< Книга Иова 9 >

1 Отвещав же Иов, рече:
Kisha Ayubu akajibu na kusema,
2 воистинну вем, яко тако есть: како бо будет праведен человек у Господа?
“kweli najua kwamba ndivyo hivyo. Lakini ni kwa namna gani mtu anakuwa na haki kwa Mungu?
3 Аще бо восхощет судитися с Ним, не послушает Его, да не преречет ко единому словеси Его от тысящи.
Kama akitaka kujibishana na Mungu, hatamjibu yeye mara moja katika elfu zaidi.
4 Премудр бо есть мыслию, крепок же и велик: кто жесток быв противу Его, пребысть?
Mungu ni mwenye hekima moyoni na ukuu katika nguvu; ni nani daima aliyejifanya mwenyewe kuwa mgumu dhidi yake na akafanikiwa? -
5 Обетшаяй горы, и не ведят, превращаяй я гневом:
ambaye huiondoa milima bila kumtahadharisha yeyote wakati akiipindua katika hasira zake -
6 трясый поднебесную из оснований, столпи же ея колеблются:
ambaye huitikisa nchi itoke mahali pake na mihimili yake hutikisika.
7 глаголяй солнцу, и не восходит, звезды же печатствует:
Ni Mungu yule yule ambaye huliamuru jua lisichomoze, nalo halichomozi, na ambaye huzihifadhi nyota,
8 прострый един небо и ходяй но морю, яко по земли:
ambaye peke yake ni mwenye kupanua mbingu na kuyatuliza mawimbi ya bahari,
9 творяй Плиады и Еспера, и Арктура и сокровища южная:
ambaye huumba Dubu, Orioni, kilima, na makundi ya nyota ya kusini.
10 творяй велия и неизследованная, славная же и изрядная, имже несть числа.
Ni Mungu yule yule atendaye mambo makuu, mambo yasiyofahamika - hasa, mambo ya ajabu yasiyohesabika.
11 Аще приидет ко мне, не имам видети: и аще мимоидет мене, никако уразумех.
Tazama, huenda karibu nami, na siwezi kumuona yeye; pia hupita kwenda mbele, lakini ni simtambue.
12 Аще возмет, кто возвратит? Или кто речет Ему: что сотворил еси?
Kama akichukua kitu chochote, nani atamzuia? Nani awezaye kumuuliza, 'unafanya nini?'
13 Сам бо отвращает гнев, слякошася под Ним кити поднебеснии.
Mungu hataondoa hasira yake; wamsaidiao Rahabu huinama chini yake.
14 Аще же мя услышит, или разсудит глаголы моя?
Je ni upungufu kiasi gani mimi nitamjibu, je nichague maneno kuhojiana naye?
15 Аще бо и праведен буду, не услышит мене, суду Его помолюся:
Hata kama ni mwenye haki, nisingelimjibu; ningeomba msamaha tu kwa hukumu yangu.
16 аще же воззову, и услышит мя, не иму веры, яко услыша глас мой.
Hata kama ningelimwita na yeye akanitikia, nisingeamini kuwa ameisikia sauti yangu.
17 Да не мглою мя потребит, многа же ми сотрения сотвори всуе,
kwa kuwa yeye anidhoofishaye kwa dhoruba na kuyaongeza majeraha yangu pasipo sababu.
18 не оставляет бо мя отдохнути, исполни же мя горести.
Yeye hataki hata kuniruhusu nipate kuvuta pumzi; badala yake, hunijaza uchungu.
19 Понеже силен есть крепостию: кто убо суду Его воспротивится?
Kama ni habari ya nguvu, tazama! yeye ni mwenye uwezo! Kama ni habari ya haki, ni nani atakaye mhukumu?
20 Аще бо буду праведен, уста моя нечестия сотворят: аще же буду непорочен, стропотен буду.
Ingawa ni mwenye haki, kinywa changu mwenyewe kitanihukumu; na ingawa ni mtakatifu, maneno yangu yatashuhudia kuwa ni mwenye kosa.
21 Аще бо нечестие сотворих, не вем душею моею: обаче отемлется ми живот.
Mimi ni mtakatifu, lakini siijali zaidi nafsi yangu; Naudharau uhai wangu mwenyewe.
22 Темже рех: велика и сильна губит гнев.
Haileti tofauti yoyote, kwa sababu hiyo nasema kwamba yeye huangamiza watu wasio na makosa na waovu pia.
23 Яко лукавии смертию лютою погибнут, обаче праведным посмеваются.
Kama hilo pigo likiua ghafla, yeye atafurahi mateso yake mtu asiye na kosa.
24 Предана есть земля в руце нечестиваго, лица судий ея покрывает: аще же не Сам есть, кто есть?
Dunia imetiwa mkononi mwa watu waovu; Mungu hufunika nyuso za waamuzi wake. kama si yeye hufanya, ni nani basi?
25 Житие же мое есть легчае скоротечца: отбегоша и не видеша.
Siku zangu zinapita haraka kuliko tarishi akimbiae; siku zangu zinakimbia mbali; wala hazioni mema mahali popote.
26 Или есть кораблем след пути, или орла летяща, ищуща яди?
Zinapita kama mashua zilizoundwa kwa mafunjo ziendazo kwa kasi, na zinakasi kama tai ashukaye upesi katika mawindo yake.
27 Аще бо реку: забуду глаголя, приникнув лицем воздохну,
Kama ni kisema kwamba mimi nitasahau kuhusu manung'uniko yangu, kwamba nitaacha kuonyesha sura ya huzuni na kuwa na furaha,
28 трясуся всеми удесы: вем бо, яко не безвинна мя оставиши.
Mimi nitaziogopa huzuni zangu zote kwa sababu nafahamu kuwa hutanihesabu kuwa sina hatia.
29 Аще же нечестив есмь, почто не умрох?
Nitahukumiwa; kwa nini, basi, nitaabike bure?
30 Аще бо измыюся снегом и очищуся руками чистыми,
Kama najiosha mwenyewe kwa maji ya theluji na kuitakasa mikono yangu na kuwa safi zaidi,
31 доволно во скверне омочил мя еси, возгнушася же мною одежда моя.
Mungu atanitumbukiza shimoni, na nguo zangu mwenyewe zitanichukia.
32 Неси бо человек, якоже аз, Емуже противопрюся, да приидем вкупе на суд.
Kwa kuwa Mungu si mtu, kama mimi, kwamba naweza kumjibu, hata tukaribiane katika hukumu.
33 О, дабы ходатай нам был, и обличаяй и разслушаяй между обема.
Hakuna hakimu baina yetu awezaye kuweka mkono wake juu yetu sote.
34 Да отимет от мене жезл, страх же Его да не смущает мене:
Hakuna hakimu mwingine ambaye anaweza kuniondolea fimbo ya Mungu, awezaye kuzuia kitisho chake kisinitie hofu. kisha ningesema na nisimuogope.
35 и не убоюся, но возглаголю, ибо тако не вем сам себе.
Lakini kama mambo yalivyo sasa, sitaweza kufanya hivyo.

< Книга Иова 9 >