< Плач Иеремии 5 >
1 Молитва Иеремии пророка. Помяни, Господи, что бысть нам: призри и виждь укоризну нашу:
Kumbuka, Ee Bwana, yaliyotupata, tazama, nawe uione aibu yetu.
2 достояние наше обратися к чуждим и домы нашя ко иноплеменником:
Urithi wetu umegeuziwa kwa wageni, na nyumba zetu kwa wageni.
3 сири быхом, несть отца, матери нашя яко вдовы.
Tumekuwa yatima wasio na baba, mama zetu wamekuwa kama wajane.
4 Воду нашу за сребро пихом, дрова наша за цену куповахом:
Ni lazima tununue maji tunayokunywa, kuni zetu zapatikana tu kwa kununua.
5 на выя нашя гоними быхом, трудихомся, не почихом.
Wanaotufuatilia wapo kwenye visigino vyetu, tumechoka na hakuna pumziko.
6 Египет даде руку, Ассур в насыщение их.
Tumejitolea kwa Misri na Ashuru tupate chakula cha kutosha.
7 Отцы наши согрешиша, и несть их, мы же беззакония их подяхом.
Baba zetu walitenda dhambi na hawapo tena, na sisi tunachukua adhabu yao.
8 Раби обладаша нами, избавляющаго несть от руку их.
Watumwa wanatutawala na hakuna wa kutuokoa mikononi yao.
9 В душах наших носихом хлеб наш, от лица меча в пустыни.
Tunapata chakula chetu kwa kuhatarisha maisha yetu kwa sababu ya upanga jangwani.
10 Кожа наша аки пещь обгоре, разседошася от лица бурей глада.
Ngozi yetu ina joto kama tanuru, kwa sababu ya fadhaa itokanayo na njaa.
11 Жен в Сионе смириша, девиц во градех Иудиных.
Wanawake wametendwa jeuri katika Sayuni, na mabikira katika miji ya Yuda.
12 Князи в руках их повешени быша, старейшины не прославишася.
Wakuu wametungikwa juu kwa mikono yao, wazee hawapewi heshima.
13 Избраннии плачь подяша, и юноши в кладе изнемогоша.
Vijana wanataabika kwenye mawe ya kusagia, wavulana wanayumbayumba chini ya mizigo ya kuni.
14 И старцы от врат оскудеша, избраннии от песней своих умолкоша.
Wazee wameondoka langoni la mji, vijana wameacha kuimba nyimbo zao.
15 Разсыпася радость сердец наших, обратися в плачь лик наш,
Furaha imeondoka mioyoni mwetu, kucheza kwetu kumegeuka maombolezo.
16 спаде венец со главы нашея: горе нам, яко согрешихом.
Taji imeanguka kutoka kichwani petu. Ole wetu, kwa maana tumetenda dhambi!
17 О сем смутися сердце наше, о сем померкнуша очи наши.
Kwa sababu hiyo, mioyo yetu inazimia, kwa sababu ya hayo, macho yetu yamefifia,
18 На горе Сионе, яко погибе, лисицы ходиша.
kwa ajili ya Mlima Sayuni, ambao unakaa ukiwa, nao mbweha wanatembea juu yake.
19 Ты же, Господи, во веки вселишися, престол Твой в род и род.
Wewe, Ee Bwana unatawala milele, kiti chako cha enzi chadumu kizazi hadi kizazi.
20 Вскую во веки забываеши нас, оставиши ли нас в продолжение дний?
Kwa nini watusahau siku zote? Kwa nini umetuacha kwa muda mrefu?
21 Обрати ны, Господи, к Тебе, и обратимся, и вознови дни нашя якоже прежде.
Turudishe kwako mwenyewe, Ee Bwana, ili tupate kurudi. Zifanye mpya siku zetu kama siku za kale,
22 Яко отревая отринул еси нас, разгневался еси на ны зело.
isipokuwa uwe umetukataa kabisa na umetukasirikia pasipo kipimo.