< Книга пророка Малахии 3 >
1 Се, Аз посылаю Ангела Моего, и призрит на путь пред лицем Моим: и внезапу приидет в церковь Свою Господь, Егоже вы ищете, и Ангел завета, Егоже вы хощете: се, грядет, глаголет Господь Вседержитель.
“Angalieni, nitamtuma mjumbe wangu, atakayeiandaa njia mbele yangu. Ndipo ghafula Bwana mnayemtafuta atakuja hekaluni mwake. Mjumbe wa Agano, ambaye mnamwonea shauku, atakuja,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
2 И кто стерпит день пришествия Его? И кто постоит в видении Его? Зане Той входит яко огнь горнила и яко мыло перущих.
Lakini ni nani atakayeweza kustahimili hiyo siku ya kuja kwake? Ni nani awezaye kusimama atakapotokea? Kwa kuwa atakuwa kama moto wa mfua fedha au kama sabuni ya afuaye nguo.
3 И сядет разваряя и очищая яко сребро и яко злато, и очистит сыны Левиины, и прелиет я яко злато и яко сребро: и будут Господеви приносяще жертву в правде.
Ataketi kama mfuaji na asafishaye fedha. Atawatakasa Walawi, naye atawasafisha kama dhahabu na fedha. Kisha Bwana atakuwa na watu watakaoleta sadaka katika haki,
4 И угодна будет Господеви жертва Иудова и Иерусалимля, якоже дние века и якоже лета преждняя.
nazo sadaka za Yuda na Yerusalemu zitakubalika kwa Bwana, kama katika siku zilizopita, kama katika miaka ya zamani.
5 И прииду к вам с судом, и буду свидетель скор на чародеи и на прелюбодейцы, и на кленущыяся именем Моим во лжу и на лишающыя мзды наемника, и на насильствующыя вдовиц и пхающыя сирыя, и на укланяющыя суд пришелца и на небоящыяся Мене, глаголет Господь Вседержитель:
“Basi nitakuja karibu nanyi ili kuhukumu. Nami nitakuwa mwepesi kushuhudia dhidi ya wachawi, wazinzi, waapao kwa uongo, wanaopunja vibarua malipo yao, wanaowaonea wajane na yatima, na wanaowanyima wageni haki, lakini hawaniogopi mimi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
6 зане Аз Господь Бог ваш, и не изменяюся, и вы сынове Иаковли не удаляетеся от грех отец ваших.
“Mimi Bwana sibadiliki. Kwa hiyo ninyi, enyi uzao wa Yakobo, hamjaangamizwa.
7 Уклонистеся от законов Моих и не сохранисте: обратитеся ко Мне, и обращуся к вам, глаголет Господь Вседержитель. И ресте: в чесом обратимся?
Tangu wakati wa baba zenu mmegeukia mbali na amri zangu nanyi hamkuzishika. Nirudieni mimi, nami nitawarudia ninyi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Lakini mnauliza, ‘Tutarudi kwa namna gani?’
8 Еда обольстит человек Бога? Зане вы обольщаете Мя. И ресте: в чесом обольстихом Тя? Яко десятины и начатцы с вами суть.
“Je, mwanadamu atamwibia Mungu? Hata hivyo mnaniibia mimi. “Lakini mnauliza, ‘Tunakuibia kwa namna gani?’ “Mnaniibia zaka na dhabihu.
9 И взирающе вы взираете, и Мене вы обольщаете.
Mko chini ya laana, ninyi taifa lote, kwa sababu mnaniibia mimi.
10 Лето скончася, и внесосте вся плоды в сокровища, и будет расхищение Его в дому Его: обратитеся убо о сем, глаголет Господь Вседержитель: аще не отверзу вам хлябий небесных и излию вам благословение Мое, дондеже удовлитеся:
Leteni zaka kamili ghalani, ili kuwe na chakula katika nyumba yangu. Nijaribuni katika hili,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, “nanyi mwone kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni na kuwamwagieni baraka nyingi mpaka mkose nafasi ya kutosha.
11 и разделю вам в брашно, и не имам истлити вам плодов земных, и не изнеможет ваш виноград на селе, глаголет Господь Вседержитель:
Nami kwa ajili yenu nitamkemea yeye alaye, wala hataharibu mazao ya ardhi yenu, wala mzabibu wenu hautapukutisha matunda yake kabla ya wakati wake,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
12 и ублажат вы вси языцы, зане будете вы земля пожеланная, глаголет Господь Вседержитель.
“Ndipo mataifa yote yatawaita mliobarikiwa, kwa maana nchi yenu itakuwa ya kupendeza sana,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
13 Отяготисте на Мя словеса ваша, глаголет Господь (Вседержитель). И ресте: о чем клеветахом на Тя?
“Mmesema vitu vigumu dhidi yangu,” asema Bwana. “Hata hivyo mnauliza, ‘Tumesema nini dhidi yako?’
14 Ресте: суетен работаяй Богу, и что более, яко сохранихом хранения Его и яко идохом молитвенницы пред лицем Господа Вседержителя?
“Mmesema, ‘Ni bure kumtumikia Mungu. Tumepata faida gani kwa kushika maagizo yake na kwenda kama waombolezaji mbele za Bwana Mwenye Nguvu Zote?
15 И ныне мы блажим чуждих, и созидаются вси творящии беззаконная, сопротивишася Богови и спасошася.
Lakini sasa wenye kiburi wanabarikiwa. Hakika watenda mabaya wanastawi, pia hata wale wanaoshindana na Mungu ndio wanaosalimika.’”
16 Сия рекоша боящиися Господа, кийждо ко искреннему своему: и внят Господь, и услыша, и написа книгу памяти пред Собою боящымся Господа и благоговеющым имя Его.
Ndipo wale waliomcha Bwana wakasemezana wao kwa wao, naye Bwana akasikiliza na akasikia. Kitabu cha kumbukumbu kikaandikwa mbele yake kuhusu wale ambao walimcha Bwana na kuliheshimu jina lake.
17 И будут Ми, глаголет Господь Вседержитель, в день, егоже Аз творю в снабдение, и изберу я, имже образом избирает человек сына своего (добре) работающа ему.
“Nao watakuwa watu wangu,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, “katika siku ile nitakapowafanya watu kuwa hazina yangu. Nitawahurumia, kama vile kwa huruma mtu amhurumiavyo mwanawe anayemtumikia.
18 И обратитеся и увидите между праведным и между беззаконным, и между служащим Богови и не служащим Ему.
Kwa mara nyingine tena utaona tofauti kati ya wenye haki na waovu, kati ya wale wanaomtumikia Mungu na wale wasiomtumikia.