< Книга Иисуса Навина 7 >
1 И прегрешиша сынове Израилевы прегрешением великим, и взяша от клятвы: взя бо Ахар сын Хармии, сына Замврии, сына Зары, от племене Иудина, от клятвы. И разгневася Господь яростию на сыны Израилевы.
Lakini watu wa Israeli hawakutenda katika uaminifu kuhusiana na vitu vilivyotengwa kwa ajili ya uharibifu. Akani mwana wa Karmi, mwana wa Zabdi, mwana wa Zera, kutoka katika kabila la Yuda, alivitwaa baadhi ya vitu hivyo vilivyokuwa vimetengwa kwa ajili ya uharibifu, na hasira ya Yahweh iliwaka juu yawatu wa Israeli.
2 И посла Иисус мужы от Иерихона в Гай, иже есть противу Вифавн на восток Вефиля, и рече им, глаголя: шедше соглядайте землю. И идоша мужие и соглядаша Гай.
Yoshua alituma watu kutoka Yeriko kwenda Ai, mji uliokuwa karibu na Bethi Aveni, mashariki mwa Betheli. Aliwaambia, “Nendeni na mkaipeleleza nchi.” Wale watu walikwea na kuipeleleza Ai.
3 И возвратишася ко Иисусу и рекоша ему: да не идут вси людие, но яко две тысящы или три тысящы мужей да идут и да воюют Гай: да не ведеши тамо всех людий, мало бо есть их (тамо).
Waliporudi kwa Yoshua, walimwambia, “Usitume watu wote kwenda Ai. Tuma tu watu elfu mbili au elfu tatu waende kuiteka Ai. Usiwafanye watu wateseke katika vita, kwani ni watu wachache.”
4 И идоша от людий тамо, аки три тысящы мужей, и побегоша от лица мужей Гайских:
Hivyo ni watu wapatao elfu tatu tu kutoka katika jeshi ndio walioenda, lakini watu hawa waliwakimbia watu wa Ai.
5 и убиша от них мужие Гайстии яко тридесять и шесть мужей, и отгнаша их от врат, дондеже сокрушиша их на стремнине: и ужасеся сердце людий, и бысть яко вода.
Watu wa Ai waliwaua watu wapatao thelathini na sita, waliwafuata katika lango la mji hadi katika machimbo ya mawe, na waliwauwa walipokuwa wakishuka katika kilima. Na mioyo ya watu ilijawa hofu na ujasiri wao ukawatoka.
6 И растерза Иисус ризы своя, и паде на земли на лице свое пред Господем даже до вечера, сам и старцы Израилевы: и посыпаша персть на главы своя.
Basi Yoshua alizirarua nguo zake. Yeye pamoja na wazewe wa Israeli waliweka mavumbi juu ya vichwa vyao na wakainamisha vichwa vyao hadi katika nchi mbele ya sanduku la Yahweh, na walibaki pale mpaka jioni.
7 И рече Иисус: молюся, Господи Господи, вскую преведе раб Твой люди сия чрез Иордан предати их Аморреом на погубление? От, да быхом пребыли и вселилися у Иордана:
Kisha Yoshua akasema, “Oo, Yahweh Bwana, kwanini umewavusha watu hawa ng'ambo ya Yordani? Kutuweka katika mikono ya Waamori ili kutuangamiza? ikiwa kama tulifanya maamuzi tofauti na tungekaa katika upande mwingine wa Yordani!
8 Господи, что реку? Понеже отврати Израиль выю свою пред враги своими:
Bwana, niseme nini, baada ya Israeli kuwatega migongo maadui zao?
9 и услышав Хананей и вси живущии на земли обыдут нас и потребят нас от земли: и что сотвориши имени Твоему великому?
Kwa kuwa Wakaanani na wenyeji wote wa nchi watakaposikia, watatuzunguka na kuwafanya watu wa nchi kulisahau jina letu. Na utafanya nini kwa ajili ya jina lako kuu?
10 И рече Господь ко Иисусу: востани, вскую ты пал еси на лице твое?
Yahweh akamwambia Yoshua, “Inuka! kwanini umelala kifudifudi?
11 Согрешиша людие и преступиша завет Мой, егоже завещах к ним, и украдше от клятвы, скрыша в сосудех своих:
Israeli imetenda dhambi. Wamevunja agano langu nililowaagiza. Wameiba baadhi ya vitu vilivyokuwa vimetengwa. Wameiba na kisha pia wakaficha dhambi yao kwa kuweka vitu vile walivyochukua miongoni mwa mali zao wenyewe.
12 сего ради не могут сынове Израилевы стати пред лицем врагов своих, но хребет обратят пред враги своими, яко клятвою сташася: не приложу ксему быти с вами, аще не измете клятвы от себе самих:
Na matokeo yake ni kwamba watu wa Israeli hawataweza kusimama mbele za maadui zao. Walitega migongo yao kwa maadui zao kwasababu wao wenyewe wametengwa kwa ajili ya uharibifu. Sitakuwa pamoja nanyi tena mpaka pale mtakapoteketeza vitu vile vilivyotakiwa kuharibiwa, lakini sasa bado viko miongoni mwenu.
13 востав очисти люди и рцы: очиститеся на утро: яко сия глаголет Господь Бог Израилев: клятва есть в вас, не возможете стати пред враги вашими, дондеже измете от себе самих клятву:
Inuka! Waweke watu wakfu kwangu, na uwaambie, 'Jiwekeeni wakfu ninyi wenyewe kesho. Kwa kuwa, Yahweh, Mungu wa Israeli asema hivi, “Kuna vitu vilitengwa ili kuteketezwa ambavyo bado viko miongoni mwenu, Israeli. Hamtaweza kusimama mbele ya maadui zenu mpaka pale mtakapoviondoa miongoni mwenu vitu vyote ambavyo vilitengwa kwa ajili ya kuteketezwa.”
14 и соберитеся вси заутра по племеном (вашым), и будет племя, еже покажет Господь, да приведете по сонмом: и сонм, егоже покажет Господь, да приведете по домом: и дом, егоже покажет Господь, да приведете по мужем:
Asubuhi, mtajisogeza wenyewe kwa makabila. Kabila lile ambalo Yahweh atalichagua litasogea karibu kwa koo zake. Ukoo ule ambao Yahweh atauchagua lazima usogee karibu kwa nyumba. Nyumba ambayo Yahweh ataichagua lazima isogee karibu kwa mtu mmoja mmoja.
15 и иже обличится, да сожжется огнем, сам и вся елика суть его, яко преступи завет Господень и сотвори беззаконие во Израили.
Itakuwa hivi mtu yule atakayechaguliwa na aliye navyo vitu hivyo vilivyotengwa kwa ajili ya kuharibiwa, atachomwa moto, yeye na kila kitu alichonacho, kwasababu amelivunja agano la Yahweh na kwasababu amefanya jambo la aibu katika Israeli.'”
16 И воста Иисус заутра, и приведе людий по племеном: и обличися племя Иудино.
Basi, Yoshua aliamka asubuhi na mapema na aliwaleta Israeli karibu, kabila kwa kabila, na kabila la Yuda lilichaguliwa.
17 И приведеся по сонмом, и обличися сонм Зараин: и приведеся сонм Зараин по мужем, и обличися дом Замвриин.
Yoshua akazisogeza koo za Yuda karibu, na ukoo wa Zera ulichaguliwa. Akausogeza karibu ukoo wa Zera mtu kwa mtu, na Zabdi alichaguliwa.
18 И приведеся дом его по мужем, и обличися Ахар сын Хармиин сына Замвриина, сына Зараня, от племене Иудина.
Akaisogeza karibu nyumba ya Zabdi mtu kwa mtu, na Akani mwana wa Karmi, mwana wa Zabdi, mwana wa Zera, kutoka kabila la Yuda, alichaguliwa.
19 И рече Иисус Ахару: сыне мой, даждь славу днесь Господу Богу Израилеву, и даждь Ему исповедание, и исповеждь ми, что сотворил еси, и не утай от мене.
Kisha Yoshua akamwambia Akani, “Mwanangu, niambie ukweli mbele za Yahweh, Mungu wa Israel, na ufanye ukiri wako kwake. Tafadhali niambie kile ulichofanya. Usinifiche.”
20 И отвеща Ахар Иисусу и рече: поистинне аз согреших пред Господем Богом Израилевым: сице и сице сотворих:
Akani akamjibu Yoshua, “Kwa kweli nimetenda dhambi mbele Yahweh, Mungu wa Israeli.
21 видех в плене ризу красну и добру и двести дидрахм сребра, и сосуд един злат, пятьдесят дидрахм вес его: и помыслив на ня взях: и се, сия сокровенна суть в земли в кущи моей, и сребро сокровенно под ними.
Nilichofanya ni hiki: Nilipoona miongoni mwa nyara mkoti mzuri kutoka Babeli, shekeli mia mbili za fedha, na kipande cha dhahabu chenye uzito wa shekeli hamsini, nilivitamani na nikavichukua. Vimefichwa chini ardhini katikati ya hema langu, na fedha iko chini yake.”
22 И посла Иисус послы, и идоша в кущу в полк: и сия бяху сокровенна в кущи его, и сребро под ними,
Yoshua akatuma wajumbe waliokimbia mpaka kwenye hema mahali palipokuwa na vile vitu. Walipoangalia, waliviona vimefichwa katika hema lake, na fedha chini yake.
23 и изнесоша я из кущи, и принесоша ко Иисусу и к старцем Израилевым, и положиша я пред Господем.
Walivichukua vitu hivyo kutoka katikati ya hema na kuvileta kwa Yoshua na watu wote wa Israeli. Walivimwaga mbele za Yahweh.
24 И взя Иисус Ахара сына Зараня, и сребро и ризу и сосуд златый, и возведе его в дебрь Ахор, и сыны его и дщери его, и телцы его и ослята его и вся овцы его, и кущу его и вся имения его, и весь Израиль по нем: и возведе я (со всем) во емек Ахор.
Kisha Yoshua na Waisraeli wote pamoja naye, walimchukua Akani mwana wa Zera, na fedha, na koti, na kipande cha dhahabu, wana na binti zake, ng'ombe zake, punda zake, kondoo zake, hema lake, na kila kitu alichokuwa nacho, na wakavileta hata bonde la Akori.
25 И рече Иисус Ахару: почто потребил еси нас? Да потребит тя Господь, якоже и днесь. И побиша его камением весь Израиль, и сожгоша вся огнем, и наметаша их камением,
Kisha Yoshua akasema, “Kwanini umetusumbua? Leo Yahweh atakutesa na wewe.” Waisraeli wote wakampiga kwa mawe. Na wakawachoma wote kwa moto, na wakawapiga mawe.
26 и наметаша на нем громаду камения велику. И преста Господь от ярости гнева Своего. Сего ради прозвася имя месту тому емек Ахор даже до дне сего.
Kisha wakaweka juu yake kichuguu kikubwa cha mawe ambayo yapo hata leo. Yahweh akaachilia mbali hasira yake. Hivyo basi, jina la mahali hapo likawa Akori hata leo.