< Псалтирь 80 >
1 В конец, о изменшихся, свидение Асафу, псалом. Пасый Израиля вонми: наставляяй яко овча Иосифа, седяй на Херувимех, явися:
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
2 пред Ефремом и Вениамином и Манассием воздвигни силу Твою, и прииди во еже спасти нас.
mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
3 Боже, обрати ны, и просвети лице Твое, и спасемся.
Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
4 Господи Боже сил, доколе гневаешися на молитву раб Твоих?
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
5 Напитаеши нас хлебом слезным, и напоиши нас слезами в меру.
Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
6 Положил еси нас в пререкание соседом нашым, и врази наши подражниша ны.
Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
7 Господи Боже сил, обрати ны, и просвети лице Твое, и спасемся.
Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
8 Виноград из Египта пренесл еси: изгнал еси языки, и насадил еси и:
Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
9 путесотворил еси пред ним, и насадил еси корения его, и исполни землю.
Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
10 Покры горы сень его, и ветвия его кедры Божия:
Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
11 простре розги его до моря, и даже до рек отрасли его.
Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
12 Вскую низложил еси оплот его, и оымают и вси мимоходящии путем?
Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
13 Озоба и вепрь от дубравы, и уединенный дивий пояде и.
Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
14 Боже сил, обратися убо, и призри с небесе и виждь, и посети виноград сей:
Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
15 и соверши и, егоже насади десница Твоя, и на сына человеческаго, егоже укрепил еси Себе.
mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
16 Пожжен огнем и раскопан: от запрещения лица Твоего погибнут.
Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
17 Да будет рука Твоя на мужа десницы Твоея и на сына человеческаго, егоже укрепил еси Себе,
Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
18 и не отступим от Тебе: оживиши ны, и имя Твое призовем.
Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
19 Господи Боже сил, обрати ны, и просвети лице Твое, и спасемся.
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.