< Книга пророка Иеремии 48 >
1 О Моаве тако рече Господь Вседержитель, Бог Израилев: о, люте Нававу, яко погибе, взяся Кариафаим, посрамися Масигаф и побежден есть.
Kuhusu Moabu: Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Ole wake Nebo, kwa maana utaharibiwa. Kiriathaimu utaaibishwa na kutekwa; Misgabu itaaibishwa na kuvunjavunjwa.
2 Несть ктому целение в Моаве, веселие во Есевоне, помыслиша нань злая: приидите и потребим я от язык: (сего ради) молчя умолкнеши, пойдет за тобою мечь.
Moabu haitasifiwa tena; huko Heshboni watu watafanya shauri baya la anguko lake: ‘Njooni na tuangamize taifa lile.’ Wewe nawe, ee Madmena, utanyamazishwa; upanga utakufuatia.
3 Глас вопля от Оронаима, погубление и сотрение велико.
Sikiliza kilio kutoka Horonaimu, kilio cha maangamizi makuu na uharibifu.
4 Сотреся Моав, возвестите вопль малых его.
Moabu utavunjwa, wadogo wake watapiga kelele.
5 Яко исполнися Алаоф плача: взыдет рыдая путем Оронаима, врази, вопль сотрения слышасте.
Wanapanda kwenda njia ya kuelekea Luhithi, wakilia kwa uchungu wanapotembea, kwenye njia inayoshuka kwenda Horonaimu, kilio cha uchungu kwa ajili ya uharibifu kinasikika.
6 Бежите и спасите душы вашя, и будете яко осел дивий в пустыни.
Kimbieni! Okoeni maisha yenu, kuweni kama kichaka jangwani.
7 Понеже имел еси надежду во оградах твоих и в сокровищих твоих, и ты ят будеши: и пойдет Хамос во преселение, и священницы его и князи его вкупе.
Kwa kuwa mmetumainia matendo yenu na mali zenu, ninyi pia mtachukuliwa mateka, naye Kemoshi atakwenda uhamishoni, pamoja na makuhani wake na maafisa wake.
8 И приидет губитель на всяк град, и не избавится ни един град, и погибнут удолия, и погубятся поля, якоже рече Господь.
Mharabu atakuja dhidi ya kila mji, wala hakuna mji utakaookoka. Bonde litaangamizwa na uwanda utaharibiwa, kwa sababu Bwana amesema.
9 Дайте знамение Моаву, яко прикосновением прикосновен будет, и вси гради его будут пусти и без живущих.
Wekeni chumvi kwa ajili ya Moabu, kwa kuwa ataangamizwa; miji yake itakuwa ukiwa, pasipo kuwa na mtu atakayeishi ndani yake.
10 Проклят (человек) творяй дело Господне с небрежением, и проклят возбраняяй мечу своему от крове.
“Alaaniwe yeye afanyaye kazi ya Bwana kwa hila! Alaaniwe yeye auzuiaye upanga wake usimwage damu!
11 Почиваше Моав от младости своея и бе уповая на славу свою: не прелияся от сосуда в сосуд и во преселение не отиде: сего ради пребысть вкус его в нем, и воня его несть пременена.
“Moabu amestarehe tangu ujana wake, kama divai iliyoachwa kwenye machujo yake, haikumiminwa kutoka chombo kimoja hadi kingine, hajaenda uhamishoni. Kwa hiyo ana ladha ile ile kama aliyokuwa nayo, nayo harufu yake haijabadilika.
12 Сего ради, се, дние грядут, глаголет Господь, и послю ему преселители, и преселят его, и сосуды его истощат и роги его сокрушат:
Lakini siku zinakuja,” asema Bwana, “nitakapotuma watu wamiminao kutoka kwenye magudulia, nao watamimina; wataacha magudulia yake yakiwa matupu na kuvunja mitungi yake.
13 и посрамится Моав от Хамоса, якоже посрамлен есть дом Израилев от Вефиля, в немже имяху надежду.
Kisha Moabu atamwonea aibu mungu wao Kemoshi, kama vile nyumba ya Israeli walivyoona aibu walipotegemea mungu wa Betheli.
14 Како глаголете: сильни есмы и мужие крепцы во бранех?
“Mwawezaje kusema, ‘Sisi ni mashujaa, watu jasiri katika vita’?
15 Погибе Моав, град его, и избраннии юноши его снидоша под мечь, глаголет Царь, Господь Вседержитель имя Его.
Moabu ataangamizwa na miji yake itavamiwa, vijana wake waume walio bora sana watachinjwa,” asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote.
16 Близ день Моавль, еже приити, и зло его скоро зело.
“Kuanguka kwa Moabu kumekaribia, janga kubwa litamjia kwa haraka.
17 Утешайте его вси, иже окрест его, и вси ведящии имя его: рцыте, како сокрушися жезл крепости, палица славна?
Ombolezeni kwa ajili yake, ninyi nyote mnaomzunguka, ninyi nyote mnaojua sifa zake, semeni, ‘Tazama jinsi ilivyovunjika fimbo ya kifalme yenye nguvu, tazama jinsi ilivyovunjika fimbo iliyotukuka!’
18 Сниди от славы и сяди, во влаге живущая, дщи Дивоня, яко губитель Моавский взыдет на тя разрушаяй ограды твоя.
“Shuka kutoka fahari yako na uketi katika ardhi iliyokauka, enyi wenyeji wa Binti wa Diboni, kwa maana yeye aangamizaye Moabu atakuja dhidi yako, na kuangamiza miji yako iliyozungushiwa maboma.
19 На пути стани и воззри, живущая во Ароире, и вопроси бежащаго и избегшаго, и рцы: что се бысть?
Simama kando ya barabara na utazame, wewe unayeishi Aroeri. Muulize mwanaume anayekimbia na mwanamke anayetoroka, waulize, ‘Kumetokea nini?’
20 Посрамися Моав, зане побежден есть: рыдайте и вопийте, возвестите во Арноне, яко погибе Моав,
Moabu amefedheheshwa, kwa kuwa amevunjavunjwa. Lieni kwa huzuni na kupiga kelele! Tangazeni kando ya Arnoni kwamba Moabu ameangamizwa.
21 и суд прииде на землю напольную, на Хелон и на Рефас и на Мофаф,
Hukumu imefika kwenye uwanda wa juu: katika Holoni, Yahasa na Mefaathi,
22 и на Девон и на Наво и на дом Девлафаим,
katika Diboni, Nebo na Beth-Diblathaimu,
23 и на Кариафаим и на Вефгамул и на дом Маонов,
katika Kiriathaimu, Beth-Gamuli na Beth-Meoni,
24 и на Кариоф и на Восора и на вся грады Моавли, иже далече и иже близ суть.
katika Keriothi na Bosra; kwa miji yote ya Moabu, iliyoko mbali na karibu.
25 Отсечен есть рог Моавль, и мышца его сокрушися, глаголет Господь:
Pembe ya Moabu imekatwa, mkono wake umevunjwa,” asema Bwana.
26 упойте его, яко на Господа возвеличися, и приразит Моав руку свою (о блевотину), и будет в посмех и сам.
“Mlevye, kwa kuwa amemdharau Bwana. Moabu na agaegae katika matapishi yake, yeye na awe kitu cha dhihaka.
27 И аще не в посмех бысть тебе Израиль, аще в татстве твоем обретеся, яко воевал еси его: преселишися инамо.
Je, Israeli hakuwa kitu chako cha kudhihakiwa? Je, alikamatwa miongoni mwa wezi, kiasi cha kutikisa kichwa chako kwa dharau kila mara unapozungumza juu yake?
28 Оставите грады и пребывайте на камени, живущии в Моаве, и будите якоже голуби гнездящиися в каменех, во устех скважни.
Ondokeni kwenye miji yenu, mkaishi katikati ya miamba, enyi mnaoishi Moabu. Kuweni kama huwa ambaye hutengeneza kiota chake kwenye mdomo wa pango.
29 Слышахом гордость Моавлю, горд бе зело: презорство его и кичение его, возношение и воздвижение сердца его.
“Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu: kutakabari kwake kwa kiburi na majivuno, kiburi chake na ufidhuli wake, na kujivuna kwa moyo wake.
30 Аз же вем дела его, глаголет Господь: не доволство ли его тако сотвори?
Ninaujua ujeuri wake, lakini ni bure,” asema Bwana, “nako kujisifu kwake hakumsaidii chochote.
31 Сего ради над Моавом возрыдайте всюду, возопийте над мужи Кирады смущения.
Kwa hiyo namlilia Moabu, kwa ajili ya Moabu yote ninalia, ninaomboleza kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi.
32 Яко плачем Иазировым восплачуся о тебе, винограде Асеримль! Леторасли твоя проидоша море, градов Иазировых коснушася, на жатву твою и на винное собирание твое хищник нападе.
Ninalia machozi kwa ajili yenu, kama Yazeri aliavyo, enyi mizabibu ya Sibma. Matawi yako yameenea hadi baharini; yamefika hadi bahari ya Yazeri. Mharabu ameyaangukia matunda yako yaliyoiva na mizabibu yako iliyoiva.
33 Отята есть радость и веселие от Кармила и от земли Моавли, и вино от точил отях: никакоже изгнетаяй винну ягоду по обычаю песни воспоет.
Shangwe na furaha vimetoweka kutoka bustani na mashamba ya Moabu. Nimekomesha kutiririka kwa divai kutoka mashinikizo; hakuna hata mmoja ayakanyagaye kwa kelele za shangwe. Ingawa kuna kelele, sio kelele za shangwe.
34 От вопля Есевонска даже до Елеала и Иаса грады их даша глас свой, от Сигора даже до Оронаима, и юница трилетная, понеже и воды Немрим во сожжение будут.
“Sauti ya kilio chao inapanda kutoka Heshboni hadi Eleale na Yahazi, kutoka Soari hadi Horonaimu na Eglath-Shelishiya, kwa kuwa hata maji ya Nimrimu yamekauka.
35 И отиму Моава, глаголет Господь, жрущаго на горах и кадящаго богом своим.
Nitakomesha wale wote katika Moabu watoao sadaka mahali pa juu, na kufukiza uvumba kwa miungu yao,” asema Bwana.
36 Того ради сердце Моава, яко цевницы звяцати будут, и сердце мое к мужем Кирады яко цевница звяцати будет: сего ради, яже пристяжа, погибоша от человек.
“Kwa hiyo moyo wangu unaomboleza kwa ajili ya Moabu kama filimbi; unaomboleza kama filimbi kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi. Utajiri waliojipatia umetoweka.
37 Всяка бо глава на всяцем месте острижена будет, и всяка брада оброснется, и всяка рука посечена будет, и на всяцем чресле вретище,
Kila kichwa kimenyolewa na kila mwenye ndevu zimekatwa; kila mkono umekatwa na kila kiuno kimefunikwa kwa nguo ya gunia.
38 и на всех храминах Моавских и на стогнах его всяк плачь, понеже сокруших Моава, якоже сосуд непотребен, глаголет Господь.
Juu ya mapaa yote katika Moabu na katika viwanja hakuna kitu chochote isipokuwa maombolezo, kwa kuwa nimemvunja Moabu kama gudulia ambalo hakuna mtu yeyote anayelitaka,” asema Bwana.
39 Како изменися? Возрыдаша, како обрати хребет Моав и посрамися? И бысть Моав в посмех и в ненависть всем окрест себе.
“Tazama jinsi alivyovunjikavunjika! Jinsi wanavyolia kwa huzuni! Tazama jinsi Moabu anavyogeuka kwa aibu! Moabu amekuwa kitu cha kudhihakiwa, kitu cha kutisha kwa wale wote wanaomzunguka.”
40 Яко тако глаголет Господь: се, якоже орел полетит и распрострет криле свои на Моава,
Hili ndilo asemalo Bwana: “Tazama! Tai anashuka chini, akitanda mabawa yake juu ya Moabu.
41 взят есть Кариоф, и ограды его обстоимы суть: и будет сердце сильных Моавских в той день, яко сердце жены родящия.
Miji itatekwa na ngome zake zitatwaliwa. Katika siku hiyo, mioyo ya mashujaa wa Moabu itakuwa kama moyo wa mwanamke katika utungu wa kuzaa.
42 И погибнет Моав от людий, яко на Господа возвеличися.
Moabu ataangamizwa kama taifa kwa sababu amemdharau Bwana.
43 Страх и пропасть и сеть на тя, о, живущий в Моаве, глаголет Господь.
Hofu kuu, shimo na mtego vinawangojea, enyi watu wa Moabu,” asema Bwana.
44 Иже убежит от лица страха, впадет в пропасть: и излазяй из пропасти имется сетию: понеже наведу сия на Моава в лето посещения их, глаголет Господь.
“Yeyote atakayeikimbia hiyo hofu kuu ataanguka ndani ya shimo, yeyote atakayepanda kutoka shimoni, atanaswa katika mtego, kwa sababu nitaletea Moabu mwaka wa adhabu yake,” asema Bwana.
45 Во стени Есевонстей сташа от силы избегше, огнь бо изыде от Есевона и пламень от среды Сеона, и пожже часть Моава и верх сынов смятения.
“Katika kivuli cha Heshboni, wakimbizi wamesimama pasipo msaada, kwa kuwa moto umezimika huko Heshboni, mwali wa moto kutoka katikati ya Sihoni; unaunguza vipaji vya nyuso za Moabu, mafuvu yao wenye kujivuna kwa kelele.
46 Горе тебе, Моаве! Погибоша людие Хамоса, яко отведошася сынове твои и дщери твоя в плен.
Ole wako, ee Moabu! Watu wa Kemoshi wameangamizwa; wana wako wamepelekwa uhamishoni na binti zako wamechukuliwa mateka.
47 И возвращу плен Моавль в последния дни, глаголет Господь. До зде суд Моавль.
“Lakini nitarudisha mateka wa Moabu, katika siku zijazo,” asema Bwana. Huu ndio mwisho wa hukumu juu ya Moabu.