< Книга Иова 33 >

1 Но послушай, Иове, словес моих и беседу мою внуши:
“Lakini Ayubu, sasa, sikiliza maneno yangu; zingatia kila kitu nitakachosema.
2 се бо, отверзох уста моя, и возглагола язык мой:
Karibu nitafungua kinywa changu; maneno yangu yapo katika ncha ya ulimi wangu.
3 чисто сердце мое во словесех, разум же устну моею чистая уразумеет:
Maneno yangu yanatoka katika moyo mnyofu; midomo yangu hunena kwa uaminifu yale niyajuayo.
4 Дух Божий сотворивый мя, дыхание же Вседержителево поучающее мя:
Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
5 аще можеши, даждь ми ответ к сим: потерпи, стани противу мене, и аз противу тебе.
Unijibu basi, kama unaweza; jiandae kunikabili mimi.
6 От брения сотворен еси ты, якоже и аз: от тогожде сотворения есмы:
Mimi ni kama wewe mbele za Mungu; mimi pia nimetolewa kwenye udongo.
7 не страх мой тя смятет, ниже рука моя тяжка будет на тя.
Huna sababu ya kuniogopa, wala mkono wangu haupaswi kukulemea.
8 Обаче рекл еси во ушы мои, и глас глагол твоих услышах, занеже глаголеши:
“Lakini umesema nikiwa ninakusikia, nami nilisikia maneno yenyewe:
9 чист есмь аз, не согрешая, непорочен же есмь, ибо не беззаконновах:
‘Mimi ni safi na sina dhambi; mimi ni safi na sina hatia.
10 зазор же на мя обрете и мнит мя, яко противника Себе:
Lakini bado Mungu amepata dosari kwangu, naye ananiona kama adui yake.
11 вложи же ногу мою в древо и надсмотрял пути моя вся.
Ananifunga miguu kwa pingu, tena anaziangalia njia zangu zote kwa karibu.’
12 Како бо глаголеши, яко прав есмь, и не послуша мене? Вечен бо есть, иже над земными.
“Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.
13 Глаголеши бо: чесо ради правды моея не услыша всяко слово?
Kwa nini unamlalamikia kwamba yeye hamjibu mwanadamu?
14 Единою бо возглаголет Господь, второе же во сне, или в поучении нощнем,
Kwa kuwa Mungu husema, wakati huu kwa njia moja, au wakati mwingine kwa njia nyingine, ingawa mwanadamu anaweza asielewe.
15 или, яко егда нападает страх лют на человеки, во дреманиих на ложи:
Mungu husema na mwanadamu katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu wasinziapo vitandani mwao,
16 тогда открыет ум человеческий, виденьми страха тацеми их устрашит,
anaweza akasemea masikioni mwao, na kuwatia hofu kwa maonyo,
17 да возвратит человека от неправды, тело же его от падения избави,
ili kumgeuza mtu kutoka kwenye kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,
18 пощаде же душу его от смерти, еже не пасти ему на брани.
kuiokoa nafsi yake na shimo, uhai wake usiangamizwe kwa upanga.
19 Паки же обличи его болезнию на ложи и множество костей его разслаби:
Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,
20 всякаго же брашна пшенична не возможет прияти, а душа его яди хощет,
kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.
21 дондеже согниют плоти его, и покажет кости его тощя:
Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.
22 приближися же на смерть душа его, и живот его во аде. (questioned)
Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.
23 Аще будет тысяща Ангел смертоносных, един от них не уязвит его: аще помыслит сердцем обратитися ко Господу, повесть же человеку свой зазор, и безумие свое покажет,
“Kama bado kuna malaika upande wake kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu, wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,
24 заступит е, еже не впасти ему в смерть, обновит же тело его якоже повапление на стене, кости же его исполнит мозга:
kumwonea huruma na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake’:
25 умягчит же его плоть якоже младенца, и устроит его возмужавша в человецех.
ndipo nyama ya mwili wake hufanywa mpya kama ya mtoto; hurudishwa upya kama siku za ujana wake.
26 Помолится же ко Господу и прият им будет, внидет же лицем веселым со исповеданием, воздаст же человеком правду свою.
Humwomba Mungu, akapata kibali kwake, huuona uso wa Mungu na kushangilia kwa furaha; Mungu humrudisha katika hali yake ya uadilifu.
27 Посем тогда зазрит человек сам себе, глаголя: яковая содевах? И не по достоинству истяза мя, о нихже согреших:
Ndipo huja mbele za watu na kusema, ‘Nilitenda dhambi na kupotosha kilichokuwa haki, lakini sikuadhibiwa kama nilivyostahili.
28 спаси душу мою, еже не внити во истление, и жизнь моя свет узрит.
Alinikomboa nafsi yangu nisitumbukie shimoni, nami nitaishi ili kuufurahia mwanga.’
29 Се, сия вся творит Крепкий (Бог) пути три с мужем:
“Mungu hufanya haya yote kwa mwanadamu; mara mbili hata mara tatu,
30 но избави душу мою от смерти, да живот мой во свете хвалит его.
ili aigeuze nafsi yake toka shimoni, ili nuru ya uzima imwangazie.
31 Внимай, Иове, и послушай мене, премолчи, и аз возглаголю:
“Ayubu, zingatia, nisikilize mimi; nyamaza, nami nitanena.
32 и аще тебе суть словеса, отвещай ми: глаголи, хощу бо оправдитися тебе:
Kama unalo lolote la kusema, unijibu; sema, kwa maana ninataka uonekane huna hatia.
33 аще же ни, ты послушай мене, умолчи, и научу тя премудрости.
Lakini kama huna la kusema, basi nisikilize mimi; nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”

< Книга Иова 33 >