< Левит 13 >
1 И рече Господь к Моисею и Аарону, глаголя:
Yahweh akazungumza na Musa na Aroni, akasema,
2 человеку емуже аще будет на кожи плоти его струп знамения или блеск, и будет на кожи плоти его язва прокажения, да приведется ко Аарону жерцу или ко единому от сынов его жерцов:
Mtu yeyote anayeonekana na uvimbe au pele au doa ling'aalo juu ya ngozi ya mwili wake, na likawa limeambukizwa ugonjwa wa ngozi mwilini mwake, ni lazima aletwe kwa Aroni kuhani mkuu au kwa mmoja wa wanawe makuhani.
3 и узрит жрец язву на кожи плоти его, и влас в язве изменится в бело, и взор язвы умален от кожи плоти его, язва проказы есть: и узрит жрец, и осквернит его.
Naye kuhanai atachunguza ugonjwa huo kwenye ngozi ya mwili wake. Iwapo malaika zilizopo eneo lenye ugonjwa zimegeuka kuwa nyeupe, na iwapo ugonjwa umejitokeza juu ya ngozi, huo ni ugonjwa wa kuambukiza. Baada cha kuhani kumchunguza, atamtangaza kuwa ni najisi.
4 Аще же и блеск бел будет на кожи плотней его, и не менший будет взор его от кожи, и влас его не изменися во влас бел, и той есть темен, и отлучит жрец язву на седмь дний:
Iwapo lile doa ling'aalo katika ngozi yake ni jeupe, na kuonekana kwake halikwenda chini zaidi ya ngozi, na iwapo malaika za eneo lenye ugonjwa hazijabadilika kuwa nyeupe, naye kuhani atamtenga mgonjwa kwa siku saba.
5 и узрит жрец язву в день седмый, и се, язва пребывает пред ним, и не изменися язва на кожи, и отлучит его жрец на другия седмь дний:
Katika siku ya saba, huyo kuhani itambidi kumchunguza tena ili kuona kama katika maamzi yake huo ugonjwa siyo mbaya, na kama haujaenea kwenye ngozi. Iwapo haujaenea, basi, kuhani atamtenga kwa siku saba zaidi.
6 и узрит его жрец в седмый день вторицею, и се, язва потемне, и не изменися язва на кожи, и очистит его жрец: знамение бо есть: и измыв ризы своя, чист будет.
Naye kuhani atamchunga tena katika siku ya saba ili kuona kama ugonjwa ubepona na haujasambaa zaidi kwenye ngozi. kama haujasambaa, basi, kuhani atamtangaza kuwa yeye ni safi. Ni upele tu. Naye atafua nguo zake, na kisha yeye yu safi.
7 Аще же изменяющееся изменится знамение на кожи, повнегда видети его жерцу еже очистити его, и явится второе жерцу: и узрит его жрец, и се, изменися знамение в кожи,
Lakini endapo ule upele utakuwa umishasambaa kwenye ngozi baada ya kuwa amejionyesha kwa kuhani kwa ajili kusafishwa kwake, itambidi kujionyesha tena kwa kuhani.
8 и да осквернит его жрец: проказа бо есть.
Naye kuhani atamchunguza ilikuona kama huo upele umsambaa zaidi ndani ya ngozi. Na endapo utakuwa umesambaa, kisha kuhani atamtangaza kuwa najisi. Huo ni ugonjwa wa kuambukiza.
9 И язва прокажения аще будет на человеце, и приидет к жерцу:
Iwapo ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza umo kwa mtu fulani, naye mtu huyo yapasa aletwe kwa kuhan.
10 и узрит жрец, и се, струп бел на кожи, и сей изменил влас бел, и от здравыя плоти живыя в струпе:
Kuhani atamchunguza ili kuona kama kunauvimbe mweupe katika ngozi yake, endapo malaika zitakuwa zimebadilika kuwa nyeupe, au kumekuwa na nyama mbichi kwenye uvimbe.
11 проказа ветха есть на кожи плоти его, и осквернит его жрец и отлучит его, яко нечист есть.
Kama ipo, basi, huo ni ugonjwa sugu wa ngozi, naye kuhani atamtangaza kuwa najisi. Hatamtenga kwa kuwa yeye tayari ni najisi.
12 Аще же процветая процветет проказа на кожи, и покрыет прокажение всю кожу язвою, от главы да ногу его, по всему взору жерцову:
Iwapo huo ugonjwa unajitokeza na kupanuka zaidi kwenye ngozi, na kuifunika ngozi ya mtu kwa ugonjwa tangu kichwani pake hata miguuni, maadamu anajitokeza kwa kuhani,
13 и узрит жрец, и се, покрыло прокажение всю кожу плоти его, да очистит жрец язву: яко вся изменися в бело, чист есть.
naye kuhani atamchunguza ili kuona kama huo ugonjwa umeshaenea mwili wake wote. Ikiwa imetokeo hivyo, kuhani atamtangaza mtu huyo aliye na ugonjwa kuwa ni safi. Ikiwa amebadilika kuwa mweupe, huyo ni safi.
14 И в оньже день аще явится на нем плоть жива, осквернится:
Lakini ikiwa nyama mbichi imeonekana juu yake, atakuwa najisi.
15 и узрит жрец плоть здраву, и осквернит его плоть здрава, яко нечиста есть, прокажение есть.
Kuhani ataiangalia hiyo nyama mbichi na kumtanga kuwa najisi kwa sababu hiyo nyama mbichi ni najisi. Huo ni ugonjwa wa kuambukiza.
16 Аще же составится плоть здрава, и изменится в бело, и приидет к жерцу:
Lakini endapo hiyo nyama mbichi inageuka kuwa nyeupe tena, naye huyo mtu hana budi kwenda kwa kuhani.
17 и узрит жрец, и се, изменися язва в бело, и очистит жрец язву, чист есть.
Kuhani atamchunguza ili kuona kama hiyo nyama imebadilika kuwa nyeupe. Kama imekuwa hivyo naye kuhani atatangaza kwamba mtu huyo kuwa ni safi.
18 И тело аще будет на кожи его болячка гнойна, и исцелеет,
Mtu anapokuwa na jipu juu yangozi yake na limishapona,
19 и будет на месте болячки струп бел, или блеск белеющься или рдящься, и явится жерцу:
na mahali pa jipu pamekuwa na uvimbe au doa lenye kung'aa, wekundu unaochanganyikana na weupe, yapasa kuonyeshwa kwa kuhani.
20 и узрит жрец, и се, взор нижае кожи, и влас его изменися в бело, и осквернит его жрец, яко блеск прокажения есть, на болячке процвете.
Naye kuhani atalichunguza ili kuona kama linaonekana limekwenda chini ya ngozi, na kama hizo malaika zimebadilika kuwa nyeupe, kama ni hivyo, kuhani atamtangaza kuwa najisi. Huo ni ugonjwa wa kuambukiza, endapo utakuwa umezalishwa mahali lilipokuwa jipu hilo.
21 Аще же увидит жрец, и се, несть в нем влас бел, и не нижае есть от кожи плотския, и сей есть темен, и отлучит его жрец на седмь дний.
Lakini endapo kuhani atakuwa amelichunguza na haoni malaika nyeupe ndani yake, na kwamba iliko chini ya ngozi bali limefifia, kisha kuhani atamtenga kwa siku saba.
22 Аще ли разсыпанием разсыплется по кожи, и осквернит его жрец, блеск прокажения есть, на болячке процвете.
Kama linaenea kwa kupanuka kwenye ngozi, kisha kuhani atamtangaza kuwa najisi. Huo ni ugonjwa wa kuambukiza.
23 Аще ли на месте своем пребывает блеск и не разсыпается, струп болячки есть, и очистит его жрец.
Lakini kama hilo doa lenye kung'ara linabaki mahali pake na halijasambaa, basi hilo ni kovu la jipu, naye kuhani atamtangaza kuwa safi.
24 И плоть аще будет на кожи его жжение огнено, и будет на кожи его исцелевшее от жжения блещащееся бело или червлено или пробелующееся:
Ngozi inapoungua na nyama mbichi ya inamekuwa na wekundu uliochanganyika na weupe au doa jeupe,
25 и узрит его жрец, и се, пременися влас бел в блещащийся, и взор ему нижае от кожи, прокажение есть, во жжении процвете, и осквернит его жрец, язва прокажения есть.
kisha kuhani ataichunguza kuona kama malaika zilizoko kwenye doa hilo zimebadilika na kuwa nyeupe, na kama limeonekana kwenda chini zaidi ya ngozi, kama limekuwa hivyo, basi huo ni ugonjwa wa kuambukiza. Umejitokeza kwenye jeraha la moto, naye kuhani atamtangaza kuwa najisi. Huo ni ugonjwa wa kuambukiza.
26 Аще же увидит его жрец, и се, несть на блещащемся влас бел, и не нижае есть от кожи, само же темно, и отлучит его жрец на седмь дний:
Lakini endapo kuahani analichunguza na naona kwamba hakuna malaika nyeupe kwenye doa, na kwamba halikuenda chini ya ngozi bali linafifia, basi, kuhani atamtenga mtu huyo kwa siku saba.
27 и узрит его жрец в день седмый, и аще разсыпанием разсыплется по кожи, и осквернит его жрец: язва прокажения есть, бо гной процвете.
Kisha yapasa kuahani kumchunguza tena katika siku ya saba. Iwapo litakuwa limesambaa kwa upana kwenye ngozi, naye kuhani atamtangaza kuwa najisi. Huo ni ugojwa wa kuambukiza.
28 Аще же на месте пребудет блещание и не разсыплется по кожи, сие же темно есть, струп сожжения есть, да очистит его жрец: образ бо сожжения есть.
Iwapo hilo doa lisalia mahali pake na halitakuwa limesambaa kwenye ngozi bali limefifia, ni uvimbe tu kutokana na kuungua moto, naye kuhani atamtangaza kuwa safi, kwa kuwa siyo zaidi ya jeraha la kuungua.
29 Мужу же или жене, аще будет на них язва прокажения на главе или на браде,
Iwapo mwanaume au mwanamke ana ugonjwa wa kuambukiza kichwani au kidevuni pake,
30 и узрит жрец язву, и се, обличие ея глубочае кожи, в нейже влас желтуяся тонок, и осквернит его жрец: вред есть, прокажение главы или прокажение брады есть.
kisha kuhani atamchunguza mtu huyo kwa ajili ya ugonjwa wa kuambukiza ili kuona kama unakwenda ndani zaidi ya ngozi, na kama kuna nywele za manjano, nyembamba ndani yake. endapo zinaonekana, kisha kuhani atamtangaza kuwa najisi. Huo ni mwasho, ugonjwa wa kuambukiza kichwani au kidevuni.
31 И аще увидит жрец язву вреда, и се, не будет обличие нижае кожи, и влас желтуяся не будет в нем, да отлучит жрец язву вреда на седмь дний:
Iwapo kuhani anachunguza ugonjwa wa mwasho na anagundu kuwa hauko chini ya ngozi, na kama hakuna nywele nyeusi ndani yake, kisha kuhani atamtenga mtu huyo mwenye ugonjwa wa mwasho kwa siku saba.
32 и узрит жрец язву в день седмый, и се, не разсыпася вред, и влас желтуяся несть в нем, и обличие вреда несть нижае кожи:
Katika siku ya saba kuhani atauchunguza tena huo ugonjwa ili kuona kama umesambaa, Endapo hakuna malaika za manjano, na iwapo ugonjwa uko usawa ngozi tu,
33 и острижет кожу, вред же да не острижется, и отлучит жрец вред на седмь дний второе:
basi, yapasa mtu huyo kunyolewa., lakini sehemu yenye ugonjwa haitanyolewa, naye kuhani atamtenga mtu huyo mwenye ugonjwa wa mwasho kwa siku saba.
34 и узрит жрец вред в день седмый, и се, не разсыпася вред по кожи по острижении его, и обличие вреда несть нижае кожи, и очистит его жрец, и измыв ризы, чист будет.
Katika siku ya saba kuhani atauchunguza tena ugonjwa ili kuona kama umacha kusambaa ndani ya ngozi. Iwapo unaonekana kuwa hukwenda chini zaidi ya ngozi, kisha kuhani atamtangaza kuwa safi. Mtu huyo yapasa kufua nguo zake, na kisha atakuwa safi.
35 Аще же разсыпанием разсыплется вред по кожи по очищении его:
Lakini ikiwa ugonjwa wa mwasho umeenea kwa sehemu kubwa kwenye ngozi baada ya kuhani kutangaza kuwa alikuwa safi,
36 и узрит его жрец, и се, не разсыпася вред по кожи, да не присетит жрец о власе желтеющемся, яко нечист есть.
naye kuhani itabidi amchunguze tena. Iwapo ugonjwa utakuwa umesambaa katika ngozi, kuhani hahitajiki kutafuta nywele za manjano. Mtu huyo ni najisi.
37 Аще же пред ним будет на месте вред, и влас черн явится в нем, исцеле вред, чист есть, и очистит его жрец.
Lakini iwapo katika mtazamo wa kuhani inaonekana kuwa huo ugonjwa wa mwasho umekoma kusambaa, basi huo ugonjwa umekwisha pona. Yeye ni safi, naye kuhani atamtangaza kuwa safi.
38 Мужу же или жене, аще будут на кожи плоти его блещания блещащая белеющаяся:
Iwapo mwanume au mwanamke ana madoa juu ya ngozi,
39 и увидит жрец, и се, на кожи плоти его блещания и блещащая белеющаяся, лишай есть, процвете на кожи плоти его, чист есть.
kisha kuhani atamchunguza mtu huyo ili kuona kama hayo madoa ni meupe kwa kufiifia, ambalo ni kovu tu lililojitokeza kwenye ngozi. Yeye yu safi.
40 Аще же кому облезе глава, плешив есть, чист есть:
Iwapo nywele za mtu zimenyonyoka kichwani, yeye ni kipara lakini yu safi.
41 аще же спреди облезе глава, взлыс есть, чист есть:
Na iwapo nywele zake zimenyonyoka upande wa mbele wa kichwa chake, na iwapo paji lake la uso lina kipara, yeye yu safi.
42 аще же будет на плеши его или на взлысине его блеск бел или червленуяся, прокажение процветающее на плеши его или на взлысине его:
Lakini endapo kuna kidonda chenye wekundu uliochanganyika na weupe, juu ya kipara chake au paji lake la uso, huo ni ugonjwa wa kuambukiza uliojitokeza.
43 и увидит его жрец, и се, обличие блеска бело или червлено на плеши его или на взлысине его, яко обличие прокажения на кожи плоти его:
Naye kuhani atamchunguza ili kuona iwapo uvimbe wa eneo linaugua juu ya upara wake au paji lake la uso lina wekundu uliochanganyika na weupe, kama kuonekana kwa ugonjwa wa kuambukiza kwenye ngozi.
44 человек прокажен есть, осквернением осквернит его жрец, на главе его блеск его.
Ikionekana hivyo, basi huyo ana ugonjwa wa kuambukiza naye ni najisi. Hakika kuhani atamtangaza kuwa najisi kwa sababu ya ugonjwa wake kichwani pake.
45 И прокажен, на немже есть язва, ризы его да будут раздраны, и глава его не покровена, и около уст своих да обвиется, и нечист прозовется:
Mtu aliye na ugojwa wa kuambukiza atavaa nguo zilizochanika, ni lazima nywele zake ziachwe wazi, na yampasa kufunika uso wake mpaka puani na kupiga kelele, 'Najisi, najisi.'
46 вся дни, в няже будет на нем язва, нечист сый, нечист будет: отлучен да седит, вне полка да будет ему пребывание.
Naye atakuwa najisi siku zote za ugonjwa wake wa kuambukiza. Kwa sababu anao ugonjwa unaosambaa, yapasa kuishi peke yake nje ya kambi.
47 И риза аще будет на ней язва прокажения, на ризе сукняне, или на изгребийней,
Kuna wakati fulani vazi la mtu hupata ukungu juu yake. Laweza kuwa vazi, ama la sufu au kitani,
48 или на прядене, или на кроках, или на льнех, или на волне, или на кожи, или на всякой кожи деланей,
au kitu chochote kilichosukwa au kufumwa kutokana na sufu au kitani, au ngozi au kitu chochote kilichotengenezwa kwa ngozi.
49 и явится язва зелена или червленуяся на кожи, или на ризе, или на пряденех, или на кроках, или на всяком деле кожанем, язва прокажения есть, и покажет жерцу:
Iwapo sehemu iliyochafuliwa ina rangi ya kijani au nyekundu katika vazi, ngozi, kifaa kilichosukwa au kufumwa, basi huo ni ukungu uanasambaa, ni lazima uonyeshwe kwa kuhani.
50 и увидит жрец язву, и отлучит жрец язву на седмь дний.
Yapasa kuhani akichunguze hicho kifaa kwa ajili ya ukungu; ni lazima akitenge kitu chochote kilicho na ukungu kwa siku saba.
51 И да увидит жрец язву в день седмый: аще же разсыпася язва по ризе, или по прядене, или по кроках, или по кожи, по всему елика творятся кожы в делании, прокажение исто есть язва, нечист есть:
Naye atauchunguza tena huo ukungu katika siku ya saba. Endapo utakuwa umesambaa katika kifaa hicho, basi ni wazi kwamba huo ni ukungu wenye kuangamiza, na hicho kifaa ni najisi.
52 да сожжет ризу, или прядения, или кроки, или на волне, или на льне, или на всяком сосуде кожане, на немже аще будет язва: понеже прокажение исто есть, на огни да сожжется.
Na mwenye kukimiliki atalazimika kukichoma na kukiteketeza kabisa hicho kifaa kilichoonekana na ukungu ndani yake, haijalishi kiwe ni kifaa cha aina gani, kwani huo ukungu unaweza kusababisha ugonjwa.
53 Аще ли узрит жрец, и не разсыплется язва по ризе, или по прядене, или по кроках, или по всякому сосуду кожану:
Iwapo kuhani anakichunguza hicho kifaa na kuona kwamba ukungu haujaenea kwenye vazi au chombo kilichosukwa au kusokotwa kutokana na sufu, kitani au ngozi,
54 и повелит жрец, и измыет, на немже будет язва, и да отлучит жрец язву на другия седмь дний:
basi atawaagiza wakisafishe hicho kifaa kilichopatikana na ukungu, naye yampasa kukitenga kwa siku saba zaidi.
55 и увидит жрец по измытии его язву, и аще не изменила язва лица своего, и язва не разсыпася, нечисто есть, на огни да сожжется: утвердися бо на ризе, или на прядене, или на кроках.
Kisha kuhani atakichunguza tena hicho kifaa chenye ukungu baada ya kuwa kimesafinshwa. Kama ukungu haukubadilika rangi yake, hata kama haukusambaa, kifaa hicho ni najisi. Yapasa kichomwe, haijalishi ni wapi ukungu huo utakuwa umekichafua.
56 И аще увидит жрец, и будет темна язва по испрании ея, да отторгнет е от ризы, или от прядена, или от крок, или от кожи.
Iwapo kuhani anakichunguza hicho kifaa, na kama ukungu umefifia baada ya kuwa umeoshwa, basi atakirarua kile kipande kilichochaufuliwa kutoka kwenye vazi au kutoka kwenye ngozi, au kutoka kwenye chombo kilichosukwa au kusokotwa.
57 И аще явится еще на ризе или на прядене, или на кроках, или на всяком сосуде кожане, прокажение процветающее есть, на огни да сожжется, на немже есть язва.
Ikiwa ukungu unazidi kuonekana katika vazi, ama katika chombo kilichosukwa au kufumwa, au katika kitu chochote kilichotengenezwa kwa ngozi, basi, ukungu utakuwa unasambaa. Kifaa chochote kilicho na ukungu ni lazima kichomwe.
58 И риза, или прядено, или кроки, или всяк сосуд кожан, еже исперется, и отступит от него язва, и измыется второе, и чисто будет.
Vazi au kitu chochote kilichosukwa au kufumwa kutokana na sufu, au kitani, au ngozi au kitu chochote kilichotengenezwa kwa ngozi—iwapo unakisafisha kifaa nao ukungu ukawa umetoka, nacho kifaa lazima kisafishwe mara ya pili, kisha kitakuwa safi.
59 Сей закон язве прокажения ризы сукняны, или изгребийны, или прядены, или куделныя, или всякаго сосуда кожана, во еже очистити е, или осквернити е.
Hii ndiyo sheria ihusuyo ukungu katika vazi la sufu au kitani, au kwenye kitu chochote kilichosukwa au kufumwa kutokana na sufu, au kitani, au kitu chochote kilichotengenewa kwa ngozi, ili kwamba mweze kuvitangaza kuwa safi au najisi.