< 2 Kralji 17 >
1 V dvanajstem letu Judovega kralja Aháza je v Samariji nad Izraelom začel kraljevati Elájev sin Hošéa [za] devet let.
Katika mwaka wa kumi na mbili wa utawala wa Ahazi mfalme wa Yuda, Hoshea mwana wa Ela akawa mfalme wa Israeli katika Samaria, akatawala kwa miaka tisa.
2 Počel je to, kar je bilo zlo v Gospodovih očeh, toda ne kakor Izraelovi kralji, ki so bili pred njim.
Akafanya maovu machoni pa Bwana, lakini si kama wafalme wengine wa Israeli waliomtangulia.
3 Zoper njega je prišel gor asirski kralj Salmanasar in Hošéa je postal njegov služabnik in mu izročil darila.
Mfalme Shalmanesa wa Ashuru akainuka dhidi ya Mfalme Hoshea, ambaye hapo mbeleni alikuwa mtumwa wake na kumlipa ushuru.
4 Asirski kralj je pri Hošéu našel zaroto, kajti ta je poslal poslance k egiptovskemu kralju Soju in ni prinesel nobenega darila k asirskemu kralju, kakor je počel leto za letom, zato ga je asirski kralj zaprl in ga zvezal v ječi.
Lakini mfalme wa Ashuru akagundua kuwa Hoshea alikuwa msaliti, kwa kuwa alikuwa ametuma wajumbe kwa So mfalme wa Misri, naye hakuendelea kulipa ushuru kwa mfalme wa Ashuru tena kama alivyokuwa anafanya kila mwaka. Kwa hiyo Shalmanesa akamkamata na kumtia gerezani.
5 Potem je asirski kralj prišel gor skozi vso deželo, se dvignil do Samarije in jo tri leta oblegal.
Mfalme wa Ashuru akaishambulia nchi yote, akapigana dhidi ya Samaria na kuizunguka kwa majeshi miaka mitatu.
6 V devetem letu kralja Hošéa, je asirski kralj zavzel Samarijo in Izraela odvedel proč v Asirijo ter jih nastanil v Haláhu in Habórju, pri reki Gozán in v mestih Medijcev.
Katika mwaka wa tisa wa Hoshea, mfalme wa Ashuru akaiteka Samaria na kuwahamishia Waisraeli huko Ashuru. Akawaweka huko Hala, na Gozani karibu na Mto Habori, na katika miji ya Wamedi.
7 Kajti bilo je tako, da so Izraelovi otroci grešili zoper Gospoda, svojega Boga, ki jih je privedel gor iz egiptovske dežele, izpod roke faraona, egiptovskega kralja in so se bali drugih bogov
Yote haya yalitokea kwa sababu Waisraeli walikuwa wametenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wao, ambaye alikuwa amewapandisha kutoka Misri akiwatoa chini ya utawala wa nguvu wa Farao mfalme wa Misri. Waliabudu miungu mingine
8 in hodili po zakonih poganov, ki jih je Gospod pregnal izpred Izraelovih otrok in [po poganskih navadah] Izraelovih kraljev, ki so si jih naredili.
na kufuata desturi za mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele yao, pamoja na desturi ambazo wafalme wa Israeli walizileta.
9 Izraelovi otroci so zoper Gospoda, svojega Boga, naskrivaj počeli te stvari, ki niso bile pravilne in si gradili visoke kraje po vseh svojih mestih, od stražarskega stolpa do utrjenega mesta.
Waisraeli wakafanya vitu kwa siri dhidi ya Bwana Mungu wao, ambavyo havikuwa sawa. Kuanzia kwenye mnara wa ulinzi hadi kwenye mji wenye maboma walijijengea wenyewe mahali pa juu pa kuabudia miungu katika miji yao yote.
10 Postavljali so si podobe in ašere na vsakem visokem hribu in pod vsakim zelenim drevesom
Wakaweka mawe ya kuabudiwa na nguzo za Ashera juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila mti uliotanda.
11 in tam zažigali kadilo na vseh visokih krajih, kakor so počeli pogani, ki jih je Gospod odvedel izpred njih in počeli zlobne stvari, da Gospoda izzivajo k jezi,
Wakafukiza uvumba kila mahali palipoinuka, kama yalivyofanya yale mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele yao. Wakafanya mambo maovu ambayo yalimghadhibisha Bwana.
12 kajti služili so malikom, o katerih jim je Gospod rekel: »Vi ne boste počeli te stvari.«
Wakaabudu sanamu, ingawa Bwana alikuwa amesema, “Msifanye mambo haya.”
13 Vendar je Gospod pričeval zoper Izraela in zoper Juda po vseh prerokih in po vseh vidcih, rekoč: »Obrnite se od svojih zlobnih poti in se držite mojih zapovedi in mojih zakonov, glede na vso postavo, ki sem jo zapovedal vašim očetom in ki sem jo poslal k vam po mojih služabnikih prerokih.«
Bwana akawaonya Israeli na Yuda kupitia kwa manabii na waonaji wake wote: “Acheni njia zenu mbaya. Shikeni amri na maagizo yangu, kufuatana na sheria yangu yote niliyowaagiza baba zenu kuitii ambayo niliileta kwenu kupitia kwa watumishi wangu manabii.”
14 Vendar niso hoteli poslušati, temveč so otrdili svoje vratove, podobno vratovom svojih očetov, da niso verovali v Gospoda, svojega Boga.
Lakini hawakusikiliza, walikuwa na shingo ngumu kama baba zao, ambao hawakumtegemea Bwana Mungu wao.
15 Zavrnili so njegove zakone in njegovo zavezo, ki jo je sklenil z njihovimi očeti in njegova pričevanja, ki jih je pričeval zoper njih. Sledili so ničevosti, postali prazni in odšli za pogani, ki so bili naokoli njih, glede katerih jim je Gospod naročil, da naj ne bi počeli kakor oni.
Walizikataa amri zake, na agano alilokuwa amelifanya na baba zao, na maonyo aliyokuwa amewapa. Wakafuata sanamu zisizofaa, nao wenyewe wakawa hawafai. Wakayaiga mataifa yaliyowazunguka, ingawa Bwana alikuwa amewaonya akiwaambia, “Msifanye kama wanavyofanya,” nao wakafanya mambo ambayo Bwana alikuwa amewakataza wasifanye.
16 Zapustili so vse zapovedi Gospoda, svojega Boga in si naredili ulite podobe, celó dve teleti, naredili ašero, oboževali vso vojsko neba in služili Báalu.
Wakayaacha maagizo yote ya Bwana Mungu wao na kujitengenezea sanamu mbili, walizozisubu katika sura ya ndama na nguzo ya Ashera. Wakasujudia mianga yote ya angani, na wakamtumikia Baali.
17 Svojim sinovom in svojim hčeram so povzročali, da gredo skozi ogenj in uporabljali so vedeževanje, izrekanje urokov in se prodajali, da počno zlo v Gospodovih očeh, da ga izzivajo do jeze.
Wakawatoa kafara wana wao na mabinti zao katika moto. Wakafanya uaguzi na uchawi, nao wakajiuza wenyewe katika kutenda uovu machoni pa Bwana, wakamghadhibisha.
18 Zato je bil Gospod zelo jezen nad Izraelom in jih odstranil iz svojega pogleda. Tam ni ostal nihče razen samo Judov rod.
Basi Bwana akawakasirikia sana Israeli na kuwaondoa kwenye uwepo wake. Ni kabila la Yuda tu lililobaki;
19 Tudi Juda se ni držal zapovedi Gospoda, svojega Boga, temveč je hodil po Izraelovih zakonih, ki so jih naredili.
na hata hivyo nao Yuda hawakuzishika amri za Bwana Mungu wao. Wakafuata desturi ambazo Israeli walikuwa wamezianzisha.
20 Gospod je zavrnil vse Izraelovo seme, jih prizadel in jih izročil v roko plenilcev, dokler jih ni pognal izpred svojega pogleda.
Kwa hiyo Bwana aliwakataa watu wote wa Israeli; akawatesa na kuwaachia katika mikono ya wateka nyara hadi alipowaondoa kutoka kwenye uwepo wake.
21 Kajti Izraela je odtrgal od Davidove hiše in Nebátovega sina Jerobeáma so postavili za kralja. Jerobeám je Izraela pregnal od sledenja Gospodu in jih primoral, da zagrešijo velik greh.
Alipokwisha kuwatenga Israeli mbali na nyumba ya Daudi, wakamfanya Yeroboamu mwana wa Nebati kuwa mfalme wao. Yeroboamu akawashawishi Israeli waache kumfuata Bwana na akawasababisha kutenda dhambi kuu.
22 Kajti Izraelovi otroci so hodili v vseh Jerobeámovih grehih, ki jih je ta storil; niso se odvrnili od njih,
Nao Israeli wakadumu katika dhambi zote za Yeroboamu mwana wa Nebati, nao hawakuziacha
23 dokler ni Gospod Izraela odstranil izpred svojega pogleda, kakor je govoril po vseh svojih služabnikih prerokih. Tako je bil Izrael odveden proč iz svoje lastne dežele, v Asirijo, do današnjega dne.
hadi Bwana alipowaondoa kutoka kwenye uwepo wake, kama vile alivyokuwa ameonya kupitia watumishi wake wote manabii. Hivyo watu wa Israeli wakaondolewa kutoka nchi yao kwenda uhamishoni Ashuru, nao wako huko mpaka sasa.
24 Asirski kralj pa je privedel može iz Babilona, iz Kute, iz Avája, iz Hamáta in iz Sefarvájima ter jih namesto Izraelovih otrok postavil v mesta Samarije. Samarijo so vzeli v last in prebivali v njenih mestih.
Mfalme wa Ashuru akawaleta watu kutoka Babeli, Kutha, Ava, Hamathi na Sefarvaimu na kuwaweka katika miji ya Samaria badala ya Waisraeli. Wakaimiliki Samaria na kuishi katika miji yake.
25 Na začetku njihovega prebivanja je bilo tam tako, da se niso bali Gospoda, zato je Gospod mednje poslal leve, ki so usmrtili nekatere izmed njih.
Wakati walianza kuishi humo, hawakumwabudu Bwana, kwa hiyo akatuma simba miongoni mwao, wakawaua baadhi ya watu.
26 Zato so asirskemu kralju govorili, rekoč: »Narodi, ki si jih odstranil in postavil v samarijska mesta, ne poznajo sodbe Boga dežele, zato je mednje poslal leve in glej, ti jih pobijajo, ker ne poznajo sodbe Boga dežele.«
Habari ikapelekwa kwa mfalme wa Ashuru, kusema: “Watu uliowahamisha na kuwaweka katika miji ya Samaria hawajui kile Mungu wa nchi hiyo anachokitaka. Ametuma simba miongoni mwao, ambao wanawaua, kwa sababu watu hawajui anachokitaka.”
27 Potem je asirski kralj zapovedal, rekoč: »Odvedite tja enega izmed duhovnikov, ki ste jih privedli od tam in naj gredo in prebivajo tam in naj jih nauči sodbe Boga dežele.«
Ndipo mfalme wa Ashuru akaamuru hivi: “Mtwae mmoja wa makuhani uliowachukua mateka kutoka Samaria ili arudi kuishi humo na awafundishe watu kile ambacho Mungu wa nchi anataka.”
28 Potem je eden izmed duhovnikov, ki so ga odvedli iz Samarije, prišel in prebival v Betelu ter jih učil, kako naj bi se bali Gospoda.
Basi mmoja wa makuhani ambaye alikuwa amepelekwa uhamishoni kutoka Samaria akaja kuishi Betheli na kuwafundisha jinsi ya kumwabudu Bwana.
29 Vendar je vsak narod izdelal svoje lastne bogove in jih postavil v hiše visokih krajev, ki so jih naredili Samarijani, vsak narod v svoja mesta, v katerih so prebivali.
Hata hivyo, kila kikundi cha taifa lililoletwa Samaria kilitengeneza miungu yao wenyewe katika miji kadhaa mahali walipoishi, nao wakaiweka mahali pa ibada za miungu ambapo watu wa Samaria walikuwa wametengeneza katika mahali pa juu.
30 Možje iz Babilona so naredili Sukót Benót, možje iz Kute so naredili Nergála, možje iz Hamáta so naredili Ašimája,
Watu kutoka Babeli wakamtengeneza Sukoth-Benothi kuwa mungu wao, watu kutoka Kutha wakamtengeneza Nergali, na watu kutoka Hamathi wakamtengeneza Ashima;
31 Avéjci so naredili Nibháza in Tartáka, Sefarvéjci pa so svoje otroke v ognju sežigali Adramélehu in Anamélehu, sefarvájimskima bogovoma.
Waavi wakatengeneza Nibhazi na Tartaki, nao Wasefarvi wakachoma watoto wao kama kafara kwa Adrameleki na Anameleki, miungu ya Sefarvaimu.
32 Tako so se bali Gospoda in si postavili najnižje izmed njih za duhovnike visokih krajev, ki so zanje žrtvovali v hišah visokih krajev.
Walimwabudu Bwana, lakini pia waliteua aina zote za watu wao ili kuwawakilisha kama makuhani katika mahali pa kuabudia miungu kwenye mahali pa juu pa ibada.
33 Bali so se Gospoda in služili svojim lastnim bogovom po običaju narodov, od katerih so jih odvedli.
Walimwabudu Bwana, lakini pia waliitumikia miungu yao kulingana na desturi za mataifa walikotoka.
34 Do tega dne počnejo po prejšnjih navadah. Ne bojijo se Gospoda niti ne delajo po njihovih zakonih ali po njihovih odredbah ali po postavi in zapovedi, ki jo je Gospod zapovedal Jakobovim otrokom, ki jih je imenoval Izrael,
Mpaka leo wanashikilia desturi zao za zamani. Hawamwabudu Bwana wala kuzishika hukumu na maagizo, sheria na amri ambazo Bwana aliwapa uzao wa Yakobo, ambaye alimwita Israeli.
35 s katerimi je Gospod sklenil zavezo in jim naročil, rekoč: »Vi se ne boste bali drugih bogov, niti se jim ne boste priklanjali, niti jim služili, niti jim žrtvovali,
Wakati Bwana alipofanya Agano na Waisraeli, aliwaamuru akisema: “Msiiabudu miungu mingine yoyote wala kuisujudia, wala kuitumikia wala kuitolea dhabihu.
36 temveč Gospoda, ki vas je privedel gor iz egiptovske dežele z veliko močjo in z iztegnjenim laktom, njega se boste bali in njega boste oboževali in njemu boste žrtvovali.
Bali imewapasa kumwabudu Bwana aliyewapandisha kutoka Misri kwa uwezo wake mkuu na kwa mkono wake ulionyooshwa. Kwake yeye mtasujudu na kwake yeye mtatoa dhabihu.
37 Zakone, predpise, odredbe in zapoved, ki vam jo je zapisal, boste obeleževali, da jih izvajate na vékomaj in ne boste se bali drugih bogov.
Imewapasa daima kuwa waangalifu kutunza hukumu na maagizo, sheria na amri alizowaandikia. Msiabudu miungu mingine.
38 Zaveze, ki sem jo sklenil z vami, ne boste pozabili niti se ne boste bali drugih bogov.
Msisahau agano nililofanya nanyi, wala msiabudu miungu mingine.
39 Temveč se boste bali Gospoda, svojega Boga in on vas bo osvobodil iz roke vseh vaših sovražnikov.«
Bali, mtamwabudu Bwana Mungu wenu, kwani yeye ndiye atakayewakomboa kutoka mikononi mwa adui zenu wote.”
40 Vendar niso prisluhnili, temveč so počeli po svoji prejšnji navadi.
Hata hivyo hawakusikiliza, lakini waliendelea na desturi zao za awali.
41 Tako so se ti narodi bali Gospoda in služili svojim rezanim podobam, tako njihovi otroci in otroci njihovih otrok, kakor so počeli njihovi očetje, tako počnejo do današnjega dne.
Hata wakati watu hawa walipokuwa wanamwabudu Bwana, walikuwa bado wakitumikia sanamu zao. Mpaka leo watoto wao na watoto wa watoto wao wanaendelea kufanya kama baba zao walivyofanya.