< Псалтирь 136 >
1 Исповедайтеся Господеви, яко благ: яко в век милость Его.
Oh, mshukuruni Yahwe; kwa kuwa ni mwema, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
2 Исповедайтеся Богу богов: яко в век милость Его.
Oh, Mshukuruni Mungu wa miungu, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
3 Исповедайтеся Господеви господей: яко в век милость Его.
Oh, mshukuruni Bwana wa mabwana, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
4 Сотворшему чудеса велия единому: яко в век милость Его.
Mshukuruni yeye ambaye peke yake hufanya maajabu makuu, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
5 Сотворшему небеса разумом: яко в век милость Его.
Yeye aliyezifanya mbingu kwa hekima zake, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
6 Утвердившему землю на водах: яко в век милость Его.
Mshukuruni yeye alitetandaza nchi juu ya maji, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
7 Сотворшему светила велия единому: яко в век милость Его:
Yeye aliyefanya mianga mikubwa, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
8 солнце во область дне: яко в век милость Его:
Mshukuruni yeye alipaye jua kutawala mchana, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
9 луну и звезды во область нощи: яко в век милость Его.
Mwezi na nyota vitawale usiku, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
10 Поразившему Египта с первенцы его: яко в век милость Его:
Mshukuruni yeye aliyewaua wazaliwa wa kwanza wa Misri, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
11 и изведшему Израиля от среды их: яко в век милость Его:
Akawatoa Waisraeli kati yao, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
12 рукою крепкою и мышцею высокою: яко в век милость Его.
Kwa mkono hodari na mkono ulio nyooshwa, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
13 Раздельшему Чермное море в разделения: яко в век милость Его:
Mshukuruni yeye aliyeigawa Bahari ya Shamu, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
14 и проведшему Израиля посреде его: яко в век милость Его:
Na kuwapitisha Waisraeli katikati yake, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
15 и истрясшему фараона и силу его в море Чермное: яко в век милость Его.
Lakini akamtupa Farao na jeshi lake katika Bahari ya Shamu, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
16 Проведшему люди Своя в пустыни: яко в век милость Его.
Mshukuruni yeye aliye waongoza watu wake jangwani, kwa maana uaminifu wa agano lake ni wa milele.
17 Поразившему цари велия: яко в век милость Его.
Yeye aliyewaua wafalme wakuu, kwa maana uaminifu wa agano lake ni wadumu milele.
18 И убившему цари крепкия: яко в век милость Его:
Mshukuruni yeye aliyewaua wafalme maarufu, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
19 Сиона царя Аморрейска: яко в век милость Его:
Sihoni mfalme wa Waamori, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
20 и Ога царя Васанска: яко в век милость Его.
Na Ogu, mfalme wa Bashani, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
21 И давшему землю их достояние: яко в век милость Его:
Mshukuruni yeye aliyewapa nchi yao kama urithi, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
22 достояние Израилю рабу Своему: яко в век милость Его.
Urithi wa Israel mtumishi wake, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
23 Яко во смирении нашем помяну ны Господь: яко в век милость Его.
Yeye aliyetukumbuka na kutusaidia katika unyonge wetu, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
24 И избавил ны есть от врагов наших: яко в век милость Его:
Mshukuruni yeye ambaye ametupa ushindi juu ya aui zetu, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
25 даяй пищу всякой плоти: яко в век милость Его.
Yeye awapaye chakula viumbe hai wote, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
26 Исповедайтеся Богу небесному: яко в век милость Его.
Oh, mshukuruni Mungu wa mbinguni, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.