< Книга пророка Иеремии 50 >

1 Слово, еже рече Господь на Вавилон и на землю Халдейскую Иеремиею пророком.
Hili ndilo neno alilosema Bwana kupitia nabii Yeremia kuhusu Babeli na nchi ya Wakaldayo:
2 Возвестите во языцех и слышано сотворите, воздвигните знамение, возопийте и не скрывайте, рцыте: пленен бысть Вавилон, посрамися Вил, победися Меродах, посрамишася изваяния его, сокрушишася кумиры их.
“Tangazeni na mhubiri katikati ya mataifa, twekeni bendera na mkahubiri; msiache kitu chochote, bali semeni, ‘Babeli utatekwa; Beli ataaibishwa, Merodaki atajazwa na hofu kuu. Sanamu zake zitaaibishwa na vinyago vyake vitajazwa hofu kuu.’
3 Яко прииде нань язык от севера, той положит землю его в запустение, и не будет живяй в ней от человека даже и до скота: подвигнушася, отидоша.
Taifa kutoka kaskazini litamshambulia, na kuifanya nchi yake ukiwa. Hakuna hata mmoja atakayeishi ndani yake, watu na wanyama wataikimbia.
4 В тыя дни и в то время, глаголет Господь, приидут сынове Израилевы, тии и сынове Иудины вкупе ходяще и плачуще пойдут и Господа Бога своего взыщут.
“Katika siku hizo, wakati huo,” asema Bwana, “watu wa Israeli pamoja na watu wa Yuda wataenda wakilia ili kumtafuta Bwana Mungu wao.
5 Во Сион испытают стези, тамо бо обративше лица своя приидут и приложатся ко Господу заветом вечным, иже забвению не предастся.
Wataiuliza njia iendayo Sayuni na kuelekeza nyuso zao huko. Watakuja na kuambatana na Bwana katika agano la milele ambalo halitasahaulika.
6 Овцы погибшыя быша людие Мои, пастырие их совратиша их и сотвориша я крытися по горам: с горы на холм ходиша.
“Watu wangu wamekuwa kondoo waliopotea; wachungaji wao wamewapotosha na kuwasababisha kuzurura juu ya milima. Walitangatanga juu ya mlima na kilima, na kusahau mahali pao wenyewe pa kupumzikia.
7 Забыша ложа своего, вси обретающии их снедаху их, и врази их рекоша: не пощадим их, зане согрешиша Господу, пажить правды, собирающему отцев их Господу.
Yeyote aliyewakuta aliwala; adui zao walisema, ‘Sisi hatuna hatia, kwa kuwa wao walitenda dhambi dhidi ya Bwana, malisho yao halisi, Bwana, aliye tumaini la baba zao.’
8 Отидите от среды Вавилона и от земли Халдейски изыдите, и будите яко козлища пред овцами.
“Kimbieni kutoka Babeli; ondokeni katika nchi ya Wakaldayo tena kuweni kama mbuzi wale waongozao kundi.
9 Яко се, Аз воздвигну и приведу на Вавилон собрания языков великих от земли полунощныя, и ополчатся нань: оттуду пленен будет, якоже стрела мужа сильна искусна и возвратится праздна.
Kwa maana nitaamsha na kuleta dhidi ya Babeli muungano wa mataifa makubwa kutoka nchi ya kaskazini. Watashika nafasi zao dhidi yake, naye kutokea kaskazini atatekwa. Mishale yao itakuwa kama mishale ya mashujaa walio hodari, ambao hawawezi kurudi mikono mitupu.
10 И будет земля Халдейска в разграбление, вси грабителе ея наполнятся глаголет Господь:
Kwa hiyo Ukaldayo utatekwa nyara; wote wamtekao nyara watapata za kutosha,” asema Bwana.
11 зане веселистеся и велеречивасте, расхищающе наследие Мое, скакасте бо яко телцы на траве и бодосте якоже волы.
“Kwa sababu hushangilia na kufurahi, wewe utekaye urithi wangu, kwa sababu unachezacheza kama mtamba anayepura nafaka, na kulia kama farasi dume,
12 Поругана бысть мати ваша зело, и посрамися родившая вас: се, последняя во языцех пуста и непроходна и суха.
mama yako ataaibika mno, yeye aliyekuzaa atatahayari. Atakuwa mdogo kuliko mataifa mengine yote, atakuwa nyika, nchi kame na jangwa.
13 От гнева Господня не поживут во век: но будет весь в запустение, и всяк ходяй сквозе Вавилон подивится и позвиждет над всякою язвою Его.
Kwa sababu ya hasira ya Bwana hatakaliwa na mtu, lakini ataachwa ukiwa kabisa. Wote watakaopita Babeli watatiwa hofu na kudhihaki kwa sababu ya majeraha yake yote.
14 Ополчитеся на Вавилон, вси окрестнии наляцающии лук, стреляйте нань, не щадите стрел ваших, понеже пред Господем согреши,
“Shikeni nafasi zenu kuzunguka Babeli, enyi nyote mvutao upinde. Mpigeni! Msibakize mshale wowote, kwa kuwa ametenda dhambi dhidi ya Bwana.
15 возмите его: ослабеша руце его, падоша основания его, сокрушишася забрала его, яко месть Господня есть: отмстите ему, якоже сотвори, сотворите ему:
Piga kelele dhidi yake kila upande! Anajisalimisha, minara yake inaanguka, kuta zake zimebomoka. Kwa kuwa hiki ni kisasi cha Bwana, mlipizeni kisasi; mtendeeni kama alivyowatendea wengine.
16 потребите семя от Вавилона, и держащаго серп во время жатвы от лица меча Еллинска, кийждо к людем своим обратится, и кийждо в землю свою убежит.
Katilieni mbali mpanzi kutoka Babeli, pamoja na mvunaji na mundu wake akivuna. Kwa sababu ya upanga wa mdhalimu kila mmoja na arejee kwa watu wake mwenyewe, kila mmoja na akimbilie kwenye nchi yake mwenyewe.
17 Овча заблуждающее Израиль, львове изнуриша е: первее яде его царь Ассур, сей же последний и кости оглода ему Навуходоносор царь Вавилонский.
“Israeli ni kundi lililotawanyika ambalo simba wamelifukuzia mbali. Wa kwanza kumla alikuwa mfalme wa Ashuru, wa mwisho kuponda mifupa yake alikuwa Nebukadneza mfalme wa Babeli.”
18 Сего ради тако глаголет Господь Вседержитель, Бог Израилев: се, Аз посещу на царя Вавилонска и на землю его, якоже посетих на царя Ассурска,
Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Nitamwadhibu mfalme wa Babeli na nchi yake kama nilivyomwadhibu mfalme wa Ashuru.
19 и возведу паки Израиля на пажить его, и упасется в Кармиле и Васане, и в горе Ефремли и в Галааде, и насытится душа его.
Lakini nitamrudisha Israeli katika malisho yake mwenyewe naye atalisha huko Karmeli na Bashani; njaa yake itashibishwa juu ya vilima vya Efraimu na Gileadi.
20 В тыя дни и в той час, глаголет Господь, поищут неправды Израилевы, и не будет, и грехов Иудиных, и не обрящутся: яко милостив буду им оставшымся.
Katika siku hizo, wakati huo,” asema Bwana, “uchunguzi utafanyika kwa ajili ya kosa la Israeli, lakini halitakuwepo, kwa ajili ya dhambi za Yuda, lakini haitapatikana hata moja, kwa kuwa nitawasamehe mabaki nitakaowaacha.
21 На землю владеющих взыди и на живущих в ней посети, разори и убий сущыя по них, глаголет Господь, и сотвори вся, елика заповедаю тебе.
“Shambulieni nchi ya Merathaimu na wale waishio huko Pekodi. Wafuatieni, waueni na kuwaangamiza kabisa,” asema Bwana. “Fanyeni kila kitu nilichowaamuru.
22 Глас брани и сотрение велико в земли Халдейстей.
Kelele ya vita iko ndani ya nchi, kelele ya maangamizi makuu!
23 Како сокрушися и сотреся млат всея земли? Како обратися в пустыню Вавилон во языцех?
Tazama jinsi nyundo ya dunia yote ilivyovunjika na kuharibika! Tazama jinsi Babeli ilivyokuwa ukiwa miongoni mwa mataifa!
24 Взыдут на тя, и пленен будеши, и не познаеши, яко Вавилон еси: обретен и ят еси, понеже разгневал еси Господа.
Nimetega mtego kwa ajili yako, ee Babeli, nawe ukakamatwa kabla haujafahamu; ulipatikana na ukakamatwa kwa sababu ulimpinga Bwana.
25 Отверзе Господь сокровища Своя и изнесе сосуды гнева Своего, яко дело есть Господу Вседержителю в земли Халдейстей:
Bwana amefungua ghala lake la silaha na kuzitoa silaha za ghadhabu yake, kwa kuwa Bwana Mwenyezi Mwenye Nguvu Zote anayo kazi ya kufanya katika nchi ya Wakaldayo.
26 яко приидоша времена его: отверзите хранилища его и испытайте и, аки вертеп, и погубите его, да не будет останка его.
Njooni dhidi yake kutoka mbali. Zifungueni ghala zake za nafaka; mlundikeni kama lundo la nafaka. Mwangamizeni kabisa na msimwachie mabaki yoyote.
27 Изсушите вся плоды его, и да снидут в заклание: горе им, яко прииде день их и час отмщения их.
Waueni mafahali wake wachanga wote; waacheni washuke machinjoni! Ole wao! Kwa kuwa siku yao imewadia, wakati wao wa kuadhibiwa.
28 Глас бежащих и избегших от земли Вавилонския, да возвестят в Сионе отмщение Господа Бога нашего, отмщение храма Его.
Wasikilizeni watoro na wakimbizi kutoka Babeli wakitangaza katika Sayuni jinsi Bwana, Mungu wetu alivyolipiza kisasi, kisasi kwa ajili ya Hekalu lake.
29 Возвестите на Вавилон многим, всем наляцающым лук, ополчитеся нань окрест: да не убежит ни един из него: воздайте ему по делом его, по всему, елика сотвори, сотворите ему, яко воста на Господа Бога Святаго Израилева.
“Waiteni wapiga mishale dhidi ya Babeli, wote wale wavutao upinde. Pigeni kambi kumzunguka kabisa, asitoroke mtu yeyote. Mlipizeni kwa matendo yake; mtendeeni kama alivyotenda. Kwa kuwa alimdharau Bwana, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
30 Сего ради падут юноши его на стогнах его, и вси мужие воинстии его низвержени будут в той день, глаголет Господь.
Kwa hiyo, vijana wake wanaume wataanguka barabarani; askari wake wote watanyamazishwa siku ile,” asema Bwana.
31 Се, Аз на тя, горде, глаголет Господь Бог Вседержитель, яко прииде день твой и час посещения твоего:
“Tazama, niko kinyume nawe, ewe mwenye majivuno,” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, “kwa kuwa siku yako imewadia, yaani, wakati wako wa kuadhibiwa.
32 и падет гордыня твоя и разрушится, и не будет возставляяй ю: и возжгу огнь в дубраве его, и пояст вся окрестная его.
Mwenye majivuno atajikwaa na kuanguka, wala hakuna yeyote atakayemuinua; nitawasha moto katika miji yake, utakaowateketeza wote wanaomzunguka.”
33 Тако глаголет Господь Вседержитель: порабощение терпят сынове Израилевы и сынове Иудины, вкупе вси пленившии их поработиша их, не хощут бо отпустити их.
Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Watu wa Israeli wameonewa, nao watu wa Yuda pia. Wote waliowateka wamewashikilia sana, wanakataa kuwaachia waende.
34 Избавитель же их сильный, Господь Вседержитель имя Ему, судом судити имать супостаты своя, яко да избавит землю, и потрясет жительми Вавилонскими.
Lakini Mkombozi wao ana nguvu; Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake. Atatetea kwa nguvu shauri lao ili alete raha katika nchi yao, lakini ataleta msukosuko kwa wale waishio Babeli.
35 Мечь на Халдеев, глаголет Господь, и на жители Вавилонския, и на князи и на мудрыя его,
“Upanga dhidi ya Wakaldayo!” asema Bwana, “dhidi ya wale waishio Babeli na dhidi ya maafisa wake na watu wenye busara!
36 мечь на обаятели его, и буии будут, и мечь на сильныя его, и ослабеют:
Upanga dhidi ya manabii wake wa uongo! Watakuwa wapumbavu. Upanga dhidi ya mashujaa wake! Watajazwa na hofu kuu
37 мечь на кони его и на колесницы его, и на вся прочыя люди, иже суть посреде его, и будут яко жены: мечь на сокровища его, и расхитятся:
Upanga dhidi ya farasi na magari yake ya vita pamoja na askari wake wote wa kigeni katika safu zake! Wao watakuwa kama wanawake. Upanga dhidi ya hazina zake! Hizo zitatekwa nyara.
38 мечь на воды его, и постыдятся, яко земля изваянных есть, и во островех хваляхуся.
Ukame juu ya maji yake! Nayo yatakauka. Kwa kuwa ni nchi ya sanamu, wao wanaenda wazimu kwa ajili ya sanamu.
39 Сего ради поживут мечты во островех, и поживут в нем дщери сиринов, и не будет живуща в нем ктому во веки, ниже соградится от рода в род.
“Kwa hiyo, viumbe vya jangwani na fisi wataishi humo, nao bundi watakaa humo. Kamwe haitakaliwa tena wala watu hawataishi humo kutoka kizazi hadi kizazi.
40 Якоже преврати Господь Содома и Гоморра и окрестныя грады их, глаголет Господь, не пребудет тамо муж, ниже поживет в нем сын человечь.
Kama vile Mungu alivyoangamiza Sodoma na Gomora pamoja na miji iliyokuwa jirani nayo,” asema Bwana, “vivyo hivyo hakuna mtu yeyote atakayeishi humo. Naam, hakuna mtu yeyote atakayekaa humo.
41 Се, людие идут от севера, и язык велик, и царие мнози востанут от конец земли,
“Tazama! Jeshi linakuja kutoka kaskazini; taifa kubwa na wafalme wengi wanaamshwa kutoka miisho ya dunia.
42 луки и щиты имуще, грозни суть и немилостиви: глас их яко море возшумит, на кони возсядут, уготовани якоже огнь на брань противу тебе, дщи Вавилоня.
Wamejifunga pinde na mikuki; ni wakatili na wasio na huruma. Wanatoa sauti kama bahari inayonguruma wanapoendesha farasi zao; wanakuja kama watu waliojipanga tayari kwa vita ili kukushambulia, ee Binti Babeli.
43 Услыша царь Вавилонский слух их, и ослабеша руце его, скорбь объят его и болезни, яко раждающую.
Mfalme wa Babeli amesikia habari kuwahusu, nayo mikono yake imelegea. Uchungu umemshika, maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa.
44 Се, яко лев изыдет от рыкания Иорданова на место Ефана, яко скоро отмщу их от него, и всякаго юношу над ним поставлю. Кто бо подобен Мне? И кто может стояти противу Мене? И кто есть пастырь сей, иже воспротивится лицу Моему?
Kama simba anayepanda kutoka vichaka vya Yordani kuja kwenye nchi ya malisho mengi, ndivyo nitamfukuza Babeli kutoka nchi yake ghafula. Ni nani aliye mteule, nitakayemweka kwa ajili ya jambo hili? Ni nani aliye kama mimi, na ni nani awezaye kunipinga? Tena ni mchungaji yupi awezaye kusimama kinyume nami?”
45 Темже слышите совет Господень, егоже совеща на Вавилон, и умышления Его, яже умысли на землю Халдейску: аще не исторгнутся агнцы овец их, аще не будет разметана (вкупе с ними) пажить их.
Kwa hiyo, sikia kile Bwana alichokipanga dhidi ya Babeli, kile alichokusudia dhidi ya nchi ya Wakaldayo: Aliye mchanga katika kundi ataburutwa mbali. Yeye ataharibu kabisa malisho yao kwa sababu yao.
46 От гласа бо пленения Вавилонскаго потрясется земля, и вопль во языцех слышан будет.
Kwa sauti ya kutekwa kwa Babeli, dunia itatetemeka; kilio chake kitasikika pote miongoni mwa mataifa.

< Книга пророка Иеремии 50 >