< 1 Kroniška 7 >
1 Torej Isahárjevi sinovi so bili: Tolá, Puvá, Jašúb in Šimrón, štirje.
Wana wa Isakari walikuwa: Tola, Pua, Yashubu na Shimroni; wote ni wanne.
2 Tolájevi sinovi: Uzí, Refajá, Jeriél, Jahmáj, Jibsám in Šemuél, poglavarji hiše njihovega očeta, namreč od Tolája. Bili so hrabri mogočni možje v svojih rodovih, katerih število je bilo v Davidovih dneh dvaindvajset tisoč šeststo.
Wana wa Tola walikuwa: Uzi, Refaya, Yerieli, Yahmai, Ibsamu na Shemueli waliokuwa viongozi wa jamaa zao. Wakati wa utawala wa Mfalme Daudi, wazao wa Tola walioorodheshwa kama wapiganaji katika ukoo wao walikuwa watu 22,600.
3 Uzíjevi sinovi: Jizrahjá; in Jizrahjájevi sinovi: Mihael, Obadjá, Joél in Jišijá, pet. Vsi izmed njih vodilni možje.
Mwana wa Uzi alikuwa: Izrahia. Wana wa Izrahia walikuwa: Mikaeli, Obadia, Yoeli na Ishia. Wote hawa watano walikuwa wakuu wao.
4 Z njimi, po njihovih rodovih, po hiši njihovih očetov, so bile čete vojakov za vojno, šestintrideset tisoč mož, kajti imeli so veliko žena in sinov.
Kulingana na ukoo wa jamaa zao, walikuwa na watu hodari wa vita wapatao 36,000, kwa sababu walikuwa na wanawake na watoto wengi.
5 Njihovi bratje med vsemi Isahárjevimi družinami so bili hrabri mogočni možje, prešteti po vseh njihovih rodovnikih, sedeminosemdeset tisoč.
Jamaa ya watu waliokuwa wapiganaji hodari kutoka koo zote za Isakari, kama ilivyoorodheshwa katika ukoo wao, jumla yao walikuwa 87,000.
6 Benjaminovi sinovi: Bela, Beher in Jediaél, trije.
Wana watatu wa Benyamini walikuwa: Bela, Bekeri na Yediaeli.
7 Belovi sinovi: Ecbón, Uzí, Uziél, Jerimót in Ir, pet; poglavarji hiše njihovih očetov, močni junaški možje; prešteti so bili po njihovih rodovnikih, dvaindvajset tisoč štiriintrideset.
Wana wa Bela walikuwa: Esboni, Uzi, Uzieli, Yeremothi na Iri; walikuwa viongozi wa jamaa zao; wote ni watano. Watu wapiganaji walioorodheshwa katika ukoo wao walikuwa 22,034.
8 Beherjevi sinovi: Zemirá, Joáš, Eliézer, Eljoenáj, Omri, Jerimót, Abíja, Anatót in Alémet. Vsi ti so Beherjevi sinovi.
Wana wa Bekeri walikuwa: Zemira, Yoashi, Eliezeri, Elioenai, Omri, Yeremothi, Abiya, Anathothi na Alemethi. Hawa wote walikuwa wana wa Bekeri.
9 Njihovo število po njihovih rodovnikih, po njihovih rodovih, poglavarjev hiš njihovih očetov, močnih junaških mož, je bilo dvajset tisoč dvesto.
Orodha ya ukoo wao iliyoandikwa viongozi wa jamaa zao walikuwa wapiganaji 20,200.
10 Tudi Jediaélovi sinovi: Bilhán. Bilhánovi sinovi: Jeúš, Benjamin, Ehúd, Kenaaná, Zetán, Taršíš in Ahišáhar.
Mwana wa Yediaeli alikuwa: Bilhani. Wana wa Bilhani walikuwa: Yeushi, Benyamini, Ehudi, Kenaana, Zethani, Tarshishi na Ahishahari.
11 Vseh teh Jediaélovih sinov, po poglavarjih njihovih očetov, močnih junaških mož, je bilo sedemnajst tisoč dvesto vojakov, primernih, da gredo ven na vojsko in bitko.
Hawa wana wote wa Yediaeli walikuwa viongozi wa jamaa zao. Kulikuwako wanaume wapiganaji 17,200 waliokuwa tayari kwenda vitani.
12 Tudi Šupím in Hupím, Irova otroka in Huším, Ahêrjevi sinovi.
Washupimu na Wahupimu walikuwa wazao wa Iri. Wahushimu walikuwa wazao wa Aheri.
13 Neftálijevi sinovi: Jahaciél, Guní, Jecer in Šalúm, Bilhini sinovi.
Wana wa Naftali walikuwa: Yahzieli, Guni, Yeseri na Shalumu; hao walikuwa wazao wa Bilha.
14 Manásejevi sinovi: Asriél, ki mu je rodila ( toda njegova arámska priležnica je rodila Mahírja, Gileádovega očeta;
Wana wa Manase walikuwa: Asirieli alikuwa mzao wake kutokana na suria wake wa Kiaramu. Huyu suria akamzaa Makiri baba wa Gileadi.
15 in Mahír je vzel za ženo sestro Hupíma in Šupíma, čigar sestri je bilo ime Maáha) in ime drugemu je bilo Celofhád; in Celofhád je imel hčere.
Makiri akatwaa mke kutoka miongoni mwa Wahupimu na Washupimu. Jina la dada yake aliitwa Maaka. Mwana wa pili wa Makiri aliitwa Selofehadi, ambaye alikuwa na wasichana tu.
16 Mahírjeva žena Maáha je rodila sina in njegovo ime imenovala Pereš; in ime njegovega brata je bilo Šereš; njegova sinova pa sta bila Ulám in Rekem.
Maaka mkewe Makiri akamzaa mwana aliyemwita Pereshi. Jina la nduguye lilikuwa Shereshi. Wana wa Pereshi walikuwa Ulamu na Rakemu.
17 Ulámovi sinovi: Bedán. To so bili sinovi Gileáda, sinú Mahírja, Manásejevega sina.
Mwana wa Ulamu alikuwa: Bedani. Hawa ndio waliokuwa wana wa Gileadi mwana wa Makiri, mwana wa Manase.
18 Njegova sestra Moléheta je rodila Išhóda, Abiézeja in Mahlája.
Dada yake aliyeitwa Hamolekethi aliwazaa Ish-Hodi, Abiezeri na Mahla.
19 Šemidájevi sinovi so bili: Ahján, Šehem, Likhí in Aniám.
Wana wa Shemida walikuwa: Ahiani, Shekemu, Liki na Aniamu.
20 Efrájimovi sinovi: Šutélah, njegov sin Bered, njegov sin Tahat, njegov sin Eladá in njegov sin Tahat,
Wana wa Efraimu walikuwa: Shuthela, ambaye alimzaa Beredi, Beredi akamzaa Tahathi, Tahathi akazaa Eleada, Eleada akamzaa Tahathi,
21 njegov sin Zabád, njegov sin Šutélah, Ecer in Elád, ki so jih usmrtil možje iz Gata, ki so bili rojeni v tej deželi, ker so prišli dol, da odvzamejo njihovo živino.
Tahathi akamzaa Zabadi, na Zabadi akamzaa Shuthela. Ezeri na Eleadi waliuawa na wenyeji wa Gathi walipokuwa wamekwenda huko kuwanyangʼanya mifugo yao.
22 Njihov oče Efrájim je mnogo dni žaloval in prišli so njegovi bratje, da ga tolažijo.
Baba yao Efraimu akawaombolezea kwa siku nyingi, na jamaa zake wakaja kumfariji.
23 Ko je odšel k svoji ženi, je spočela, rodila sina in njegovo ime je imenoval Berijá, ker je z njegovo hišo šlo slabo.
Kisha akakutana kimwili na mke wake tena, naye akachukua mimba, akamzalia mwana. Akamwita Beria, kwa sababu ya misiba iliyoipata nyumba yake.
24 (Njegova hči je bila Šeêra, ki je zgradila spodnji in zgornji Bet Horón ter Uzén Šeêro.)
Beria alikuwa na binti jina lake Sheera. Huyu ndiye aliijenga miji ya Beth-Horoni ya Juu na Beth-Horoni ya Chini, pamoja na Uzen-Sheera.
25 Refah je bil njegov sin, tudi Rešef in njegov sin Telah in njegov sin Tahan,
Beria akamzaa pia Refa, naye Refa akamzaa Reshefu, Reshefu akamzaa Tela, Tela akamzaa Tahani,
26 njegov sin Ladán, njegov sin Amihúd, njegov sin Elišamá,
Tahani akamzaa Ladani, Ladani akamzaa Amihudi, Amihudi akamzaa Elishama,
27 njegov sin Non in njegov sin Ješua.
Elishama akamzaa Nuni, Nuni akamzaa Yoshua.
28 Njihove posesti in prebivališča so bila Betel in njegova mesta, proti vzhodu Naára, proti zahodu Gezer s svojimi mesti; tudi Sihem in njegova mesta, do Gaze in njenih mest;
Nchi zao na makazi yao yalijumuisha Betheli na vijiji vilivyouzunguka, Naarani ilikuwa upande wa mashariki, Gezeri pamoja na vijiji vyake upande wa magharibi, pia Shekemu na vijiji vyake hadi kufikia Aya na vijiji vyake.
29 in pri mejah Manásejevih otrok, Bet Šeán in njegova mesta, Taanáh in njegova mesta, Megída in njegova mesta ter Dor in njegova mesta. V teh so prebivali otroci Izraelovega sina Jožefa.
Katika mipaka ya Manase walikuwepo Beth-Shani, Taanaki, Megido na Dori pamoja na vijiji vyake. Wana wa Yosefu mwana wa Israeli waliishi katika miji hii.
30 Aserjevi sinovi: Jimnáh, Jišvá, Jišví, Berijá in njihova sestra Sêraha.
Wana wa Asheri walikuwa: Imna, Ishva, Ishvi na Beria. Dada yao alikuwa Sera.
31 Berijájeva sinova: Heber in Malkiél, ki je Birzájitov oče.
Wana wa Beria walikuwa: Heberi na Malkieli, aliyekuwa baba yake Birzaithi.
32 Heber je zaplodil Jafléta, Šomerja, Hotáma in njihovo sestro Šuo.
Heberi akawazaa Yafleti, Shomeri na Hothamu, na Shua dada yao.
33 Jaflétovi sinovi: Pasáh, Bimhál in Ašvát. To so Jaflétovi sinovi.
Wana wa Yafleti walikuwa: Pasaki, Bimhali na Ashvathi. Hawa walikuwa wana wa Yafleti.
34 Šemerjevi sinovi: Ahí, Rohgá, Hubá in Arám.
Wana wa Shemeri walikuwa: Ahi, Roga, Yehuba na Aramu.
35 Sinovi njegovega brata Heléma: Cofah, Jimná, Šeleš in Amál.
Wana wa Helemu ndugu yake walikuwa: Sofa, Imna, Sheleshi na Amali.
36 Cofahovi sinovi: Suah, Harnéfer, Šuál, Berí, Jimrá,
Wana wa Sofa walikuwa: Sua, Harneferi, Shuali, Beri, Imra,
37 Becer, Hod, Šamá, Šilšá, Jitrán in Beerá.
Bezeri, Hodu, Shama, Shilsha, Ithrani na Beera.
38 Jeterjevi sinovi: Jefuné, Pispá in Ará.
Wana wa Yetheri walikuwa: Yefune, Pispa na Ara.
39 Ulájevi sinovi: Aráh, Haniél in Ricjá.
Wana wa Ula walikuwa: Ara, Hanieli na Risia.
40 Vsi ti so bili Aserjevi otroci, poglavarji njihovih očetnih hiš, izbrani in močni junaški možje, vodje princev. Število tistih, ki so bili po rodovniku zmožni za vojno in bitko, je bilo šestindvajset tisoč mož.
Hawa wote ndio waliokuwa wazao wa Asheri, viongozi wa jamaa zao, watu bora, mashujaa walio hodari na viongozi maarufu. Idadi ya watu waliokuwa tayari kwa vita, kama ilivyoorodheshwa katika ukoo wao, walikuwa 26,000.