< Числа 12 >

1 И возглаголаста Мариам и Аарон на Моисеа жены ради Ефиопляныни, юже поя Моисей, ибо жену поя Ефиопляныню,
Miriamu na Aroni walianza kuzungumza dhidi ya Mose kwa sababu ya mke wake Mkushi, kwa kuwa alikuwa ameoa Mkushi.
2 и рекоста: еда Моисею единому глагола Господь? Еда и нам не глаголаше? И услыша Господь.
Waliuliza, “Je, Bwana amesema kupitia Mose peke yake? Je, hajasema kutupitia sisi pia?” Naye Bwana akasikia hili.
3 И человек Моисей кроток зело паче всех человек сущих на земли.
(Basi Mose alikuwa mtu mnyenyekevu sana, mnyenyekevu kuliko mtu mwingine yeyote katika uso wa dunia.)
4 И рече Господь внезапу к Моисею и Аарону и Мариаме: изыдите вы трие в скинию свидения.
Ghafula Bwana akawaambia Mose, Aroni na Miriamu, “Njooni katika Hema la Kukutania, ninyi nyote watatu.” Kwa hiyo wote watatu wakaenda.
5 И изыдоша трие в скинию свидения. И сниде Господь в столпе облачне ста над дверми скинии свидения: и призва Аарона и Мариам. И изыдоста оба.
Kisha Bwana akashuka katika nguzo ya wingu, akasimama kwenye ingilio la Hema, akawaita Aroni na Miriamu. Wakati wote wawili waliposogea mbele,
6 И рече к ним: послушайте словес Моих: аще будет в вас пророк Господнь, в видении ему познаюся, и во сне возглаголю ему:
Bwana akasema, “Sikilizeni maneno yangu: “Akiwapo nabii wa Bwana miongoni mwenu, nitajifunua kwake kwa maono, nitanena naye katika ndoto.
7 не тако якоже раб Мой Моисей, во всем дому Моем верен есть:
Lakini sivyo kwa mtumishi wangu Mose; yeye ni mwaminifu katika nyumba yangu yote.
8 усты ко устом возглаголю ему яве, и не гаданием, и славу Господню виде: и почто не убоястеся глаголати на раба Моего Моисеа?
Kwake nitanena naye uso kwa uso, waziwazi wala si kwa mafumbo; yeye ataona umbo la Bwana. Kwa nini basi ninyi hamkuogopa kuzungumza kinyume cha mtumishi wangu Mose?”
9 И гнев ярости Господни (бысть) на них. И отиде.
Hasira ya Bwana ikawaka dhidi yao, akawaacha.
10 И облак отступи от скинии, и се, Мариам прокажена бысть яко снег: и воззре Аарон на Мариам, и се, прокажена.
Wakati hilo wingu liliinuka kutoka juu ya Hema, Miriamu akawa tayari ana ukoma, mweupe kama theluji. Aroni akamgeukia, akaona ana ukoma.
11 И рече Аарон к Моисею: молю тя, господи, не возлагай на ны греха, понеже не ведяхом, яко согрешихом:
Kisha Aroni akamwambia Mose, “Tafadhali, bwana wangu, usituhesabie dhambi hii ambayo tumeifanya kwa upumbavu.
12 да не будет сия яко мертва, яко изверг извержен из ложесн матерних, и (се, уже) пояде пол плоти ея.
Usimwache awe kama mtoto mchanga aliyezaliwa akiwa mfu, ambaye nusu ya mwili wake imeharibika hapo atokapo katika tumbo la mama yake.”
13 И возопи Моисей ко Господу, глаголя: Боже, молютися, исцели ю.
Hivyo Mose akamlilia Bwana akisema, “Ee Mungu, nakuomba umponye!”
14 И рече Господь к Моисею: аще бы отец ея плюя заплевал в лице ея, не посрамится ли седмь дний? Да отлучится седмь дний вне полка, и по сих да внидет.
Bwana akamjibu Mose, “Je, kama baba yake angemtemea usoni, asingeona aibu kwa siku saba? Mfungie nje ya kambi kwa siku saba; baada ya hapo anaweza kurudishwa kambini.”
15 И отлучися Мариам вне полка на седмь дний: и людие не воздвигошася, дондеже очистися Мариам.
Kwa hiyo Miriamu akafungiwa nje ya kambi kwa siku saba, nao watu hawakuendelea na safari mpaka aliporudishwa kambini.
16 И по сих воздвигошася людие от Асирофа и ополчишася в пустыни Фарани.
Baada ya hayo, watu waliondoka Haserothi, wakapiga kambi katika Jangwa la Parani.

< Числа 12 >