< 2 Kralji 23 >

1 Kralj je poslal in k njemu so zbrali vse starešine iz Juda in iz Jeruzalema.
Kisha mfalme akawaita pamoja wazee wote wa Yuda na Yerusalemu.
2 Kralj je šel gor v Gospodovo hišo in vsi Judovi možje in vsi prebivalci Jeruzalema z njim, duhovniki, preroki, vse ljudstvo, tako mali kakor veliki, in v njihova ušesa je bral vse besede knjige zaveze, ki je bila najdena v Gospodovi hiši.
Akapanda kwenda hekaluni mwa Bwana pamoja na watu wa Yuda, watu wa Yerusalemu, makuhani na manabii, watu wote wakubwa kwa wadogo. Akasoma wakiwa wanasikia maneno yote ya Kitabu cha Agano, ambacho kilikuwa kimepatikana katika Hekalu la Bwana.
3 Kralj je stal pri stebru in sklenil zavezo pred Gospodom, da hodijo za Gospodom in se držijo njegovih zapovedi, njegovih pričevanj in njegovih zakonov z vsem svojim srcem in vso svojo dušo, da izpolnjujejo besede te zaveze, ki so bile zapisane v tej knjigi. In vse ljudstvo je pristopilo k zavezi.
Mfalme akasimama karibu na nguzo, na kufanya upya agano mbele za Bwana: yaani kumfuata Bwana na kuzishika amri zake, maagizo na sheria kwa moyo wake wote na kwa roho yake yote, hivyo kuyathibitisha maneno ya agano yaliyoandikwa katika kitabu hiki. Kisha watu wote wakajifunga wenyewe kwa kiapo katika agano.
4 Kralj je zapovedal vélikemu duhovniku Hilkijáju, duhovnikom drugega reda in čuvajem vrat, da iz Gospodovega templja prinesejo vse posode, ki so bile narejene za Báala, za ašero in za vso vojsko neba, in sežgal jih je zunaj Jeruzalema, na poljih Kidrona in njihov pepel odnesel v Betel.
Mfalme akamwamuru Hilkia kuhani mkuu, makuhani waliomfuata kwa cheo, na mabawabu kuondoa kutoka kwenye Hekalu la Bwana vyombo vyote vilivyofanywa kwa ajili ya Baali na Ashera na jeshi lote la mianga ya angani! Akavichoma nje ya Yerusalemu katika mashamba ya Bonde la Kidroni, na kuyachukua hayo majivu mpaka Betheli.
5 Odstavil je malikovalske duhovnike, ki so jih Judovi kralji določili, da zažigajo kadilo na visokih krajih po Judovih mestih in v krajih naokoli Jeruzalema. Tudi tiste, ki so zažigali kadilo Báalu, soncu, luni, planetom in vsej vojski neba.
Akawafukuza makuhani wa kipagani waliokuwa wameteuliwa na wafalme wa Yuda kufukiza uvumba katika mahali pa juu pa kuabudia miungu katika miji ya Yuda na ile iliyozunguka Yerusalemu, yaani wale waliofukiza uvumba kwa Baali, kwa jua na mwezi, kwa makundi ya nyota, na jeshi lote la angani.
6 Iz Gospodove hiše je prinesel ašero, ven iz Jeruzalema, do potoka Kidron in jo sežgal pri potoku Kidronu in jo zdrobil v droben prah in njen prah vrgel na grobove otrok ljudstva.
Akaiondoa nguzo ya Ashera kutoka kwenye Hekalu la Bwana, na kuipeleka kwenye Bonde la Kidroni nje ya Yerusalemu, akaiteketeza huko. Akaisaga hadi ikawa unga na kusambaza hilo vumbi juu ya makaburi ya watu wa kawaida.
7 Porušil je hiše posvečenih vlačugarjev, ki so bile pri Gospodovi hiši, kjer so ženske tkale tanke preproge za ašero.
Akabomoa pia nyumba za mahanithi wa mahali pa ibada za miungu, zilizokuwa ndani ya Hekalu la Bwana na mahali wanawake walipofuma kwa ajili ya Ashera.
8 Vse duhovnike je privedel iz Judovih mest in omadeževal visoke kraje, kjer so duhovniki zažigali kadilo od Gebe do Beeršébe in porušil visoke kraje velikih vrat, ki so bile pri vhodu velikih vrat mestnega voditelja Józueta, ki so bila na moževi levici pri velikih vratih mesta.
Yosia akawaleta makuhani wote wa Bwana kutoka miji yote ya Yuda, na kunajisi mahali pa juu pa kuabudia miungu, kuanzia Geba hadi Beer-Sheba, mahali pote ambapo hao makuhani wa miungu walifukiza uvumba. Akabomoa mahali pa kuwekea vitu vya ibada za miungu palipokuwa katika malango, kwenye ingilio la Lango la Yoshua, mtawala wa mji, lililoko upande wa kushoto wa lango la mji.
9 Vendar duhovniki visokih krajev niso prišli gor h Gospodovemu oltarju v Jeruzalemu, temveč so med svojimi brati jedli nekvašen kruh.
Ingawa makuhani wa mahali pa juu pa kuabudia miungu hawakuhudumu katika madhabahu ya Bwana katika Yerusalemu, walikula mikate isiyotiwa chachu miongoni mwa ndugu zao.
10 In omadeževal je Tofet, ki je v dolini Hinómovih otrok, da noben človek ne bi mogel pripraviti svojega sina ali svoje hčere, da gre skozi ogenj k Molohu.
Kisha mfalme akanajisi Tofethi, palipokuwa katika Bonde la Ben-Hinomu, ili mtu yeyote asiweze kupatumia kumtoa kafara mwanawe au binti yake katika moto kwa mungu Moleki.
11 Odstranil je konje, ki so jih Judovi kralji podarili soncu ob vhodu v Gospodovo hišo, poleg sobe Netán Meleha, glavnega dvornega upravitelja, ki je bila v predmestjih in sončne bojne vozove sežgal z ognjem.
Akaondoa kutoka kwenye ingilio la Hekalu la Bwana wale farasi ambao wafalme wa Yuda walikuwa wamewaweka wakfu kwa ajili ya jua. Walikuwa kwenye ua karibu na chumba cha afisa aliyeitwa Nathan-Meleki. Basi Yosia akayachoma moto yale magari yaliyokuwa yamewekwa wakfu kwa jua.
12 Oltarje, ki so bili na vrhu gornje Aházove sobe, ki so jih naredili Judovi kralji, in oltarje, ki jih je naredil Manáse v dveh dvorih Gospodove hiše, je kralj porušil, jih odstranil od tam in njihov prah vrgel v potok Kidron.
Alizivunja madhabahu ambazo wafalme wa Yuda walikuwa wamezijenga kwenye paa la ghorofa ya Ahazi, pia madhabahu alizokuwa amezijenga Manase katika nyua mbili za Hekalu la Bwana. Akaziondoa huko, akazivunja vipande vipande, na kutupa hicho kifusi katika Bonde la Kidroni.
13 Visoke kraje, ki so bili pred Jeruzalemom, ki so bili na desni roki gore izprijenosti, ki jo je Salomon zgradil za Astarto, ogabnost Sidóncev in za Kemoša, ogabnost Moábcev in za Milkóma, gnusobo Amónovih otrok, je kralj omadeževal.
Mfalme pia akanajisi mahali pa juu pa kuabudia miungu, palipokuwa mashariki ya Yerusalemu upande wa kusini wa Kilima cha Uharibifu, pale ambapo Solomoni mfalme wa Israeli alikuwa amejenga kwa ajili ya Ashtorethi mungu mke chukizo la Wasidoni, kwa ajili ya Kemoshi mungu chukizo la Wamoabu, na kwa ajili ya Moleki mungu chukizo la watu wa Amoni.
14 Podobe je zlomil na koščke, posekal ašere in njihove kraje napolnil s človeškimi kostmi.
Yosia akapasua yale mawe ya kuabudiwa na kuzikatakata nguzo za Ashera. Kisha akafunika hayo maeneo kwa mifupa ya wanadamu.
15 Poleg tega oltar, ki je bil pri Betelu in visok kraj, ki ga je naredil Nebátov sin Jerobeám, ki je Izraela primoral grešiti, tako oltar kot visok kraj je porušil, požgal visok kraj, ga zdrobil v prah in sežgal ašero.
Hata madhabahu yaliyokuwa huko Betheli, mahali pa juu pa kuabudia miungu palipokuwa pamejengwa na Yeroboamu mwana wa Nebati, ambaye aliwafanya Israeli watende dhambi, alibomoa hata hayo madhabahu na mahali pa juu pa kuabudia miungu. Alipateketeza kwa moto hapo mahali pa juu pa kuabudia miungu na kupasaga hadi pakawa vumbi, na kuichoma hiyo nguzo ya Ashera pia.
16 Ko se je Jošíja obrnil, je ogledal mavzoleje, ki so bili na gori, poslal in iz mavzolejev vzel kosti in jih sežgal na oltarju, ga oskrunil, glede na Gospodovo besedo, ki jo je razglasil Božji mož, ki je razglasil te besede.
Kisha Yosia akatazama huku na huko, naye alipoona makaburi yaliyokuwa huko kwenye kilima, akaamuru mifupa itolewe humo na akaichoma juu ya madhabahu ya Betheli ili kupanajisi. Hili lilitokea kulingana na neno la Bwana lililosemwa na mtu wa Mungu ambaye alitangulia kusema mambo haya.
17 Potem je rekel: »Kakšen steber je to, kar vidim?« Ljudje iz mesta so mu rekli: » To je mavzolej Božjega moža, ki je prišel iz Juda in razglasil te stvari, ki si jih storil zoper betelski oltar.«
Mfalme akauliza, “Lile kaburi lenye mnara wa ukumbusho ninaloliona ni kwa ajili gani?” Watu wa mji wakasema, “Hii ni alama ya kaburi la mtu wa Mungu aliyekuja kutoka Yuda, naye akanena dhidi ya hii madhabahu ya Betheli mambo yale yale uliyoifanyia leo.”
18 Rekel je: »Pustite ga pri miru. Naj noben človek ne premakne njegovih kosti.« Tako so pustili pri miru njegove kosti, s kostmi preroka, ki je prišel iz Samarije.
Akasema, “Liacheni, msiliguse. Msimruhusu mtu yeyote kuiondoa mifupa yake.” Basi wakaiacha mifupa yake pamoja na ile ya yule nabii ambaye alikuwa amekuja kutoka Samaria.
19 Tudi vse hiše visokih krajev, ki so bile v samarijskih mestih, ki so jih naredili Izraelovi kralji, da bi Gospoda izzivali k jezi, je Jošíja odstranil in jim storil glede na vsa dejanja, ki jih je storil v Betelu.
Kama alivyokuwa amefanya huko Betheli, Yosia akabomoa na kunajisi mahali pa kuabudia miungu kwenye mahali pa juu ambapo wafalme wa Israeli walikuwa wamejenga ndani ya miji ya Samaria, ambayo ilikuwa imemghadhibisha Bwana.
20 Vse duhovnike visokih krajev, ki so bili tam, je usmrtil na oltarjih in na njih sežgal človeške kosti in se vrnil v Jeruzalem.
Yosia akawachinja makuhani wote wa mahali pa juu pa kuabudia miungu katika madhabahu zao wenyewe, na kuchoma mifupa ya wanadamu juu yake. Kisha akarudi Yerusalemu.
21 Kralj je vsemu ljudstvu zapovedal, rekoč: »Praznujte pasho Gospodu, svojemu Bogu, kakor je to zapisano v knjigi te zaveze.«
Mfalme akatoa agizo hili kwa watu wote: “Adhimisheni Pasaka kwa Bwana Mungu wenu, kama ilivyoandikwa katika Kitabu hiki cha Agano.”
22 Zagotovo tam ni bilo takšne pashe od dni sodnikov, ki so sodili Izraelu, niti v vseh dneh Izraelovih kraljev, niti Judovih kraljev,
Hapakuwahi kuwepo na adhimisho lingine la Pasaka kama hilo tangu nyakati za Waamuzi walioongoza Israeli, wala katika nyakati zote za wafalme wa Israeli na wafalme wa Yuda.
23 kot [je bila ta] v osemnajstem letu kralja Jošíja, v katerem se je praznovala ta pasha Gospodu v Jeruzalemu.
Lakini katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Mfalme Yosia, Pasaka hii iliadhimishwa kwa Bwana huko Yerusalemu.
24 Poleg tega je Jošíja odstranil delavce z osebnimi duhovi, čarovnike, podobe, malike in vse ogabnosti, ki so bile ogledane v Judovi deželi in v Jeruzalemu, da bi lahko izpolnil besede postave, ki so bile zapisane v knjigi, ki jo je duhovnik Hilkijá našel v Gospodovi hiši.
Zaidi ya hayo, Yosia akawaondoa waaguzi, wanaoabudu mizimu, sanamu za kuagulia, sanamu za kuabudiwa, na vitu vingine vyote vya machukizo vilivyoonekana huko Yuda na Yerusalemu. Aliyafanya haya ili kutimiza matakwa ya sheria iliyoandikwa ndani ya kile kitabu ambacho Hilkia kuhani alikipata ndani ya Hekalu la Bwana.
25 Pred njim ni bilo nobenega kralja, ki bi bil podoben njemu, ki bi se z vsem svojim srcem obrnil h Gospodu, z vso svojo dušo in z vso svojo močjo, glede na vso Mojzesovo postavo niti za njim ni vstal nihče, ki bi mu bil podoben.
Kabla wala baada ya Mfalme Yosia hapakuwepo na mfalme mwingine yeyote ambaye alimpenda Bwana kwa moyo wake wote, kwa roho yake yote, na kwa nguvu zake zote, sawasawa na Sheria yote ya Mose.
26 Vendar Gospod ni odvrnil okrutnosti svojega velikega besa, s čimer je bila vneta njegova velika jeza zoper Juda zaradi vseh izzivanj, s katerimi ga je izzival Manáse.
Hata hivyo, Bwana hakuacha ghadhabu yake iliyowaka dhidi ya Yuda kwa sababu ya yale yote ambayo Manase alikuwa amefanya kumghadhibisha.
27 Gospod je rekel: »Prav tako bom iz svojega pogleda odstranil Juda, kakor sem odstranil Izraela in zavrgel bom to mesto Jeruzalem, ki sem ga izbral in hišo, o kateri sem rekel: ›Tam bo moje ime.‹«
Hivyo Bwana akasema, “Nitamwondoa Yuda mbele zangu kama nilivyomwondoa Israeli, nami nitaukataa Yerusalemu, mji niliouchagua, na Hekalu hili, ambalo nilisema, ‘Jina langu litakaa humo.’”
28 Torej preostala izmed Jošíjevih dejanj in vse, kar je storil, mar niso zapisana v kroniški knjigi Judovih kraljev?
Matukio mengine ya utawala wa Yosia na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
29 V njegovih dneh je faraon Neho, egiptovski kralj, odšel gor zoper asirskega kralja, k reki Evfrat, in kralj Jošíja je odšel zoper njega, in ko ga je [faraon] zagledal ga je usmrtil pri Megídu.
Yosia alipokuwa mfalme, Farao Neko mfalme wa Misri akapanda mpaka Mto Frati kumsaidia mfalme wa Ashuru. Mfalme Yosia akatoka kwenda kupigana naye, lakini Neko akamkabili na kumuua huko Megido.
30 Njegovi služabniki so ga na bojnem vozu odnesli mrtvega od Megíde, ga prinesli v Jeruzalem in ga pokopali v njegovem lastnem mavzoleju. Ljudstvo dežele pa je vzelo Jošíjevega sina Joaháza, ga mazililo in ga postavilo [za] kralja namesto njegovega očeta.
Watumishi wa Yosia wakauleta mwili wake katika gari la vita kutoka Megido hadi Yerusalemu, wakamzika kwenye kaburi lake mwenyewe. Nao watu wa nchi wakamchukua Yehoahazi mwana wa Yosia, wakamtia mafuta na kumfanya mfalme mahali pa baba yake.
31 Joaház je bil star triindvajset let, ko je začel kraljevati, in v Jeruzalemu je kraljeval tri mesece. Ime njegove matere je bilo Hamutála, hči Jeremija iz Libne.
Yehoahazi alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitatu alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miezi mitatu. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia kutoka Libna.
32 Počel je to, kar je bilo zlo v Gospodovih očeh, glede na vse, kar so počeli njegovi očetje.
Akafanya maovu machoni mwa Bwana, kama baba zake walivyofanya.
33 Faraon Neho ga je vklenil v Ribli, v Hamovi deželi, da ne bi mogel kraljevati v Jeruzalemu in deželo je podvrgel davku stotih talentov srebra in talenta zlata.
Farao Neko akamfunga kwa minyororo huko Ribla katika nchi ya Hamathi ili asiweze kutawala huko Yerusalemu, naye akatoza kodi ya talanta mia moja za fedha, na talanta moja ya dhahabu katika Yuda.
34 Faraon Neho je postavil Jošíjevega sina Eljakíma za kralja namesto njegovega očeta Jošíja in njegovo ime spremenil v Jojakím in odstranil Joaháza. Ta je prišel v Egipt in tam umrl.
Farao Neko akamfanya Eliakimu mwana wa Yosia kuwa mfalme mahali pa baba yake Yosia, na kulibadilisha jina la Eliakimu kuwa Yehoyakimu. Lakini akamchukua Yehoahazi na kumpeleka Misri, naye akafia huko.
35 Jojakím je dal faraonu srebro in zlato, toda obdavčil je deželo, da izroča denar glede na faraonovo zapoved. Od ljudstva dežele je zahteval srebro in zlato, od vsakogar glede na njegovo obdavčitev, da to izroči faraonu Nehu.
Yehoyakimu akamlipa Farao Neko ile fedha na dhahabu aliyodai. Ili kuweza kufanya hivyo, Yehoyakimu akatoza nchi kodi na kulipiza fedha na dhahabu kutoka kwa watu wa nchi kulingana na makadrio ya mapato yao.
36 Jojakím je bil petindvajset let star, ko je začel kraljevati in v Jeruzalemu je kraljeval enajst let. Ime njegove matere je bilo Zebúda; hči Pedajája iz Rume.
Yehoyakimu alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Zebida binti Pedaya kutoka Ruma.
37 Počel je to, kar je bilo zlo v Gospodovih očeh, glede na vse, kar so počeli njegovi očetje.
Naye akafanya maovu machoni mwa Bwana, kama baba zake walivyokuwa wamefanya.

< 2 Kralji 23 >