wako kutoka ukutani, na baadhi ya watu wa mfalme wakafa. Zaidi ya hayo, Uria, Mhiti, mtumishi wako amekufa.”
25 Potem je David rekel poslancu: »Tako boš rekel Joábu: ›Ne dopusti, da te ta stvar razžali, kajti meč požre enega kakor drugega. Svojo bitko zoper mesto naredi močnejšo in ga premagaj. Ohrabri ga.‹«
Daudi akamwambia mjumbe, “Ukamwambie Yoabu hivi, ‘Jambo hili lisikutie wasiwasi, upanga hula huyu sawa na ulavyo mwingine. Zidisha mashambulizi dhidi ya mji na uangamize.’ Mwambie Yoabu hivi ili kumtia moyo.”
26 Ko je Urijájeva žena slišala, da je bil njen soprog Urijá mrtev, je žalovala za svojim soprogom.
Mke wa Uria aliposikia kwamba mumewe amekufa, akamwombolezea.
27 Ko je žalovanje minilo, je David poslal in jo privedel k svoji hiši in postala je njegova žena in mu rodila sina. Toda stvar, ki jo je David storil, je razžalila Gospoda.
Baada ya muda wa maombolezo kwisha, Daudi akamtaka aletwe nyumbani kwake, naye akawa mkewe, na akamzalia mwana. Lakini jambo alilokuwa amefanya Daudi lilimchukiza Bwana.

< 2 Samuel 11 >