< Книга пророка Иеремии 13 >

1 Сия глаголет Господь ко мне: иди и стяжи себе чресленик льняный и препояши того на чреслех твоих, и в воду да не внесеши того.
Bwana aliniambia hivi, “Nenda ukape nguo ya kitani na kuiweka karibu na kiuno chako, lakini usiiweke kwenye maji kwanza.”
2 И стяжах чресленик по словеси Господню и обложих окрест чресл моих.
Kwa hiyo nilinunua vazi kama vile Bwana alivyoagiza, na nikafunga karibu na kiuno changu.
3 И бысть слово Господне ко мне вторицею, рекущее:
Ndipo neno la Bwana likanijia mara ya pili, kusema,
4 возми чресленик, егоже стяжал еси, иже есть окрест чресл твоих, и востани и иди ко Евфрату, и скрый того тамо во разселине каменне.
“Twaa vazi lako ulilolinunua lililo karibu na kiuno chako, uinuke, ukasafiri mpaka Frati. Ukaifiche huko katika mwamba wa jabali.
5 И идох и скрых того во Евфрате, якоже заповеда мне Господь.
Basi nikaenda na kuificha katika Frati kama vile Bwana alivyoniamuru.
6 И бысть по днех мнозех, и рече Господь ко мне: востани и иди ко Евфрату, и возми оттуду чресленик, егоже заповедах тебе скрыти тамо.
Baada ya siku nyingi, Bwana akaniambia, “Simama, urudi Frati. Ukaichukue nguo ambayo nilikuambia ufiche.”
7 И идох ко Евфрату и раскопах, и взях чресленик от места, идеже скрых его, и се, изгнил бе (чресленик), яко ни на чтоже быти потребну ему.
Kwa hiyo nikarudi Frati na kuchimba na kuchukua nguo mahali pale nilipoificha. Lakini tazama! Nguo hiyo ilikuwa imeharibika; haikuwa nzuri kabisa.
8 И бысть слово Господне ко мне, рекущее: сия глаголет Господь:
Ndipo neno la Bwana likanijia tena, kusema,
9 тако согнити сотворю гордыню Иудину и гордыню Иерусалимлю, многую гордыню сию людий сих строптивых,
“Bwana asema hivi, Nitakiangamiza kiburi cha Yuda na Yerusalemu.
10 иже не хотят послушати словес Моих, ходящих во строптивстве сердца своего и шедших вслед богов чуждих, да служат им и да покланяются им: и будут якоже чресленик той, иже ни к чему потребен.
Watu hawa waovu wanaokataa kusikia neno langu, ambao huenda katika ugumu wa mioyo yao, ambao hufuata miungu mingine ili kuabudu na kuinama-watakuwa kama hii nguo isiyofaa kwa lolote.
11 Зане, якоже придержится чресленик ко чреслом мужа, тако прилепих Мне (весь) дом Израилев и весь дом Иудин, рече Господь: да будут Мне в люди имениты, и в хвалу и в славу, и не послушаша Мене.
Kwa maana kama vile vazi lililofungwa kwenye viuno vya mtu, ndivyo nimefainya nyumba yote ya Israeli na nyumba yote ya Yuda zimefungwa kwangu- hili ndilo tamko la Bwana-wawe watu wangu, ili kunifanya jina, sifa, na heshima. Lakini hawakunisikiliza.
12 И речеши к людем сим словеса сия: тако рече Господь Бог Израилев: всяк мех исполнится вина. И будет, аще рекут к тебе: еда ведяще не увемы, яко всяк мех исполнится вина?
Basi uwaambie neno hili, 'Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi Kila chupa itajazwa divai.' Watakuambia, 'Je, hatujui kwamba kila chupa itajazwa divai?'
13 И речеши к ним: сия глаголет Господь: се, Аз исполню всех обитателей земли сея, и царей их седящих от колена Давидова на престоле их, и священники и пророки, и Иуду и всех обитающих во Иерусалиме пиянством,
Basi uwaambie,' Bwana asema hivi: Tazama, nitawajaza kila mkaaji wa nchi hii ulevi, na wafalme wanaokaa kiti cha Daudi, na makuhani, na manabii, na wenyeji wote wa Yerusalemu.
14 и расточу их, мужа и брата его, и отцы их и сыны их вкупе: не пожелаю, рече Господь, не пощажу, и не умилосердюся, еже не погубити их.
Ndipo nitawagonganisha kila mtu na mwenzake baba na watoto wao pamoja; hili ndilo tamko la Bwana-sitawahurumia au kuwa na huruma, wala sitawarehemu kutoka kwenye uharibifu.
15 Слышите и внемлите, и не возноситеся, яко Господь глаголал есть.
Sikilizeni na makini. Msiwe na kiburi, kwa kuwa Bwana amesema.
16 Дадите Господу Богу вашему славу прежде даже не смеркнется и прежде даже не преткнутся нозе ваши ко горам темным: и пождете света, и тамо сень смертная, и положени будут во мрак.
Mtukuze Bwana, Mungu wako, kabla ya hajaleta giza, na kabla ya kuifanya miguu yako kuwa na mashaka juu ya milima wakati wa jioni. Kwa maana unatarajia mwanga, lakini ataugeuza kuwa mahali pa giza, na kuwa giza nene.
17 Аще же не послушаете, в тайне восплачется душа ваша от лица гордыни и плачя восплачет, и изведут очи ваши слезы, яко сотрено есть стадо Господне.
Kwa hiyo ikiwa husikilizi, nitaomboleza peke yangu kwa sababu ya kiburi chako. Hakika macho yangu yatalia na kutoa machozi, kwa sababu kundi la Bwana limechukuliwa mateka.
18 Рцыте царю и владыкам: смиритеся, сядите, яко взятся от главы вашея венец славы вашея.
“Mwambieni mfalme na mama wa malkia, 'Jinyenyekezeni, na kukaa chini, kwa maana taji juu ya kichwa chako, kiburi chako na utukufu wako, umeanguka.'
19 Грады южнии затворени суть, и несть отверзаяй: преведен есть весь Иуда, совершиша преселение совершенное.
Miji ya Negebu itafungwa, bila mtu wa kufungua. Yuda watachukuliwa mateka, wote uhamishoni.
20 Воздвигни очи твои, Иерусалиме, и виждь приходящыя от севера: где стадо даное тебе, овцы славы твоея?
Inua macho yako na angalia wale wanaokuja kutoka kaskazini. Je, ni kundi gani alilokupa, kundi ambalo lilikuwa zuri sana kwako?
21 Что речеши, егда посетят тя? И ты научил еси их на тя учением в началство: еда не оымут тя болезни яко жену родящую?
Je, unasema nini wakati Mungu anawaweka wale ambao uliwafundisha kuwa marafiki? Je, huu si mwanzo wa maumivu ya utungu ambayo yatakuchukua kama mwanamke aliye katika kuzaa?
22 Аще же речеши в сердцы твоем: почто приидоша ми сия? За множество беззакония твоего откровена суть задняя твоя, да обруганы будут стопы твоя.
Kisha unaweza kusema moyoni mwako, 'Kwa nini mambo haya yanatokea kwangu?' Itakuwa kwa uovu wa maovu yako ambapo marinda yako yamefunuliwa na umeumizwa.
23 Аще пременит Ефиоплянин кожу свою, и рысь пестроты своя, и вы можете благотворити научившеся злу.
Je, watu wa Kushi hubadilisha rangi yao ya ngozi, au chui hubadilisha madoa yake? Ikiwa ndivyo, basi wewe mwenyewe, ingawa unazoea uovu, utaweza kufanya mema.
24 И развею их, яко стеблие носимое ветром в пустыню.
Kwa hiyo nitawaangamiza kama makapi ambayo yanaangamia katika upepo wa jangwa.
25 Сей жребий твой и часть непокорства твоего на Мя, глаголет Господь, яко забыл еси Мя и надеялся на лжу:
Hii ndiyo niliyokupa, sehemu ambayo nimekuagiza kwako-hili ndilo tamko la Bwana - kwa sababu umenisahau na kuamini katika udanganyifu.
26 темже и аз обнажу бедры твоя противу лица твоего, и явится срамота твоя
Kwa hiyo mimi mwenyewe nitaondoa nguo zako, na sehemu zako za siri zitaonekana.
27 и прелюбодейство твое, и ржание твое и отчуждение блуда твоего: на горах и на селех видех мерзости твоя. Горе тебе, Иерусалиме, яко не очистился еси, последуя мне. Доколе еще?
Uzinzi na ubembe wako, aibu ya tabia yako ya uasherati kwenye milima na katika mashamba! Nitayafanya yaonekane, mambo haya ya machukizo! Ole wako, Yerusalemu! Hutaki kuwa safi. Je! Hili litaendelea kwa muda gani?”

< Книга пророка Иеремии 13 >