< Левит 3 >
1 Аще же жертва спасения дар его Господу, аще убо от говяд е принесет, аще мужеск пол или женск, непорочен да принесет и пред Господа:
“‘Kama sadaka ya mtu ni sadaka ya amani, naye akatoa ngʼombe kutoka kundi, akiwa dume au jike, atamleta mnyama asiye na dosari mbele za Bwana.
2 и возложит руце свои на главу дара, и да заколет и пред Господем у дверий скинии свидения: и да возлиют сынове Аарони жерцы кровь на олтарь всесожжений окрест,
Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka yake na kumchinja penye ingilio la Hema la Kukutania. Ndipo makuhani wana wa Aroni watanyunyiza damu yake pande zote za madhabahu.
3 и да принесут от жертвы спасения принос Господу, тук покрывающий утробу, и весь тук иже на утробе,
Kutoka kwenye hiyo sadaka ya amani ataleta sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto: mafuta yote ya mnyama yafunikayo sehemu za ndani, ama yanayoungana na hizo sehemu za ndani,
4 и обе почки, и тук иже на них и иже на стегнах, и препонку, яже на печени, с почками отимет:
figo zote pamoja na mafuta yote yanayozizunguka karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo atayaondoa pamoja na figo.
5 и да вознесут я сынове Аарони жерцы, на олтарь во всесожжения на дрова сущая на огни, яже на олтари: принос воня благовония Господу.
Kisha wana wa Aroni wataiteketeza juu ya madhabahu, juu ya ile sadaka ya kuteketezwa iliyoko juu ya kuni zinazowaka, kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
6 Аще же от овец дар его жертва спасения Господу, мужеск пол или женск, непорочен да принесет,
“‘Kama akitoa kondoo au mbuzi kutoka kundi kama sadaka ya amani kwa Bwana, atamtoa dume au jike asiye na dosari.
7 аше агнца принесет дар свой, да приведет его пред Господа,
Kama akimtoa mwana-kondoo, atamleta mbele za Bwana.
8 и да возложит руку на главу дара своего, и да заколет его у дверий скинии свидения: и да пролиют сынове Аарони жерцы кровь на олтарь окрест,
Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka yake, naye atamchinja mbele ya Hema la Kukutania. Kisha wana wa Aroni watanyunyiza damu yake kwenye madhabahu pande zote.
9 и да принесет от жертвы спасения принос Господу, тук и чресла чиста с лядвиями да отлучит и: и весь тук покрывающий утробу, и весь тук иже на утробе,
Kutoka kwenye hiyo sadaka ya amani ataleta dhabihu iliyotolewa kwa Bwana kwa moto: mafuta yake, mafuta yote ya mkia uliokatwa karibu na uti wa mgongo, mafuta yote yanayofunika sehemu za ndani au yale yanayounganika nazo,
10 и обе почки, и тук иже на них, иже на стегнах: и препонку, яже на печени, с почками отемь,
figo mbili pamoja na mafuta yanayozizunguka yaliyo karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo atayatoa pamoja na figo.
11 да вознесет жрец на олтарь: воня благоухания, принос Господви.
Kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu kama chakula, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
12 Аще же от козлов дар его Господу, да принесет пред Господа:
“‘Kama sadaka yake ni mbuzi, ataileta mbele za Bwana.
13 и возложит руце на главу его, и да заколют е пред Господем у дверий скинии свидения: и да пролиют сынове Аарони жерцы кровь на олтарь около:
Ataweka mkono wake juu ya kichwa chake na kumchinja mbele ya Hema la Kukutania. Kisha wana wa Aroni watanyunyiza damu yake kwenye madhabahu pande zote.
14 и да вознесет от него принос Господу тук покрывающий утробу, и весь тук иже на утробе,
Kutokana na ile sadaka anayotoa, atatoa sadaka hii kwa Bwana kwa moto: mafuta yote yanayofunika sehemu za ndani na yale yanayoungana nazo,
15 и обе почки, и весь тук, иже на них, иже на стегнах, и препонку, яже на печени, с почками отлучит:
figo zote mbili pamoja na mafuta yaliyo juu yake karibu na kiuno na yanayofunika ini, ambayo atayaondoa pamoja na figo.
16 и да вознесет жрец на олтарь, принос воня благовония Господу: весь тук Господу.
Kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu kama chakula, sadaka iliyotolewa kwa moto, harufu nzuri. Mafuta yote ya mnyama ni ya Bwana.
17 Законное в веки в роды вашя, во всяком обитании вашем: всякаго тука и всякия крове да не ясте.
“‘Hii ni kanuni ya kudumu kwa vizazi vijavyo, popote muishipo: Msile mafuta yoyote ya mnyama wala damu.’”