< Книга Судей израилевых 21 >
1 И сынове Израилевы кляшася в Массифе, глаголюще: муж от нас да не даст Вениамину дщере своея в жену.
Wana wa Israeli walikuwa wameapa kwa kiapo kule Mispa: “Hapana mtu yeyote atakayemwoza binti yake kwa Wabenyamini.”
2 И приидоша людие в Вефиль и седеша тамо до вечера пред Богом: и воздвигоша глас свой, и плакашася плачем велиим, и рекоша:
Watu wakaenda Betheli, wakaketi mbele za Mungu mpaka jioni, wakapaza sauti zao, wakalia sana.
3 вскую, Господи Боже Израилев, бысть сице днесь во Израили, еже оскудети от Израиля племени единому?
Wakasema, “Ee Bwana, Mungu wa Israeli, kwa nini jambo hili limewapata Waisraeli? Kwa nini kabila moja la Israeli limekosekana?”
4 И бысть на утрия, и обутреша людие, и соградиша тамо олтарь, и вознесоша всесожжение спасения, и рекоша сынове Израилевы:
Kesho yake asubuhi na mapema watu wakajenga madhabahu na kuleta sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani.
5 кто не взыде в сонм от всех племен Израилевых ко Господу? Яко велика клятва бяше не вшедшым ко Господу в Массифу, глаголюще: смертию да умрет.
Ndipo Waisraeli wakasema, “Ni kabila lipi la Israeli ambalo halikufika katika mkutano kumkaribia Bwana?” Kwa kuwa walikuwa wameweka kiapo kikuu kuwa yeyote asiyefika mbele za Bwana huko Mispa, kwa hakika angeuawa.
6 И умилишася сынове Израилевы о Вениамине брате своем, и рекоша: изсечено днесь едино племя от Израиля:
Basi Waisraeli wakaghairi kwa ajili ya ndugu zao Wabenyamini, wakasema, “Leo kabila moja limekatiliwa mbali na Israeli.
7 что сотворим оставшымся о женах? И мы кляхомся Господем не дати им от дщерей наших в жены.
Sasa tutawezaje kuwapa mabinti zetu wawe wake zao kwa hao waliobaki maadamu tumeapa kwa Bwana kuwa hatutawapa binti zetu kuwa wake zao?”
8 И рекоша: кто един от племен Израилевых, иже не взыде ко Господу в Массифу? И се, ни един прииде в полк от Иависа Галаадова в сонм.
Ndipo wakasema, “Ni kabila lipi la Israeli ambalo halikufika mbele za Bwana huko Mispa?” Wakagundua kuwa hakuna hata mmoja aliyetoka Yabeshi-Gileadi aliyefika kambini kwa ajili ya kusanyiko la mkutano.
9 И соглядаша людий, и се, не бяше тамо мужа от живущих во Иависе Галаадове.
Walipohesabu waliona hakuna mtu yeyote wa Yabeshi-Gileadi aliyekuwepo.
10 И послаша тамо сонм дванадесять тысящ мужей от сынов силы и заповедаша им, глаголюще: идите и избийте живущыя во Иависе Галаадове оружием жены и народы:
Ndipo mkutano wakatuma askari 12,000 na wakawaamuru kwenda Yabeshi-Gileadi na kuwaua wale wote waishio huko, walikuwepo wake na watoto.
11 и сие сотворите: всяк мужеский пол и всяку жену, познавшую ложе мужеско, побиете: девицы же снабдите. И сотвориша тако.
Wakasema, “Hilo ndilo mtakalofanya. Ueni kila mtu mume na mke ambaye si bikira.”
12 И обретоша от живущих во Иависе Галаадове четыре ста отроковиц дев, яже не познаша ложа мужеска: и приведоша я в полк в Силом, иже есть в земли Ханаани.
Wakakuta kati ya watu walioishi Yabeshi-Gileadi wanawali mia nne ambao hawajakutana kimwili na mwanaume, nao wakawachukua kwenye kambi huko Shilo katika nchi ya Kanaani.
13 И послаша весь сонм и глаголаша к сыном Вениаминовым, иже в камени Реммони, и призваша их с миром.
Ndipo mkutano ukatuma ujumbe wa amani kwa Wabenyamini huko katika mwamba wa Rimoni.
14 И возвратися Вениамин к сыном Израилевым в то время, и даша им сынове Израилевы жены, яже живо сохраниша от дщерей Иависа Галаадова: и угодно бысть им тако.
Basi Wabenyamini wakarudi nyumbani mwao, wakapewa wale wanawali wa Yabeshi-Gileadi waliowaponya. Lakini hawakuwatosha wanaume wote.
15 И людие умилишася о Вениамине, яко сотвори Господь истребление в племенех Израилевых.
Waisraeli wakasikitika kwa ajili ya Wabenyamini, kwa kuwa Bwana ameweka ufa katika makabila ya Israeli.
16 И рекоша старейшины сонма: что сотворим оставшым о женах? Яко погибе от Вениамина жена:
Viongozi wa kusanyiko wakasema, “Kwa kuwa wanawake wa Wabenyamini wameangamizwa, tufanyeje ili kuwapatia wake wale wanaume waliosalia?
17 и како будет наследие уцелевших от Вениамина, да не погибнет племя от Израиля?
Wale waliopona wa Wabenyamini ni lazima tuwape wake, ili wawe na warithi, ili kabila lolote katika Israeli lisifutike.
18 И мы не возможем дати им жен от дщерей наших, яко кляшася сынове Израилевы, глаголюще: проклят даяй жену Вениамину.
Hatuwezi kuwapa binti zetu kuwa wake, kwa kuwa sisi Waisraeli tumeapa kiapo hiki: ‘Alaaniwe mtu yeyote ampaye Mbenyamini mke.’”
19 И рекоша: се, праздник Господень в Силоме от дний во дни, иже есть от севера Вефиля, на восток солнца на пути восходящем от Вефиля в Сихем, и от юга Левоны.
Ndipo waliposema, “Tazama iko sikukuu ya kila mwaka ya Bwana katika Shilo, kaskazini ya Betheli na mashariki mwa ile barabara itokayo Betheli kwenda Shekemu, upande wa kusini wa Lebona.”
20 И заповедаша сыном Вениаминим, глаголюще: идите и засядите в виноградех,
Hivyo wakawaelekeza Wabenyamini wakisema, “Nendeni mkajifiche kwenye mashamba ya mizabibu,
21 и узрите, и се, егда изыдут дщери живущих в Силоме плясати в лики, да изыдете из виноградов и восхитите муж жену себе от дщерей Силомлих, и идите на землю Вениаминю:
nanyi mwangalie. Wasichana wa Shilo watakapojiunga kwenye kucheza, ninyi tokeni kwenye hayo mashamba ya mizabibu na kila mmoja akamate mwanamke mmoja toka miongoni mwa hao wasichana wa Shilo na mwende nao katika nchi ya Benyamini.
22 и будет егда приидут отцы их или братия их судитися к нам, и речем им: помилуйте нас ими, яко не взя муж жены своея в полце: понеже вы не дали есте им яко жребий, согрешисте.
Baba zao au ndugu zao waume watakapotulalamikia, tutawaambia, ‘Kuweni wakarimu kwetu, nanyi mturuhusu tuwe nao kwa kuwa hatukuweza kumpa kila mtu mke tulipopigana. Lakini ninyi pia hamna hatia, kwa kuwa hamkuwapa wao binti zenu kuwa wake.’”
23 И сотвориша тако сынове Вениамини, и пояша жены по числу своему от пляшущих, яже восхитиша: и отидоша и возвратишася в наследие свое, и создаша грады и вселишася в них.
Basi hivyo ndivyo Wabenyamini walivyofanya. Wakati wasichana walipokuwa wakicheza, kila mtu akamkamata msichana mmoja akamchukua akaenda naye ili awe mke wake. Kisha wakarudi katika urithi wao na kuijenga upya miji na kuishi humo.
24 И отидоша оттуду сынове Израилевы в то время, муж во племя свое и в род свой: и изыде оттуду муж в наследие свое.
Wakati huo Waisraeli wakaondoka sehemu ile na kwenda nyumbani kwao, kwenye makabila yao na kwa jamaa zao, kila mmoja kwenye urithi wake mwenyewe.
25 И в тыя дни не бяше царя во Израили: муж еже угодно пред очима его, творяше.
Katika siku hizo kulikuwa hakuna mfalme katika Israeli; kila mtu alifanya kile alichoona ni sawa machoni pake mwenyewe.