< Книга Иова 3 >

1 Посем отверзе Иов уста своя и прокля день свой,
Baada ya hayo, Ayubu akafunua kinywa chake na kuilani siku aliyozaliwa.
2 глаголя:
Akasema,
3 да погибнет день, в оньже родихся, и нощь оная, в нюже реша: се, мужеск пол:
“Na ipotelee mbali siku niliyozaliwa mimi, usiku uliosema, 'Mimba ya mtoto wa kiume imetungwa.'
4 та нощь буди тма, и да не взыщет ея Господь свыше, ниже да приидет на ню свет,
Siku hiyo na iwe giza; Mungu toka juu asiifikilie, wala mwanga usiiangazie.
5 и да приимет ю тма и сень смертная, да приидет на ню сумрак: проклят буди день той
Ishikwe na giza na giza la mauti liwe lake. Wingu na likae juu yake; kila kitu kiifanyacho siku kuwa giza kweli na kiitishe.
6 и нощь оная: да постигнет ю тма, да не будет во днех лета, ниже да вчислится во днех месяцей:
Usiku huo, na ukamatwe na giza tororo. Usihesabiwe miongoni mwa siku za mwaka; na usiwekwe katika hesabu ya miezi.
7 но нощь оная да будет болезнь, и да не приидет на ню веселие и радость,
Tazama, usiku huo na uwe tasa; na sauti ya shangwe isiwe ndani yake.
8 но да прокленет ю проклинаяй той день, иже имать одолети великаго кита:
Na wailani siku hiyo, hao wafahamuo namna ya kumuamsha lewiathani.
9 да померкнут звезды тоя нощи, да ожидает и на свет да не приидет, и да не видит денницы возсиявающия,
Nyota za mapambazuko yake zitiwe giza. Siku hiyo iutafute mwanga, lakini isiupate; wala makope ya mapambazuko isiyaone,
10 яко не затвори врат чрева матере моея: отяла бо бы болезнь от очию моею:
kwasababu haikuifunga milango ya tumbo la mama yangu, na kwasababu haikunifichia taabu machoni pangu.
11 почто бо во утробе не умрох? Из чрева же изшед, и абие не погибох?
Kwanini si-kufa wakati lipotokeza katika tumbo la uzazi? Kwanini sikuitoa roho yangu hapo mama aliponizaa?
12 Почто же мя прияша на колена? Почто же ссах сосца?
kwanini magoti yake yalinipokea? Kwanini maziwa yake yanipokee hata ninyonye?
13 Ныне убо уснув умолчал бых, уснув же почил бых
Kwa sasa ningelikuwa nimelala chini kimya kimya. Ningelala usingizi na kupata pumziko
14 со царьми и советники земли, иже хваляхуся оружии,
pamoja na wafalme na washauri wa dunia, ambao walijijengea makaburi ambayo sasa ni magofu.
15 или со князи, имже много злата, иже наполниша домы своя сребра,
Au Ningelikuwa nimelala pamoja na wakuu wenye dhahabu, waliozijaza nyumba zao fedha.
16 или якоже изверг излазяй из ложесн матерних, или якоже младенцы, иже не видеша света:
Au pengine ningekuwa sijazaliwa, kama watoto wachanga wasio uona mwanga kabisa.
17 тамо нечестивии утолиша ярость гнева, тамо почиша претружденнии телом,
Huko waovu huacha kusumbua; huko waliochoka hupumzika.
18 вкупе же в веце сем бывшии не слышат гласа собирающаго дань:
Huko wafungwa kwa pamoja hupata amani; hawaisikii sauti ya msimamizi wa watumwa.
19 мал и велик тамо есть, и раб не бояйся господина своего:
Wote wadogo na watu maarufu wako huko; mtumishi yuko huru kwa bwana wake huko.
20 почто бо дан есть сущым в горести свет и сущым в болезнех душам живот,
Kwa nini yeye aliye mashakani kupewa mwanga? Kwa nini hao wenye uchungu moyoni kupewa uhai,
21 иже желают смерти и не получают, ищуще якоже сокровища,
ambao hutamani mauti lakini hawapati; ambao huyachimbulia mauti zaidi ya kutafuta hazina iliyofichika?
22 обрадовани же бывают, аще улучат (смерть)?
Kwa nini kupewa mwanga ambao hushangilia mno na kufurahi walionapo kaburi?
23 Смерть бо мужу покой, егоже путь сокровен есть, затвори бо Бог окрест его:
Kwanini kupewa mwanga mtu ambaye njia zake zimefichika, mtu ambaye Mungu amemzungushia uwa?
24 прежде бо брашен моих воздыхание ми приходит, слезю же аз одержимь страхом,
Kwa kuwa kushusha kwangu pumzi kwatokea badala ya kula; kuugua kwangu kumemiminika kama maji.
25 страх бо, егоже ужасахся, прииде ми, и егоже бояхся, срете мя:
Maana jambo lile niliogopalo limenipata; nalo linitialo hofu limenijilia.
26 ни умирихся, ниже умолчах, ниже почих, и найде ми гнев.
Mimi sioni raha, sipati utulivu, na sipati pumziko; badala yake huja taabu.”

< Книга Иова 3 >