< Псалтирь 31 >
1 В конец, псалом Давиду, изступления. На Тя, Господи, уповах, да не постыжуся во век: правдою Твоею избави мя и изми мя.
Kwa kiongozi wa muziki. Zaburi ya Daudi. In wewe, Yahwe, nakimbilia usalama; usiniache niaibishwe. Katika haki yako uniokoe.
2 Приклони ко мне ухо Твое, ускори изяти мя: буди ми в Бога защитителя и в дом прибежища, еже спасти мя.
Unisikie; uniokoe haraka; uwe mwamba wangu wa usalama, ngome ya kuniokoa.
3 Яко держава моя и прибежище мое еси Ты: и имене Твоего ради наставиши мя и препитаеши мя.
Kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu; kwa hiyo kwa ajili ya jina lako, uniongoze na unielekeze.
4 Изведеши мя от сети сея, юже скрыша ми: яко Ты еси защититель мой, Господи.
Unitoe katika mtego ambao wameuficha kwa ajili yangu, kwa kuwa wewe ni usalama wangu.
5 В руце Твои предложу дух мой: избавил мя еси, Господи Боже истины.
Mikononi mwako naikabidhi roho yangu; nawe utaniokoa, Yahwe, mwenye kuaminika.
6 Возненавидел еси хранящыя суеты вотще: аз же на Господа уповах.
Ninawachukia wale wanaotumikia miungu isiyo na maana, bali ninaamini katika Yahwe.
7 Возрадуюся и возвеселюся о милости Твоей, яко призрел еси на смирение мое, спасл еси от нужд душу мою
Nitafurahi na kushangilia katika uaminifu wa agano lako, kwa kuwa uliyaona mateso yangu; wewe uliijua dhiki ya moyo wangu.
8 и неси мене затворил в руках вражиих, поставил еси на пространне нозе мои.
Wewe haujaniweka kwenye mkono wa maadui zangu. Nawe umeiweka miguu yangu mahali pa wazi papana.
9 Помилуй мя, Господи, яко скорблю: смятеся яростию око мое, душа моя и утроба моя.
Uniurumie, Yahwe, kwa maana niko katika dhiki; macho yangu yanafifia kwa huzuni pamoja na moyo wangu na mwili wangu.
10 Яко изчезе в болезни живот мой, и лета моя в воздыханиих: изнеможе нищетою крепость моя, и кости моя смятошася.
Kwa kuwa maisha yangu yamechoshwa kwa huzuni na miaka yangu kwa kuugua kwangu. Nimekuwa dhaifu kwa sababu ya dhambi zangu, na mifupa yangu inachakaa.
11 От всех враг моих бых поношение, и соседом моим зело, и страх знаемым моим: видящии мя вон бежаша от мене.
Kwa sababu ya maadui zangu wote, watu wananibeza; majirani zangu wanaishangaa hali yangu, na wale wanao nifahamu wanashtuka. Wale wanionao mitaani hunikimbia.
12 Забвен бых яко мертв от сердца: бых яко сосуд погублен.
Nimesahaulika kama mtu aliye kufa ambaye hakuna mtu anaye mfikiria. Niko kama chungu kilicho pasuka.
13 Яко слышах гаждение многих живущих окрест: внегда собратися им вкупе на мя, прияти душу мою совещаша.
Kwa maana nimesikia minong'ono ya wengi, habari za kutisha kutoka pande zote kwa pamoja wamepanga njama kinyume na mimi. Wao wanapanga njama ya kuniua.
14 Аз же на Тя, Господи, уповах, рех: Ты еси Бог мой.
Bali mimi ninakuamini wewe, Yahwe; Ninasema, “Wewe ni Mungu wangu.”
15 В руку Твоею жребии мои: избави мя из руки враг моих и от гонящих мя.
Hatima yangu iko mikononi mwako. Uniokoe mikononi mwa maadui zangu na wale wanao nifukuzia.
16 Просвети лице Твое на раба Твоего: спаси мя милостию Твоею.
Nuru ya uso wako imuangazie mtumishi wako; uniokoe katika uaminifu wa agano lako.
17 Господи, да не постыжуся, яко призвах Тя: да постыдятся нечестивии, и снидут во ад. (Sheol )
Usiniache niaibishwe, Yahwe; kwa maana ninakuita wewe! Waovu waaibishwe! Na wanyamaze kimya kuzimuni. (Sheol )
18 Немы да будут устны льстивыя, глаголющыя на праведнаго беззаконие, гордынею и уничижением.
Na inyamazishwe midomo midanganyifu ambayo husema maneno mabaya kuhusu watu wenye haki huku wakiwa na kiburi na dharau.
19 Коль многое множество благости Твоея, Господи, юже скрыл еси боящымся Тебе, соделал еси уповающым на Тя, пред сыны человеческими:
Uzuri wako ni wa namna gani nao umeuhifadhii kwa ajili ya wale wanao kuheshimu sana, ambao wewe huufanya kwa ajili ya wale ambao hukimbilia kwako kwa ajili ya usalama mbele ya watoto wote wa wanadamu!
20 скрыеши их в тайне лица Твоего от мятежа человеческа, покрыеши их в крове от пререкания язык.
Katika makao ya uwepo wako, wewe huwaficha mbali na njama za watu. Wewe huwaficha mahali salama na ndimi zenye vurugu.
21 Благословен Господь, яко удиви милость Свою во граде ограждения.
Atukuzwe Yahwe, kwa maana yeye alinionesha maajabu ya uaminifu wa agano lake mahali nilipoishi.
22 Аз же рех во изступлении моем: отвержен есмь от лица очию Твоею: сего ради услышал еси глас молитвы моея, внегда воззвах к Тебе.
Ingawa kwa haraka zangu nilisema, “Nimeondolewa machoni pako,” bali wewe ulisikia kusihi kwangu nilipokulilia wewe.
23 Возлюбите Господа, вси преподобнии Его: яко истины взыскает Господь и воздает излише творящым гордыню.
Enyi wafuasi waaminifu, mpendeni Yahwe, Yahwe huwalinda waaminifu, lakini huwalipa wakaidi ipasavyo.
24 Мужайтеся, и да крепится сердце ваше, вси уповающии на Господа.
Iweni imara na jasiri, ninyi nyote mnao mwamini Mungu kuwasaidia.