< Книга пророка Иоиля 2 >
1 Вострубите трубою в Сионе, проповедите в горе Моей святей, и да смятутся вси живущии на земли, яко предстоит день Господень, яко близ,
Pigeni tarumbeta katika Sayuni; pigeni mbiu katika mlima wangu mtakatifu. Wote waishio katika nchi na watetemeke, kwa kuwa siku ya Bwana inakuja. Iko karibu,
2 день тмы и бури, день облака и мглы: якоже утро разлиются по горам людие мнози и крепцы, подобни им не быша от века, и по них не приложится до лет в род и род:
siku ya giza na huzuni, siku ya mawingu na utusitusi. Kama mapambazuko yasambaavyo toka upande huu wa milima hata upande mwingine jeshi kubwa na lenye nguvu linakuja. Jambo kama hili halijakuwepo tangu zamani wala halitakuwepo tena kamwe kwa vizazi vijavyo.
3 яже пред ним огнь потребляяй, и яже за ним возгараяся пламень: якоже рай Сладости земля пред лицем его, и яже созади его поле пагубы, и спасающагося не будет им:
Mbele yao moto unateketeza, nyuma yao miali ya moto inawaka kwa nguvu. Mbele yao nchi iko kama bustani ya Edeni, nyuma yao ni jangwa lisilofaa: hakuna kitu kinachowaepuka.
4 якоже вид конский вид их, и якоже конницы, тако проженут:
Wanaonekana kama farasi; wanakwenda mbio kama askari wapanda farasi.
5 якоже глас колесниц на верхи гор востекут, и яко глас пламене огненна попаляюща тростие, и яко людие мнози и крепцы воополчающиися на брань.
Wanatoa sauti kama magari ya vita, wanaporukaruka juu ya vilele vya milima, kama mlio wa miali ya moto ilayo mabua, kama jeshi kubwa lililojipanga kwa ajili ya vita.
6 От лица их сокрушатся людие: всякое лице аки опаление горнца.
Wanapoonekana, mataifa yanakuwa katika maumivu makuu; kila uso unabadilika rangi.
7 Якоже борцы потекут, и якоже мужие храбри взыдут на ограды: и кийждо в путь свой пойдет, и не совратят путий своих,
Wanashambulia kama wapiganaji wa vita; wanapanda kuta kama askari. Wote wanatembea katika safu, hawapotoshi safu zao.
8 и кийждо от брата своего не отступит: отягощени оружии своими пойдут и в стрелах своих падут, но не скончаются.
Hakuna anayemsukuma mwenzake; kila mmoja anakwenda mbele moja kwa moja. Wanapita katika vizuizi bila kuharibu safu zao.
9 Града имутся, и на забрала востекут, и на храмины взлезут, и оконцами внидут, якоже татие.
Wanaenda kasi kuingia mjini; wanakimbia ukutani. Wanaingia ndani ya nyumba; kwa kuingilia madirishani kama wevi.
10 Пред лицем его смятется земля и потрясется небо: солнце и луна померкнут, и звезды угасят свет свой.
Mbele yao dunia inatikisika, anga linatetemeka, jua na mwezi vinatiwa giza, na nyota hazitoi mwanga wake tena.
11 И Господь даст глас Свой пред лицем силы Своея, яко мног есть зело полк Его, яко крепка дела словес Его: зане велик день Господень, велик и светел зело, и кто будет доволен ему?
Bwana anatoa mshindo wa ngurumo mbele ya jeshi lake; majeshi yake hayana idadi, ni wenye nguvu nyingi wale ambao hutii agizo lake. Siku ya Bwana ni kuu, ni ya kutisha. Ni nani anayeweza kuistahimili?
12 И ныне глаголет Господь Бог ваш: обратитеся ко Мне всем сердцем вашим в посте и в плачи и в рыдании,
“Hata sasa,” asema Bwana, “nirudieni kwa mioyo yenu yote, kwa kufunga, kwa kulia na kuomboleza.”
13 и расторгните сердца ваша, а не ризы ваша, и обратитеся ко Господу Богу вашему, яко милостив и щедр есть, долготерпелив и многомилостив и раскаявайся о злобах.
Rarueni mioyo yenu na siyo mavazi yenu. Mrudieni Bwana, Mungu wenu, kwa maana yeye ndiye mwenye neema na mwingi wa huruma, si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa upendo, huona huruma, hujizuia kuleta maafa.
14 Кто весть, обратится ли, и раскается, и оставит за собою благословение и жертву и возлияние Господу Богу вашему?
Ni nani ajuaye? Yeye aweza kugeuka na kuwa na huruma na kuacha baraka nyuma yake: sadaka za nafaka na sadaka za vinywaji kwa ajili ya Bwana Mungu wenu.
15 Вострубите трубою в Сионе, освятите пост, проповедите цельбу,
Pigeni tarumbeta katika Sayuni, tangazeni saumu takatifu, liiteni kusanyiko takatifu.
16 соберите люди, освятите церковь, изберите старейшины, совокупите младенцы ссущия сосцы: да изыдет жених от ложа своего, и невеста от чертога своего.
Wakusanyeni watu, wekeni wakfu kusanyiko; waleteni pamoja wazee, wakusanyeni watoto, wale wanyonyao maziwa. Bwana arusi na atoke chumbani mwake na bibi arusi naye atoke katika chumba chake.
17 Между степеньми жертвенника восплачутся жерцы служащии Господу и рекут: пощади, Господи, люди Твоя и не даждь достояния Твоего на укоризну, да не обладают ими языцы, да не рекут во языцех: где есть Бог их?
Makuhani, ambao wanahudumu mbele za Bwana, na walie katikati ya ukumbi wa Hekalu na madhabahu. Waseme, “Wahurumie watu wako, Ee Bwana. Usifanye urithi wako kitu cha kudharauliwa, neno la dhihaka kati ya mataifa. Kwa nini wasemezane miongoni mwao, ‘Yuko wapi Mungu wao?’”
18 И возревнова Господь о земли Своей и пощаде люди Своя.
Kisha Bwana atakuwa na wivu kwa ajili ya nchi yake na kuwa na huruma juu ya watu wake.
19 И отвеща Господь людем Своим и рече: се, Аз вам послю пшеницу и вино и масло древяное, и насытитеся их, и не дам вас ксему на поругание во языцех:
Bwana atawajibu: “Ninawapelekea nafaka, mvinyo mpya na mafuta, vya kuwatosha ninyi hadi mridhike kabisa; kamwe sitawafanya tena kitu cha kudharauliwa na mataifa.
20 и сущаго от севера отжену от вас и отрину его на землю безводную, и погублю лице его в мори первем и задняя его в мори последнем, и взыдет гнилость его, и взыдет смрад его, яко возвеличи дела своя.
“Nitafukuza jeshi la kaskazini likae mbali nanyi, nikilisukuma ndani ya jangwa, askari wa safu za mbele wakienda ndani ya bahari ya mashariki na wale wa safu za nyuma katika bahari ya magharibi. Uvundo wake utapaa juu; harufu yake itapanda juu.” Hakika ametenda mambo makubwa.
21 Дерзай, земле, радуйся и веселися, яко возвеличи Господь, еже сотворити.
Usiogope, ee nchi; furahi na kushangilia. Hakika Bwana ametenda mambo makubwa.
22 Дерзайте, скоти польстии, яко прозябнуша поля пустыни, яко древо принесе плод свой, виноград и смокви даша силу свою.
Msiogope, enyi wanyama pori, kwa kuwa mbuga za malisho yenu zinarudia ubichi. Miti nayo inazaa matunda, mtini na mzabibu inatoa utajiri wake.
23 И чада Сионя, радуйтеся и веселитеся о Господе Бозе вашем, яко даде вам пищу в правду и одождит вам дождь ранний и поздный, якоже и прежде:
Furahini, enyi watu wa Sayuni, shangilieni katika Bwana Mungu wenu, kwa kuwa amewapa mvua za vuli kwa kipimo cha haki. Anawapelekea mvua nyingi, mvua ya vuli na ya masika, kama mwanzoni.
24 и наполнятся гумна ваша пшеницы, и преизлиются точила вином и елеем.
Sakafu za kupuria zitajaa nafaka, mapipa yatafurika mvinyo mpya na mafuta.
25 И воздам вам вместо лет, в няже поядоша прузи и мшица, и сиплеве и гусеницы, сила Моя великая, юже послах на вы:
“Nitawalipa kwa ajili ya miaka ile iliyoliwa na nzige: parare, madumadu na tunutu, jeshi langu kubwa ambalo nililituma katikati yenu.
26 и снесте ядуще и насытитеся, и похвалите имя Господа Бога вашего, Яже сотвори с вами чудеса: и не посрамятся людие Мои во век.
Mtakuwa na wingi wa vyakula mpaka mshibe, na mtalisifu jina la Bwana Mungu wenu, ambaye amefanya maajabu kwa ajili yenu; kamwe watu wangu hawataaibishwa tena.
27 И уведите, яко посреде Израиля Аз есмь, и Аз Господь Бог ваш, и несть иного разве Мене: и не посрамятся ктому людие Мои во век.
Ndipo mtakapojua kwamba mimi niko katika Israeli kwamba mimi ndimi Bwana Mungu wenu, na kwamba hakuna mwingine; kamwe watu wangu hawataaibika tena.
28 И будет по сих, и излию от Духа Моего на всяку плоть, и прорекут сынове ваши и дщери ваша, и старцы ваши сония узрят, и юноты ваши видения увидят:
“Hata itakuwa, baada ya hayo, nitamimina Roho wangu juu ya wote wenye mwili. Wana wenu na binti zenu watatabiri, wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu wataona maono.
29 ибо на рабы Моя и на рабыни Моя во дни оны излию от Духа Моего:
Hata juu ya watumishi wangu, wanaume kwa wanawake, katika siku zile nitamimina Roho wangu.
30 и дам чудеса на небеси и на земли, кровь и огнь и курение дыма:
Nami nitaonyesha maajabu katika mbingu na duniani: damu, moto na mawimbi ya moshi.
31 солнце обратится во тму, и луна в кровь, прежде неже приити дню Господню великому и просвещенному:
Jua litageuzwa kuwa giza na mwezi kuwa mwekundu kama damu, kabla ya kuja siku ya Bwana ile kuu na ya kutisha.
32 и будет, всяк иже призовет имя Господне, спасется: яко в горе Сионе и во Иерусалиме будет спасаемый, якоже рече Господь, и благовествуемии, ихже Господь призва.
Na kila mtu atakayeliitia jina la Bwana ataokolewa. Kwa maana juu ya Mlima Sayuni na katika Yerusalemu kutakuwepo wokovu, kama Bwana alivyosema, miongoni mwa walionusurika ambao Bwana awaita.