< Псалтирь 102 >
1 Молитва нищаго, егда уныет и пред Господем пролиет моление свое. Господи, услыши молитву мою, и вопль мой к Тебе да приидет.
Maombi ya mtu aliyechoka. Anapoteseka na kumimina malalamiko yake kwa Bwana. Ee Bwana, usikie maombi yangu, kilio changu cha kuomba msaada kikufikie.
2 Не отврати лица Твоего от мене: в оньже аще день скорблю, приклони ко мне ухо Твое: в оньже аще день призову Тя, скоро услыши мя.
Usinifiche uso wako ninapokuwa katika shida. Unitegee sikio lako, ninapoita, unijibu kwa upesi.
3 Яко изчезоша яко дым дние мои, и кости моя яко сушило сосхошася.
Kwa kuwa siku zangu zinatoweka kama moshi, mifupa yangu inaungua kama kaa la moto.
4 Уязвлен бых яко трава, и изсше сердце мое, яко забых снести хлеб мой.
Moyo wangu umefifia na kunyauka kama jani, ninasahau kula chakula changu.
5 От гласа воздыхания моего прильпе кость моя плоти моей.
Kwa sababu ya kusononeka kwangu kwa uchungu, nimebakia ngozi na mifupa.
6 Уподобихся неясыти пустынней, бых яко нощный вран на нырищи.
Nimekuwa kama bundi wa jangwani, kama bundi kwenye magofu.
7 Бдех и бых яко птица особящаяся на зде.
Nilalapo sipati usingizi, nimekuwa kama ndege mpweke kwenye paa la nyumba.
8 Весь день поношаху ми врази мои, и хвалящии мя мною кленяхуся.
Mchana kutwa adui zangu hunidhihaki, wale wanaonizunguka hutumia jina langu kama laana.
9 Зане пепел яко хлеб ядях и питие мое с плачем растворях,
Ninakula majivu kama chakula changu na nimechanganya kinywaji changu na machozi
10 от лица гнева Твоего и ярости Твоея: яко вознес низвергл мя еси.
kwa sababu ya ghadhabu yako kuu, kwa maana umeniinua na kunitupa kando.
11 Дние мои яко сень уклонишася, и аз яко сено изсхох.
Siku zangu ni kama kivuli cha jioni, ninanyauka kama jani.
12 Ты же, Господи, во век пребываеши, и память Твоя в род и род.
Lakini wewe, Ee Bwana, umeketi katika kiti chako cha enzi milele, sifa zako za ukuu zaendelea vizazi vyote.
13 Ты воскрес ущедриши Сиона: яко время ущедрити его, яко прииде время.
Utainuka na kuihurumia Sayuni, kwa maana ni wakati wa kumwonyesha wema; wakati uliokubalika umewadia.
14 Яко благоволиша раби Твои камение его, и персть его ущедрят.
Kwa maana mawe yake ni ya thamani kwa watumishi wako, vumbi lake lenyewe hulionea huruma.
15 И убоятся языцы имене Господня, и вси царие земстии славы Твоея:
Mataifa wataogopa jina la Bwana, wafalme wote wa dunia watauheshimu utukufu wako.
16 яко созиждет Господь Сиона и явится во славе Своей.
Kwa maana Bwana ataijenga tena Sayuni na kutokea katika utukufu wake.
17 Призре на молитву смиренных и не уничижи моления их.
Ataitikia maombi ya mtu mkiwa, wala hatadharau hoja yao.
18 Да напишется сие в род ин, и людие зиждемии восхвалят Господа:
Hili na liandikwe kwa ajili ya kizazi kijacho, ili taifa litakaloumbwa baadaye waweze kumsifu Bwana:
19 яко приниче с высоты святыя Своея, Господь с небесе на землю призре,
“Bwana alitazama chini kutoka patakatifu pake palipo juu, kutoka mbinguni alitazama dunia,
20 услышати воздыхание окованных, разрешити сыны умерщвленных:
kusikiliza vilio vya uchungu vya wafungwa na kuwaweka huru wale waliohukumiwa kufa.”
21 возвестити в Сионе имя Господне и хвалу Его во Иерусалиме,
Kwa hiyo jina la Bwana latangazwa huko Sayuni na sifa zake katika Yerusalemu,
22 внегда собратися людем вкупе и царем, еже работати Господеви.
wakati mataifa na falme zitakapokusanyika ili kumwabudu Bwana.
23 Отвеща Ему на пути крепости Его: умаление дний моих возвести ми:
Katika kuishi kwangu alivunja nguvu zangu, akafupisha siku zangu.
24 не возведи мене во преполовение дний моих: в роде родов лета Твоя.
Ndipo niliposema: “Ee Mungu wangu, usinichukue katikati ya siku zangu; miaka yako inaendelea vizazi vyote.
25 В началех Ты, Господи, землю основал еси, и дела руку Твоею суть небеса.
Hapo mwanzo uliweka misingi ya dunia, nazo mbingu ni kazi ya mikono yako.
26 Та погибнут, Ты же пребываеши: и вся яко риза обетшают, и яко одежду свиеши я, и изменятся.
Hizi zitatoweka, lakini wewe utadumu, zote zitachakaa kama vazi. Utazibadilisha kama nguo nazo zitaondoshwa.
27 Ты же тойжде еси, и лета Твоя не оскудеют.
Lakini wewe, U yeye yule, nayo miaka yako haikomi kamwe.
28 Сынове раб Твоих вселятся, и семя их во век исправится.
Watoto wa watumishi wako wataishi mbele zako; wazao wao wataimarishwa mbele zako.”