< Книга пророка Наума 3 >
1 О, граде кровей, весь лживый, полн неправды! Не осяжется ловитва.
Ole kwa mji uliojaa damu! Wote umejaa uongo na mali za wizi; wahanga wapo kwake daima.
2 Глас бичей и глас труса колес, и коня текуща и колесницы шумящия,
Lakini sasa kunasauti ya mijeledi na sauti za kugongesha matairi, farasi wakicheza, na magari ya vita yanaruka ruka.
3 и конника едуща, и блистающа меча и блистающих оружий, и множества язвеных и тяжкаго падения, и не бяше конца языком ея: и изнемогут в телесех своих от множества блужения.
Kuna wapanda farasi wanashambulia, Upanga unang'ara, mikuki inametameta, marundo ya maiti, mafungu makubwa ya miili; hakuna ukomo wa miili, washambuliaji wanajikwaa juu yake.
4 Блудница добра и приятна, началница волхвований, продающая языки во блужении своем и племена в чародеяниих своих.
Hii inatokea kwa sababu ya matendo ya tamaa ya kahaba mzuri, mzoefu wa uchawi, mwenye kuuza taifa kwa umalaya wake, na watu kwa njia ya matendo yake ya kichawi.
5 Се, Аз на тя, глаголет Господь Бог Вседержитель, и открыю задняя твоя к лицу твоему, и покажу языком срамоту твою и царствам безчестие твое,
“Tazama, mimi nipo kinyume na wewe- hili ni neno la Yehova wa majeshi- sketi yako nitaiinua juu ya uso wako na kuzionyesha sehemu zako za siri kwa mataifa, aibu yako kwa falme.
6 и возвергу на тя огнушение по нечистотам твоим, и положу тя в притчу.
Nitarusha uchafu wa kuchukiza na kukufanya uwe mbaya sana; nitakufanya uwe mtu wa kutazamwa na kila mmoja.
7 И будет, всяк видяй тя снидет с тебе и речет: окаянная Ниневиа, кто постенет по ней? Откуду взыщу утешение ей?
Itakuwa kwamba kila mmoja anayekutazama atakukimbia na kusema, “Ninawi ameharibika; ni nani ataomboleza kwa ajili yake?' Ni wapi nitampata mtu anayeweza kukufariji?”
8 Уготовити часть, устроити струну, уготовити часть Аммону, живущая в реках, вода окрест ея, ейже начало море, и вода забрала ея:
Ninawi, je wewe ni bora kuliko Noamoni, uliojengwa juu ya Mto Naili, uliokuwa umezungukwa na maji, ambao ulinzi wake ilikuwa bahari, ambao ukuta wake ilikuwa bahari yenyewe?
9 и Ефиопиа крепость ея и Египет, и несть конца бегству твоему: и Фуд и Ливиане быша помощницы ея.
Ethiopia na Misri zilikuwa nguvu zake, na mwisho wake haukuwepo; Putu na Libya walikuwa rafiki zake.
10 И сия в преселение пойдет пленница, и младенцы ея разбиют в началех всех путий ея, и о всех славных ея вергут жребия, и вси воеводы ея свяжутся путы.
Lakini Noamoni alichukuliwa; alikwenda kwenye mateka; watoto wake wadogo walivunjwa vipande vipande katika kila makao makuu ya mtaa; adui zake walipiga kura kwa watu wake wenye heshima na wakuu wake wote walifungwa minyororo.
11 И ты упиешися и будеши презрена, и ты сама себе взыщеши помощи от враг.
Wewe pia utalewa; utajaribu kujificha, na utatafuta makimbilio kutoka kwa adui yako.
12 Вся твердели твоя яко смоквичие стражу имущее: аще поколеблются, впадут во уста ядущаго.
Ngome zako zote zitakuwa kama mitini yenye tini zilizoiva mapema: kama zikitikiswa, zitaangukia kwenye kimywa cha mlaji.
13 Се, людие твои, яко жены в тебе: врагом твоим отворяема отворятся врата земли твоея, и пояст огнь вереи твоя.
Tazama, watu miongoni mwenu ni wanawake; malango ya nchi yako yamefunguliwa sana kwa ajili ya adui zako; moto umeharibu bawaba zake.
14 Воду одержания восхити себе сама и утверди твердели твоя: влези в брение и поперися в плевах, утверди паче плинфа.
Nenda ukachote maji kwenye boma iliyozingirwa; ziimarishe ngome zako; nenda kwenye udongo na kandamiza matope; finyanga kwa ajili ya matofali.
15 Тамо пояст тя огнь, потребит тя мечь, поядят тя аки прузи, и отягчаеши аки мшица.
Moto utakuteketeza pale, na upanga utakuangamiza. Utateketezwa kama nzige wachanga wanavyoteketeza kila kitu. Ninyi wenyewe mjitengeneze kuwa wengi kama nzige wachanga, na wengi kama nzinge waliopevuka.
16 Умножила еси купли твоя паче звезд небесных: мшицы устремишася и возлетеша.
Umezidisha wafanyabiashara wako zaidi kuliko nyota mbinguni; lakini wapo kama tunutu: wanapora nchi na kisha kuruka kwenda mbali.
17 Возскочи аки пруг смесник твой, аки акрида восходящая на ограду в день студеный: солнце взыде, и отлете, и не познася место ея: люте им!
Wafalme wenu wapo wengi kama zinge, na wakuu wenu wa majeshi ni kama kundi la wadudu wenye kuweka kambi katika ukuta wakati wa baridi. Lakini jua linapowaka wanaruka kwenda mbali ambako hakuna anayepajua.
18 Воздремашася пастуси твои, царь Ассирийск успи сильныя твоя, воздвигошася людие твои на горы, и не бяше приемлющаго.
Mfalme wa Ashuru, wachungaji wako wamelala; watawala wako wamejilaza chini kupumzika. Watu wako wametawanyika juu ya milima, na hakuna hata mmoja wa kuwakusanya.
19 Несть цельбы сокрушению твоему, разгореся язва твоя: вси слышащии весть твою восплещут руками о тебе: понеже на кого не найде злоба твоя всегда?
Hakuna uponyaji unaowezekana kwa ajili ya vidonda vyako. Vidonda vyako ni vikubwa. Wanaosikia habari juu yako watapiga makofi kwa furaha juu yako. Ni nani aliyejiepusha kwa uovu wako wa daima?