< Книга Иова 40 >
1 И отвеща Господь Бог ко Иову и рече:
Bwana akamwambia Ayubu:
2 еда суд со Всесильным укланяется? Обличаяй же Бога отвещати имать Ему.
“Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
3 Отвещав же Иов, рече Господеви:
Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
4 почто еще аз прюся, наказуемь и обличаемь от Господа, слышай таковая ничтоже сый? Аз же кий ответ дам к сим? Руку положу на устех моих:
“Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
5 единою глаголах, вторицею же не приложу.
Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
6 Паки же отвещав Господь, рече ко Иову из облака:
Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
7 ни, но препояши яко муж чресла твоя: вопрошу же тя, ты же Ми отвещай.
“Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
8 Не отвергай суда Моего: мниши ли Мя инако тебе сотворша, разве да явишися правдив?
“Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
9 Еда мышца ти есть на Господа, или гласом на Него гремиши?
Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
10 Приими же высоту и силу, в славу же и в честь облецыся:
Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
11 пусти же Ангелы гневом и всякаго укорителя смири,
Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
12 величава же угаси и согной нечестивыя абие:
mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
13 скрый же в землю вне вкупе и лица их безчестия исполни.
Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
14 Исповем, яко может десница твоя спасти.
Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
15 Но убо се, зверие у тебе, траву аки волове ядят:
“Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
16 се убо, крепость его на чреслех, сила же его на пупе чрева:
Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
17 постави ошиб яко кипарис, жилы же его (яко уже) сплетены суть,
Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
18 ребра его ребра медяна, хребет же его железо слияно.
Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
19 Сиесть начало создания Господня: сотворен поруган быти Ангелы Его:
Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
20 возшед же на гору стреминную, сотвори радость четвероногим в тартаре:
Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
21 под всяким древом спит, при рогозе и тростии и ситовии:
Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
22 осеняют же над ним древеса велика с леторасльми и ветви напольныя:
Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
23 аще будет наводнение, не ощутит: уповает, яко внидет Иордан во уста его:
Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
24 во око свое возмет его, ожесточився продиравит ноздри.
Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?