< Плач Иеремии 3 >

1 Алеф. Аз муж видя нищету (мою) в жезле ярости Его на мя:
Mimi ni mwanaume nilyeona maangaiko chini ya gongo la hasira ya Yahweh.
2 поят мя и отведе мя во тму, а не во свет.
Amenifukuza na kunisababisha kutembea kwenye giza kuliko kwenye nuru.
3 Обаче на мя обрати руку Свою весь день,
Hakika amenigeuzia mkono wake dhidi yangu tena na tena, siku yote.
4 беф. Обетши плоть мою и кожу мою, кости моя сокруши:
Amefanya mwili wangu na ngozi yangu kufifia; amevunja mifupa yangu.
5 согради на мя и объя главу мою и утруди,
Amejenga vifusi vya udogo dhidi yangu, na kunizingira na uchungu na ugumu.
6 в темных посади мя, якоже мертвыя века:
Amefanya ni ishi sehemu za giza, kama hao walio kufa zamani.
7 гимель. Согради на мя, и не изыду, отяготи оковы моя,
Amejenga ukuta kunizunguka na siwezi kutoroka. Amefanya minyororo yangu mizito
8 и егда воскричу и возопию, загради молитву мою:
na japo nina ita na kulilia msaada, anazima maombi yangu.
9 возгради пути моя, загради стези моя, возмяте.
Ameziba njia yangu kwa ukuta wa mawe ya kuchonga; amefanya njia yangu mbaya.
10 Далеф. Бысть яко медведь ловяй, (приседяй ми) яко лев в сокровенных,
Yeye ni kama dubu anasubiri kunishambulia, simba katika maficho;
11 гна отступившаго, и упокои мя, положи мя погибша:
amegeuza pembeni njia zangu, amenifanya ukiwa.
12 напряже лук Свои, и постави мя яко знамение на стреляние,
Amepindisha upinde wake na kunifanya mimi kama lengo la mshale wake.
13 ге. Пусти в лядвия моя стрелы тула Своего.
Ametoboa maini yangu kwa mishale ya mfuko wake.
14 Бых в смех всем людем моим, песнь их весь день.
Nilikuwa kichekesho kwa watu wangu wote, kielelezo cha dhihaka yao siku nzima.
15 Насыти мя горести, напои мя желчи
Amenijaza kwa uchungu na kunilazimisha kunywa maji machungu.
16 вав. И изя каменем зубы моя, напита мя пепелом
Alivunja meno yangu na kokoto; amenisukuma chini kwenye fumbi.
17 и отрину от мира душу мою. Забых благоты
Nafsi yangu imenyimwa amani; nimesahau furaha ni nini.
18 и рех: погибе победа моя и надежда моя от Господа.
Hivyo na sema, “Ustahimilivu wangu umeangamia na pia tumaini langu kwa Yahweh.”
19 Заин. Помяни нищету мою и гонение мое.
Kumbuka mateso yangu na kuangaika kwangu, maji machungu na uchungu.
20 Горесть и желчь мою помяну, и стужит во мне душа моя.
Ninaendelea kukumbuka na nimeinama ndani yangu.
21 Сия положу в сердцы моем, сего ради потерплю.
Lakini ni vuta hili akilini mwangu na hivyo nina matumaini:
22 Иф. Милость Господня, яко не остави мене, не скончашася бо щедроты Его: пребываяй во утриих, помилуй, Господи, яко не погибохом, не скончашася бо щедроты Твоя.
Upendo dhabiti wa Yahweh haukomi na huruma zake haziishi,
23 Новая во утриих, многа есть вера Твоя.
ni mpya kila asubui; uaminifu wako ni mkubwa.
24 Часть моя Господь, рече душа моя: сего ради пожду Его.
“Yahweh ni urithi wangu,” Nilisema, hivyo nitamtumainia.
25 Теф. Благ Господь надеющымся Нань:
Yahweh ni mwema kwao wanao msubiri, kwa anaye mtafuta.
26 души ищущей Его благо (есть), и надеющейся с молчанием спасения Божия.
Ni vizuri kusubiri taratibu kwa uwokovu wa Yahweh.
27 Благо есть мужу, егда возмет ярем в юности своей:
Ni vizuri kwa mtu kubeba nira katika ujana.
28 иод. Сядет на едине и умолкнет, яко воздвигну на ся:
Acha aketi peke yake katika utulivu, inapo kuwa imewekwa juu yake.
29 положит во прахе уста своя, негли како будет надежда:
Acha aeke mdomo wake kwenye vumbi - kunaweza bado kuwa na matumaini.
30 подаст ланиту свою биющему, насытится укоризн.
Acha atoa shavu lake kwa yeye anaye mpiga, na ajazwe tele kwa aibu.
31 Каф. Яко не во век отринет Господь,
Kwa kuwa Bwana hatatukataa milele,
32 яко смиривый помилует по множеству милости Своея,
lakini japo anatia uzuni, ata kuwa na huruma kwa kadiri ya mwingi wa upendo wake dhabiti.
33 не отрину от сердца Своего и смири сыны мужеския.
Kwa kuwa haadhibu kutoka moyoni mwake au kutesa watoto wa mwanadamu.
34 Ламед. Еже смирити под нозе его вся узники земныя,
Kukanyaga chini ya mguu wafungwa wote wa dunia,
35 еже уклонити суд мужа пред лицем Вышняго,
kumnyima haki mtu mbele ya uwepo wa Aliye Juu,
36 осудити человека, внегда судитися ему, Господь не рече.
mkunyima haki mtu - Bwana hataidhinisha vitu kama hivyo!
37 Мем. Кто есть той, иже рече, и быти, Господу не повелевшу?
Ni nani aliye zungumza na ikatimia, kama sio Bwana kutamka?
38 Из уст Вышняго не изыдет зло и добро.
Sio kutoka mdomoni mwa Aliye Juu majanga na mazuri yanakuja?
39 Что возропщет человек живущь, муж о гресе своем?
Mtu aliye hai anawezaje kulalamika? Mtu anawezaje kulalamika kwa adhabu ya dhambi zake?
40 Нун. Изыскася путь наш и испытася, и обратимся ко Господу.
Natujichunguze njia zetu na kuzijaribu, na tumrudie Yahweh.
41 Воздвигнем сердца наша с руками к Богу высокому на небеси.
Na tunyanyue mioyo yetu na mikono yetu kwa Yahweh mbinguni:
42 Мы согрешихом и нечествовахом, сего ради не помиловал еси:
“Tumekosea na kuasi, na haujasamehe.
43 самех. Покрыл еси яростию и отгнал еси нас, убил и не пощадел еси:
Umejifunika na hasira na kutukimbiza, umeua na haujanusuru.
44 покрылся еси облаком, да не дойдет к Тебе молитва,
Umejifunika na wingu ili kwamba kusiwe na ombi linaloweza kupita.
45 сомжити очи мои и отринути, положил еси нас посреде людий.
Umetufanya kama uchafu na taka miongoni mwa mataifa.
46 Аин. Отверзоша на ны уста своя вси врази наши.
Maadui wetu wote wametulaani,
47 Страх и ужас бысть нам, надмение и сокрушение:
wasiwasi na shimo limetujia, maafa na uharibifu.
48 исходища водная излиет око мое о сокрушении дщере людий моих.
Macho yangu yanatiririka na miferiji ya machozi kwasababu ya watu wangu.
49 Фи. Око мое погрязну: и не умолкну, еже не быти ослаблению,
Macho yangu yatatoa machozi pasipo kikomo; pasipo hauweni,
50 дондеже приклонится и увидит Господь с небесе.
mpaka atakapo tazama chini na Yahweh ataona kutoka mbinguni.
51 Око мое закрывается о души моей, паче всех дщерей града.
Macho yangu yana ni sababishia uzuni kwasababu ya mabinti wa mji wangu.
52 Цади. Ловяще уловиша мя яко врабия врази мои туне:
Nimewindwa kama ndege hao walio kuwa maadui zangu; wameniwinda pasipo sababu.
53 умориша в рове жизнь мою и возложиша на мя камень.
Wamenitupa kwenye shimo na wakanitupia jiwe,
54 Возлияся вода выше главы моея: рех: отриновен есмь.
na maji yaka mwagika juu ya kichwa changu. Nilisema, “Nimekatwa mbali!”
55 Коф. Призвах имя Твое, Господи, из рова преисподняго:
Nililiita jna lako, Yahweh, kutoka kina cha shimo.
56 глас мой услышал еси: не покрый ушес Твоих на мольбу мою:
Ulisikia sauti yangu. Ulisikia sauti yangu nilipo sema, “Usifunge sikio lako kwa kilio changu cha msaada.”
57 на помощь мою приближился еси, в день, в оньже призвах Тя, рекл ми еси: не бойся.
Ulikuja karibu siku niliyo kuiita; ulisema, “Usiogope”
58 Реш. Судил еси, Господи, прю души моея, избавил еси жизнь мою:
Bwana, ulitetea kesi yangu, uliokoa maisha yangu!
59 видел еси, Господи, смятения моя, разсудил еси суд мой:
Yahweh, umeona mabaya waliyo ni fanyia, hukumu kesi yangu.
60 веси все отмщение их и вся помышления их на мя.
Umeona matusi yao, mipango yao yote dhidi yangu -
61 Шин. Слышал еси укоризны их, вся советы их на мя,
Umesikia dhihaka yao, Yahweh, na mipango yao kunihusu.
62 устне востающих на мя и поучение их на мя весь день,
Midomo ya hao wanao inuka kinyume changu, na mashtaka yao, inakuja dhidi yangu siku nzima.
63 седение их и востание их: призри на очи их.
Ngalia jinsi wanavyo keti na kuinuka; wana nidhihaki na nyimbo zao.
64 Фав. Воздаси им, Господи, воздаяние по делом руку их:
Walipize, Yahweh, kwa kadiri ya waliyo fanya.
65 воздаси им заступление, сердца моего труд.
Utaacha mioyo yao bila lawama! Hukumu yako iwe juu yao!
66 Ты их проженеши во гневе и потребиши их под небесем, Господи.
Una wakimbiza kwa hasira na kuwaharibu nchini ya mbingu, Yahweh!

< Плач Иеремии 3 >