< Книга Иова 40 >

1 И отвеща Господь Бог ко Иову и рече:
Yahweh aliendelea kuongea na Ayubu na kusema,
2 еда суд со Всесильным укланяется? Обличаяй же Бога отвещати имать Ему.
“Je mtu yeyote anayetaka kukosoa na ajaribu kumsahihisha Mwenye enzi? Na yeye anayehojiana na Mungu, na ajibu yeye.”
3 Отвещав же Иов, рече Господеви:
Ndipo Ayubu akamjibu Yahweh na kusema, “
4 почто еще аз прюся, наказуемь и обличаемь от Господа, слышай таковая ничтоже сый? Аз же кий ответ дам к сим? Руку положу на устех моих:
Tazama, mimi si mtu muhimu; je nawezaje kukujibu? Ninauweka mkono wangu juu ya mdomo wangu.
5 единою глаголах, вторицею же не приложу.
Ninazungumza mara moja, na sitakujibu; hakika, mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.”
6 Паки же отвещав Господь, рече ко Иову из облака:
Kisha Yahweh akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kusema,
7 ни, но препояши яко муж чресла твоя: вопрошу же тя, ты же Ми отвещай.
“Jifunge sasa mkanda kiunoni mwako kama mwanaume, kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
8 Не отвергай суда Моего: мниши ли Мя инако тебе сотворша, разве да явишися правдив?
Je waweza kusema kwa hakika kwamba mimi si mwenye haki? Je utanihukumu mimi ili useme wewe ni mwenye haki?
9 Еда мышца ти есть на Господа, или гласом на Него гремиши?
Je una mkono kama wa Mungu? Je waweza kutoa kishindo kwa sauti kama yeye?
10 Приими же высоту и силу, в славу же и в честь облецыся:
Jivike sasa katika utukufu na katika utu; jivalie mwenyewe heshima na enzi.
11 пусти же Ангелы гневом и всякаго укорителя смири,
Sambaza ziada ya hasira yako; mtazame kila mmoja mwenye kiburi na umshushe chini.
12 величава же угаси и согной нечестивыя абие:
Mwangalie kila mmoja mwenye kiburi na umweke chini; wakanyage chini watu waovu mahali wanaposimama.
13 скрый же в землю вне вкупе и лица их безчестия исполни.
Wazike ardhini pamoja; zifunge nyuso zao katika sehemu zilizositirika.
14 Исповем, яко может десница твоя спасти.
Ndipo pia nitakapokubali ya kwamba mkono wako wa kulia waweza kukuokoa.
15 Но убо се, зверие у тебе, траву аки волове ядят:
Mwangalie sasa kiboko, ambaye niliwafanya kama nilivyokufanya wewe; anakula nyasi kama ng'ombe.
16 се убо, крепость его на чреслех, сила же его на пупе чрева:
Ona sasa, nguvu zake ziko katika viuno vyake; nguvu zake zi katika mishipa ya tumbo lake.
17 постави ошиб яко кипарис, жилы же его (яко уже) сплетены суть,
Yeye huuondoa mkia wake kama mti wa mwerezi; mishipa ya paja lake imeunganishwa pamoja.
18 ребра его ребра медяна, хребет же его железо слияно.
Mifupa yake ni kama ya mirija ya shaba; na miguu yake ni kama kipande cha chuma.
19 Сиесть начало создания Господня: сотворен поруган быти Ангелы Его:
Yeye ni mkuu wa viumbe vya Mungu. Ni Mungu pekee, ambaye alimwumba, anaweza kumshinda.
20 возшед же на гору стреминную, сотвори радость четвероногим в тартаре:
Kwa kuwa milima humpatia chakula; hayawani wa mashambani hucheza karibu.
21 под всяким древом спит, при рогозе и тростии и ситовии:
Hujilaza chini ya mimiea ya kivuli katika makao ya mianzi, na katika bwawa la matope.
22 осеняют же над ним древеса велика с леторасльми и ветви напольныя:
Miti yenye vivuli humfunika katika vivuli vyake; mierebi ya kijito inamzunguka pande zote.
23 аще будет наводнение, не ощутит: уповает, яко внидет Иордан во уста его:
Tazama, kama mto utazigharikisha kingo zake, hatikisiki; yeye anajiamini, hata kama Mto wa Yordani unajaa hadi katika pua yake.
24 во око свое возмет его, ожесточився продиравит ноздри.
Je mtu yeyote aweza kumnasa kwa ndoano, au kuichoma pua yake kwa mtego?

< Книга Иова 40 >