< Псалтирь 48 >

1 Псалом песни сынов Кореовых, вторыя субботы. Велий Господь и хвален зело во граде Бога нашего, в горе святей Его,
Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
2 благокоренным радованием всея земли: горы Сионския, ребра северова, град Царя великаго.
Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
3 Бог в тяжестех его знаемь есть, егда заступает и.
Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
4 Яко се, царие земстии собрашася, снидошася вкупе:
Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
5 тии видевше тако, удивишася, смятошася, подвигошася:
walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
6 трепет прият я тамо, болезни яко раждающия.
Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
7 Духом бурным сокрушиши корабли Фарсийския.
Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
8 Якоже слышахом, тако и видехом во граде Господа сил, во граде Бога нашего: Бог основа и в век.
Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
9 Прияхом, Боже, милость Твою посреде людий Твоих.
Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
10 По имени Твоему, Боже, тако и хвала Твоя на концах земли: правды исполнь десница Твоя.
Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
11 Да возвеселится гора Сионская, и да возрадуются дщери Иудейския, судеб ради Твоих, Господи.
Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
12 Обыдите Сион и обымите его, поведите в столпех его:
Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
13 положите сердца ваша в силу его, и разделите домы его, яко да повесте в роде инем.
yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
14 Яко Той есть Бог наш во век и в век века: Той упасет нас во веки.
Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.

< Псалтирь 48 >