< Левит 11 >
1 И рече Господь к Моисею и Аарону, глаголя:
Yahweh akazungumza na Musa na Aroni, akasema,
2 рцыте сыном Израилевым, глаголюще: сии скоти, ихже имате ясти от всех скотов, иже на земли:
“Sungumzeni na watu wa Israeli muwaambie, 'Hivi ndivyo viumbe vyenye uhai ambavyo mwaweza kula miongoni mwa wanyama walioko juu ya nchi.
3 всяк скот раздвояющь копыто и пазнокти имеющь на двое, и отрыгаяй жвание в скотех, сия да ясте:
Mnaweza kula mnyama yeyote aliye na kwato zenye kugawanyika na ambaye pia hucheua.
4 токмо от сих да не снесте от отрыгающих жвание и от раздвояющих копыта и делящих пазнокти: велблюда, яко сей износит жвание, но пазноктей не делит на двое, нечист сей вам:
Hata hivyo, kuna baadhi ya wanyama ambao ama hawacheui au hana kwato zilizogawanyika, nanyi msiwale hao, wanyama kama ngamia, kwa sababu yeye hucheua lakini hana kwato zilizogawanyika. Kwa hiyo ngamia ni najisi kwenu.
5 и хирогриля, яко износит жвание, а пазноктей не делит, нечист сей вам:
Pimbi pia: kwa sababu yeye hucheua lakini hana kwato zilizogawanyika mara mbili, huyo pia ni najisi kwenu.
6 и заяца, иже отрыгает жвание, но пазноктей не делит на двое, нечист сей вам:
Na sungura pia: kwa sababu yeye hucheua lakini hana kwato zilizogawanyika mara mbili, huyu naye ni najisi kwenu.
7 и свинии, яко делит пазнокти на двое и копыто раздвояет, но не отрыгает жвания, нечиста сия вам:
Na nguruwe pia: ingawaje yeye anazo kwato zilizogawanyika lakini hacheui, kwa hiyo yeye ni najisi kwenu.
8 от мяс их да не ясте и мертвечине их да не прикасаетеся, нечиста сия вам.
Msile aina yoyote ya nyama yao, wala msiiguse mizoga yao. Hao ni najisi kwenu.
9 И сия да ясте от всех, яже в водах: вся, имже суть перия и чешуя в водах, и в морях и в езерах, сия да ясте:
Nao wanyama waishio majini mnaoweza kuwala ni wale wote walio na mapezi na magamba, iwe waliomo baharini au mitoni.
10 и всем, Имже несть перие ни чешуи в водах, и в морях и в езерах, от всех, яже износят воды, и всяка душа живущая в воде, скверна есть, и скверна да будут вам:
Lakini viumbe wote hai wasio na mapezi na magamba waliomo baharini au mitoni, pamoja na wale waendao majini na viumbe hai waliomo majini —watakuwa chukizo kwenu.
11 от мяс их да не ядите и мертвечины их гнушайтеся:
Kwa kuwa watakuwa chukizo, msile nyama yao, pia mizoga yao sharti itakuwa chukizo.
12 и вся, имже несть перия и чешуи, иже в водах, скверна сия суть вам.
Chochote kisichokuwa na mapezi au magamba kilichomo majini ni lazima kiwe chukizo kwenu.
13 И сих гнушайтеся от птиц, и да не ясте их, гнусни суть: орла и грифа и морскаго орла,
Nao ndege mtakaowachukia na msiopaswa kuwala ni hawa wafuatao: tai, furukombe, kipungu,
14 и неясыти и иктина и подобных сим:
mwewe mwekundu, aina yoyote ya kipanga,
15 и струфа и совы, и сухолапля и подобных им:
kila aina ya kunguru,
16 и всякаго врана и подобных ему: и ястреба и подобных ему:
kiruka-njia, kipasuasanda, Shakwe, na aina yoyote ya mwewe.
17 и врана нощнаго и лилика и ивина,
Ni lazima pia bundi mdogo na bundi mkubwa muwaone kuwa chukizo, mnandi,
18 и порфириона и пелекана и лебедя,
bundi mweupe na mwari,
19 и еродиа и харадриона и подобных ему: и вдода и нощнаго нетопыря.
korongo na ina zote za koikoi, huduhudi na popo pia.
20 И вся гады птичия, иже ходят на четырех, мерзость есть вам:
Wadudu wote wenye mabawa wanatembea kwa miguu minne kwenu ni machukizo.
21 но сия да ясте от всех гад птичных, иже ходят четвероножны, иже имут голени выше плесну своею, скакати ими по земли:
Lakini manaweza kula wadudu wenye mabawa wanaotembea kwa miguu minne ya kurukia ardhini yenye vifundo.
22 и сия да ясте от сих: вруха и подобная ему, и аттака и подобная ему, офиомаха и еже подобно к нему, и акриду и подобная ей:
Na manaweza kula kula aina zote za nzige, senene, parare, au panzi.
23 и всяк гад от птиц, имже суть четыри ноги, мерзость есть вам, и в сих да не осквернитеся:
Lakini wadudu wote warukao wenye miguu minne ni chulkizo kwenu.
24 всяк прикасаяйся мертвечине их нечист будет до вечера:
Nanyi mtakuwa najisi hata jioni kutokana na wanyama hawa endapo mtagusa mizogo yao.
25 и всяк вземляй мертвечину их да измыет ризы своя и нечист будет до вечера.
Na yeyote atakayeokota mojawapo wa mizoga yao ni lazima atazifua ngua zake naye atakuwa najisi hata jioni.
26 Во всех скотех, иже раздвояет копыто и пазнокти имеет, а жвания не отрыгает, нечиста да будут вам: всяк прикасаяйся мертвечине их нечист будет даже до вечера:
Mnyama yeyote ambaye anazo kwato ziliachana ambazo hazikugawanyika kabisa au hacheui huyo ni najisi kwenu. Yeyote awagusaye atakuwa najisi.
27 и всяк иже ходит на лапах, во всех зверех, иже ходят на четырех, нечиста будут вам: всяк прикасаяйся мертвечине их нечист будет до вечера:
Mnyama yeyote anayetembea kwa vitanga vyake miongoni mwa wanyama waendao kwa miguu yote minne ni najisi kwenu. Yeyote agusaye mzoga kama huo atakuwa najisi hata jioni.
28 и вземляй мертвечину их да исперет ризы своя и нечист будет до вечера: нечиста сия будут вам.
Na yeyote aokotaye mzoga kama huo ni zazima atazifua nguo zake na kuwa najisi hata jioni. Wanyama hawa watakuwa najisi kwenu.
29 И сия вам нечиста от гад плежущих по земли: ласица и мыш и крокодил земный,
Kuhusiana na wanyama wataambaao juu ya ardhi, hawa ndiyo walio najisi kwenu: kicheche, panya, aina zote za mijusi mikubwa, guruguru,
30 мигали и хамелеон, и халавотис и ящер и кроторыя:
kenge, mijusi ya ukutani, goromoe, na kinyonga.
31 сии нечисти вам от всех гад плежущих по земли: всяк прикасаяйся мертвечине их нечист будет до вечера.
Wanyama hawa wote ambao hutambaa, hawa ndiyo watakuwa najisi kwenu. Yeyote awagusaye atakuwa njisi hata jioni.
32 И всяко, в неже аше впадет от них нечто от мертвечины их, нечист будет всяк сосуд древян, или риза, или кожа, или вретище: всякий сосуд, в немже творится дело, в воде погрузится и нечист будет до вечера, и по сих чист будет:
Na iwapo mmoja wao anakufa na kuanguka juu ya chombo, chombo hicho kitakuwa najisi, ama kiwe kimetengenezwa kwa mbao, nguo, ngozi, au gunia. Kiwe chombo cha namna gani na kiwe kwa matumizi gani, ni lazima kitalowekwa katika maji nacho kitakuwa najisi hata jio. Kisha kitakuwa safi.
33 и всяк сосуд глинян, в оньже аще впадет от сих внутрь, елика суть в нем, нечиста будут, и сосуд да разбиется.
Kwa hiyo kila chungu ambacho mnyama najisi atakiangukia juu yake au ndani yake, chochote kilichomo kwenye chungu hicho kitakuwa najisi, na ni lazima mtakivunja chungu hicho.
34 И всяка снедь юже ясте, на нюже аще возлиется вода, нечиста будет вам: и всякое питие, еже пиете во всяком сосуде, нечисто будет (вам):
Vyakula vyote ambavyo ni safi na kilichuhusiwa kuliwa, lakini kikaingiwa na maji kutoka kwenye chungu najisi kilichoanguka, nacho kitakuwa najisi.
35 и все, еже аще впадет в не от мертвечины их, нечисто будет: пещи и огнища да сокрушатся, нечиста сия суть и нечиста будут вам.
Na kitu chochote kinachoweza kunywewa kutoka kwenye chungu kama hicho kitakuwa najisi. Kila kitu kitakachoangukiwa juu yake na kipande cha mzoga wa mnyama najisi nacho kitakuwa najisi, ama liwe ni jiko au vyungu vya kupikia. Ni najisi na ni lazima kiwe najisi kwenu.
36 Кроме источник водных и поток, и собраний водных, будут чисти: а иже прикасается мертвечинам их, нечист будет.
Chemchemi au kisima cha maji ya kunywa yanapokusanyika patabaki kuwa safi iwapo kiumbe najisi kama hicho kitaangukia humo. Lakini ikiwa yeyote anaugusa mzoga wa mnyama aliye najisi uliomo ndani ya maji, yeye atakuwa najisi.
37 Аще же впадет от мертвечины их на всяко семя семянное, еже сеется, чисто будет:
Iwapo sehehemu yoyote ya mzoga wa mnyama aliyenajisi inaangukia juu ya mbegu zozote zilizo kwa ajili ya kupanda. Mbegu hizo zitakuwa bado zingali safi.
38 аще же возлиется вода на всяко семя, и впадет от мертвечины их на не, нечисто будет вам.
Lakini kama maji yanawekwa juu ya mbegu, na kama sehemu ya mzoga unaangukia juu yake, nazo zitakuwa najisi kwenu.
39 Аще же умрет от скота, егоже вам ясти, прикасаяйся мертвечине его, нечист будет до вечера:
Iwapo mnyama yeyote awezaye kuliwa anakufa, naye yeyote amgusaye atakuwa najisi hata jioni.
40 и ядый от мертвечин сих да исперет ризы своя и нечист будет до вечера: и вземляй мертвечину их да измыет ризы своя и измыется водою, и нечист будет до вечера.
Na yeyote alaye chochote cha mzoga huo atalazimika kufua nguo zake naye atakuwa anjisi hata jioni. Na yeyote aokotaye mzoga kama huo atafua nguo zake na kuwa najisi hata jioni.
41 И всяк гад плежущий по земли мерзость вам есть сие, да не снестся.
Kila mnyama atambaaye juu ya ardhi atakuwa chukizo; hatakuwa wa kuliwa.
42 И всяко ходящее на чреве, и всяко ходящее на четырех всегда, и (всяко) многоножное во всех гадех, иже плежут по земли, да не снесте е, яко мерзость вам есть:
Chochote kitambaacho kwa kujivuta juu ya tumbo lake, na chochote kitembeacho kwa miguu yake yote minne, au chochote kilicho na miguu mingi—wanyama wote ambao hutambaa juu ya nchi, hawa msiwale, kwa sababu watakuwa machukizo.
43 и да не омерзите душ ваших во всех гадех плежущих по земли, и да не осквернитеся ими, и да не будете нечисти в них,
Msijinajisi wenyewe kwa kiumbe chochote nnajisi kitaambacho; msijinasi wenyewe kwavyo, ili kwamba msije mkachafuliwa navyo.
44 яко Аз есмь Господь Бог ваш: и да освятитеся и будете святи, яко свят есмь Аз Господь Бог ваш: и да не оскверните душ ваших во всех гадех движущихся по земли,
Kwa kuwa Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu. Nanyi lazima muwe watakatifu, kwa hiyo na iweni watakatifu, kwa sababu Mimi ni mtakatifu. Haiwapasi kujichafua kwa aina yoyote ya kiendacho juu ya nchi.
45 яко Аз есмь Господь, изведый вас из земли Египетския, да буду вам Бог, и будете святи, яко свят есмь Аз Господь.
Kwa kuwa Mimi ndimi Yahweh, aliyewaleta ninyi kutoka nchi ya Misri, ili niwe Mungu wenu. Kwa hiyo lazima muwe watakatifu, kwa kuwa Mimi ni mtakatifu.
46 Сей закон о скотех и о птицах, и всякой души движущейся в водах и всякой души пресмыкающейся по земли,
Hii ndiyo sheria kuhusu wanyama, ndege, kila kiumbe hai kiendacho majini, na ya kila kiumbe kitambaacho juu ya nchi,
47 разлучити между нечистыми и между чистыми, и научити сыны Израилевы между оживляющими ядомая и между оживляющими не ядомая.
kwa jili ya kilie kinachopaswa kutofautishwa kati ya kilicho najisi na kilicho safi, na kati ya vitu vilivyokufa na vilivyo hai ambavyo vyaweza kuliwa na vitu vyenye uihai visivyoweza kuliwa.”