< Книга Судей израилевых 4 >

1 И приложиша сынове Израилевы сотворити злое пред Господем: и Аод умре.
Baada ya Ehudi kufa, Waisraeli wakafanya tena maovu machoni pa Bwana.
2 И отдаде их Господь в руку Иавина царя Ханаанска, иже царствова во Асоре. И воевода силы его Сисара, и той живяше во Арисофе языков.
Hivyo Bwana akawatia mikononi mwa Yabini, mfalme wa Kanaani, aliyetawala huko Hazori. Jemadari wa jeshi lake alikuwa Sisera, aliyeishi huko Haroshethi-Hagoyimu
3 И возопиша сынове Израилевы ко Господу, яко девять сот колесниц железных бяше ему: и той озлоби Израиля зело лет двадесять.
Kwa kuwa Sisera alikuwa na magari ya chuma yapatayo 900, naye alikuwa amewatesa Waisraeli kwa ukatili kwa muda wa miaka ishirini, Waisraeli wakamlilia Bwana wakaomba msaada.
4 И Деввора, жена пророчица, жена Лафидофова, сия судяше Израилю в то время:
Debora, nabii mwanamke, mkewe Lapidothi, ndiye alikuwa anaamua Israeli wakati ule.
5 и сия живяше под Фиником Деввора между Рамою и между Вефилем, в горе Ефремли: и восхождаху сынове Израилевы к ней тамо на суд.
Debora alikuwa akiketi chini ya Mtende wa Debora uliokuwa kati ya Rama na Betheli katika nchi ya vilima ya Efraimu, nao Waisraeli wakaja kwake ili awaamue.
6 И посла Деввора, и призва Варака сына Авинеемля из Кедеса Неффалимова, и рече к нему: не заповеда ли тебе Господь Бог Израилев? И пойдеши в гору Фавор, и поймеши с собою десять тысящ мужей от сынов Неффалимлих и от сынов Завулоних:
Akatuma wamwite Baraka mwana wa Abinoamu kutoka Kedeshi huko Naftali na kumwambia, “Bwana, Mungu wa Israeli, anakuagiza: ‘Nenda, chukua wanaume 10,000 toka Naftali na Zabuloni, mwende Mlima Tabori.
7 и приведу к тебе в водотечь Кисонь Сисару воеводу силы Иавини, и колесницы его, и множество (вой) его, и предам его в руки твоя.
Nitamshawishi Sisera, jemadari wa jeshi la Yabini, pamoja na magari yake na jeshi lake, hadi Mto Kishoni na kumtia mikononi mwako.’”
8 И рече к ней Варак: аще пойдеши со мною, пойду, и аще не пойдеши со мною, не пойду: яко не вем дне, в оньже благоустроит Господь Ангела со мною.
Baraka akamwambia, “Ukienda pamoja nami nitakwenda, lakini usipokwenda pamoja nami, sitakwenda.”
9 И рече Деввора к нему: идущи пойду с тобою: обаче веждь, яко не будет тебе слава на пути, в оньже ты идеши: понеже в руку женску предаст Господь Сисару. И воста Деввора и пойде с Вараком до Кадиса.
Debora akamwambia, “Hakika nitakwenda pamoja nawe, lakini njia unayoiendea haitakupa heshima wewe, kwa kuwa Bwana atamtia Sisera mikononi mwa mwanamke.” Hivyo Debora akaenda pamoja na Baraka mpaka Kedeshi,
10 И воззва Варак Завулона и Неффалима до Кадиса, и поидоша вслед его десять тысящ мужей, и иде с ним Деввора.
mahali ambapo Baraka aliwaita Zabuloni na Naftali. Watu 10,000 wakamfuata Baraka, na Debora pia akaenda pamoja naye.
11 И Хавер Киней отлучися от Кены и от сынов Иовава, ужика Моисеова: и потче кущу свою под дубом Почивающих, иже есть при Кедесе.
Basi Heberi, Mkeni, alikuwa amejitenga na Wakeni wengine, yaani, wazao wa Hobabu, mkwewe Mose, naye akapiga hema lake karibu na ule mti mkubwa wa mwaloni ulioko Saananimu, karibu na Kedeshi.
12 И возвестиша Сисаре, яко взыде Варак сын Авинеемль на гору Фавор.
Sisera alipoambiwa kuwa Baraka mwana wa Abinoamu alikuwa amepanda Mlima Tabori,
13 И созва Сисара вся колесницы своя, девять сот колесниц железных, и вся люди иже с ним, от Арисофа языков в водотечь Кисонь.
Sisera akakusanya pamoja magari yake yote 600 ya chuma na watu wote waliokuwa pamoja naye, kuanzia Haroshethi-Hagoyimu mpaka Mto wa Kishoni.
14 И рече Деввора к Вараку: востани, яко сей день, в оньже предаде Господь Сисару в руку твою, зане Господь изыдет пред тобою. И сниде Варак с горы Фавор, и десять тысящ мужей вслед его.
Ndipo Debora akamwambia Baraka, “Nenda! Hii ndiyo siku ambayo Bwana amemtia Sisera mikononi mwako. Je, Bwana hakukutangulia mbele yako?” Hivyo Baraka akashuka kutoka Mlima Tabori, akifuatwa na watu 10,000.
15 И сотре Господь Сисару и вся колесницы его и весь полк его острием меча пред Вараком. И сниде Сисара с колесницы своея и побеже ногами своими.
Bwana akamfadhaisha Sisera na magari yake yote, pamoja na jeshi lake lote kwa upanga mbele ya Baraka, naye Sisera akaliacha gari lake na kukimbia kwa miguu.
16 И Варак гоняй вслед колесниц его и вслед полка, даже до Дубравы языков. И паде весь полк Сисарин острием меча: не остася ни един.
Lakini Baraka akafuata magari pamoja na jeshi mpaka Haroshethi-Hagoyimu. Jeshi lote la Sisera likaanguka kwa upanga, wala hakuna hata mtu mmoja aliyesalia.
17 И Сисара убеже ногами своими в кущу Иаили, жены Хавера Кинеева: яко мир бяше между Иавином царем Асорским и между домом Хавера Кинеева.
Sisera, hata hivyo, akakimbia kwa miguu mpaka kwenye hema la Yaeli, mkewe Heberi, Mkeni, kwa sababu palikuwa na uhusiano wa kirafiki kati ya Yabini mfalme wa Hazori na ukoo wa Heberi, Mkeni.
18 И изыде Иаиль во сретение Сисаре и рече к нему: уклонися, господине мой, уклонися ко мне, не бойся. И уклонися к ней в кущу: и покры его одеждею своею.
Yaeli akaenda kumlaki Sisera na kumwambia, “Karibu, bwana wangu, karibu ingia ndani kabisa. Usiogope.” Basi Sisera akaingia ndani ya hema ya Yaeli, naye akamfunika kwa blanketi nene.
19 И рече Сисара к ней: напой мя мало воды, яко возжаждах. И отреши мех млечный, и напои его, и покры его.
Akamwambia, “Nina kiu, tafadhali nipe maji ya kunywa.” Ndipo akafungua kiriba cha maziwa na kumpa akanywa, kisha akamfunika.
20 И рече к ней Сисара: стани во дверех кущи, и будет аще кто приидет к тебе, и вопросит тя, и речет: есть ли зде муж? И речеши: несть.
Naye Sisera akamwambia, “Simama mlangoni pa hema na mtu yeyote akija na kukuuliza, ‘Je, kuna mtu yeyote hapa?’ sema, ‘Hapana.’”
21 И взя Иаиль, жена Хаверова, кол кущный, и взя млат в руку свою, и вниде к нему тихо, и водрузи кол во скрании его, и пронзе до земли: и сей утруждся спаше, и издше.
Ndipo Yaeli, mkewe Heberi, akatwaa kigingi cha hema, akachukua nyundo mkononi mwake, akamwendea polepole, akiwa amelala usingizi, akiwa amechoka. Akakigongomea kile kigingi kwenye paji la uso wake, kikapenya hata kuingia ardhini, naye akafa.
22 И се, Варак гоняй Сисару. И изыде Иаиль во сретение ему и рече ему: прииди, и покажу тебе мужа, егоже ты ищеши. И вниде к ней, и се, Сисара лежаше мертв, и кол во скрании его.
Baraka akakaribia akimfuatia Sisera, Yaeli akatoka kumlaki. Akamwambia, “Njoo, nitakuonyesha mtu unayemtafuta.” Hivyo wakaingia ndani ya hema wakiwa wamefuatana na tazama Sisera alikuwa amelala humo, akiwa amekufa, na hicho kigingi cha hema kikiwa kimegongomewa kupitia paji la uso wake.
23 И покори Господь Бог в той день Иавина царя Ханааня пред сыны Израилевыми:
Basi siku ile Mungu akamshinda Yabini, mfalme wa Kanaani, mbele ya Israeli.
24 и хождаше рука сынов Израилевых ходящи, и ожесточися на Иавина царя Ханаанска, дондеже истребиша его.
Nao mkono wa Waisraeli ukaendelea kuwa na nguvu zaidi na zaidi dhidi ya Yabini, mfalme wa Kanaani, mpaka wakamwangamiza.

< Книга Судей израилевых 4 >