< 2 Kralji 5 >
1 Torej Naamán, poveljnik vojske sirskega kralja, je bil plemenit mož pri svojem gospodarju in častitljiv, ker je po njem Gospod dal Siriji osvoboditev. Bil je tudi mogočen mož v hrabrosti, toda bil je gobavec.
Wakati huu, Naamani alikuwa jemadari wa jeshi la mfalme wa Aramu. Alikuwa mtu mkuu mbele ya bwana wake na aliyeheshimiwa sana, kwa sababu kupitia kwake, Bwana alikuwa amewapa Aramu ushindi. Alikuwa askari shujaa, lakini alikuwa na ukoma.
2 Sirci so hodili ven po skupinah in iz izraelske dežele odvedli ujetnico, malo deklico; in ta je čakala na Naamánovo ženo.
Siku hizo vikosi kutoka Aramu vilikuwa vimekwenda na vikawa vimemteka msichana kutoka Israeli, naye akamtumikia mkewe Naamani.
3 Svoji gospodarici je rekla: »Da bi Bog dal, da bi bil moj gospodar s prerokom, ki je v Samariji! Kajti on bi odvzel njegovo gobavost.«
Akamwambia bibi yake, “Kama bwana wangu angelimwona nabii aliyeko Samaria! Angemponya ukoma wake.”
4 Nekdo je vstopil in to povedal svojemu gospodarju, rekoč: »Tako in tako je govorila služabnica, ki je iz Izraelove dežele.«
Naamani akaenda kwa bwana wake na kumwambia alichosema yule msichana kutoka Israeli.
5 Kralj Sirije je rekel: »Odpravi se, pojdi, jaz pa bom poslal pismo Izraelovemu kralju.« Odpotoval je in s seboj vzel deset talentov srebra, šest tisoč koščkov zlata in deset zamenjav oblačil.
Mfalme wa Aramu akamjibu, “Hakika, nenda. Nitatuma barua kwa mfalme wa Israeli.” Kwa hiyo Naamani akaondoka, akiwa amechukua talanta kumi za fedha, shekeli 6,000 za dhahabu, na mivao kumi ya mavazi.
6 Izraelovemu kralju je prinesel pismo, rekoč: »Sedaj, ko je to pismo prišlo k tebi, glej, sem z njim poslal k tebi svojega služabnika Naamána, da mu lahko odvzameš njegovo gobavost.«
Barua aliyopelekea mfalme wa Israeli iliandikwa hivi: “Pamoja na barua hii ninamtuma mtumishi wangu, Naamani, kwako ili uweze kumponya ukoma wake.”
7 Pripetilo se je, ko je Izraelov kralj prebral pismo, da je pretrgal svoja oblačila in rekel: » Sem jaz Bog, da ubijem in oživim, da je ta človek poslal k meni, da možu odvzamem njegovo gobavost? Zatorej preudarite, prosim vas in glejte, kako zoper mene išče spor.«
Mara mfalme wa Israeli alipomaliza kuisoma ile barua, akararua mavazi yake na kusema, “Je, mimi ni Mungu? Je, mimi naweza kuua na kufufua tena? Kwa nini huyu mtu anamtuma mtu ili mimi nipate kumponya ukoma wake? Tazama jinsi anavyotafuta kuanzisha ugomvi nami!”
8 Bilo je tako, ko je Božji mož Elizej slišal, da je Izraelov kralj pretrgal svoja oblačila, da je poslal h kralju, rekoč: »Zakaj si pretrgal svoja oblačila? Naj torej pride k meni in vedel bo, da je v Izraelu prerok.«
Elisha mtu wa Mungu aliposikia kwamba mfalme wa Israeli alikuwa amerarua mavazi yake, akamtumia ujumbe huu: “Kwa nini umerarua mavazi yako? Mwamuru mtu huyo aje kwangu, naye atajua ya kuwa yuko nabii katika Israeli.”
9 Tako je Naamán prišel s svojimi konji in s svojim bojnim vozom in obstal pri vratih Elizejeve hiše.
Kwa hiyo Naamani akaenda, akiwa na farasi zake na magari yake, na kusimama mlangoni mwa nyumba ya Elisha.
10 Elizej pa je k njemu poslal poslanca, rekoč: »Pojdi in se sedemkrat umij v Jordanu in tvoje meso bo ponovno prišlo k tebi in boš čist.«
Elisha akamtuma mjumbe kumwambia, “Nenda uoge katika Yordani mara saba, na nyama ya mwili wako itapona, nawe utatakasika.”
11 Toda Naaman je bil ogorčen in odšel ter rekel: »Glej, mislil sem: ›Zagotovo bo prišel ven k meni, obstal in klical k imenu Gospoda, svojega Boga in s svojo roko udaril nad mestom in odvzel gobavost.‹
Lakini Naamani akaondoka akiwa amekasirika, akasema, “Hakika nilidhani kwamba angetoka nje, asimame na kuliitia jina la Bwana Mungu wake, na kuweka mkono wake juu ya mahali pagonjwa, aniponye ukoma wangu.
12 Mar nista Abána in Parpár, reki v Damasku, boljši kakor vse Izraelove vode? Ali se ne bi mogel umiti v njima in bi bil čist?« Tako se je obrnil in v besu odšel proč.
Je, Abana na Farpari, mito ya Dameski, si bora zaidi kuliko mito yoyote ya Israeli? Je, nisingeweza kuoga ndani ya hiyo mito na kutakasika?” Basi akageuka na kuondoka kwa hasira kuu.
13 Njegovi služabniki so prišli blizu, mu spregovorili in rekli: »Moj oče, če bi ti prerok naročil, da storiš neko veliko stvar, ali ne bi ti tega storil? Koliko bolj potem, ko ti je rekel: ›Umij se in bodi čist?‹«
Watumishi wa Naamani wakamwendea na kumwambia, “Baba yangu, kama huyo nabii angekuambia kufanya jambo lililo kubwa, je, usingelifanya? Je, si zaidi sana basi, anapokuambia, ‘Oga na utakasike!’”
14 Potem je odšel dol, se sedemkrat potopil v Jordanu, glede na izrek Božjega moža in njegovo meso je ponovno prišlo kakor meso majhnega otroka in bil je čist.
Hivyo akashuka na kujizamisha ndani ya Yordani mara saba, kama vile huyo mtu wa Mungu alivyokuwa amemwambia, nayo nyama ya mwili wake ikapona na kutakasika kama ya mwili wa mvulana mdogo.
15 Vrnil se je k Božjemu možu, on in vsa njegova skupina in prišel ter obstal pred njim in rekel: »Glej, sedaj vem, da ni Boga na vsej zemlji, razen v Izraelu. Sedaj torej, prosim te, vzemi blagoslov od svojega služabnika.«
Kisha Naamani na wahudumu wake wote wakarudi kwa yule mtu wa Mungu. Akasimama mbele yake na kusema, “Sasa najua kwamba hakuna Mungu katika ulimwengu wote isipokuwa katika Israeli. Tafadhali sasa upokee zawadi kutoka kwa mtumishi wako.”
16 Toda on je rekel: » Kakor živi Gospod, pred katerim stojim, ne bom ničesar sprejel.« Silil ga je, da to vzame; toda zavrnil je.
Nabii akajibu, “Hakika kama Bwana aishivyo, ambaye ninamtumikia, sitapokea kitu hata kimoja.” Ingawa Naamani alimsihi sana, yeye alikataa.
17 Naamán je rekel: »Ali ne bo, prosim te, dano tvojemu služabniku, tovor prsti za dve muli? Kajti tvoj služabnik odslej ne bo daroval niti žgalne daritve niti klavne daritve drugim bogovom, razen Gospodu.
Naamani akasema, “Ikiwa hutapokea, tafadhali mtumishi wako na apewe udongo kiasi cha mzigo wa kuweza kubebwa na punda wawili, kwa sababu mtumishi wako hatatoa tena sadaka ya kuteketezwa na dhabihu kwa mungu mwingine isipokuwa Bwana.
18 V tej stvari pa naj Gospod odpusti svojemu služabniku, da ko gre moj gospodar v Rimónovo hišo, da tam obožuje in se naslanja na mojo roko in se priklonim v Rimónovi hiši. Ko se priklonim v Rimónovi hiši, naj Gospod v tej stvari odpusti svojemu služabniku.«
Lakini Bwana na amsamehe mtumishi wake kwa kitu hiki kimoja: Wakati bwana wangu atakapoingia kwenye hekalu la Rimoni ili kusujudu, naye akiwa anauegemea mkono wangu, nami nikasujudu huko pia, wakati nitakaposujudu ndani ya hekalu la Rimoni, Bwana na amsamehe mtumishi wako kwa ajili ya jambo hili.”
19 Rekel mu je: »Pojdi v miru.« Tako je odšel od njega del poti.
Elisha akamwambia, “Nenda kwa amani.” Baada ya Naamani kusafiri umbali fulani,
20 Toda Gehazí, služabnik Božjega moža Elizeja, je rekel: »Glej, moj gospodar je prizanesel temu Sircu Naamánu v tem, da iz njegovih rok ni sprejel tega, kar je prinesel. Toda kakor živi Gospod bom stekel za njim in od njega nekaj vzel.«
Gehazi, mtumishi wa Elisha mtu wa Mungu, akajiambia mwenyewe, “Bwana wangu amemwachia kirahisi sana Naamani, huyu Mwaramu, kwa kutokupokea kutoka kwake vile alivyovileta. Hakika kama Bwana aishivyo, nitamkimbilia na kupata kitu kutoka kwake.”
21 Tako je Gehazí sledil Naamánu. Ko ga je Naamán videl teči za seboj, je upočasnil bojni voz, da ga sreča in rekel: » Ali je vse dobro?«
Hivyo Gehazi akaharakisha kumfuatilia Naamani. Naamani alipomwona akikimbia kumwelekea, akashuka chini kutoka kwenye gari lake na kwenda kumlaki. Akauliza, “Je, mambo yote ni sawa?”
22 Ta je rekel: »Vse je dobro. Moj gospodar me je poslal, rekoč: ›Glej, celo sedaj sta prišla k meni z gore Efrájim dva mladeniča izmed preroških sinov. Daj jima, prosim te, talent srebra in dve menjavi oblačil.‹«
Gehazi akajibu, “Mambo yote ni sawa. Bwana wangu amenituma nikuambie, ‘Vijana wawili kutoka kwa wana wa manabii wamenijia kutoka nchi ya vilima ya Efraimu. Tafadhali wape talanta ya fedha na mivao miwili ya mavazi.’”
23 Naamán je rekel: »Bodi zadovoljen, vzemi dva talenta.« Silil ga je in dva talenta srebra povezal v dve vreči, z dvema menjavama oblačil in jih položil na dva izmed svojih služabnikov in nosila sta jih pred njim.
Naamani akasema, “Hakika, chukua talanta mbili za fedha.” Akamsihi Gehazi azipokee, kisha akafunga talanta mbili za fedha katika mifuko miwili pamoja na mivao miwili ya mavazi. Akawapa watumishi wake wawili mizigo hiyo, nao wakaibeba wakitangulia mbele ya Gehazi.
24 Ko je prišel k stolpu, jih je vzel iz njune roke in jih shranil v hiši, moža pa je pustil oditi in sta odšla.
Gehazi alipofika kwenye kilima, akavichukua vile vitu kutoka kwa wale watumishi na kuvificha ndani ya nyumba. Akawaaga wale watu, nao wakaondoka.
25 Toda sam je vstopil in obstal pred svojim gospodarjem. Elizej mu je rekel: »Od kod prihajaš, Gehazí?« Rekel je: »Tvoj služabnik ni šel nikamor.«
Kisha akaingia ndani na kusimama mbele ya Elisha bwana wake. Elisha akamuuliza, “Gehazi, ulikuwa wapi?” Gehazi akajibu, “Mtumishi wako hakwenda popote.”
26 Rekel mu je: »Mar ni moje srce odšlo s teboj, ko se je mož ponovno obrnil nazaj iz svojega bojnega voza, da te sreča? Mar je čas, da prejemaš denar, da prejemaš obleke, oljčne nasade, vinograde, ovce, vole, služabnike in dekle?
Lakini Elisha akamwambia, “Je, roho yangu haikuwa pamoja nawe wakati yule mtu aliposhuka kutoka kwenye gari lake ili kukulaki? Je, huu ni wakati wa kupokea fedha au kupokea nguo, mashamba ya mizeituni, mashamba ya mizabibu, makundi ya kondoo na mbuzi, makundi ya ngʼombe, au watumishi wa kiume na wa kike?
27 Zato se bo Naamánova gobavost trdno prijela tebe in tvojega semena na veke.« In izpred njegove prisotnosti je odšel gobav, tako bel kakor sneg.
Ukoma wa Naamani utakushika wewe na wazao wako milele.” Kisha Gehazi akaondoka mbele ya Elisha, mwenye ukoma, mweupe kama theluji.