< 2 Kroniška 25 >
1 Amacjá je bil star petindvajset let, ko je začel kraljevati in v Jeruzalemu je kraljeval devetindvajset let. Ime njegove matere je bilo Joadána iz Jeruzalema.
Amazia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Yehoadani kutoka Yerusalemu.
2 Delal je to, kar je bilo pravilno v Gospodovih očeh, toda ne s popolnim srcem.
Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, lakini sio kwa moyo wake wote.
3 Pripetilo se je torej, ko mu je bilo kraljestvo utrjeno, da je usmrtil svoja služabnika, ki sta ubila kralja, njegovega očeta.
Baada ya ufalme kuimarika mikononi mwake, aliwaua maafisa waliomuua mfalme baba yake.
4 Toda njunih otrok ni usmrtil, temveč je storil, kakor je to zapisano v postavi Mojzesove knjige, kjer je Gospod zapovedal, rekoč: ›Očetje ne bodo umrli zaradi otrok niti ne bodo otroci umrli zaradi očetov, temveč bo vsak človek umrl zaradi svojega lastnega greha.‹
Hata hivyo hakuwaua watoto wao, lakini akafanya sawasawa na ilivyoandikwa katika Sheria, katika Kitabu cha Mose, ambako Bwana aliamuru: “Baba hawatauawa kwa ajili ya watoto wao, wala watoto hawatauawa kwa ajili ya baba zao. Kila mmoja atakufa kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe.”
5 Poleg tega je Amacjá zbral skupaj Juda in jih postavil za tisočnike in stotnike, glede na hiše njihovih očetov, po vsem Judu in Benjaminu. Preštel jih je od starosti dvajset let navzgor in jih našel tristo tisoč izbranih mož, zmožnih iti na vojno, ki so lahko zgrabili sulico in ščit.
Amazia akawaita watu wa Yuda pamoja, akawaweka chini ya majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia kufuatana na jamaa zao katika Yuda yote na Benyamini. Kisha akawahesabu wale wenye umri wa miaka ishirini au zaidi na akakuta kwamba walikuwa wanaume 300,000 watu walio tayari kwa utumishi wa jeshi, walio na uwezo wa kutumia mkuki na ngao.
6 Najel je tudi sto tisoč močnih junaških mož iz Izraela za sto talentov srebra.
Akawaajiri pia watu 100,000 wapiganaji kutoka Israeli kwa talanta 100 za fedha.
7 Toda tam je prišel k njemu Božji mož, rekoč: »Oh kralj, naj Izraelova vojska ne gre s teboj, kajti Gospod ni z Izraelom, namreč z vsemi Efrájimovi otroci.
Lakini mtu wa Mungu akamjia na kumwambia, “Ee mfalme, haya majeshi kutoka Israeli kamwe usiyaruhusu yaende pamoja na wewe kwa kuwa Bwana hayuko pamoja na Israeli, wala hayupo pamoja na yeyote wa watu wa Efraimu.
8 Toda če ti hočeš iti, stori to, bodi močan za bitko. Bog ti bo storil, da padeš pred sovražnikom, kajti Bog ima moč, da pomaga in da podere.«
Hata kama ukienda na kupigana kwa ujasiri katika vita, Mungu atakufanya ukimbie mbele ya adui, kwa kuwa Mungu anao uwezo wa kusaidia au wa kuangusha.”
9 Amacjá je rekel Božjemu možu: »Toda kaj naj storimo zaradi stotih talentov, ki sem jih dal Izraelovi vojski?« Božji mož je odgovoril: » Gospod ti je zmožen dati veliko več kakor to.«
Amazia akamuuliza yule mtu wa Mungu, “Lakini itakuwaje kwa zile talanta 100 za fedha nilizolipa kwa ajili ya haya majeshi ya Israeli?” Yule mtu wa Mungu akajibu, “Bwana aweza kukupa zaidi sana ya hizo.”
10 Potem jih je Amacjá ločil, namreč vojsko, ki je prišla k njemu iz Efrájima, da gre ponovno domov. Zato je bila njihova jeza silno vžgana zoper Juda in domov so se vrnili v veliki jezi.
Hivyo Amazia akayaondoa yale majeshi yaliyokuwa yamekuja kutoka Efraimu na kuyarudisha nyumbani. Waliwakasirikia sana Yuda, nao wakarudi nyumbani wakiwa na hasira kali.
11 Amacjá se je okrepil in vodil svoje ljudstvo in odšel v solno dolino in jih izmed Seírovih otrok pobil deset tisoč.
Ndipo Amazia akajitia nguvu na kuliongoza jeshi lake kwenye Bonde la Chumvi, ambako aliua watu 10,000 wa Seiri.
12 Drugih deset tisoč pa so Judovi otroci pustili žive, jih odvedli ujete in jih privedli na vrh skale ter jih vrgli dol iz vrha skale, da so bili razbiti na koščke.
Jeshi la Yuda pia likawateka watu 10,000 wakiwa hai, likawapandisha juu ya jabali na kuwatupa chini kwa nguvu hata wote wakavunjika vipande vipande.
13 Toda vojaki vojske, ki jih je Amacjá poslal nazaj, da ne bi šli z njim na bitko, so vpadli na Judova mesta od Samarije celo do Bet Horóna in pobili tri tisoč izmed njih in zajeli veliko plena.
Wakati huo yale majeshi Amazia aliyoyarudisha na ambayo hakuyaruhusu kushiriki katika vita, yalivamia miji ya Yuda kuanzia Samaria hata Beth-Horoni. Yakawaua watu 3,000 na kuchukua kiasi kikubwa sana cha mateka.
14 Pripetilo se je torej, potem ko je Amacjá prišel od pokola Edómcev, da je prinesel bogove Seírjevih otrok in jih postavil, da bodo njegovi bogovi, se priklanjal pred njimi in jim zažigal kadilo.
Amazia aliporudi kutoka kuwachinja Waedomu, alileta pia kutoka huko miungu ya watu wa Seiri. Akaisimamisha kama miungu yake mwenyewe, akaisujudia na kuitolea kafara za kuteketezwa.
15 Zato je bila Gospodova jeza vžgana zoper Amacjá in mu je poslal preroka, ki mu je rekel: »Zakaj si iskal za bogovi ljudstva, ki niso mogli rešiti svoje lastno ljudstvo iz tvoje roke?«
Hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Amazia, naye akamtuma nabii kwake, ambaye alisema: “Kwa nini unauliza kwa miungu ya hawa watu, ambayo haikuweza kuwaokoa watu wake wenyewe kutoka mkononi mwako?”
16 Pripetilo se je, ko je govoril z njim, da mu je kralj rekel: »Mar si postavljen za kraljevega svetovalca? Odnehaj. Zakaj bi bil udarjen?« Potem je prerok odnehal in rekel: »Vem, da je Bog določil, da te uniči, ker si to storil in nisi prisluhnil mojemu nasvetu.«
Wakati nabii alipokuwa angali anazungumza, mfalme akamwambia, “Je, wewe tumekuchagua kuwa mshauri wa mfalme? Nyamaza, ya nini uuawe?” Hivyo nabii akanyamaza lakini akasema, “Najua kuwa Mungu ameazimia kukuangamiza kwa sababu umefanya jambo hili na hukusikiliza shauri langu.”
17 Potem je Judov kralj Amacjá sprejel nasvet in poslal k Jehoášu, Joaházovemu sinu, Jehújevemu sinu, Izraelovemu kralju, rekoč: »Pridi, poglejva drug drugemu v obraz.«
Baada ya Amazia mfalme wa Yuda kushauriana na washauri wake akatuma ujumbe kwa Yehoashi, mwana wa Yehoahazi mwana wa Yehu, mfalme wa Israeli kusema: “Njoo tukabiliane uso kwa uso.”
18 Izraelov kralj Jehoáš pa je poslal k Judovemu kralju Amacjáju, rekoč: »Osat, ki je bil na Libanonu, je poslal k cedri, ki je bila na Libanonu, rekoč: ›Daj svojo hčer mojemu sinu za ženo.‹ In tam mimo je šla divja zver, ki je bila na Libanonu in pomendrala osat.
Lakini Yehoashi mfalme wa Israeli akamjibu Amazia mfalme wa Yuda, “Mbaruti uliokuwa Lebanoni ulituma ujumbe kwa mwerezi uliokuwa Lebanoni, ‘Mtoe binti yako aolewe na mwanangu.’ Kisha mnyama wa mwituni aliyekuwa Lebanoni akaja na kuukanyaga ule mbaruti.
19 Ti praviš: ›Glej, udaril si Edómce in tvoje srce te je povzdignilo do bahanja. Ostani torej doma, zakaj bi se vmešaval v svojo bolečino, da bi padel, celó ti in Juda s teboj?‹«
Wewe unasema moyoni mwako kwamba umemshinda Edomu, nawe sasa unajigamba na kujivuna. Lakini kaa nyumbani kwako! Kwa nini utafute matatizo na kujiletea anguko lako mwenyewe na la Yuda pia?”
20 Toda Amacjá ni hotel slišati, kajti to je prišlo od Boga, da bi jih on lahko izročil v roko njihovih sovražnikov, ker so iskali za edómskimi bogovi.
Hata hivyo, Amazia hakutaka kusikia, kwa kuwa Mungu alifanya hivyo ili awatie mikononi mwa Yehoashi, kwa sababu waliitafuta miungu ya Edomu.
21 Tako je Izraelov kralj Jehoáš odšel gor in videla sta drug drugega v obraz, tako on in Judov kralj Amacjá, pri Bet Šemešu, ki pripada Judu.
Hivyo Yehoashi mfalme wa Israeli akakwea kuwashambulia. Yeye na Amazia mfalme wa Yuda wakakabiliana uso kwa uso huko Beth-Shemeshi katika Yuda.
22 Juda je bil na slabšem pred Izraelom in pobegnili so vsak mož k svojemu šotoru.
Yuda ikashindwa na Israeli na kila mtu akakimbilia nyumbani kwake.
23 Izraelov kralj Jehoáš je prijel Judovega kralja Amacjá, Joáševega sina, Joaházovega sina pri Bet Šemešu in ga privedel v Jeruzalem in porušil jeruzalemsko obzidje od Efrájimovih velikih vrat do vogalnih velikih vrat, štiristo komolcev.
Yehoashi mfalme wa Israeli akamteka Amazia mfalme wa Yuda, mwana wa Yoashi, mwana wa Ahazia, huko Beth-Shemeshi. Kisha Yehoashi akamleta Yerusalemu na kuubomoa ukuta wa Yerusalemu kuanzia lango la Efraimu hadi Lango la Pembeni, sehemu yenye urefu wa kama dhiraa 400.
24 Vzel je vse zlato, srebro in vse posode, ki so bile najdene v Božji hiši z Obéd Edómom in zaklade kraljeve hiše, tudi talce in se vrnil v Samarijo.
Akachukua dhahabu yote, fedha na vyombo vyote vilivyopatikana katika Hekalu la Mungu, ambavyo vilikuwa chini ya uangalizi wa Obed-Edomu, pamoja na hazina za jumba la mfalme na mateka, kisha akarudi Samaria.
25 Joášev sin Amacjá, kralj Juda, je po smrti Izraelovega kralja, Joaházovega sina Jehoáša, živel petnajst let.
Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda aliishi miaka kumi na mitano baada ya kifo cha Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli.
26 Torej preostala izmed Amacjájevih dejanj, prva in zadnja, glej, mar niso zapisana v knjigi Judovih in Izraelovih kraljev?
Kwa habari ya matukio mengine katika utawala wa Amazia, kuanzia mwanzo hadi mwisho, je, hayakuandikwa katika kitabu cha wafalme wa Yuda na wa Israeli?
27 Torej po času, ko se je Amacjá odvrnil od sledenja Gospodu, so v Jeruzalemu zoper njega skovali zaroto; on pa je pobegnil v Lahíš. Toda poslali so za njim v Lahíš in ga tam usmrtili.
Kuanzia wakati ule Amazia alipogeuka na kuacha kumfuata Bwana walifanya shauri baya dhidi yake huko Yerusalemu naye akakimbilia Lakishi, lakini wakawatuma watu wamfuatilie huko Lakishi nao wakamuulia huko.
28 Pripeljali so ga na konjih in ga pokopali z njegovimi očeti v Judovem mestu.
Akarudishwa kwa farasi na akazikwa pamoja na baba zake katika Mji wa Yuda.