< От Иоанна святое благовествование 13 >
1 Прежде же праздника Пасхи, ведый Иисус, яко прииде Ему час, да прейдет от мира сего ко Отцу, возлюбль Своя сущыя в мире, до конца возлюби их.
Ilikuwa kabla ya sikukuu ya Pasaka. Yesu alijua kwamba saa yake ya kuondoka ulimwenguni na kwenda kwa Baba ilikuwa imefika. Alikuwa amewapenda daima watu wake walioko duniani; naam, aliwapenda mpaka mwisho!
2 И вечери бывшей, диаволу уже вложившу в сердце Иуде Симонову Искариотскому, да Его предаст,
Basi, Yesu na wanafunzi wake walikuwa mezani kwa chakula cha jioni. Ibilisi alikwisha mtia Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti, nia ya kumsaliti Yesu.
3 ведый Иисус, яко вся даде Ему Отец в руце, и яко от Бога изыде и к Богу грядет:
Yesu alijua kwamba Baba alikuwa amemkabidhi kila kitu, na kwamba alikuwa ametoka kwa Mungu na anarudi kwa Mungu.
4 воста от вечери и положи ризы, и приемь лентион, препоясася:
Basi, Yesu aliondoka mezani, akaweka kando vazi lake, akachukua kitambaa na kujifunga kiunoni.
5 потом влия воду во умывалницу и начат умывати ноги учеником и отирати лентием, имже бе препоясан.
Kisha akatia maji katika bakuli, akaanza kuwaosha wanafunzi wake miguu na kuipangusa kwa kile kitambaa alichojifungia.
6 Прииде же к Симону Петру, и глагола Ему той: Господи, Ты ли мои умыеши нозе?
Basi, akamfikia Simoni Petro; naye Petro akasema, “Bwana, wewe utaniosha miguu mimi?”
7 Отвеща Иисус и рече ему: еже Аз творю, ты не веси ныне, уразумееши же по сих.
Yesu akamjibu, “Huelewi sasa ninachofanya lakini utaelewa baadaye.”
8 Глагола Ему Петр: не умыеши ногу моею во веки. Отвеща ему Иисус: аще не умыю тебе, не имаши части со Мною. (aiōn )
Petro akamwambia, “Wewe hutaniosha miguu kamwe!” Yesu akamjibu, “Nisipokuosha hutakuwa na uhusiano nami tena.” (aiōn )
9 Глагола Ему Симон Петр: Господи, не нозе мои токмо, но и руце и главу.
Simoni Petro akamwambia, “Bwana, nioshe, si miguu tu, bali na mikono yangu na kichwa pia.”
10 Глагола ему Иисус: измовенный не требует, токмо нозе умыти, есть бо весь чист: и вы чисти есте, но не вси.
Yesu akamwambia, “Aliyekwisha oga hana lazima ya kunawa isipokuwa miguu, maana amekwisha takata mwili wote. Ninyi mmetakata, lakini si nyote.”
11 Ведяше бо предающаго Его: сего ради рече, яко не вси чисти есте.
(Yesu alimjua yule ambaye atamsaliti, ndiyo maana alisema: “Ninyi mmetakata, lakini si nyote.”)
12 Егда же умы ноги их, прият ризы Своя, возлег паки, рече им: весте ли, что сотворих вам?
Alipokwisha waosha miguu na kuvaa tena vazi lake, aliketi mezani, akawaambia, “Je, mmeelewa hayo niliyowatendeeni?
13 Вы глашаете Мя Учителя и Господа, и добре глаголете: есмь бо.
Ninyi mwaniita Mwalimu na Bwana, nanyi mwasema vyema, kwa kuwa ndimi.
14 Аще убо Аз умых ваши нозе, Господь и Учитель, и вы должни есте друг другу умывати нозе:
Basi, ikiwa mimi niliye Bwana na Mwalimu, nimewaosha ninyi miguu, nanyi pia mnapaswa kuoshana miguu.
15 образ бо дах вам, да, якоже Аз сотворих вам, и вы творите.
Nimewapeni mfano, ili nanyi pia mfanye kama nilivyowafanyieni.
16 Аминь, аминь глаголю вам: несть раб болий господа своего, ни посланник болий пославшаго его.
Kweli nawaambieni, mtumishi si mkuu zaidi kuliko bwana wake, wala mtume si mkuu zaidi kuliko yule aliyemtuma.
17 Аще сия весте, блажени есте, аще творите я.
Basi, ikiwa mwayajua hayo, mtakuwa na heri mkiyatekeleza.
18 Не о всех вас глаголю: Аз (бо) вем, ихже избрах: но да Писание сбудется: ядый со Мною хлеб воздвиже на Мя пяту свою.
“Haya nisemayo hayawahusu ninyi nyote. Mimi nawajua wale niliowachagua. Lakini lazima yatimie Maandiko Matakatifu yasemayo: Yule aliyeshiriki chakula changu amegeuka kunishambulia.
19 Отселе глаголю вам, прежде даже не будет, да, егда будет, веру имете, яко Аз есмь.
Mimi nimewaambieni mambo haya sasa kabla hayajatokea, ili yatakapotokea mpate kuamini kuwa mimi ndimi.
20 Аминь, аминь глаголю вам: приемляй, аще кого послю, Мене приемлет: а приемляй Мене приемлет Пославшаго Мя.
Kweli nawaambieni anayempokea yule ninayemtuma anaponipokea mimi; na anayenipokea mimi, anampokea yule aliyenituma.”
21 Сия рек Иисус возмутися духом и свидетелствова и рече: аминь, аминь глаголю вам, яко един от вас предаст Мя.
Alipokwisha sema hayo, Yesu alifadhaika sana rohoni, akasema wazi, “Kweli nawaambieni, mmoja wenu atanisaliti!”
22 Сзирахуся убо между собою ученицы, недоумеющеся, о ком глаголет.
Wanafunzi wakatazama wasiweze kabisa kujua anasema nani.
23 Бе же един от ученик Его возлежя на лоне Иисусове, егоже любляше Иисус:
Mmoja wa wanafunzi, ambaye Yesu alikuwa anampenda sana, alikuwa ameketi karibu na Yesu.
24 поману же сему Симон Петр вопросити, кто бы был, о немже глаголет.
Basi, Simoni Petro akamwashiria na kusema: “Mwulize anasema juu ya nani.”
25 Напад же той на перси Иисусовы, глагола Ему: Господи, кто есть?
Mwanafunzi huyo akasogea karibu zaidi na Yesu, akamwuliza, “Bwana, ni nani?”
26 Отвеща Иисус: той есть, емуже Аз омочив хлеб подам. И омочь хлеб, даде Иуде Симонову Искариотскому.
Yesu akajibu, “Yule nitakayempa kipande cha mkate nilichochovya katika sahani, ndiye.” Basi, akatwaa kipande cha mkate, akakichovya katika sahani, akampa Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti.
27 И по хлебе тогда вниде в онь сатана. Глагола убо ему Иисус: еже твориши, сотвори скоро.
Yuda alipokwisha pokea kipande hicho, Shetani akamwingia. Basi Yesu akamwambia, “Unachotaka kufanya, kifanye haraka!”
28 Сего же никтоже разуме от возлежащих, к чесому рече ему.
Lakini hakuna hata mmoja wa wale waliokaa pale mezani aliyefahamu kwa nini alikuwa amemwambia hivyo.
29 Нецыи же мняху, понеже ковчежец имяше Иуда, яко глаголет ему Иисус: купи, еже требуем на праздник: или нищым да нечто даст.
Kwa kuwa Yuda alikuwa na wajibu wa kuutunza mfuko wa fedha, baadhi yao walidhani kwamba Yesu alikuwa amemwambia anunue vilivyohitajiwa kwa sikukuu, au kwamba alikuwa amemwambia akatoe chochote kwa maskini.
30 Приим же он хлеб, абие изыде: бе же нощь. Егда изыде,
Basi, Yuda alipokwisha twaa kile kipande cha mkate, akatoka nje mara. Na ilikuwa usiku.
31 глагола Иисус: ныне прославися Сын Человеческий, и Бог прославися о Нем:
Baada ya Yuda kuondoka, Yesu akasema, “Sasa Mwana wa Mtu ametukuzwa, naye Mungu ametukuzwa ndani yake.
32 аще Бог прославися о Нем, и Бог прославит Его в Себе, и абие прославит Его.
Na kama utukufu wa Mungu umefunuliwa ndani ya Mwana, basi, naye Mungu ataudhihirisha utukufu wa Mwana ndani yake mwenyewe, na atafanya hivyo mara.
33 Чадца, еще с вами мало есмь: взыщете Мене, и якоже рех Иудеом, яко аможе Аз иду, вы не можете приити: и вам глаголю ныне.
“Watoto wangu, bado niko nanyi kwa muda mfupi tu. Mtanitafuta, lakini sasa nawaambieni yale niliyowaambia viongozi wa Wayahudi: Niendako ninyi hamwezi kwenda!
34 Заповедь новую даю вам, да любите друг друга: якоже возлюбих вы, да и вы любите себе:
Nawapeni amri mpya: pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda ninyi.
35 о сем разумеют вси, яко Мои ученицы есте, аще любовь имате между собою.
Mkipendana, watu wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu.”
36 Глагола Ему Симон Петр: Господи, камо идеши? Отвеща ему Иисус: аможе (Аз) иду, не можеши ныне по Мне ити: последи же по Мне идеши.
Simoni Petro akamwuliza, “Bwana, unakwenda wapi?” Yesu akajibu, “Niendako huwezi kunifuata sasa, lakini utanifuata baadaye.”
37 Глагола Ему Петр: Господи, почто не могу ныне по Тебе ити? (ныне) душу мою за Тя положу.
Petro akamwambia “Bwana, kwa nini siwezi kukufuata sasa? Niko tayari kufa kwa ajili yako!”
38 Отвеща ему Иисус: душу ли твою за Мя положиши? Аминь, аминь глаголю тебе: не возгласит алектор, дондеже отвержешися Мене трищи.
Yesu akajibu, “Je, uko tayari kweli kufa kwa ajili yangu? Kweli nakwambia, kabla jogoo hajawika utanikana mara tatu!”