< Псалтирь 59 >

1 В конец, да не растлиши, Давиду в столпописание, внегда посла Саул и стреже дом его, еже умертвити его. Изми мя от враг моих, Боже, и от востающих на мя избави мя:
Uniokoe dhidi ya adui zangu, Mungu wangu; uniweke mahali pa juu mbali na wale wanaoinuka dhidi yangu.
2 избави мя от делающих беззаконие, и от муж кровей спаси мя.
Uniweke salama mbali na wafanyao kazi ya uovu, na uniokoe dhidi ya watu wenye kiu ya damu.
3 Яко се, уловиша душу мою, нападоша на мя крепцыи: ниже беззаконие мое, ниже грех мой, Господи:
Maana, tazama, wanasubiria uvamizini waniue. Wafanya maovu wenye nguvu hujikusanya wenyewe pamoja dhidi yangu, lakini sio kwa sababu ya makosa yangu au dhambi yangu, Yahwe.
4 без беззакония текох и исправих: востани в сретение мое и виждь.
Wao wanajiandaa kunikimbiza ingawa sina kosa; amka unisaidie na unitazame.
5 И Ты, Господи Боже сил, Боже Израилев, вонми посетити вся языки: да не ущедриши вся делающыя беззаконие.
Ewe, Yahwe Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, inika uwaadhibu mataifa yote; usiwe na huruma kwa mhalifu mwovu yeyote. (Selah)
6 Возвратятся на вечер, и взалчут яко пес, и обыдут град.
Wao wanarudi jioni, wanabweka kama mbwa na kuuzungukia mji.
7 Се, тии отвещают усты своими, и мечь во устнах их: яко кто слыша?
Tazama, wanapiga kelele mbaya kwa midomo yao; panga ziko kwenye midomo yao, maana wanasema, “Ni nani anaye tusikia?”
8 И Ты, Господи, посмеешися им, уничижиши вся языки.
Lakini wewe, Yahwe, utawacheka; wewe huwadhihaki mataifa yote.
9 Державу мою к Тебе сохраню: яко Ты, Боже, заступник мой еси.
Mungu, nguvu yangu, nitakuwa msikivu kwako; wewe ni mnara wangu mrefu.
10 Бог мой, милость Его предварит мя: Бог мой, явит мне на вразех моих.
Mungu atakutana nami akiwa na uaminifu wa agano lake; Mungu atanifanya nione shauku yangu juu ya adui zangu.
11 Не убий их, да не когда забудут закон Твой: расточи я силою Твоею и низведи я, защитниче мой, Господи,
Usiwaue, hivyo watu watasahau. Uwatawanye kwa nguvu zako na uwaangushe, Bwana ngao yetu.
12 грех уст их, слово устен их: и яти да будут в гордыни своей, и от клятвы и лжи возвестятся в кончине,
Kwa ajili ya dhambi za midomo yao na maneno ya midomo yao, wakamatwe katika majivuno yao, na kwa laana na uongo ambao wao huelezea.
13 во гневе кончины, и не будут: и уведят, яко Бог владычествует Иаковом и концы земли.
Uwamalize katika gadhabu yako, uwamalize ili kwamba wasiwepo tena; wajue kuwa Mungu anatawala katika Yakobo na mwisho wa nchi. (Selah)
14 Возвратятся на вечер, и взалчут яко пес, и обыдут град:
Wakati wa jioni wao hurudi, wakibweka kama mbwa wakiuzungukia mji.
15 тии разыдутся ясти: аще ли же не насытятся, и поропщут.
Wanatangatanga wakitafuta chakula na wanabweka kama mbwa kama hawajatosheka.
16 Аз же воспою силу Твою и возрадуюся заутра о милости Твоей: яко был еси заступник мой и прибежище мое в день скорби моея.
Lakini nitaimba kuhusu nguvu zako, na asubuhi nitaimba kuhusu upendo wako imara! maana umekuwa mnara wangu mrefu na kimbilio la usalama katika siku ya taabu.
17 Помощник мой еси, Тебе пою: яко Бог заступник мой еси, Боже мой, милость моя.
Kwako, nguvu yangu, nitaimba sifa; kwa kuwa Mungu ni mnara wangu mrefu, Mungu wa uaminifu wa agano.

< Псалтирь 59 >