< От Иоанна святое благовествование 11 >

1 Бе же некто боля Лазарь от Вифании, от веси Мариины и Марфы сестры ея.
Mtu mmoja aitwaye Lazaro, mwenyeji wa Bethania, alikuwa mgonjwa. (Kijiji cha Bethania kilikuwa mahali walipokaa Maria na Martha, dada yake.
2 Бе же Мариа помазавшая Господа миром и отершая нозе Его власы своими, еяже брат Лазарь боляше.
Maria ndiye yule aliyempaka Bwana marashi na kumpangusa kwa nywele zake. Lazaro, kaka yake, ndiye aliyekuwa mgonjwa.)
3 Посласте убо сестре к Нему, глаголюще: Господи, се, егоже любиши, болит.
Basi, hao dada wakatuma ujumbe huu kwa Yesu: “Bwana, rafiki yako ni mgonjwa!”
4 Слышав же Иисус рече: сия болезнь несть к смерти, но о славе Божии, да прославится Сын Божий ея ради.
Yesu aliposikia hivyo akasema, “Ugonjwa huo hautaleta kifo, ila ni kwa ajili ya kumtukuza Mungu; ameugua ili kwa njia hiyo Mwana wa Mungu atukuzwe.”
5 Любляше же Иисус Марфу и сестру ея и Лазаря.
Yesu aliwapenda Martha, dada yake na Lazaro.
6 Егда же услыша, яко болит, тогда пребысть на немже бе месте два дни.
Alipopata habari kwamba Lazaro ni mgonjwa, Yesu aliendelea kukaa mahali hapo alipokuwa kwa siku mbili zaidi.
7 Потом же глагола учеником: идем во Иудею паки.
Kisha akawaambia wanafunzi wake, “Twendeni tena Yudea!”
8 Глаголаша Ему ученицы: Равви, ныне искаху Тебе камением побити Иудее, и паки ли идеши тамо?
Wanafunzi wakamwambia, “Mwalimu! Muda mfupi tu umepita tangu Wayahudi walipotaka kukuua kwa mawe, nawe unataka kwenda huko tena?”
9 Отвеща Иисус: не два ли надесяте часа еста во дни? Аще кто ходит во дни, не поткнется, яко свет мира сего видит:
Yesu akajibu, “Je, saa za mchana si kumi na mbili? Basi, mtu akitembea mchana hawezi kujikwaa kwa kuwa anauona mwanga wa ulimwengu huu.
10 аще же кто ходит в нощи, поткнется, яко несть света в нем.
Lakini mtu akitembea usiku atajikwaa kwa maana mwanga haumo ndani yake.”
11 Сия рече и посем глагола им: Лазарь друг наш успе: но иду, да возбужу его.
Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, akawaambia, “Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini mimi nitakwenda kumwamsha.”
12 Реша убо ученицы Его: Господи, аще успе, спасен будет.
Wanafunzi wake wakamwambia, “Bwana, ikiwa amelala, basi atapona.”
13 Рече же Иисус о смерти его: они же мнеша, яко о успении сна глаголет.
Wao walidhani kwamba alikuwa amesema juu ya kulala usingizi, kumbe alikuwa amesema juu ya kifo cha Lazaro.
14 Тогда рече им Иисус не обинуяся: Лазарь умре:
Basi, Yesu akawaambia waziwazi, “Lazaro amekufa;
15 и радуюся вас ради, да веруете, яко не бех тамо: но идем к нему.
Lakini nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini. Haya, twendeni kwake.”
16 Рече же Фома, глаголемый Близнец, учеником: идем и мы, да умрем с ним.
Thoma (aitwaye Pacha) akawaambia wanafunzi wenzake, “Twendeni nasi tukafe pamoja naye!”
17 Пришед же Иисус, обрете его четыри дни уже имуща во гробе.
Yesu alipofika huko alikuta Lazaro amekwisha kaa kaburini kwa siku nne.
18 Бе же Вифаниа близ Иерусалима, яко стадий пятьнадесять,
Kijiji cha Bethania kilikuwa karibu na Yerusalemu umbali upatao kilomita tatu.
19 и мнози от Иудей бяху пришли к Марфе и Марии, да утешат их о брате ею.
Wayahudi wengi walikuwa wamefika kwa Martha na Maria kuwafariji kwa kifo cha kaka yao.
20 Марфа убо егда услыша, яко Иисус грядет, срете Его: Мариа же дома седяше.
Basi, Martha aliposikia kwamba Yesu alikuwa anakuja, akaenda kumlaki; lakini Maria alibaki nyumbani.
21 Рече же Марфа ко Иисусу: Господи, аще бы еси зде был, не бы брат мой умерл:
Martha akamwambia Yesu, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa!
22 но и ныне вем, яко елика аще просиши от Бога, даст Тебе Бог.
Lakini najua kwamba hata sasa chochote utakachomwomba Mungu, atakupa.”
23 Глагола ей Иисус: воскреснет брат твой.
Yesu akamwambia, “Kaka yako atafufuka.”
24 Глагола Ему Марфа: вем, яко воскреснет в воскрешение, в последний день.
Martha akamjibu, “Najua kwamba atafufuka wakati wa ufufuo, siku ya mwisho.”
25 Рече (же) ей Иисус: Аз есмь воскрешение и живот: веруяй в Мя, аще и умрет, оживет:
Yesu akamwambia, “Mimi ndimi ufufuo na uzima. Anayeniamini mimi hata kama anakufa, ataishi:
26 и всяк живый и веруяй в Мя не умрет во веки. Емлеши ли веру сему? (aiōn g165)
na kila anayeishi na kuniamini, hatakufa kamwe. Je, waamini hayo?” (aiōn g165)
27 Глагола Ему: ей, Господи: аз веровах, яко Ты еси Христос Сын Божий, иже в мир грядый.
Martha akamwambia, “Ndiyo Bwana! Naamini kwamba wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yule ajaye ulimwenguni.”
28 И сия рекши, иде и пригласи Марию сестру свою тай, рекши: Учитель пришел есть и глашает тя.
Baada ya kusema hayo, Martha alikwenda kumwita Maria, dada yake, akamwabia faraghani, “Mwalimu yuko hapa, anakuita.”
29 Она (же) яко услыша, воста скоро и иде к Нему.
Naye aliposikia hivyo, akainuka mara, akamwendea Yesu.
30 Не уже бо бе пришел Иисус в весь, но бе на месте, идеже срете Его Марфа.
Yesu alikuwa hajaingia kijijini, ila alikuwa bado mahali palepale Martha alipomlaki.
31 Иудее (же) убо сущии с нею в дому и утешающе ю, видевше Марию, яко скоро воста и изыде, по ней идоша, глаголюще, яко идет на гроб, да плачет тамо.
Basi, Wayahudi waliokuwa nyumbani pamoja na Maria wakimfariji walipomwona ameinuka na kutoka nje ghafla, walimfuata. Walidhani alikuwa anakwenda kaburini kuomboleza.
32 Мариа же яко прииде, идеже бе Иисус, видевши Его, паде Ему на ногу, глаголющи Ему: Господи, аще бы еси был зде, не бы умерл мой брат.
Basi, Maria alipofika mahali pale Yesu alipokuwa na kumwona, alipiga magoti, akamwabia, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa!”
33 Иисус убо, яко виде ю плачущуся и пришедшыя с нею Иудеи плачущя, запрети духу и возмутися Сам
Yesu alipomwona analia, na wale Wayahudi waliokuja pamoja naye wanalia pia, alijawa na huzuni na kufadhaika moyoni.
34 и рече: где положисте его? Глаголаша Ему: Господи, прииди и виждь.
Kisha akawauliza, “Mlimweka wapi?” Wakamwambia, “Bwana, njoo uone.”
35 Прослезися Иисус.
Yesu akalia machozi.
36 Глаголаху убо Жидове: виждь, како любляше его.
Basi, Wayahudi wakasema, “Tazameni jinsi alivyompenda!”
37 Нецыи же от них реша: не можаше ли Сей, отверзый очи слепому, сотворити, да и сей не умрет?
Lakini baadhi yao wakasema, “Je, huyu aliyemfumbua macho yule kipofu, hakuweza kumfanya Lazaro asife?”
38 Иисус же паки претя в себе, прииде ко гробу. Бе же пещера, и камень лежаше на ней.
Basi, Yesu akiwa amehuzunika tena moyoni, akafika kaburini. Kaburi lenyewe lilikuwa pango, na lilikuwa limefunikwa kwa jiwe.
39 Глагола Иисус: возмите камень. Глагола Ему сестра умершаго Марфа: Господи, уже смердит: четверодневен бо есть.
Yesu akasema, “Ondoeni hilo jiwe!” Martha, dada yake huyo aliyekufa, akamwambia, “Bwana, amekwishaanza kunuka; amekaa kaburini siku nne!”
40 Глагола ей Иисус: не рех ли ти, яко аще веруеши, узриши славу Божию?
Yesu akamwambia, “Je, sikukwambia kwamba ukiamini utaona utukufu wa Mungu?”
41 Взяша убо камень, идеже бе умерый лежя. Иисус же возведе очи горе и рече: Отче, хвалу Тебе воздаю, яко услышал еси Мя:
Basi, wakaliondoa lile jiwe. Yesu akatazama juu mbinguni, akasema, “Nakushukuru Baba kwa kuwa wewe wanisikiliza.
42 Аз же ведех, яко всегда Мя послушаеши: но народа ради стоящаго окрест рех, да веру имут, яко Ты Мя послал еси.
Najua kwamba unanisikiliza daima. Lakini nimesema hayo kwa ajili ya watu hawa waliopo hapa ili wapate kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma.”
43 И сия рек, гласом великим воззва: Лазаре, гряди вон.
Alipokwisha sema hayo, akaita kwa sauti kubwa: “Lazaro! Toka nje!”
44 И изыде умерый, обязан рукама и ногама укроем, и лице его убрусом обязано. Глагола им Иисус: разрешите его и оставите ити.
Huyo aliyekuwa amekufa akatoka nje, huku amefungwa sanda miguu na mikono, na uso wake umefunikwa. Yesu akawaambia, “Mfungueni, mkamwache aende zake.”
45 Мнози убо от Иудей пришедшии к Марии и видевше, яже сотвори Иисус, вероваша в Него:
Basi, Wayahudi wengi waliokuwa wamefika kwa Maria walipoona kitendo hicho alichokifanya Yesu wakamwamini.
46 нецыи же от них идоша к фарисеом и рекоша им, яже сотвори Иисус.
Lakini baadhi yao walikwenda kwa Mafarisayo wakatoa taarifa ya jambo hilo alilofanya Yesu.
47 Собраша убо архиерее и фарисее сонм и глаголаху: что сотворим? Яко Человек Сей многа знамения творит:
kwa hiyo makuhani wakuu na Mafarisayo wakafanya kikao cha Baraza kuu, wakasema, “Tufanye nini? Mtu huyu anafanya ishara nyingi mno.
48 аще оставим Его тако, вси уверуют в Него: и приидут Римляне и возмут место и язык наш.
Tukimwacha tu watu wote watamwamini, nao Waroma watakuja kuliharibu Hekalu letu na taifa letu!”
49 Един же некто от них Каиафа, архиерей сый лету тому, рече им: вы не весте ничесоже,
Hapo, mmoja wao aitwaye Kayafa, ambaye alikuwa Kuhani Mkuu mwaka huo, akawaambia, “Ninyi hamjui kitu!
50 ни помышляете, яко уне есть нам, да един человек умрет за люди, а не весь язык погибнет.
Je, hamwoni kwamba ni afadhali kwenu mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, kuliko taifa zima liangamizwe?”
51 Сего же о себе не рече, но архиерей сый лету тому, прорече, яко хотяше Иисус умрети за люди,
Yeye hakusema hivyo kwa hiari yake mwenyewe, bali kwa vile alikuwa Kuhani Mkuu mwaka huo, alibashiri kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa lao;
52 и не токмо за люди, но да и чада Божия расточеная соберет во едино.
na wala si kwa ajili yao tu, bali pia apate kuwaleta pamoja watoto wa Mungu waliotawanyika.
53 От того убо дне совещаша, да убиют Его.
Basi, tangu siku hiyo viongozi wa Wayahudi walifanya mipango ya kumwua Yesu.
54 Иисус же ктому не яве хождаше во Иудеех, но иде оттуду во страну близ пустыни, во Ефрем нарицаемый град, и ту хождаше со ученики Своими.
Kwa hiyo, Yesu hakutembea tena hadharani kati ya Wayahudi, bali alitoka hapo, akaenda mahali karibu na jangwa, katika mji uitwao Efraimu. Akakaa huko pamoja na wanafunzi wake.
55 Бе же близ Пасха Иудейска, и взыдоша мнози во Иерусалим от стран прежде Пасхи, да очистятся.
Sikukuu ya Wayahudi ya Pasaka ilikuwa karibu, na watu wengi walikwenda Yerusalemu ili wajitakase kabla ya sikukuu hiyo.
56 Искаху убо Иисуса и глаголаху к себе, в церкви стояще: что мнится вам, яко не имать ли приити в праздник?
Basi, wakawa wanamtafuta Yesu; nao walipokusanyika pamoja Hekaluni wakaulizana, “Mwaonaje? Yaonekana kwamba haji kabisa kwenye sikukuu, au sivyo?”
57 Даша же архиерее и фарисее заповедь, да аще кто ощутит (Его), где будет, повесть, яко да имут Его.
Makuhani wakuu na Mafarisayo walikuwa wametoa amri kwamba mtu akijua mahali aliko Yesu awaarifu kusudi wamtie nguvuni.

< От Иоанна святое благовествование 11 >